Uchaguzi 2020 Kwanini Paul Makonda ametoswa na Patrobas Katambi amepata uteuzi?

Uchaguzi 2020 Kwanini Paul Makonda ametoswa na Patrobas Katambi amepata uteuzi?

Kwa kuwateua wale waliokataliwa na wajumbe kuwa wagombea,ccm[JIWE] imeweka credibility yake on the line. Msije mkashangaa kuwa wote wakashindwa kwani wajumbe ndio wapiga debe huko kwenye constituencies!!!! Kushindwa kwao kutaonesha kutokubalika kwa JIWE.

Wewe Ni CCM au.
 
Mabeberu walifikisha faili la Makonda, hivyo ikawa hakuna namna ikabidi Mzee baba atengeneze mazingira ya kumuondoa kwa njia iliyofanyika. Win win situation serikali ya CCM imeepukana na mbinyo bila wananchi kujua kuwa ni mbinyo wa mabeberu, wakati mwingine kama alivyosema Palamagamba Kabudi masuala mengine yanafanyika kwa siri kulinda heshima.

Uzuri wa watz maswali wanatunga wao. Then wanasema Ni mtihani na majibu wanatoa wao. Mambo yangekuwa rahisi namna hiyo kuyaelewa Basi Siasa ingekuwa sio Siasa.
 
johnthebaptist,

CCM Wanaona mbali kinoma. Walijua kabisa kama makonda angeteuliwa kigambonino! Hiyo kwa upande wa upinzani ingekuwa ni sehemu ya ajenda yao! Na pia kwa upande mwingine ingemuasiri magu kwenye kampeni zake hasa kwa upande wa DSM.

Walimtoa kijanja kwenye ukuu wa mkoa ili wapinzani wakose cha kuongea juu ya makonda! Na hata kama wakiongea kitakuwa hakina mashiko. Take my word! Makonda anaenda kuwa naibu waziri Tamisemi.
 
Habari ni kuwa Makonda alikuwa atumbuliwe kabla ya kampeni kuanza ili impe JPM credit , sasa yeye akaustukia machezo akajiengua mapema! Hizo hazikuwa habari njema kwa mkuu, akakasirika sana kwani amemharibia mahesabu. Kwa sababu hiyo sioni ajabu Makonda kutopata uteuzi wa Ubunge.

Mkuu Nani alimteua Makonda kwenye Tume ya katiba na then ukuu wa wilaya. Ni JPM au MWINYI. Nimesahau nikumbushe.
 
Mkuu Nani alimteua Makonda kwenye Tume ya katiba na then ukuu wa wilaya. Ni JPM au MWINYI. Nimesahau nikumbushe.

Kikwete ndio alimteua huko na Baadae baada ya kujikomba kwa mtoto wa Kikwete kwa Kufunga gidamu za vitautu vyake akaambulia kuwa DC!! Baadae alipoingia JIWE akawageuka na kuwafitini wale wa Msoga!!!
 
Isingekuwa in afya ya siasa kwa CCM kumteua bwana makonda angewapa wapinzani cha kuongea,yeye asubiri kuteuliwa tu mahal at a viti maalum alaf ndo mengine ya kumpandisha yataendelea
 
Kwan pale shinyanga mjin si ndo lilikuwa jimbo la yule mbunge masele ? Jamaa alikuwa bright sana
 
Dogo Katambi kabebwa, kule wana CCM wanamtaka Masele; kama unabisha basi fika Shinyanga town sasa hivi uone kinachoendelea.

Jimbo ni kama limekabidhiwa upinzani rasmi...hakuna namna yoyote yule kijana wa x- CDM anaweza kutoboa pale...yaani kabebwa waziwazi huku wakati wafia chama....miaka nenda rudi wakiachwa midomo wazi!!

Wana CCM asili wamesema kubebana sasa basi kama ni kampeni makao makuu wahamie jimboni wampigie dogo kama wataweza.

Kamati ROHO MBAYA muda huu inaendelea na kikao chake.
 
Kumwacha Makonda imekuwa ni namna ya kumsaidia.

Kama angepitishwa, angepata pingamizi la udanganyifu wa jina halisi, elimu na vyeti vya masomo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom