Kwanini huwa tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati ardhi tumeikuta ipo bure? Why?

Kwanini huwa tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati ardhi tumeikuta ipo bure? Why?

Yesu alishamaliza huu utata siku nyingi, aliwaambia ya Kaizari mpeni Kaizari.

Wengi hawajui Yesu alikuwa analipa kodi, kwahiyo Hakuna kiumbe yoyote wa kushindana na mfumo huu, huu siyo mfumo kristo, huu ni mfumo Babylon.
Sasa nimeweka jengo ambalo serikali hailimiliki wala haina ubia kisha inanidai kodi.

Soon wataleta air regulators watulazimishe tuzivae ili tulipie kodi ya oksijeni
 
Yesu alishindwa kuwajibu Wayahudi swali hili hili, akawaambia ya Kaizari mpeni Kaizari.

Kumbuka Yesu alikuwa analipa kodi na kuna watu wanaamini Yesu ni Mungu, Imagine.
Hilo andiko kalisome vizuri hujalielewa!
Hapa tunaongelea kwanini tunalipia kodi ya ardhi wakati ardhi ni BURE! Bali miundombinu ndiyo inalipiwa na huwa tunailipia? Tunalipia kila kitu tunakatwa kodi kila idara V.A.T
 
Sasa nimeweka jengo ambalo serikali hailimiliki wala haina ubia kisha inanidai kodi.

Soon wataleta air regulators watulazimishe tuzivae ili tulipie kodi ya oksijeni
Unajuwa kimsingi Watanzania wengi sana wana uwezo wa kumiliki magari kwa bei yanaouzwa huko Japan na ulaya, lakini wakishaingia TRA tu hapo ni nuksi tayari hata hamu ya gari inakuisha hapohapo.

Niliwahi kusikia Ghaddafi kwenye utawala wake Libya aliifuta kodi ya VAT.
 
Kumbe ardhi ni bure kisa kaumba Mungu mbona mimi sina Basi ngoja nikajikatie kipande changu pale posta na mimi niwe naye
Hujaelewa mada.
Tofautisha kati ya kodi na mauziano.
Mauziano ya ardhi huwa ni makabidhiano ya ardhi kutoka kwa mmiliki wa mwanzo aliyewahi kwenda kwa mmiliki mpya(aliyechelewa kuipata) na malipo hufanyika mara moja tu.
Lakini kodi ni tozo kwa mmiliki wa ardhi na ambayo hujirudia mara kwa mara na hii ndio hoja ya mtoa mada
 
Mambo mengine mtu ukiwaza unaona kabisa maisha ni mepesi kimtindo lakini kuna baadhi ya wanadam wenye dhamana ya uongozi ndiyo waliyoyafanya maisha yawe magumu!

Tumeumbwa ardhi ilikuwapo, tumepata Uhuru, ardhi ilikuwapo milele hadi milele yote!

Sasa kwanini tunalipia kodi ya pango la ardhi wakati tayali ipo BURE?
Huduma zingine za kijamii tunazolipia naelewa ni sawa zinazalishwa viwandani hivyo ni mhimu kulipia!
Sasa hili la kodi ya pango ya ardhi kwanini tulipie wakati tumekuja duniani ili tuishi kwenye ardhi halisi BURE?
yaani kwa lugha nyepesi Ardhi ipo kundi moja na hewa! Kama tunalipia kodi ya ardhi kwanini tusilipie na kodi ya hewa?

Naomba kueleweshwa! Vinginevyo naomba serikali ifute hii TOZO ya ARDHI ya ardhi mara moja!r
Ardhi Haipaswi kabisa kutozwa kodi TUMEPEWA BURE ! WACHA TUISHI NAYO BURE!
Ili wengine wanunue V8
 
Unajuwa kimsingi Watanzania wengi sana wana uwezo wa kumiliki magari kwa bei yanaouzwa huko Japan na ulaya, lakini wakishaingia TRA tu hapo ni nuksi tayari hata hamu ya gari inakuisha hapohapo.

Niliwahi kusikia Ghaddafi kwenye utawala wake Libya aliifuta kodi ya VAT.
Serikali yetu huwa inafuata masharti ya WB na IMF. Haijawwhi kusikia na kupokea maoni ya raia wake.

Bahati nzuri asilimia kubwa ya watendaji ni wezi wa rasilimali na fedha za umma na wwkistaafu wanajisimika madarakani kupitia CCM.

Mabadiliko ni muhimu
 
Unaweza kunionesha hewa? Mimi naweza kukuonesha oxygen inayotozwa kodi.
Hewa ni pamoja na oksjeni katika mchanganyiko wake halisia!
Ukiichakata kiwandani unakuwa kama unaivuna!
Hivyo unapoitoa katika uhalisia maana yake umewekeza unatafta faida!
Ardhi ni udongo katika uhalisia wake ukichambua udongo ili upate kokoto ni halali kuuza na kuuziwa!
Lakini katika uhalisia wake ardhi hatutakiwi kutozwa kodi ya ardhi kabisa! Maana bila mkono wa binadam ardhi IPO tayali kama hewa!
 
Hii ni moja ya makosa yaliyofanywa na watangulizi wetu baada ya kupata uhuru. Nadhani wakati huo walioelimika aidha kwa kutokujua au kwa kufuata mkumbo tu waliamua kuweka mipaka ya nchi na kumilikisha kipande cha ardhi iliyopimwa yaani Tanganyika kwa kikundi kidogo cha wajanja wajanja kinachoitwa "Serikali".

Uporaji huu kwa jina la kupata uhuru na kujitawala ndio ulioleta haya mambo ya kodi kwa lengo la dude Serikali kupata pesa za kujiendesha kwa kukiuka misingi ya haki asilia ya mwananchi kumilika ardhi. Kimsingi Serikali ndio inapaswa kuwalipa wananchi kodi ya pango na kulipa fidia pale inapotaka kutwaa ardhi ya mtu.

Nchi hii inatakiwa kusukwa upya kwa kutengeneza katiba itakayo zingatia suala la ardhi kuwa mali ya mtu mmoja mmoja na sio huu ulaghai wa ardhi kuwa mali ya Serikali chini ya uangalizi wa taasisi ya Rais.

Kwa ufupi,
1. Kodi lazima ilipwe kwa mfalme. Hiyo ni tanguy zama hizo.
2. Kumpa mtu umiliki kamili (absolute ownership) wa ardhi ambaye hana uwezo wa kuilinda kisheria, kiusalama, kijeshi nk. ni hatari kwa mstakabali mzima wa taifa lolote. Ukisema ardhi, maana yake ni nyumbani, maana yake ni nchi. Sasa vitus kama hivi haviwezi kuachwa vivi hivi.
3. Sheria inatambua kuwa ardhi ni Mali ya umma. Ikimaanisha mimi na wewe na yule, lakini usimamizi amepewa Rais. Hivyo haki ya kumiliki na kutumia kisheria iko sawa kwa wote, lakini kwa kufuata taratibu zilizowekwa.
 
Kwa mujibu wa Sheria, Hakuna Ardhi iliyokaa bure tu, Ardhi ni mali ya umma na msimamizi mkuu ni Rais, wewe unakuwa umepewa tu hati ya kuimiliki kwa miaka kadhaa lakini lazima uendelee kulipa kodi kwa msimamizi mkuu (Rais)
Hiyo sheria wakati wa Nyerere na Mwinyi ilikuwepo au ni mpya?
 
Hujaelewa mada.
Tofautisha kati ya kodi na mauziano.
Mauziano ya ardhi huwa ni makabidhiano ya ardhi kutoka kwa mmiliki wa mwanzo aliyewahi kwenda kwa mmiliki mpya(aliyechelewa kuipata) na malipo hufanyika mara moja tu.
Lakini kodi ni tozo kwa mmiliki wa ardhi na ambayo hujirudia mara kwa mara na hii ndio hoja ya mtoa mada
Hoja ya msingi hapa ni BURE! Bure kama hewa tunayovuta ambayo hulipii chochote. Kama kuipata ardhi ni kwa kununua maana yake ardhi ina thamani na inatakiwa kulipiwa kodi. Just my thinking.
 
Halafu hili suala la ardhi yote kumilikiwa na Raisi ni bongo tu.

Hapo Kenya ardhi ni Mali binafsi hivyo kurahisisha maendeleo na muendelezo wake.

Kifupi ukifatilia historia ya Kodi haikuanza miaka mingi na raia walichangia serikari kipindi Cha Vita.

Kodi ilianzishwa ili kutozaa matajiri ila Serikari ilivyoanza kuonja fedha taratibu wakaiweka kwa jamii nzima.

Sasa kutokana na mlundikano wa Kodi tumekuwa State Slaves.

Hii kutozwa Kodi mara mbili kwenye kitu kile kile inakera kwa kweli(Double Taxation)
Fikiria unalipa Kodi ya ardhi na jengo kwenye kiwanja kile kile.

Ardhi ni mali ya umma. Ila rais kapewa kama msimamizi.
 
Hiyo ardhi unayolipia umeipata wapi wakati ardhi yetu wote binadamu ya asili unajimilikishaje
Aliyewahi kuichukua ndio anahesabika ni mmiliki kisha yeye ataamua kummilikisha mtu mwingine kwa malipo fulani,hiyo ndio asili yake ilikoanzia.
Bila hivyo ingekuwa vurugu ingekuwa kiwanja kimoja wanajazana watu 100.
Na kumbuka si wamiliki wote wa ardhi walinunua kwa pesa,wengine waliwahi tu mapori wakajimilikisha
 
Hoja ya msingi hapa ni BURE! Bure kama hewa tunayovuta ambayo hulipii chochote. Kama kuipata ardhi ni kwa kununua maana yake ardhi ina thamani na inatakiwa kulipiwa kodi. Just my thinking.
Sio wamiliki wote wa ardhi walinunua,wewe unanunua ardhi kwa sababu umechelewa kuja kuitafuta kwa hiyo unampa fidia tu mtu aliyeiwahi na kuitunza kwa ajili yako
 
Back
Top Bottom