Kwa vichwa vilivyopo Wizara ya Fedha sasa, Tanzania itakuwa mbali sana kiuchumi kufikia 2030

Ungekuwa na akili kama ungekuja na facts kuthibitisha sio vichwa
Umeshawahi kusikiliza interview za Mafuru akiongelea uchumi, salaleeh; ata simple economic concepts kuzidadavua vizuri hawezi.

Nehemia ata investment hawezi ameenda kuitengenezea serikali madeni balaa na uwekezaji wake wa ovyo NHC their financial statements says it all. Magufuli akaona upuuzi alipotaka kuwekewa government guarantee aendelee kukopa.

Huyo Bade ndio fisadi la kutupa alipokuwa TRA.

Mwigulu ndio salaleh anajua tozo tu, kukopa na uelewa wake wa taxation close to zero.

Ni team ya mapoyoyo mno, vichwa kwa viwango vya JK tu but for the rest of us uwezo wao ni mdogo mno hao watu.
 
Kwa maneno yako umejawa na chuki tu

Kama ni mfuatiliaji wa sekta ya fedha Tanzania huwezi acha kuwakubali Mchechu na Rished Bade walioongoza foreign banks zilizopo Tanzania kwa mafanikio.

Ukiona Taasis ya nje ya Tanzania inamchagua Mtanzania kuiongoza basi muheshimu sana huyo Mtanzania. Taasis nyingi za nje ya Tanzania zinazofanya kazi Tz zinaongozwa na wa SA, Kenya, Zimbabweans na Nigerians.


Punguza chuki
 
Kuna orodha iliwekwa humu leo na chanzo ni jariba moja la masuala ya uchumi la hukohuko duniani.

Tanzania haipo kwenye top 10 ya nchi za kiafrika zisizopika data.
 
Uwezo wa kuelewa maswala ya biashara na uchumi ni mdogo ndio maana unaweza kuwaona hao watu vipanga.

Ebu tupe mfano wa successful ‘financial product’ iliyobuniwa na hao watu walipokuwa bankers, thamani yake as an intangible asset kwa wengine leo au hata imetengeneza kiasi gani ndani ya hizo bank.

Kufanya kazi bank, hakukufanyi kuwa successful banker; Mafuru nimemsikiliza anapwaya sana ata kwenye simple economic concepts.

Wana uwezo kwa vigezo vya Tanzania tu, na nafasi wanazopewa Tanzania wakienda Kenya ata sidhani kama tawi la high street bank wanaweza pewa.

Banker unamjua au unaropoka tu.
 
Kweli ni makini maana ndoo wamebadilisha perdiem kutoka 150000 hadi 250000 .250000 ni kama mshahara wa mtu kima cha chini
 
Huyo huyo anafanya vyema sana
Ulitegemea nini wakati waliongeza tozo kila kona ya uchumi, number looks good lakini shilingi nayo imeporomoka vibaya sana kutokana na inflation iliyochangiwa kwa kiasi kikubwa na sera mbovu , kilichofanyika ni double maumivu kwa mwananchi wa kawaida, inflation na tozo vimekula pesa yake yote na kuifanya haina thamani, shilingi 1000 ya mwaka jana ni kama 300 ya leo halafu mnasifia uchumi mzuri, mmesoma wapi nyie au ni uchawa tuu
 
Walikuwepo watu kama Kighoma Malima je nchi ilifika wapi kiuchumi
 
Dah TZ kuna Maajabu na hili ni moja wapo. Kweli kabisa unasema hivo??! Dah haya ngoja tuone
 
Kweli tukianza kutumia watu makini tulio nao na tukaacha kugawa vyeo kama zawadi tutapiga hatua kubwa kimaendeleo.
 
Shilingi imeporomokaje ?
 
Maguru ktk Uchumi wa kukopa na kununua V8?????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…