Kwanini huwa tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati ardhi tumeikuta ipo bure? Why?

Kwanini huwa tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati ardhi tumeikuta ipo bure? Why?

Wazo zuri ila wapangaji ndio walipaji wakuu kweny kununua LUKU.
Yaani mwenye nyumba anachukua. Chake na mweny nchi anachukua humo humo
 
Hiyo miundombinu mbona tunailipia? Ingekuwa mtu akijenga anasogezewa Huduma zote BURE sawa lakini huduma zote tunauziwa ni BIASHARA!
Ndo maana nikasema kimsingi hatuipati.

Barabara
Madaraja
Taa za barabarani
Mifereji
Je tunavipata hivyo?
 
In short

Nothing is for free,hizo Kodi Kwa kifupi tunajikata sisi wenyewe na kuzichanga kwenye mfuko unaoitwa Serikali Ili zitufae wote(theoretically)

Nasema wote Kwa kuwa hii ardhi wanaimiliki walio Serikalini na wasio Serikalini Kwa kumiliki viwanja
Ndio hivyo ukisoma universal law na ukaielewa hupati tabu,
 
Hii ni moja ya makosa yaliyofanywa na watangulizi wetu baada ya kupata uhuru. Nadhani wakati huo walioelimika aidha kwa kutokujua au kwa kufuata mkumbo tu waliamua kuweka mipaka ya nchi na kumilikisha kipande cha ardhi iliyopimwa yaani Tanganyika kwa kikundi kidogo cha wajanja wajanja kinachoitwa "Serikali".

Uporaji huu kwa jina la kupata uhuru na kujitawala ndio ulioleta haya mambo ya kodi kwa lengo la dude Serikali kupata pesa za kujiendesha kwa kukiuka misingi ya haki asilia ya mwananchi kumilika ardhi. Kimsingi Serikali ndio inapaswa kuwalipa wananchi kodi ya pango na kulipa fidia pale inapotaka kutwaa ardhi ya mtu.

Nchi hii inatakiwa kusukwa upya kwa kutengeneza katiba itakayo zingatia suala la ardhi kuwa mali ya mtu mmoja mmoja na sio huu ulaghai wa ardhi kuwa mali ya Serikali chini ya uangalizi wa taasisi ya Rais.
Na hapo ujanja ni wewe kujichomeka Serikalini
 
Kwa mujibu wa Sheria, Hakuna Ardhi iliyokaa bure tu, Ardhi ni mali ya umma na msimamizi mkuu ni Rais, wewe unakuwa umepewa tu hati ya kuimiliki kwa miaka kadhaa lakini lazima uendelee kulipa kodi kwa msimamizi mkuu (Rais)
Halafu hili suala la ardhi yote kumilikiwa na Raisi ni bongo tu.

Hapo Kenya ardhi ni Mali binafsi hivyo kurahisisha maendeleo na muendelezo wake.

Kifupi ukifatilia historia ya Kodi haikuanza miaka mingi na raia walichangia serikari kipindi Cha Vita.

Kodi ilianzishwa ili kutozaa matajiri ila Serikari ilivyoanza kuonja fedha taratibu wakaiweka kwa jamii nzima.

Sasa kutokana na mlundikano wa Kodi tumekuwa State Slaves.

Hii kutozwa Kodi mara mbili kwenye kitu kile kile inakera kwa kweli(Double Taxation)
Fikiria unalipa Kodi ya ardhi na jengo kwenye kiwanja kile kile.
 
Hewa haiuzwi wala kununuliwa , ardhi inauzwa na kununuliwa , lazima itozwe kodi mana ipo ndani ya mipaka ya kimamlaka
 
Ngoja tusubiri ufafanuzi kutoka kwa wasomi
Hili halihitaji usomi, ni kujuwa tu sheria za Ardhi.

Ardhi yote ni Mali ya serikali, tena zamani ilisomeka kama Mali ya Rais wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania.
.unalipa kodi ya Ardhi kwa sababu serikali imekupangisha kwa miaka 33 au 100 na siyo milele.

Serikali ikiwa na Mipango yake inachukuwa Ardhi yake kwa kuthaminisha na kukulipa fidia, hata uwe umejenga nini, sanasana utalipwa pesa na kupewa Ardhi nyingine.
 
Ndo maana nikasema kimsingi hatuipati.

Barabara
Madaraja
Taa za barabarani
Mifereji
Je tunavipata hivyo?
Road licence tunakatwa kwenye mafuta!
Kadri unavyosafili ndivyo unalipia zaidi;
Mwaka Jana nilipiga hesabu mafuta niliyonunua kwa mwaka asilimia niliyokatwa kwenye road license inafikia laki 7!
Hii inachangia ujenzi wa barabaranj, madaraja, taa na mifereji, hapo hujaweka Tarula parking fees!
 
Mambo mengine mtu ukiwaza unaona kabisa maisha ni mepesi kimtindo lakini kuna baadhi ya wanadam wenye dhamana ya uongozi ndiyo waliyoyafanya maisha yawe magumu!

Tumeumbwa ardhi ilikuwapo, tumepata Uhuru, ardhi ilikuwapo milele hadi milele yote!

Sasa kwanini tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati tayali ipo BURE?
Huduma zingine za kijamii tunazolipia naelewa ni sawa zinazalishwa viwandani hivyo ni mhimu kulipia!
Sasa hili la kodi ya pango ya ardhi kwanini tulipie wakati tumekuja duniani ili tuishi kwenye ardhi halisi BURE?
yaani kwa lugha nyepesi Ardhi ipo kundi moja na hewa! Kama tunalipia kodi ya ardhi kwanini tusilipie na kodi ya hewa?

Naomba kueleweshwa! Vinginevyo naomba serikali ifute hii TOZO ya ARDHI ya ardhi mara moja!r
Ardhi Haipaswi kabisa kutozwa kodi TUMEPEWA BURE ! WACHA TUISHI NAYO BURE!

Ni wizi mtupu ,wachumi ndiyo walivyofikiria "kubwinu mbwinu" za kuongezea mapato serikalini yaani haina tofauti na ule wizi wa Service charge TANESCO ambao Late JPM aliuondoa.

Kwa viwanja vilivyopimwa unalipia kila mwaka kodi Ardhi na Pia Kila mwezi unakatwa kodi ya jengo kupitia Tanesco yaani ni WEEZY WEEZY.
 
Ardhi ni mali ya serikali kwa mujibu wa sheria za ardhi. Shangaa hata makaburi uhamishwa wakitaka kupitisha barabara hapo au kujenga majengo hapo. Bora tu serikali imiliki ardhi vinginevyo ingekuwa ni vurugu tupu kwa wababe kunyang'anya wenzao ardhi wanazojenga na kulima. Ardhi ina mali nyingi kama madini mabepari wanaitaka, utageuzwa kabwela pepari likimiliki ardhi
 
Hili halihitaji usomi, ni kujuwa tu sheria za Ardhi.

Ardhi yote ni Mali ya serikali, tena zamani ilisomeka kama Mali ya Rais wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania.
.unalipa kodi ya Ardhi kwa sababu serikali imekupangisha kwa miaka 33 au 100 na siyo milele.

Serikali ikiwa na Mipango yake inachukuwa Ardhi yake kwa kuthaminisha na kukulipa fidia, hata uwe umejenga nini, sanasana utalipwa pesa na kupewa Ardhi nyingine.
Hiyo sheria kwanini isingewekwa na kwenye hewa!?
Yaani walitungia sheria kitu ambacho siyo man made! (Siyo cha kwako unakitungiaje sheria kujimilikisha?)

Yaani unalitungia sheria jua, mwezi, ardhi, hewa hii si sawa hata kidogo! Wakaiboreshe!
 
Kodi ya ardhi sawa kwa sababu tunapata miundombinu ambayo kimsingi ni haki yetu.

Lakini kodi ya jengo ni wizi kwa mujibu wa sheria. Serikali inanidai vibali kabla sijajenga na hainipi unafuu wowote kipindi cha ujenzi. Vifaa vya ujenzi nalipia kodi na bado inanitaka kulipia kodi ya jengo.

Huu ni wizi unaolindwa na sheria.
Yesu alishamaliza huu utata siku nyingi, aliwaambia ya Kaizari mpeni Kaizari.

Wengi hawajui Yesu alikuwa analipa kodi, kwahiyo Hakuna kiumbe yoyote wa kushindana na mfumo huu, huu siyo mfumo kristo, huu ni mfumo Babylon.
 
Yesu alishamaliza huu utata siku nyingi, aliwaambia ya Kaizari mpeni Kaizari.

Wengi hawajui Yesu alikuwa analipa kodi, kwahiyo Hakuna kiumbe yoyote wa kushindana na mfumo huu, huu siyo mfumo kristo, huu ni mfumo Babylon.
Kwanini hewa isitozwe kodi?
 
Serikali angalieni namna kuifuta hii kodi ya ARDHI Vinginevyo wanasheria watanzania mnaoipenda Tanzania naomba mkafungue kesi ya kupinga hili!
Vitu vya asilia tuviache vibakie katika uasili wake!
Kuomba kodi ya ardhi ni kama kutuingilia kinyume na maumbile wananchi!
Tunapolaani ushoga tulaani na hili la kutozwa kodi ya ardhi!
It sucks but taxes are necessary wether we want them or not..You never really own land..You rent it from the Government forever.

Huu ndio mfumo wa Kiutawala Kiongozi Dunia nzima..Point yako imeeleweka but You have to understand where the money is going. Property taxes are the ONLY way that the city/town makes money. So no property taxes=no police, no schools, shitty roads, ect.
 
Ni sawa na Wasaudia walivokuta mafuta ya bure kwny ardhi yao afu useme wayagawe bure,I doesn't make any sense
 
Hiyo sheria kwanini isingewekwa na kwenye hewa!?
Yaani walitungia sheria kitu ambacho siyo man made! (Siyo cha kwako unakitungiaje sheria kujimilikisha?)

Yaani unalitungia sheria jua, mwezi, ardhi, hewa hii si sawa hata kidogo! Wakaiboreshe!
Yesu alishindwa kuwajibu Wayahudi swali hili hili, akawaambia ya Kaizari mpeni Kaizari.

Kumbuka Yesu alikuwa analipa kodi na kuna watu wanaamini Yesu ni Mungu, Imagine.
 
Back
Top Bottom