Kwanini Magufuli aliwaogopa sana Nape na January Makamba?

Kwanini Magufuli aliwaogopa sana Nape na January Makamba?

Kuna kitu kinafanywa na wote, wenye uthubutu wa kufanya hivyo ndio huonekana wa kwanza hata kama wako wengi.
Hiyo ndio ccm haijalishi yupo Magufuli, Nape au January.
 
Mlishindwa mwelewa JPM, ni hili ndo kosa kubwa alilolifanya .

Kikawaida Adui, mtafune na ummalize jumla jumla.

Ila Kwakua JPM , mkiristo wa watu ,mahili asiyekua na makuu.

Yeye baada ya kuwashughuli awali kama funzo, na akawaona kama Vijana wake ambao walihitaji tu kuelekezwa, aliamua kuwasamehe.

Na aliwasamehe Kwa Moyo mweupe kabisaaa , akiombwa na kubembelezwa na wazee !!.

Mzee wa watu akawasamehee, na wao wakamuaminisha hawana kinyongo.!!.


Leo tunaambiwa "Watu wazuri hawafi"....




Aliwasamehe, lakini je wao - Makamba, Nape walikuwa wa kweli?
 
Unadhani hatujui tofauti ama?
Hizo tofauti ni muendelezo wa pale mlipoishia, wenyewe mlikuwa mmesharidhika na aina ya chaguzi za Tanzania zisizo na haki Magufuli kaongeza episodes tu na mtazoea tu. Kama vile Magufuli alivyozuia mikutano ya siasa kwa upinzani ila Samia na ccm wameendelea na huo utaratibu wa mtangulizi.
 
Hizo tofauti ni muendelezo wa pale mlipoishia, wenyewe mlikuwa mmesharidhika na aina ya chaguzi za Tanzania zisizo na haki Magufuli kaongeza episodes tu na mtazoea tu. Kama vile Magufuli alivyozuia mikutano ya siasa kwa upinzani ila Samia na ccm wameendelea na huo utaratibu wa mtangulizi.

Ni kweli hazikuwa za haki, lakini still wapinzani walikuwa wanazidi kuzoa viti. Ingekuwa vinapungua hapo sawa.
 
Ni kweli hazikuwa za haki, lakini still wapinzani walikuwa wanazidi kuzoa viti. Ingekuwa vinapungua hapo sawa.
Bado ccm walikuwa wengi bungeni na ndio walikuwa na nguvu, na huo ni upande wa wabunge tu ambao ndio walikuwa wanaachia mgombanie ila kwenye urais huko hata upinzani wamsimamishe Kikwete hawatoboi.
 
Sasa Nape na January walikuwa na nini cha kumtisha Rais wa nchi ambaye tunaambiwa alikuwa dikteta tena mwenye kuuwa sana watu? Hebu niambie kwa mfano angewafukuza tu kule ccm nini unadhani kingetokea ambacho pengine ndio alichoogopa rais wa nchi ambaye ni dikteta?

Mimi narudi kusema kwamba Magufuli mlikuwa mnakuza tu kwenye huo ubaya, dikteta muuwaji wa mamia ya watu bila kuogopa ndio aje kuzidiwa ubabe na Nape na Makamba?
Magufuli aliwafukuza Jesca Msambatavangu na Sofia Simba kisa tu hawakukubaliana na kitendo cha CCM kumkata Lowassa, Magufuli aliagiza Tundu Lissu kupigwa risasi kisa alimuita dikteta uchwara,
 
Aliwaogopa au wao ndo walimuogopa?,alisubiri kuja kuwatumia Kisiasa
Ila wao ndio wakamtumia... Kama Nape alienda kule Kusini kabla ya kura za maoni akamnadi kwelikweli wajumbe wasije kumkataa
 
Hivi kile chuma ni cha kuogopa hawa wadudu kweli jamani!
Nape alikwenda ikulu kwa magoti ambayo ni ishara ya woga uliopindukia!
Makamba wote 2 walitafuta hadi mashimo ya kuingia kumkimbia 🗝️🔑🤣
Nape una video au picha yake akipiga magoti?
 
Wote waliohusika kumsema Magufuli kwenye zile sauti zilizovuja, wote walipotezwa kisiasa kasoro Nape na Makamba.

Ngelejea japo hakuwa mshiriki mkubwa na kuwa wa kwanza kuomba msamaha lakini alipotezwa kwenye ubunge baada ya Magufuli kumfadhili mshindani wake.

Membe alifukuzwa, Kinana nae akawa suspended kwenye chama(hata hivyo baadae Magufuli alimrudisha licha ya Kinana kutoomba msamaha rasmi).

Lakini Nape na Makamba japo ndio walikuwa viongozi wakuu wa uasi ule, Magufuli aliwaacha wakapita kwenye kura za maoni ndani CCM na majina yao hakuyakata na wakarudi bungeni na sasa ni mawaziri wenye nguvu kwenye serikali ya Samia.

Sasa nauliza kwa nini Magufuli alikuwa anaogopa kuwaadhibu hawa watu?

Leo hii wafuasi wa Magufuli wanateseka sana wakiona Nape na Makamba wanavyotesa na kuvimba huku wakiwatupia vijembe.
Ukimuacha nyoka aliekukosakosa ukiwa shambani au kwenye Banda la kuku awamu ijayo atatafuta uficho mzuri wa kukumaliza. Mungu kaamua ugomvi imagine hii kauli !!
 
Hivi kile chuma ni cha kuogopa hawa wadudu kweli jamani!
Nape alikwenda ikulu kwa magoti ambayo ni ishara ya woga uliopindukia!
Makamba wote 2 walitafuta hadi mashimo ya kuingia kumkimbia 🗝️🔑🤣
Wanajifanya wamesahau,
Eti aliwaogopa wakati jiwe kawajambisha mpk kutembea na magoti mtu nusu kilomita mchezo.
Hao wengine walihama mji kabisa wakakaa kwa kutulia shamba huko.
 
Kumbe Tundu Lissu ni kiroboto na upigwaji wake risasi hauhusiki Kwa serikali wala mkuu wa serikali aliekuwepo?....oohho nimekupata
Alipigwa risasi na nani unayemjua wewe?
Tupe ushahidi
 
Bado ccm walikuwa wengi bungeni na ndio walikuwa na nguvu, na huo ni upande wa wabunge tu ambao ndio walikuwa wanaachia mgombanie ila kwenye urais huko hata upinzani wamsimamishe Kikwete hawatoboi.

Wingi wa wabunge wa CCM ulikuwa ukienda ukipungua, fahamu msemo usemao bandubandu humaliza gogo. Nguvu ya wabunge wa CCM haikuwa kwenye hoja huko bungeni, bali kura. Na wananchi walikuwa wanazidi kuamka kwani walikuwa wanaangalia ubora na sio wingi.
 
Makamba ndiye aliyeingilia mfumo wa tume ya uchaguzi na kupunguza kura za Lowasa ili za jiwe zitoshe.

Nape ndiye aliyepiga kampeni mpk akavunja mkono huko vijijini kabisa ili watu wampigie kura jiwe maana by then ccm ilikuwa imekanwa kabisa na watanzania.

In short ,these two guys are smarter by far than jiwe, hence jiwe was haunted by unspeakable fear for them.
Nani aliyeisababisha CCM ikataliwe na watanzania 2015 ? Wakati CCM inakataliwa na watanzania nape na january walikuwa ndani ya CCM au walikuwa nje ya CCM?
 
Mlishindwa mwelewa JPM, ni hili ndo kosa kubwa alilolifanya .

Kikawaida Adui, mtafune na ummalize jumla jumla.

Ila Kwakua JPM , mkiristo wa watu ,mahili asiyekua na makuu.

Yeye baada ya kuwashughuli awali kama funzo, na akawaona kama Vijana wake ambao walihitaji tu kuelekezwa, aliamua kuwasamehe.

Na aliwasamehe Kwa Moyo mweupe kabisaaa , akiombwa na kubembelezwa na wazee !!.

Mzee wa watu akawasamehee, na wao wakamuaminisha hawana kinyongo.!!.


Leo tunaambiwa "Watu wazuri hawafi"....




JPM alikuwa mpuuzi anayevaa suti. unawadukua watu ili iweje? unawadukua watu kisha unataka kuombwa msamaha? yaani umfanyie mtu kosa kisha akuombe msamaha? hata mungu hajawahi fanya hivyo
 
Walikuwa bado makinda wadogo wakilelewa ndani ya ccm
Januari alikuwa MSAIDIZI WA RAIS IKULU na Baadaye Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Katibu na Siasa Kimataifa wa CCM, Naibu Waziri wa Mawasiliano huo ukinda ndani ya CCM umeutoa wapi, Nape alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM huo ukinda umeutoa wapi.
 
Back
Top Bottom