Kwanini Watanzania wengi hawafanikiwi kutokana na kazi zao?

Sijafanya research ya kuweza kuhalalisha majibu yangu.

Ila nitatoa mfano.

Kesho unatakiwa kuukata mti.

Unajihimu Alfajiri na vitendea kazi, unafika pale na kuanza kukata mti. Unajitoa kweli kweli, unatumia msumeno, unatumia shoka na unatumia panga.

Lakini muda wote huo ulikua hauahangaiki kukata shina, ulikua unakata mizizi na matawi.

Kufika jioni mti haujakatika.

Kesho unarudi tena, na kwenda na routine ile ile.

Kwa maoni yangu WaTz wengi wanaoonekana wanafanya kazi angalia kama kazi yao inashughulikia tatizo. Utakuta ni inalizunguka tatizo.

Angalia wanasiasa, timu za mpira, hata maofisini n.k. ni wachache wanaaddress tatizo.

Ninaamini ndiyo sababu tunaonekana tunafanya kazi ila mafanikio hayaji au yanakuja kiduchu
 
βœ…πŸ™
 
Israel je?

Mwaka 2013 makusanyo ya mapato ya mwezi 1 ya Israel yalikuwa sawa na bajeti ya JMT ya miaka 2.

Maana yake ni kuwa kama JMT tungepewa makusanyo ya mapato ya mwezi 1 ya Israel basi hakuna Mtz angeenda shamba, ofisini, biashara, kuvua, kuchunga wala viwandani, yaani unaamka una kula na kunywa kwa miaka 2m.

Israel ni nchi ya ajabu pekee kwenye sayari ambayo uchumi wake unapaa ndani ya vita visivyoisha tangu uhuru mwaka 1948 hata sasa miaka 75.
 
Mbona kuna Wahindi walikuja Tanzania wakiwa na hali duni kiuchumi, wakapanga vyumba vya kawaida Uswahilini, lakini baada ya muda wakawa mabilionea?
Tofauti na Wahindi wa kwanza walioletwa na ukoloni wahindi wengine wote waliokuja baadaye na wakafanikiwa huletwa na ndugu zao ambao tayari wameshafanikiwa au wameona fursa na wangetaka kuhakikisha mafanikio hayo na siri za kufanikiwa kwao vinabaki ndani ya familia zao kwa watu wanaowaamini kwa muda mrefu.
 
Tatizo kazi nyingi za watanzania hazileti kitu kipya katika labda kwa uchache wa tu kama akina diamond ndio wamefanikiwa zaidi na pia wapo wengine ktk fani mbalimbali waliofanikiwa ila tu hatufanyi ugunduzi na pia hata tukiufanya hatuufanyii promotion sana lakini pia sekta binafsi ndio yenye watu wengi na yenye potential ya kuleta maajabu ya kunufaika kwa watu ila nayo imekuwa ikipigwa vita na serikali kwa kutokuwekea jitihada za makusudi kukua tokea uhuru hii ilichangiwa na sera zetu za ujamaa japo kwa sasa inabadilika sana siku sekta binafsi ikishika hatamu basi watanzania watanufaika zaidi na zaidi kwa kumiliki gunduzi zao na kuzifanya ziwainguzie kupata na pia kujenga utamaduni wa kuinovate kimaslahi.
 
Kale "kanchi" kadoogo, kenye watu wachaache", katuzidi kiasi hicho?

Mkuu, mimi sikubaliani na jibu lako! Nimelikataa kwa "makusudi", na sitaki kuchungulia mtandaoni kwa sababu nikilikuta jibu lako lipo sahihi nitaona aibu mie.

Acha "nijifariji" kuwa kanchi kadoogo, Israel, hakawezi kutuzidi kimapato hata siku moja!
 
Jambo lingine la mafanikio ni uwepo wa fursa au mazingira ya kufanikwa, wakati mwingine fursa hiyo huja kwa bahati, kurithi, kipaji, wizi n.k. Uwepo wa hiyo fursa+bidii wakati mwingine ndipo unaona watu wanafanikiwa
Kama hakuna hiyo fursa ya kufanikiwa hata ufanye kazi kama punda hautafanikiwa, mafanikio utayasikia kwenye bomba tu.
 
Mimi binfsi Kama ntatoa wazo kuwa tufanye nini ili tutoke katika umasikini na kupata mafanikio tuanze tuwekeze katika Akili zetu .

Mtu mwenye maarifa na akili nzuri ambaye katumia muda mwingi kuwekeza huko anakuwa na uwezo Wa kufanikiwa Kwa haraka kuliko yule anayefanya kazi Kwa bidii.


Tatizo la Africa kutotoboa lipo kichwani . hivyo thesis yangu nitakayoiandika itajikita katika Elimu ya utambuzi kuwa inabidi kufundishwa shule ili MTU ajipate mapema
 
βœ…πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ™πŸ™πŸ™

Go for it DrπŸ™
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…