Kwanini waajiriwa wengi hawana utamaduni wa kufanya savings nchini?

Kwanini waajiriwa wengi hawana utamaduni wa kufanya savings nchini?

Watu wengi wanashindwa kusave kwa sababu ya asilimia zinazowek2a na watoa ushauri wa saving.


Mtu anapokea mshahara 400,000 alafu anaambiwa asave 20% yaani 80000 nzima wakati huo ana majukumu kibao yanamsubiri.

Tuangale mtu kama huyu wa kipato hiko anaweza akasave asilimia tano inatosha kwa sababu hakuna akiba ndogo kamwe.

Mtu anapokea laki nne sio mbaya akaweka pembeni 20000 ambayo hatoigusa kwa lolote,lakini akiiweka 80000 akilini mwake itakuwa anasema ipo 80000 ipo 80000 ipo 80000 ipo 80000 yaani akipata shida kidogo tu anarudi kwenye 80000 anaanza kuitawanya.

aatleast ukiweka 20000 au hata 15000 inatosha sana hakuna akiba ndogo kamwe wakuu.

usifuate ushauri wa watu wanaosema weka 20% au 30% wakati hawajui unaishi vipi na unapokea pesa ngapi na una majukumu gani.

Hakikisha unaweza akiaba hata kama ni 5000 kwa mwezi hiyo ni kubwa na ni yako.

Haya mambo ya asilimia tusiyazingatie sana..
Yani umeongea point kubwa sana....save at your own risk...yanii hata kama unapata 1M save hata 70k ambayo haitaguswa kamwe...haya mambo ya savings yaendane na uhalisia wa kipato, mahitaji na majukumu..na usisahau kuishi.
 
Sababu kubwa ni ya kitabia na mazoea. Ili ufanikiwe saving anza tabia hiyo tangu ukiwa na umri wa miaka 20.

Sababu nyingine ni vipato duni ambavyo haviendani na uhalisia wa maisha. Wengi ujikuta wanaishi with deficity budget . Solution wafanyakazi wajifunze kutanua vyanzo vya kipato. Tabia hii ianze punde tu unapoanza kujitambua kua pesa inahitajika.

Sababu nyingine ni unyonyaji wa kimfumo. Watumishi Kila mwenzi wanahitajika kisheria kusave 10% ya mishahara Yao. Pia serikali inawachangia another 10% that mount to 20%. Hizi pesa zinachukuliwa na mifuko ya hifadhi ya jamii kama NSSF and PSSSF. Lakini mifumo ya operation and return kwa wafanyakazi sio rafiki coz pesa hizo watumishi hawana access nazo hadi watakapostaafu. Ni vyema mapitio ya kisera yafanyike ili pesa hizi wafanyakazi wazitumie kufanya shughuri za maendeleo kama kuwa bond ya mikopo ya nyumba n.k
 
Sababu kubwa ni ya kitabia na mazoea. Ili ufanikiwe saving anza tabia hiyo tangu ukiwa na umri wa miaka 20.

Sababu nyingine ni vipato duni ambavyo haviendani na uhalisia wa maisha. Wengi ujikuta wanaishi with deficity budget . Solution wafanyakazi wajifunze kutanua vyanzo vya kipato. Tabia hii ianze punde tu unapoanza kujitambua kua pesa inahitajika.

Sababu nyingine ni unyonyaji wa kimfumo. Watumishi Kila mwenzi wanahitajika kisheria kusave 10% ya mishahara Yao. Pia serikali inawachangia another 10% that mount to 20%. Hizi pesa zinachukuliwa na mifuko ya hifadhi ya jamii kama NSSF and PSSSF. Lakini mifumo ya operation and return kwa wafanyakazi sio rafiki coz pesa hizo watumishi hawana access nazo hadi watakapostaafu. Ni vyema mapitio ya kisera yafanyike ili pesa hizi wafanyakazi wazitumie kufanya shughuri za maendeleo kama kuwa bond ya mikopo ya nyumba n.k
Umeongea point kubwa sana, kusave ni tabia na utamaduni unaojengwa angali mdogo, pia pesa za mifuko ni Kama serikali imezifanya zakwao hata hivyo wamezitumia karibia zote
 
M naona kwanza lazima ujue unasave kwa ajili ya lengo gani mfano kama kwa ajili ya emergency, kwa ajili ya kununua kitu flani au kwa ajili ya vacation, baada ya hapo ndio utajua kiwango gani cha kusave kwa muda gani ili uweze kufanikisha hilo lengo,nimependa wazo la jamaa hapo Save kiwango ambacho unaweza kukimudu, maisha mengine lazima ya endelee.
 
Wengi Wana usemi huo huo, anaepokea 500k, anaepokea 1M, anaepokea 2M. Wote wanakuambia mshahara kidogo hatuwezi kusave, Ila Kuna mtu alikuwa anaepokea laki 6, alikuwa anajibana anasave, baadae umesaidia sana na maisha yamebadilika, kwani alisevu akainvest
Hakika mkuu, tukiambiana ukweli kama huu uliosema watu wengi watatoboa, mwaka 1 mpaka 5 ndani ya ajira hutoa tathimini ya maisha ya mtu ya miaka inayofuata. Unakuta huyu anaepokea 500,000 hana familia na ametoka katika familia ya kawaida sana hivyo kama akijiongeza anaweza akachukua room moja tu 50,000 to 70,000 ambayo ipo maeneo ambayo yanafikika kiurahisi kutoka kwenye mihangaiko yake. Inabaki 430,000 ambapo savings 200,000 kwa mwezi na 230,000 inabaki ya matumizi mengine. (baada ya mwaka si atakuwa amefika pazuri)

Kwa maisha ya sasa ukishindwa kujipanga mwanzoni kabisa yaani mwaka 1 mpaka 5 kabla hujawa na familia, usitegemee kufanya savings wakati una familia, na kama ni mwanaume utaishia kuwalaumu wanawake wanapenda ela.
 
Nimejaribu kufanya tathmini na nimegundua watanzania hasa hawa waajiriwa wa Serikalini hawana tamaduni za kutunza pesa, Wazungu wanaita savings.

Ni vema watanzania wengi tukaanza kupiga mfumo wa Wazungu kuwa unapopata kamshahara kako basi angalau asilimia 20 itunze, halafu ndo uanze matumizi kwa hiyo 80 iliyobaki. Hali hii ya kutotunza pesa imekuwa mbaya kiasi kwamba mtu amefanya kazi miaka 10 lakini akisimamishwa kazi Mwezi mmoja anageuka kuwa omba omba, na anashindwa kuendesha familia hata kwa miezi miwili Bali ni mizinga tu.

Hali hii pia inachangiwa na ugonjwa unaoitwa spending/shopping addiction yaani ukipata pesa unakuja na kimuhemuhe Cha kuzitumia. Pia kutunza pesa kwa waajiriwa ni changamoto wengi wakisema extended family zinawanyonya sana kiasi kwamba huwezi kutunza shilingi kumi.

Wafanyabiashara Tanzania kwenye hili wanajitahidi sana, na wengi ni watunza pesa wazuri kuliko waajiriwa.
Na Hali ya uhakika wa kupata pesa kila mwisho wa Mwezi unafanya watu kubweteka.

Ukitunza pesa itakusaidia wakati wa emergency na kukuondolea aibu ya kuomba omba pindi unapopata na shida.

Mnaonaje wadau, je ni muhimu kutunza angalau asilimia 20 ya mshahara wako wa Mwezi au ni kuzitandika zote?
Ni wazo zuri sana ili, shida utokea muda wowote ule
 
Nimejaribu kufanya tathmini na nimegundua watanzania hasa hawa waajiriwa wa Serikalini hawana tamaduni za kutunza pesa, Wazungu wanaita savings.

Ni vema watanzania wengi tukaanza kupiga mfumo wa Wazungu kuwa unapopata kamshahara kako basi angalau asilimia 20 itunze, halafu ndo uanze matumizi kwa hiyo 80 iliyobaki. Hali hii ya kutotunza pesa imekuwa mbaya kiasi kwamba mtu amefanya kazi miaka 10 lakini akisimamishwa kazi Mwezi mmoja anageuka kuwa omba omba, na anashindwa kuendesha familia hata kwa miezi miwili Bali ni mizinga tu.

Hali hii pia inachangiwa na ugonjwa unaoitwa spending/shopping addiction yaani ukipata pesa unakuja na kimuhemuhe Cha kuzitumia. Pia kutunza pesa kwa waajiriwa ni changamoto wengi wakisema extended family zinawanyonya sana kiasi kwamba huwezi kutunza shilingi kumi.

Wafanyabiashara Tanzania kwenye hili wanajitahidi sana, na wengi ni watunza pesa wazuri kuliko waajiriwa.
Na Hali ya uhakika wa kupata pesa kila mwisho wa Mwezi unafanya watu kubweteka.

Ukitunza pesa itakusaidia wakati wa emergency na kukuondolea aibu ya kuomba omba pindi unapopata na shida.

Mnaonaje wadau, je ni muhimu kutunza angalau asilimia 20 ya mshahara wako wa Mwezi au ni kuzitandika zote?
kaka wazo zuri lakini imagine mtu analipwa net pay laki mbili kwa mfano baada ya deductions hapoa natakiwa kula nauli alipie makazi sasa hapo ata save nini lets get real jamani
 
Kipato Tsh 500,000. Mahitaji Tsh 700,000.
Hapo savings inatoka wapi?
Savings inaweza kupatikana iwapo baba na mama wanaoamka asubuhi kwenda kazini wanagawana majukumu... Baba akilipia umeme, mama alipie maji!
Tatizo wanawake wengi siku hizi ni goi goi. Kazi za nyumbani anatakiwa azifanye yeye. Basi kama yeye kaamua kwenda kazini kutafuta basi mama ndio alitakiwa amlipe house girl mshahara kwa kumsaidia majukumu yake lakini kinyume chake unakuta baba ndio anamlipa house girl mshahara. Huu ni unyonyaji.
Kwenye familia za kiafrika, baba ni mtu anayenyonywa sana kwa kuwa yeye ndie anayebebeshwa mzigo mkubwa wa kuendesha familia hata kama mama ana kipato kizuri unakuta contribution yake ni ndogo sana...
Wacheni kujitweza na uongo mwingi wa kuwa kila kitu munalipia nyinyi wababa.

Mfanyakazi huwa analipwa na mama kwa vile nyinyi munagoma kulipa mishahara yao. Mavazi ya watoto yanalipiwa na mama nyinyi munajifanya kama hamuna habari kwamba watoto huwa wana mahitaji ya kuvaa.

Na hao waarabu unaowatolea mfano ni kweli mwanamke huwa hafanyi kazi lakini pia huwekewa mfanyakazi na kuhudumiwa kikamilifu.

Kijana, hakuna mshahara unaotosheleza hata siku moja maana kila ukipata nyongeza basi unajipandisha cheo na wewe.

La muhimu ni kujiwekea discipline ya kusave, hakuna ujanja mwengine wowote.
 
mtu anayelipwa laki 9 ni sawa na elfu 30 kutwa

mama na baba 200000
pango 150000
chakula 300000
pretrol 100000
saluni, bar, michepuko, fegi, bangi n.k 100000
nguo, viatu, na mpesa kwa ndugu 100000

kila mwezi unabaki na deni la 50000
 
Back
Top Bottom