Kwahili la Mabasi kusafiri Usiku, nampongeza Mbunge Tulia Ackson

Kwahili la Mabasi kusafiri Usiku, nampongeza Mbunge Tulia Ackson

Kama tuna wasiwasi na vyombo vya ulinzi haviwezi kumlinda msafiri na mali yake na akafika salama safari yake basi hawafai kuwepo, tunaposafiri masaa 24 wajipange highway patrol, na vituo vya ukaguzi viwepo muda wote ili kudhibiti pia magendo na biashara haramu kufanyika kwa mwanza wa kusafiri usiku,
 
Kama tuna wasiwasi na vyombo vya ulinzi haviwezi kumlinda msafiri na mali yake na akafika salama safari yake basi hawafai kuwepo, tunaposafiri masaa 24 wajipange highway patrol, na vituo vya ukaguzi viwepo muda wote ili kudhibiti pia magendo na biashara haramu kufanyika kwa mwanza wa kusafiri usiku,
Hakika kabisa ndugu yangu
 
Kuna changamoto ya uendeshaji wa hovyo usiku hasa kwa malori.

Usiku malori yanatimua mbio kiasi kwamba wenye magari madogo wanaweza kusukumizwa mtaroni, imenikuta hii alafu jamaa hakusimama wala nini nashukuru Mungu nilinusurika ila gari iliharibika so nilikesha pale kuhangaikia matengenezo
 
Zambia, Botswana, zimbabwe, Swaziland, Namibia, Msumbiji, DRC , Angola, na Baba lao SA. Wewe bahati ushafika kote huko umevuruga hivi ukiona vyuma wanavyokokota barabarani unaweza kudhani sisi ndio hatuna bandari
Nawaona ndugu zangu kama tumerogwa hapo Botswana ukiliona Ford Ranger au Toyota GD harafu lipo kituo cha polisi dogo kalipaki akitoka anatambaa nalo home wewe hata upite na gari gani hashangai wala hata kukagua chochote ulichobeba ndani zaidi onyesha document utembee Tz sasa unalipia gari kodi kubwa harafu wanakuja kukuuliza hii Tv vip au rice cooker mpaka unawaambia Wazee tumerogwa nini mbona tuna Roho za kupenda vitu visiingie Tanzania?
 
Halafu hua kodi za Tanzania maajabu matupu Haiwezekani Rwanda simu iwe bei rahisi kuliko Tanzania yaani watu wanatoka Tanzania kwenda Rwanda kununua simu bei rahisi tena hawana habari ya fake hadi tunatia huruma
Simu Watanzania wanafata SA kwa sababu hawa jamaa kodi kwenye simu sio kubwa Bongo sasa kitu cha kawaida kodi kubwa kinapelekea watu wake kutumia vitu vya hovyo hovyo wakiamini ni bora kumbe hata hizo simu bora hazina bei hiyo ni vile Serikali haijali watu wake tupo busy tunahangaika na used ya Dubai,China na SA kumbe kukiwa na kodi rafiki maduka ya simu bora yataanzishwa nyumbani...
 
Kuna changamoto ya uendeshaji wa hovyo usiku hasa kwa malori.

Usiku malori yanatimua mbio kiasi kwamba wenye magari madogo wanaweza kusukumizwa mtaroni, imenikuta hii alafu jamaa hakusimama wala nini nashukuru Mungu nilinusurika ila gari iliharibika so nilikesha pale kuhangaikia matengenezo
Unapopishana na lori usiku mwenye gari ndogo punguza sana mwendo na unatakiwa utanue bara bara hasa kwa wale wanaojihami kwa kuwasha hadi zile taa za juu...madereva wa malori hata mchana wanalala nimeona ajali ya Arusha exp hapo Dodoma bus lilifatwa upande wake..
 
watu watabinuka hapa waje walaumiwe ofisi ya majanaga ya waziri mkuu kwa kutotoa msaada haraka.

wenzenu wanaangalia biashara zao wanatoa mawazi haya.

wengine wanaangalia takwimu,kitaalamu wanaona ni heri usiku zisiwepo.
 
Halafu hua kodi za Tanzania maajabu matupu Haiwezekani Rwanda simu iwe bei rahisi kuliko Tanzania yaani watu wanatoka Tanzania kwenda Rwanda kununua simu bei rahisi tena hawana habari ya fake hadi tunatia huruma

Nishaenda Kigali mara 3 eeh banae hawana vitu copy hata mtumba wa kuvaa tu ni kuwango sema bei uki-convert faranga yao ni kubwa kuliko Tsh. Ila wapo smart mno cha ajabu ni gari aina ya noah ndo sijawahi iona huko!
 
Enzi zile Sirari Nairobi bus za Otange Nyamira na Akamba kutekwa ilikuwa kawaida sana tuliwahi tekwa tukaambiwa shuka uchi kila ulichonacho weka kwa mfuko kumbe bana watekaji wanagawana majukum wawili ndani na mitutu 1 nje mlangoni na mfuko mkubwa ukishuka tu unaweka kwenye mfuko kila ulicho nacho wengine wapo wawili ni maelekezo lala chini kichwa iangalie chini Eeh sitosahau hiyo siku jamaa ye hadi nguo kaweka kwa mfuko tumerudi ndani mwenzetu yupo uchi mama kampatia kanga mwingine kampa kitenge basi bana tumetoka pale kufika Bomet tunaenda kureport polisi polisi anasema geuza gari twende penye hiyo place wakora wamechukua hizo vitu nilishangaa sana turudi kufanya nn? [emoji16] Mwanangu acha tu kutwekwa kusikie na walet ndo ukawa mwisho wangu kuitumia hadi leo hii [emoji112]
 
Kwa muda mrefu nilitaka kuandika hili la Sababu za "kitoto" za kuzuia magari yasisafiri usiku, hatimae Mbunge Tulia ameliona Hilo, tusubiri mamlaka zitekeleze. Mimi ni mdau wa safari za usiku sana, kwahio Wacha niwape experience....
1. Zile Coaster za Arusha zinazuiliwa pale Mkata wa saa Tano, matokeo yake, mkifika pale mnachangishana gari inaongeza wese mnazungukia Handeni, hii ni hatari.
2. Pale pale Mkata Kuna uchochoro, kwahio Dereva anazima Taa mnapita kwenye huo uchochoro kwenye makazi ya Watu, risk inazidi kuongezeka. Unajiuliza, hivi barabara ya Dar to Arusha Ina hatari Gani Hadi hizi gari zizuiliwe kama sio kutengeneza mazingira ya Rushwa tu?
3. Coaster za Dar to Mbeyaz wakifika Moro waliweka Picha ya Marehemu kuwa wanasafirisha msiba...tunajua kilichotokea, laiti ingekua ni route Hali.
4. Hivi kuna umuhimu Gani wa mabasi yote kuanza kufukuzana Pale stand kuu saa 12 asubuhi? Mfano, basi linalokwenda Kigoma, Kasulu, Musoma, n.k kwanini wasiondoke saa tatu asubuhi? Au saa Nne? Ili wasilale? Maana madereva ni wawili wawili, sasa watakimbizana kutwa nzima then watalala Kaliua saa nne usiku Hadi saa 12 asubuhi
5. Hivi kwanini Mabasi ya Bukoba, Ngara, Burundi, nk walazimishwe kulala Kahama na sio Nyakanazi? Siku hizi eneo lote liko salama.
6. Kwanini Mamlaka husika wasiruhu mabasi ambayo madereva wake na mabasi Yao yanatambulika kuliko hii ya kukata Kibali Cha Coaster Kila baada ya muda? Hatuna uhakika wa zile Coaster Wala madereva wake....

Inaendelea..

Inaendelea....

Muda huu ninapoandika hili ni 21:45 ukienda pale Mbezi Kituo Cha Daladala au pale Ubungo Kimara Kuna abiria wengi sana, hawa wanakwenda Mbeya, Dodoma, Mwanza na kwingine, huu ni mfano tu lakini situation kama hio utaikuta Dodoma CBE, Singida pale Nje, Makambako, Mbeya, Moro, Mombo-Tanga, na kwingine.....

Hawa wote wana-risk maisha Yao, kwanini tusiukubali ukweli kuwa route za usiku haziepukiki? Tuhalalishe hizi safari tupunguze ajali za magari ya IT na zile za magazeti, mfano, ndani ya miezi 36 MAGARI ya magazeti yameondoka na maisha ya watu wasiopungua Kumi, coaster za Usiku zimeondoka na maisha mengi the same to IT na Malori. Tukihalalisha tutapunguza tatizo

=====

“SERIKALI IRUHUSU MAGARI YA ABIRIA KUSAFIRI WAKATI WOTE HADI USIKU”- DKT. TULIA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ameitaka Serikali kuangalia upya utaratibu uliowekwa katika baadhi ya maeneo nchini wa kuyazuia magari ya abiria kufanya shughuli za usafirishaji nyakati za usiku kitu ambacho kinarudisha nyuma maendeleo ya kiuchumi.

Dkt. Tulia ameyasema hayo leo Novemba 10, 2022 wakati aliposhiriki Semina kwa Wabunge kuhusu usalama Barabarani iliyoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliyofanyika katika ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.

Amesema kuwa ni lazima ifike wakati sasa Wananchi waweze kufanya shughuli zao muda wote na kuondoa dhana iliyozoeleka ya magari ya abiria kuwekewa vikwazo vya kufanya kazi kwa sababu zizisokuwa rasmi wakati magari mengine yakiwemo ya mizigo yanaruhusiwa.

“Kunashida gani ya kuzuia gari ya abiria kusafiri usiku? Tunatamani nchi yetu kuchangamka Zaidi kiuchumi sasa kwanini magari haya yawe na zuio wakati magari mengine yanaruhusiwa kusafiri hadi usiku. Kama ni changamoto ya miundombinu basi ishughulikiwe na shughuli zifanyike” amesisitiza Dkt. Tulia
View attachment 2416034
Hongera Betina.
 
Kabla yayote, Magari yoteya Abiria na Malori yawekew speed lemit, kama wanavo fanya South Africa. Hapo sasa safari zausiku zinaweza ruhsiwa!
 
Ni wachawi tu ndio mambo yao ni usiku, nguvu zao ni za giza.

Safari za usiku ni safari za kutoana kafara kwa nchi yetu, bado tupo nyuma sana kwa safari za usiku.
Mawazo ya kijima kabisa haya, imagine sasa hivi unatoka Mpanda mpaka Dar barabara ni lami, unataka watu wasisafiri usiku? Halafu unataka uwe uchumi wa kati au uchumi wa juu?? Thubutuuu!!!
 
Tujiandae na kulia sana
Ajali nyingi mchana Usiku itakuwaje
Wakati wa kuwekewa mawe barabarani/Kitonga ni nyakati za Usiku
Watakaoteseka ni wamama wazee na watoto
Hii nchi inazidi kurudi nyuma…
Mawazo ya kimasikini sana haya, narudia miaka ya 80 kuja 90 ma Bus yalikuwa yanasafiri usiku, alfajiri unaingia Dar unafanya mishe zako weee ikifika saa 10 jioni uko Kisutu au pale Mnazi mmoja unachukua bus unarudi zako mkoani. Hii pia ilisaidia anayerudi mkoani akifika asubuhi kama anaenda wilayani anakuta usafiri anaunganisha. Huwezi kuwa na jamii iliyoendelea inayofanya kazi asubuhi mpaka saa 9 au saa 10 tuu, no way.
 
Wakati serikali ya Mwinyi inapiga marufuku mabasi ya abiria kutembea usiku nilikuwa Bado mdogo ila naikumba ile ajali ilikuwa mbaya sana kama sijakosea lile Bus lilichanika ubavuni abiria wakawa wanamwagika kama Michele

Changamoto za safari za usiku
1) Barabara zetu hazina taa hivyo dereva anategemea ta za Gali tu

2) Barabara zetu ni nyembamba sana

3) Maloli yanayo haribika barabarani huwa hayatolewi na kuwekwa katika road reserve kama nchi nyingine hapa kwetu Loli linakaa hata siku 3 barabarani

4) Kuna ukungu pia ni chanzo kikubwa sana Cha ajali kwa Magali yanayosafiri usiku

5) Mabusi ya siku hizi Yana speed sana madereva lazima watashawishika kutembea kwa speed kubwa

6) kwa Sasa barabara ya Dar to Dom ipo bize sana na ajali nyingi zitatokea hapo
Watu wenye mawazo kama haya mimi huwaita vikwazo vya maendeleo. Badala ya kuruhusu bus zisafiri usiku ili kuona changamoto na kuzitatua, bado mna mawazo ya mzee Mwinyi ya miaka hiyoo wakati network ya barabara nchini yenye lami was maybe 30%... 60 yrs unawaza kusafiri usiku siyo salama?? Really??
 
Back
Top Bottom