Kwanini Rais Samia mpaka sasa hajaongea na waandishi wa habari kuhusiana na sakata la Bandari?

Kwanini Rais Samia mpaka sasa hajaongea na waandishi wa habari kuhusiana na sakata la Bandari?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Ni zaidi ya mwezi sasa hili suala la bandari limeendelea kuwa gumzo, kinyume na matarajio yangu!

Mwanzoni nilidhani lilikuwa ni upepo tu upitao kama yalivyo masuala mengine.

La hasha. Haijawa hivyo.

Kila kunapokucha, gumzo la bandari zetu ndo linatawala vinywa vya wananchi.

Hali hii imenifanya nijiulize maswali kadha wa kadha;

Kwa vile ni gumzo ambalo limeendelea kutawala mazungumzo ya watu kwa muda mrefu [kwa zama hizi za utandawazi, umma kuongelea jambo moja kwa zaidi ya mwezi, ni muda mrefu!], basi ni wazi kuwa wananchi wengi wanaliona kuwa ni suala la muhimu sana.

Sasa kwa nini mpaka sasa Rais Samia hajaitisha mkutano wa habari na waandishi wa habari ili kulizungumzia na kulitolea ufafanuzi na kujibu maswali ya wananchi?

Badala yake, ni kama vile kajificha nyuma ya makada wa chama chake pamoja na baadhi ya wateule wake serikalini ambao wao ndo wamejaribu kulizungumzia, lakini kila wafanyapo hivyo, wanaishia kuzua maswali mengi zaidi.

Ni kwamba hana taarifa za kutosha za kumwezesha kulizungumzia hilo suala mbele ya waandishi wa habari?

Au hajiamini kuongea na waandishi wa habari?

Come on Samia….talk to the press [and the nation].

If everything is above board….is on the up and up, it shouldn’t be that difficult for you to talk to the press and take their questions.

Ona huyu alivyokuwa anakabiliana na waandishi wa habari wa kimataifa…

 
Muhimu ni kwamba wataalam kama kina shivji washaongea sasa we shivji unaona hana akili?mtu ka publish mavitu yanasomwa chuo kikuu Leo hii aongee kitu kuhusu tasnia yake me nimpinge..sorry kwanza kwani rais mama samia kasomeaga nini??
 
Haihusu.

Wapo wenye kazi zao juzi waliitisha kongamano wakajibu maswali yote, na wamekubaliana kikao kijacho itakuwa ni mdahalo na wale wamaopinga.


Mama ana mengi sana ya kufanya, hana sababu za kubishana na wajinga.
 
Haihusu.

Wapo wenye kazi zao juzi waliitisha kongamano wakajibu maswali yote, na wamekubaliana kikao kijacho itakuwa ni mdahalo na wale wamaopinga.


Mama ana mengi sana ya kufanya, hana sababu za kubishana na wajinga.
Inahusu sana tu. Mjinga ni anayeogopa kukabiliana na waandishi wa habari.

Huyu alikuwa na mambo mengi sana na hakuwa anajificha katika kuongea na waandishi wa habari!!

 
Haihusu.

Wapo wenye kazi zao juzi waliitisha kongamano wakajibu maswali yote, na wamekubaliana kikao kijacho itakuwa ni mdahalo na wale wamaopinga.


Mama ana mengi sana ya kufanya, hana sababu za kubishana na wajinga.
Yaani WEWE
 
IMG-20230716-WA0024.jpg
 
Tumeliwa Sana Ndugu Zangu
Tulaliwa Sana Ndugu Zangu
Tumegongwa Mno Ndugu Zangu
Tumehomolwa Sana Ndugu Zangu

Vyovyote Mtakavyosema Najua Mmenielewa Sana, Majizi Hata Ccm Yapo
Tutahakikisha Tunalala Nayo Mbele
By Mzilankende Mnyango
 
Haihusu.

Wapo wenye kazi zao juzi waliitisha kongamano wakajibu maswali yote, na wamekubaliana kikao kijacho itakuwa ni mdahalo na wale wamaopinga.


Mama ana mengi sana ya kufanya, hana sababu za kubishana na wajinga.
Kwahiyo wewe unaona bandari ni jambo dogo?? Huo ushungi ulivaa umepita hapo bandarini.
 
Faiza mtajie tu Magufuli, uone atakavyochomoka nduki! Nadhani alikua na kesi ya uhujumu uchumi enzi za mwendazake ndio maana alipotea from 2016 Hadi 2023 alivyoona kumepoa
Huyu faiza ni nani nchi hii anajihusisha na shughuli gani kwanini anapambana sana wakati huu hasa sakata hili la bandari si usiku si mchana yupo active tofauti kabisa na kipindi cha magufuli
 
Samia hana jibu, wala usipoteze muda wako kumsubiri atolee ufafanuzi hilo suala la bandari, kimsingi wanachojibu kina Mbarawa ndio ujinga huo huo uliopo kwenye kichwa cha Samia, hana ajualo.

Ameshajipambanua siku nyingi yeye ni kiongozi wa kuwaachia wasaidizi wake wafanye kile kitu, yeye ni kama ceremonial president.

Hujiulizi kwanini licha ya kukaa kimya muda mrefu, lakini alipozungumza juzi wakati akiwaapisha kina Kitila bado aliongea pumba, akasema wakenya nao wamekimbilia uwekezaji wa DPW.

Kama vile hatutaki uwekezaji, wakati shida yetu ni terms za hovyo zinazotunyonya kwenye ule mkataba wa bandari, na unapomlinganisha na Nyerere ndio unatenda dhambi nyingine kubwa zaidi, huyo ungemuwekea mfano wa Kikwete tu inatosha.
 
Ni zaidi ya mwezi sasa hili suala la bandari limeendelea kuwa gumzo, kinyume na matarajio yangu!

Mwanzoni nilidhani lilikuwa ni upepo tu upitao kama yalivyo masuala mengine.

La hasha. Haijawa hivyo.

Kila kunapokucha, gumzo la bandari zetu ndo linatawala vinywa vya wananchi.

Hali hii imenifanya nijiulize maswali kadha wa kadha;

Kwa vile ni gumzo ambalo limeendelea kutawala mazungumzo ya watu kwa muda mrefu [kwa zama hizi za utandawazi, umma kuongelea jambo moja kwa zaidi ya mwezi, ni muda mrefu!], basi ni wazi kuwa wananchi wengi wanaliona kuwa ni suala la muhimu sana.

Sasa kwa nini mpaka sasa Rais Samia hajaitisha mkutano wa habari na waandishi wa habari ili kulizungumzia na kulitolea ufafanuzi na kujibu maswali ya wananchi?

Badala yake, ni kama vile kajificha nyuma ya makada wa chama chake pamoja na baadhi ya wateule wake serikalini ambao wao ndo wamejaribu kulizungumzia, lakini kila wafanyapo hivyo, wanaishia kuzua maswali mengi zaidi.

Ni kwamba hana taarifa za kutosha za kumwezesha kulizungumzia hilo suala mbele ya waandishi wa habari?

Au hajiamini kuongea na waandishi wa habari?

Come on Samia….talk to the press [and the nation].

If everything is above board….is on the up and up, it shouldn’t be that difficult for you to talk to the press and take their questions.

Ona huyu alivyokuwa anakabiliana na waandishi wa habari wa kimataifa…


Nafsi inamsuta
 
Back
Top Bottom