Kwanini Balozi Mulamula alikuwa anaonekana smart sana na kuheshimika huko Ugenini?

Kwanini Balozi Mulamula alikuwa anaonekana smart sana na kuheshimika huko Ugenini?

Hebu futa takataka yako, unaelewa hata unachoandika? Hebu acheni mafumbo ya kipumbavu, Rais ni Taasisi kubwa, tuipe heshima.
Kwahiyo unataka kuniambia mama Samia japo kaenda marekani zaidi ya mara 2, lakin Biden amempuuza tu..
 
Kama wazungu walikuwa hawamuelewi Samia kwasababu ya kuwa makamu wa Rais wa Magufuli aliyeharibu uhusiano wetu wa kimataifa, huyu mama alikuwa kiungo mzuri sana.

Kwenye mazingira kama haya kuleta habari za "collective responsibility" ni ujinga mtupu, hiyo "collective responsibility" ndio iliharibu mwanzo ikashindwa kumshauri vizuri yule aliyeharibu, then unamteua anayeaminika huko nje ili akatengeneze, ajabu baadae nae unamuondoa kwasababu ya kukumbatia mawazo ya wale waliofeli!.

Huyu mama alikuwa anatengeneza connection nzuri ya kurudisha imani ya wazungu kwa Samia na serikali yake, lakini kwa kuondolewa kwake, naona Samia ataendelea kupokewa na kina Mange kila akienda US.
Wachaaaa
 
Hapa kwa huyu mama ndiyo 'end of the road'.. Mara unapokuwa nje ya 'system' huwezi kufurukuta tena na hata ukipata dili la Mashirika ya Kimataifa nje ya nchi lazima waombe ruhusa kwa Serikali yako kukutumia..
Kwa sasa atabaki na cheo chake cha Ubalozi tu..
 
Nafasi ya waziri wa mambo ya nje tangu mwanzo ilikuwa ikmnyemelea Tax Stergoma baada ya kutoka SADC ila sijui ilitokeaje akapewa Mulamula?
 
Ni raia wa Marekani huyu. Si ajabu anaweza kuwa ni agent wao pia....

Marekani sasa inatishwa sana na uwepo wa China barani Afrika na inahaha mno kupata mahali pa kujishikiza ili kupindua meza japo kwa kuchelewa. Kutokana na mabadiliko ya kasi ya tabia nchi, kuna uwezekano mkubwa kwamba nafasi ya Afrika kama mzalishaji mkuu wa raslimali ghafi na hasa zinazohusu nishati safi na salama itazidi kuongezeka. Tanzania tuna Helium, gesi asili na Uraniamu ya kutosha. Kwa hivyo huyu mama ni mtu wa muhimu sana kwa Wamarekani si kwa Tanzania tu bali hata nchi jirani.

Nimemuona Kigogo anashangaa eti katoa wapi dola milioni 1.7 za kununua mjengo Maryland na kupeleka familia nzima visiwa vya Caribbean kutumbua kwa siku 10+. Dola milioni 2 kwa mtu kama huyu si vijisenti tu kama vya Chenge?

Hana shida huyu. Atarudi kukaa zake Maryland na kazi yake aliyokuwa amepewa si ajabu atakuwa keshaimaliza. Kama unabisha kamuulize hata Magufuli atakwambia....
View attachment 2376533
Well, huyo mama simjui na kama ana sifa nzuri tu za kiutendaji na bado akatumbuliwa na mteuzi wake basi naichukulia kwamba huyo mteuzi wake hakuridhika naye aidha kikazi au kibinafsi.

Ila miongoni mwa sifa zake za kuimba hapa haiwezi kuwa eti kwa vile anajulikana na marais wa Marekani. Moja, kuwa na ukaribu sana na Marekani haimaanishi kwamba huko ndio kutetea maslahi ya nchi. Watu wengi walio close na Marekani wengi ni maagents tu wa ubeberu. Pili, picha na viongozi wa marekani inadhihirisha jambo moja tu, opportunism ya kujifanya connected. Ni ujanja ujanja tu wa mjini wa kutafuta fursa za kuonekana upo connected. Connection zinaweza kuwa zimemsaidia huyo mama Mulamula kwenye mambo yake binafsi lakini sisi kama nchi ya Tanzania we dont care anymore about personal glories.


Huyo hajatafuta connection yoyote kwa umri wake atafute connection zinasaidia nini , connection zinamfata mwenyewe

amepelekwa Kua balozi na serikali ya Tanzania , Leo hii anekua Agent wa Marekani baada ya kuanza ku outshine mamlaka ya Tanzania ( hili ndio Kosa lake na amekosea kibongo bongo )
 
Imani ya wazungu kwa Samia?

Aisee mtu mweusi sijui anakwama wapi. Kwa akili hizi wallahi waafrika hatutoboi. We ndugu yangu wazungu ni watu wa kawaida kama mimi na wewe, Samia haitaji kufanya chochote kurudisha imani au kupoteza imani ya wazungu. Samia anawajibika tu kwa familia yake na kwa watanzania pekee.
Wazungu sio watu wa kawaida wale hata kidogo. Tusijipe moyo kwa mambo ya uongo. Those guys have nukes but we Africans have polygamy.
 
Nimeshangaa sana yeye ni kwanini alikuwa anapafa fursa hizi? Jamaa yangu mmoja yupo USA.

Anasema huyu dada alikuwa anaheshimika sana na walikuwa wanamwona very smart hata katika maongezi. Anasema ni nadra sana kwa mtu ambaye haheshimiki kuonana na akina Obama na Biden namna hii.

Kuna watu tena Marais huenda kule na kukaa hadi mwezi hawajapata nafasi hata ya kukutana na Biden kwenye korido katika meetings zake.

May be CIA walimu-recruit, ndio maana SSH alikuwa anaongelea Siri, may be aliunnguza picha, wajanja wakamnasa anauza classified info
 
Nimeshangaa sana yeye ni kwanini alikuwa anapafa fursa hizi? Jamaa yangu mmoja yupo USA.

Anasema huyu dada alikuwa anaheshimika sana na walikuwa wanamwona very smart hata katika maongezi. Anasema ni nadra sana kwa mtu ambaye haheshimiki kuonana na akina Obama na Biden namna hii.

Kuna watu tena Marais huenda kule na kukaa hadi mwezi hawajapata nafasi hata ya kukutana na Biden kwenye korido katika meetings zake.

Smart kwa hilo komwe kama boga?
 
Huyo alikua balozi wa marekani nchini tanzania.
Viongozi waliopo hawaijui Katiba, hawajawahi isoma yote, huishika na KUAPA bila kujua kilichoandikwa ndani.

Mtu mwenye URAIA pacha aliwezaje kuteuliwa waziri mambo ya nje???

What if ni Agent??🙃🙃🙃. Muda wa matazamio umekwisha, maamuzi magumu yanahitajika.
 
Huyo hajatafuta connection yoyote kwa umri wake atafute connection zinasaidia nini , connection zinamfata mwenyewe

amepelekwa Kua balozi na serikali ya Tanzania , Leo hii anekua Agent wa Marekani baada ya kuanza ku outshine mamlaka ya Tanzania ( hili ndio Kosa lake na amekosea kibongo bongo )
Mnavipa vitu thamani ambavyo havipaswi kupewa thamani. Kupiga picha na Biden hakuna thamani yoyote kwa maslahi ya Tanzania. Mbona hamjielewi nyie watu. Hata huyo Samia angeenda akapiga picha na Biden still kwetu sisi wapiga kura wa Tanzania tuna vipaumbele vyetu tofauti na wanavyofikiria wao au unavyofikiria wewe.
 
Pamoja na madhaifu yote ya viongozi wetu ila hata wao kuna point wakifika wanaweka maslahi ya nchi mbele ndo maana hadi leo TZ ni salama kwenye mipaka yake na hakuna shinikizo kubwa toka kwa wageni. Huyu mama inavyoonekana aliegemea kwa mabeberu zaidi. Wazungu ukiwa na maslahi nao hawana noma hata chai utaitwa kunywa nao... hiyo ndo style ya bepari.
MamaSamia2025
 
Mkuu, hata hao Pyongyang ni level za mbali sana kutuzidi sisi. Africans wengi tunaendekeza masuala ya hovyo ndio maana hatuendelei sana.
Unatamani Afrika ipige hatua za maendeleo lakini hatuwezi kufika huko kwa fikra na approach mlizo nazo nyie. Afrika ikitaka kuendelea lazima ijikate kwenye mnyororo wa kuwa vibaraka. Kwani Pyongyang walifikaje hapo? Kwa kujigonga kwa mmarekani? Iran leo hii ni moto wa kuotea mbali. Wamefika hapo kwa kujigonga gonga kwa mmarekani?

Ni kweli Afrika inaendekeza mambo ya ovyo sana tu miongoni mwa mambo hayo ya ovyo ni haya ya kushangilia akina Mulamula kupiga picha na Biden.
 
Unatamani Afrika ipige hatua za maendeleo lakini hatuwezi kufika huko kwa fikra na approach mlizo nazo nyie. Afrika ikitaka kuendelea lazima ijikate kwenye mnyororo wa kuwa vibaraka. Kwani Pyongyang walifikaje hapo? Kwa kujigonga kwa mmarekani? Iran leo hii ni moto wa kuotea mbali. Wamefika hapo kwa kujigonga gonga kwa mmarekani?

Ni kweli Afrika inaendekeza mambo ya ovyo sana tu miongoni mwa mambo hayo ya ovyo ni haya ya kushangilia akina Mulamula kupiga picha na Biden.
Mkuu, hivi unafahamu kwamba wakati tunapata uhuru miaka ya 1960s, uchumi katika nchi nyingi za Afrika zililingana na nchi za Asia kama Korea Kusini na Singapore? Leo tupo wapi? Nini kilitokea? Mpaka sasa kipi kimefanywa kurekebisha makosa yale? Mkuu kuwa mzalendo haina maana ya sasa mtu afumbie macho ukweli kama askari wa Ukraine.
 
Back
Top Bottom