Uchaguzi 2020 Kwanini Paul Makonda ametoswa na Patrobas Katambi amepata uteuzi?

Uchaguzi 2020 Kwanini Paul Makonda ametoswa na Patrobas Katambi amepata uteuzi?

johnthebaptist,

Katika hili nimeamini kuwa Jiwe ni mtu anayeheshimu sana mikataba. Haya yalikuwa baadhi ya makubaliano makuu ya 'kuunga mkono juhudi' na ameonesha kuyaheshimu liwake, inyeshe!!

Pili, hao 'waunga mkono juhudi' si wafuasi wa CCM per se (na ndio maana wajumbe waliwatosa, kihalali kabisa), bali ni waumini kindakindaki wa magufulism. Kumbuka Jiwe anapenda sana ufalme (akikooa mnapiga makofi, akiwatukana mnapiga makofi) na anatengeneza waumini ambao ndio watakuwa nguzo ya kumtawazisha ufalme.
 
Hapana aisee kwa haya ni wazi kuwa Paul Makonda kaonewa sana. Nimejikuta nikipata huruma juu yake maana si kwa faulo hii iliyochezwa.

Yani mfano kwa Shinyanga mjini mtu kakataliwa na wajumbe 456 kapata kura 12 tu eti ndiye amepitishwa? Hapana!

Pia nimegundua kumbe ile hama hama ilikuwa ni makubaliano endelevu.
Makonda umeonewa na nasimama na wewe leo.
G Sam , sasa mgombea wa CDM awapitie hao wajumbe 450 "awapike"
 
Huwezi jua mzee baba ana Dhahabu gani aliyomwekea kama atapita anyway!
 
Mnasahau kwamba huyo Paul hata elimu yake ni shida
Yeye safari hii atabaki kulea mwanae wa kichina tuu hakuna namna
Madeko jamani wee madeko, haya wee!!! wa-kichina ndiyo gani mtoto? mbona mnavituko wana JF?
 
Tusipompigania kama alivyokipigania chama atapotea kabisa.

Natoa rai njooni tumpiganie kama yeye alivyompiganaji.

Kwanini Gwajima na sio yeye?

Natoa Rai.
 
Ohoo!! Yaani Masele kaachwa, kachukuliwa Katambi?

Huyu Masele alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Pan
Unachanganya Mafaili mkuu..
Huyo Makamu mwenyekiti Bunge la pan Ni masele wa Jimbo la Mbogwe Geita.
Na huyo masele mwingine ni Mbunge wa Shy Mjini alipopitishwa Katambi
 
Kwa kuwateua wale waliokataliwa na wajumbe kuwa wagombea,ccm[JIWE] imeweka credibility yake on the line. Msije mkashangaa kuwa wote wakashindwa kwani wajumbe ndio wapiga debe huko kwenye constituencies!!!! Kushindwa kwao kutaonesha kutokubalika kwa JIWE.
Magufuli hakubaliki ndani wala nje ya ccm, hilo hata yeye mwenyewe analijua.

Aliyekuwa anamkubali ni mzee Mkapa na wachumia tumbo tu.
 
Makonda hakuwa mjanja. Angejikita Kawe angepita. Ndungulile baba yake alikuwa ni mtu wa system. Hao hawakatwi, huoni akina Nape, January wamesarvive pamoja na ukaidi wao hapo nyuma.
Hakuna anayejua Jiwe anampangia cheo gani! kama Jiwe atapita
 
CCM inaangamia kwa watu wake kukosa maarifa yakiwemo hata maarifa madogo tu ya kusoma alama za nyakati.

Kwa kutompitisha Makonda,naweza sema walau hapa wamesoma alama za nyakati kwani kwa kumpitisha, ingewagharimu CCM nchi nzima mpaka mgombea wao wa uraisi.

Kwa upande wa Katambi, Katambi atakataliwa na wana-CCM ,wapinzani na wasio na vyama pia.
Katambi ni kiongozi mahiri ndio maana hata Mbowe alikuwa anamkumbatia.
 
Unafiki ni mmojawapo ya vigezo kupata uongozi huko CCM.
View attachment 1543085
Ndio sababu watu hawana imani ya kupigia kura mbunge au diwani kwa tiketi ya upinzani.Hiyo mass exodus waiofanya kuhamia CCM imetuacha njia panda. Ni vigumu kumjua pandikizi au polical prostitute kwa hali ya kawaida ukisikiza tu hotuba murua lakini kumbe ni mafisi.
 
Back
Top Bottom