Kwanini Dar es Salaam magari binafsi aina ya Landcruiser V8 yako mengi sana?


Hao sio wa mishahara,
 
Utajiri upo kila mahali
Watz hatuna tu macho. Niliwaambia classmates zangu tukiwa shuleni ambao wengi sasa wapo USA, UK, Nk wakiwa wamechukua uraia wa huko kabisa kwamba Mimi siwezi nikaondoka tza nikaacha utajiri wote huu. Usipotajirika Tza huwezi tajirika popote

Na rafiki zangu wa Thailand na Srilanka wao ni ndege ni kama uber wanakaa tza wanakusanya madini vijijini wanajaza hao kwao wiki wanarudi wanakaa mwezi tza mzigo ukijaa hao kwao.

Tza ni shambani wanayapeleka madini kwao kuyaongeza thamani kisha wanauza ulaya kwa pesa ndefu.
Usipotajirika TANZANIA utakuwa masikini milele
 
Magar ya serikal meng baada ya 5yrs huwa wanajiuzia wenyew kwa bei za kutupa ndomana wakurugenz huhakikisha wanachkua kitu 0 km ili badae afta5 yrs liwe na hal nzur wauE au wajigawie
Hakika hili linafanyika.
- V8 inanunuliwa kwa bei ya PASSO
 
1. Congo
2.South Africa
3. Tanzania
Shida kubwa ya afrika imekosa mifumo bora ya uongozi.
Ni afrika pekee ndipo viongozi wake Wana Kinga ya kutokushtakiwa ikiwa na maana ya ruhusa ya kufanya chochote kwa raia wao ikiwemo ufisadi. Afrika mtawala ni Mungu, kwa wenzetu kiongozi,raisi ni mtumishi wa watu ukifanya ufisadi, wizi, nk unaondolewa hadhi yako ya uraisi au uongozi unashughulikiwa bila huruma ikibidi kupotea kabisa.
Thus wao Wana maendeleo.
 
Tunawezaje kupata fursa huko kwenye madini?

Sent from my SAMSUNG-SM-N920A using JamiiForums mobile app
Mengi tu ya KILA aina karibu KILA sehemu nchi nzima yamejaa, siku hizi wachina wameleta technology nyingi rahisi za uchimbaji vikiwemo vifaa vya kujua wapi na umbali gani ardhini madini yaliyo.
Sio kama zamani unajichimbia local au kudanganywa na waganga.
 
Good Spirit mkuu.
 
Sehemu rahisi kupiga pesa ya halali na ukawa tajiri ni kwenye
1.Madini
2.Recycling, kusaga taka za plastic na kuuza nje ya nchi.
3.Export, yaani kucheza na soko la India, China na Kenya kujua wanataka nini. India na China population zao ni kubwa sana na wanahitaji Sana vitu vingi toka TANZANIA uwe mtundu tu wa kusaka taarifa kwenye mitandao.

Wakenya wanaitumia Sana fursa hio kupitia TANZANIA Shamba la bibi wanakuja wananunua Tza wanaexport, mfano maparachichi, matunda,madini nk.

4.Ukiagiza nje mashine za kuzalisha vifaa vya ujenzi mbadala wa cement, nondo na bati utapata pesa nyingi Sana nchini kwa kutumia raw materials zinazopatikana nchini bure utauza bei mudu kwa wengi maana vifaa vya ujenzi bei hazishikiki kwa sasa, mtajenga kwa pension na sio kwa mishahara tena. Zipo technology nyingi na rahisi sana za ujenzi wa nyumba bora za kisasa pasipotumia cement, nondo wala bati na nyumba ikadumu zaidi ya miaka 200 kwa ubora ulele kwa gharama nusu ya ujenzi wa kutumia cement, nondo na bati.
 
Jumla ya v8 zote za serikali sio chini ya 600 kwa thamani ya zaidi ya milioni 250 KILA moja linapokuja suala la jambo lihusulo wananchi serikali huwa haina pesa jambo la kwao au la wanasiasa pesa zipo tele ikibidi hata kukopa.

Serikali ikiamua kugawa mashine za kutengeneza matofali na vigae KILA kijiji wapewe kumi kumi Ili watanzania wajenge nyumba bora za kisasa wasikae nyumba za nyasi kama panya inawezekana.Kama tunaweza nunua ndege cash na zikapark au kutumia zaidi ya mabilioni siku moja tu Ili kusherekea birthday ya UHURU tu ambao sio lazima, haishindwi interlocking brick mashine si zaidi ya laki 5 na mashine moja ya kutengeneza viezekeo haifiki hata laki 2 hela za Kitza.
 
Yangoso muachie Ngoso
 
Hahahahah mzungu alicheleweshwa sana huyo😅!

Huku watu wanajenga majengo mpaka ya billion 3 kwa pesa zao binafsi hawaombi hata sh.100 kwa mtu! Kuna watu ni mafogo yani sema wako Low Key kichizi hutakaa ujue yani.

Ambao ni maskini ni kundi kubwa ila liko maeneo ya vijijini sio rahisi kwa wao kusikika maana wanakuwa covered na wenye kipato cha kati na cha juu. Mijini humu asilimia kubwa watu wana Mawe😅
 
Ngoja nikudokeze kitu.
Hizo V8 zinanunuliwa serikalini baada ya kutimiza kilometa za matumizi ya kiserikali na zingine baada ya kupata changamoto za kiufundi
Ukipeleka garage nzuri inabondwa body inakuwa mpya kabisa.
Ukienda tra wanaipa namba D.
Ukiihitaji gari aina ya V8 na zingine zinazoshahabiana nione.
Serikalini zinauzwa mpaka million 9, 10, n.k.
Jambo jingine ni hivi ukiingia Be forward Japan hiyo V8 unaweza kuipata mpaka kwa ml.50-100 pesa ambayo watu wengi tu haiwapigi chenga.
Kanuni za kiuchumi ziko wazi ukiona mafukara wanaongezeka ujue matajiri wananeemeka.
 
Mkuu, baada ya miaka 5 na mimi ntavuta huyu mnyama ndio roho yangu itulie, View attachment 2051678
Hahahahah unataka kumvuta “KAKADU” mjini 😅 wakati huo kutakuwa kuna kitu kinaitwa Toyota Bz4 hio itakuwa ni ndoto ya watu wengi maana ni kama Tesla kutoka Toyota.

Watakwenda Fully electric na wamejipanga mpaka kufikia 2030 waache production ya ICE cars! Zitakuwepo zile hydrogen cars ila kwa sie wa soko la mtumba tutaendelea kumenya tu gari zilizope scrape yard za Japan.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…