Kweli nimeamini, ukimfadhili mwanamke usitegemee kwamba atakuja kukusaidia wakati wowote

Kweli nimeamini, ukimfadhili mwanamke usitegemee kwamba atakuja kukusaidia wakati wowote

Sawasawa mkuu. Ila mimi ningekuwa yeye ningefanya kitu kuonesha shukrani. Tunatofautiana na hivyo naheshimu maamuzi yake.
Na ndio maana wewe sio yeye. Na usimsimange kwa msaada uliompa hata baraka huwezi kupata sasa, what if hakuwa katika nafasi ya kukusaidia kabisa?
 
Hawa viumbe ni mashetani bro...sema ndio hivyo mashetani wenyewe mbususu zao tamu[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Wewe kabisaaaa wa kutusimanga hivyo kweli?
 
Ulihiari mwenyewe kumsaidia. Sio lazima saana alipe ulichmfanyia. Ndio maana waswahili wakaja na Msemo Tenda wema nenda zako usingoje shukrani. Hata hivyo, kuwa earning ya 2.5 M ni kitu kimoja na kuwa cash always in hand ni kitu kingine. Ninapendekeza muendelee na urafiki n kusaidiana.

Sasa hapo kuna kusaidiana gani tena wakati upande mwingin hutaki kusaidia.
 
Binafsi sijaona tatizo kwa kushindwa kukisaidia hiyo pesa.

Ila, kutorespond ujumbe kwa muda wa majuma mawili.
 
Kumbe ukiwa haujaolewa ndio unakuwa hauna majukumu!! Mkuu jifunze kuwa unapotoa msaada usiiweke kama deni kwa muhusika, lakini pia si kwamba kwasababu ulimsaidia basi wakati wowote atakuwa ana pesa tu zinasubiri akusaidie. Usimpangie mtu na mshahara wake maana kweli huwezi jua ana majukumu gani.
Wadada kwa kuteteana hamjambo. Kama umesoma vizuri basi utaona tatizo kubwa ni yeye kukaa kimya. Kama pale aliposoma ujumbe angenijibu kwamba hana wala isingekuwa tatizo. Alichofanya ni kama kunionesha kwamba umwamba.
 
Na ndio maana wewe sio yeye. Na usimsimange kwa msaada uliompa hata baraka huwezi kupata sasa, what if hakuwa katika nafasi ya kukusaidia kabisa?
Ni simple kabisa, angeniambia wakati ule basi kisingeharibika kitu.
 
Inawezekana ni kweli hizo pesa hakuwanazo na angekuwa nazo angekusaidia. Huenda hizo wiki mbili alikuwa anazitafuta hizo pesa ili akusaidie, na aliposhindwa kabisa ndiyo akakutumia jibu hilo la kukushauri utafute alternative.
Inawezekana kabisa, angenipa taarifa wakati ule basi kisingeharibika kitu.
 
Na Bado hilo Treila kwenye kikao tulishakubaliana ila wewe umekiuka.Hatawahi kukusaidia hata elfu 10, pambana mwenyewe mpaka ufe
 
Huyu dada alipitia changamoto baada ya kupoteza wazazi na nikaamua kumsaidia. Tukawa na mahusiano kama mwaka mmoja hivi.

Baadae nikamwambia naona tulikutana ili nikusaidie lakini moyo wangu hauko na furaha kuendelea na uhusiano. Aliumia sana japo niliendelea kumsaidia kwa kulipa ada zake chuo.

Miaka zaidi ya saba imepita na tumekuwa tukiwasiliana kawaida kama kaka na dada. Alipomaliza chuo alipata kazi kampuni kubwa sana hapa dar na alinitumia meseji nyingi sana kushukuru.

Wiki kadhaa zilizopita nilipata changamoto kwenye biashara zangu na kuna malipo fulani yalichelewa sana kuingia na nikawa natakiwa kulipia baadhi ya huduma kwa haraka.

Kwasababu huwa tunawasiliana nikamtumia ujumbe whatsap kuomba anisaidie 400k (ninafahamu mshahara wake upo kwenye 2.5m). Alisoma ujumbe halafu hakujibu kwa wiki mbili.

Sasa amenijibu kuwa anayo majukumu mengine, nitafute alternative ingawa najua bado hajaolewa.

Nimeanza kuelewa kwanini moyo wangu ulikataa kumuoa.
Mbona Inaonesha Wazi ulikua unamuhonga na kumtumia kingono....kwa kigezo cha Kumsaidia....ndoo maana na yeye Kauku"tema kiroho mbaya....
 
Mbona Inaonesha Wazi ulikua unamuhonga na kumtumia kingono....kwa kigezo cha Kumsaidia....ndoo maana na yeye Kauku"tema kiroho mbaya....
Rudia kusoma boss maana mida hii ni usiku sana.😄
 
Wadada kwa kuteteana hamjambo. Kama umesoma vizuri basi utaona tatizo kubwa ni yeye kukaa kimya. Kama pale aliposoma ujumbe angenijibu kwamba hana wala isingekuwa tatizo. Alichofanya ni kama kunionesha kwamba umwamba.
Tatizo kubwa ni wewe kumsaidia na yeye kushindwa kukusaidia, soma title yako. Hata angekujibu bado ungekuwa na notion hiyo hiyo maana ndicho unacholalamikia. Mara nyingi watu huwa tunaona matatizo tuliyonayo ndio makubwa kuliko ya wenzetu.
 
Hakunaga msaada wa watu wa jinsia mbili tofauti ambao hakuna udugu baina yao .

Mwanaume ukianza kumsaidia mwanamke huwa kinafuata kutegwa muwe mahawara.

Wapo wanaume walianza kwa kujifanya kuwasaidia wanawake mwisho wakaangukia kwenye ngono hadi kupelekea ndoa zao kuvunjika na kubaki historia.

Na hiyo huwatokea hata wanaume ambao ni watumishi wa Mungu , wengi wamejikuta wakianguka kwenye uzinzi na uasherati baada ya kuanza kuwasaidia wanawake wenye shida ikiwemo wajane.

Mwanamke skisaidiwa na Mwanaume ambaye si ndugu yake wa damu huyo Mwanaume anayetoa msaada ajiandae kufanya ngono na huyo mwanamke husika ,

Wanawake wanaosaidiwa na wanaume hutoa miili yao kama shukrani kwa wale wanaume walowasaidia,

Na wanawake hujitoa miili yao kingono kwa wanaume wakijua watawashika zaidi hao wanaume na wengine kuwategeshea mimba.

Wanaume msiwachukulie Poa wanawake hata kama akjifanya mkimya kama kondoo lakini moyoni huwa wamejaa hila na uovu mkubwa wa kuangamiza ndoa yako!
 
Tatizo kubwa ni wewe kumsaidia na yeye kushindwa kukusaidia, soma title yako. Hata angekujibu bado ungekuwa na notion hiyo hiyo maana ndicho unacholalamikia. Mara nyingi watu huwa tunaona matatizo tuliyonayo ndio makubwa kuliko ya wenzetu.
Sawa, ngoja nikupe ushindi wa mezani. Itakuwa mimi ndio nina tatizo kwenye mtazamo wangu.
 
Back
Top Bottom