Kwa tabia hii una tofauti gani na Ibilisi?

Noma sana!
 
Noma sana!
 
Astaghfirullah

Subhaanallah

Ametakasika Allah na kila aina ya upungufu, haikuwa kwa Allah kumuiamrisha Iblis kumsujudia Adam ila kwa hekma iliyokuwa kubwa, na yeye (Allah) haulizwi kwa anayoyafanya, sio kwa kutakabari bali kwa ukamilifu wa hekma yake.

Sasa wewe ni nani mpaka kumkosoa Allah?

Na ulivyomjinga kosa umeliona ni kwa Ibilisi kutomsujudia Adam, na huoni utukufu wa aliyetoa amri.

Malaika pamoja na Ibilisi walitakiwa kumsujudia Adamu kwa amri ya Allah na wala sio kwa utashi wa Adamu.

Hivyo Ibilisi alilaaniwa kwa kukaidi amri ya Mola wake, ama sababu aliyeitoa haina mashiko na inaonyesha ni kiasi gani Iblisi alikuwa na kibri, jambo ambalo ni chukizo kubwa mbele ya Allah.

Allah subhaanahu wataa'la anasema:-

"Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam! Walimsjudia isipo kuwa Iblisi. Yeye alikuwa miongoni mwa majini, na akavunja amri ya Mola wake Mlezi."(18:50)
 
Jamaa alikuwa na demu wake Mzumbe lecture akawa anamtaka binti, binti kachomoa, lecture kafatilia jamaa ndio anaemiliki, lecture akajenga bifu na jamaa, kila jamaa akipambana anakula sapu tu anakamatwa, akamfuata lecture kulikoni shida nini mbona unanikamata hali nafanya vizuri, lecture akamwambia jamaa " hatma ya maisha yako ipo mikononi mwangu" lecture anamkomoa jamaa kisa yupo na binti amtakae.
Jamaa akaona isiwe tabu akaacha Mzumbe akaenda Muhimbili kusoma udaktari, akahitimu udaktari, miaka imepita zaidi ya 10 na kitu.
Siku moja akaambiwa zamu YAKO kuna mgonjwa ICU nenda kaokoe uhai wake jamaa akaenda chumbani, wakati akiendelea na matibabu akavuta kumbukumbu nyuma akaikumbuka hio sura akasema " huyu ni lecture yule alijifanyia ubaya kisa binti hatma ya maisha yake ipo mikononi mwangu" akamuomba MUNGU akapambana Sana hadi mgonjwa akakaa sawa akarejeshwa wodini, akiwa wodini akawa Akiendelea kumtibu hadi mgonjwa kumbukumbu zikarudi sawa, akiwa ni daktari wa mgonjwa. Kuna siku akamkumbusha mgonjwa ' nitazame vizuri unanikumbuka" Mwalimu hawezi mkukumbuka mwanafunzi, labda kupitia kisa au tukio. Akamkumbusha kisa cha binti na jinsi alivyomwambia chuoni " hatma ya maisha yako ipo mikononi mwangu" mgonjwa akakumbuka, daktari akamwambia sasa wewe hatma ya maisha YAKO ilikuwa mikononi mwangu ningeweza kulipa kisasi ningekudozi ufe lakini sikutaka kulipa ubaya. Mgonjwa akalia Sana na kuomba msamaha.
FUNZO maisha ni mzunguko usimtende ubaya mtu.
 
Asante studio. Kwa upande wangu nilivyosoma mada na maoni ya watu wengi humu, nimederive kwamba kiburi kinatokea kwenye fullness, completeness, satisfaction.

Mahali popote pale ukiwa juu yani ukiwa nafasi ya juu everywhere iwe kwa sifa za watu ama uwezo ama afya ama uchumi ama elimu ama kipaji..etc ni rahisi sana kupata kiburi. Hivyo independence ama kujiamini na kiburi kuna a very thin line.

Shetani alikataa kusujudu kwa sabbu alijiona tayari yuko level za juu. Wengi wetu kiburi tunakipata kutoka katika ile feeling ya independence. Nesi atakipata kwa sabbu anaona yeye kashazalisha wengi ama kuhudumia wengi na amepata mafanikio..wewe na shida zako leo unamletea afu yuko fresh kiafya, kiuchumi, kielimu, kiakili. Kama ana Roho wa Mungu sawa, lakin kama ndo leader wa kuzimu kashampa cheo chap tu lazima uipate pate. Hasa kama wewe ni level ya chini yake.

Similarly sehemu yoyote ile. Tunakuwa na kiburi kwa sabbu afya, akili, uchumi ,watoto, ndoa, familia ziko vizuri. So unaona ninyenyekee ili iweje?Niwe mpole ili nini labda? Nimsaidie kisa nini? Sisemi kwamba its always kiburi maana kuna muda tunahitaji mipaka baina yetu na watu lakini mipaka inapokuwa mikubwa hugeuka kuwa kiburi hasa kama unamuwekea muumba wako akupaye uzima mipaka na kutotaka kujishusha.

Na kiburi mara nyingi huondoka kwa kuserve wengine. Popote pale ukitaka uwe na mafanikio lakin usiwe na kiburi give out. Iwe ni muda wako, kipaji chako, sadaka, nguvu zako, kushiriki na wenzako katika mambo mbalimbali. Na zaidi ibada ya kweli kutoka moyoni. Itakusaidia sana kuweza kukishinda kiburi. Nimejaribu kuandika kwa mtazamo wangu, am open to more info..
 
Kweli kabisa mkuu na yapo matukio mengi Sana kama hayo huwatokea watu

Hii yote Mungu anataka wajifunze kitu Fulani katika Maisha.

Ndio maana tunaambiwa tusidharauriane kwasababu hatujui ni Nani atakuwa msaada katika kesho yetu.

Shukrani Sana mkuu
 

"Similarly sehemu yoyote ile. Tunakuwa na kiburi kwa sabbu afya, akili, uchumi ,watoto, ndoa, familia ziko vizuri. So unaona ninyenyekee ili iweje?Niwe mpole ili nini labda? Nimsaidie kisa nini? Sisemi kwamba its always kiburi maana kuna muda tunahitaji mipaka baina yetu na watu lakini mipaka inapokuwa mikubwa hugeuka kuwa kiburi hasa kama unamuwekea muumba wako akupaye uzima mipaka na kutotaka kujishusha."

Asante Sana pamoja na mengi mazuri Sana uliyosema Mademoiselle nimependa niquote na hayo hapo.

Usiwe unanichoka mara nikutafutapo huwa napata mchango mzuri kutoka kwako.

Shukrani Sana.
 
Shukrani Eturgul Bey 🙂
 
Nilikuwa busy kiasi halafu usiwazungumzie wanachuoni wetu kama wanafunzi fulani wa day care, hao ni watu waheshimiwa na warithi wa mitume kwasababu mitume hawajarithisha dirham wala dinar bali wamerithisha elimu, na wapokezi wa hiyo elimu ni wanawachuoni wabobezi kwenye elimu hata allah جلّ و على akauunganisha ushahidi wake na wa malaika na wanawachuoni kuonesha hadhi yao na nafasi mbele zake.

"Ameshuhudia allah ya kwamba hapana muabudiwa wa haki isipokuwa yeye tu, na malaika na wenye elimu {nao wanashuhudia hilo}, hali ya kuwa yeye ni mwenye kusimamia uadilifu, hapana muabudiwa wa haki isipokuwa yeye mwenye nguvu na mwenye hekma.."

Qur'an 3:18

Kwa kukuweka sawa kuna madh-hab nne mbele ya ahlu sunnah nayo ni madh-hab ya imaam abuu hanifa, imaam maalik, imaam shafiiy na imam ahmad allah awarehemu wote, hawa wametofautiana katika mambo ya kifiqhi tu na wala hawajatofautiana katika itikadi, so ukitoa mifano ya mwezi na swala ya idi au mwezi wa kitaifa na kimataifa watakucheka watu wenye maarifa siku nyingine usirudie.

Tukirudi kwa ibliys alielaaniwa zimetujia khabari kwa wingi kwenye quran juu ya uovu wake na azma yake ya kuwapoteza wana wa aadam mpaka siku itakapofika ajali yake, wala hakuna faida kujua alikuwa muovu kabla ya kuamrishwa kusujudu kwani hilo halibadili chochote.
 
Hakuna nia kwenye kujiita jina baya namna hiyo sisi tumekatazwa kuitana majina mabaya kwenye quran.

".....wala msivunjiane heshima, wala msiitane kwa majina ya kejeli, ni uovu ulioje kutumia jina baya baada ya kuwa mmeamini......"

Qur'an 49:11

Bali zimepokewa athari nyingi kutoka kwa mtume swala na salaam ziwe juu yake akiwabadilisha watu majina baada ya kuwa wana majina ya kijaahiliya yenye maana mbaya kama matatizo, shida, nuksi n.k na akiashiria majina yana athari kwa mtoto.

Wewe unatoa wapi ujasiri wa kujiita ibliys bin shetani? haya hapo juu tumeona unamkosoa allah eti alikosea sana kumwamrisha ibliys kumsujudia aadam, hujakutwa na athari ya jina ulilojibandika bado?.
 
Aliumbwa na moto alafu akapewa adhabu ya kwenda motoni kwake hiyo ni adhabu kweli?
Yeye ameumbwa kwa ndimi za moto, na aya nyingine imekuja kwa joto la moto lisilo na moshi linalounguza.

Yote ni uweza wa allah tabaaraka wa ta'ala na yeye ndiye amewaandalia mashetani adhabu ya moto wa jahannam sasa sifa ya moto wa jahannam si sawa na moto huu tunaotumia sisi sembuse moto walioumbiwa mashetani.

Katika hadithi sahihi mtume swala na salaam ziwe juu yake anasema: "hivi mnadhani moto wa jahannam ni kama mfano wa moto wenu huu? hakika hiyo jahannam ni nyeusi mno kuliko lami." sahihi

Na allah ni muweza juu ya kila kitu.
 
Mungu ana sifa zote uazozijua ziwe mbaya au nzuri
Allah hana sifa mbaya, sifa zake zote ni za ukamilifu na ni nzuri na majina yake ni katika sifa zake.

"Na ana allah majina mazuri basi muombeni kwa majina hayo, na waacheni wale ambao hukengeuka kuachana na majina yake watalipwa kwa yale waliyoyatenda"

Qur'an 7:180

So allah anasifika kwa majina na sifa nzuri tu tena za ukamilifu na ametakasika utakasifu wa juu kabisa kutokana na sifa za upungufu au kufanana na viumbe vyake, na vyovyote vile utakavyomtafakari basi yuko tofauti na fikra zako kwani yeye hafikiwi na fikra wala mawazo سبحانه وتعالى.
 
Na je kila kilichopo duniani mungu aliumba yeye au matokeo ya fikra za watu
Sio kilichopo duniani bali yeye ameumba kila kitu ambacho sio yeye, kila kisichokuwa allah basi ni kilimwengu au kwa lugha nyingine kila kisichokuwa yeye basi kimeumbwa na yeye.

"Allah ndiye muumba wa kila kitu, na yeye ndiye mlinzi juu ya kila kitu.."

Qur'an 39:62

Fikra haziwezi kuumba ilihali na zenyewe zimeumbwa.
 
Ibliys hakuonewa bali alifanya kiburi cha hali ya juu mbele ya mola wake, malaika wabora na watukufu walikubali kumsujudia aadam yeye ni nani akatae wakati ni jini tu miongoni mwa majini? ukiwa na kiburi na husda umechukua sehemu katika tabia za ibliys na ukiwa mwepesi wa kuomba msamaha na maghfirah umechukua sehemu katika tabia za baba yako aadam alayhi ssalaam.

"Na kumbuka tulipowaambia malaika msujudieni aadam! wakasujudu isipokuwa ibliys yeye alikuwa miongoni mwa majini basi akaifanyia uovu amri ya mola wake, basi je! hivi mnamfanya yeye na kizazi chake kuwa ni vipenzi kinyume na mimi na hali ya kuwa wao kwenu ni maadui? si ubaya ulioje mbadala huu kwa wenye kudhulumu!!!!.."

Qur'an 18:50


Maneno mazito mno haya yenye kutetemesha nyoyo za wale wenye chembe ya iymaan katika vifua vyao.

Mkuu kwa kumalizia sisi waanadamu ni watukufu mno na wenye daraja ya juu miongoni mwa viumbe wa allah, na katika uislamu kukidogesha na kukidharau kile ambacho allah amekitukuza ni ukafiri.

"Kwa hakika tumewatukuza wana wa aadam, na tumewabeba wao nchi kavu na baharini {kwa kuwapa vipando vya nchi kavu na baharini}, na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri, na tumewafadhilisha kwa fadhila kubwa juu ya wengi miongoni mwa tuliowaumba.."

Qur'an 17:70

Allahul mustaan.
 
Mkuu kama ulivyosema na kutoa mfano hapo huyu shwaini hajaonewa wewe mwenyewe umetoa mfano katika Biblia jinsi alivyo haribu

Anastahili kupita huku huyo.
Mkuu kuna faida kutoka katika hadithi ya abuu hurayrah kwamba mtume swala na salaam ziwe juu yake amesema:

".لا تسبوا الشيطان وتعوذوا بالله من شره"
"msimtukane shetani, na muombeni hifadhi allah kutokana na shari yake"


ameipokea imaam daaraqutni na wametofautiana wanachuoni kunako usahihi wake, naona vyema mkuu tukamuita pasi na kumtukana na allah ameweka uadilifu katika kila kitu.

Na allah ndiye mjuzi zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…