Hapa umeonyesha akili hunaHata kama mbadala haujapatikana, maamuzi aliyochua Kafulila ni sahihi ili kuokoa maisha ya wananchi.
Nimeshajua aina ya mtu ninayejadiliana naye.Hapa umeonyesha akili huna
Kwa hiyo LATRA wamezidiwa akili na mkuu wa Mkoa moja tu kwa akili. Wenyewe wamekaa tu pfisini hawana ubunifu wowote. Siyo ifunjwe litaasisi ambalo halina kazi? Noah ziondolewe barabarani, huwezi kusafirisha abiria kM 150 kutumia Noah na abiria wamebanana, line ya abiria watatu wao wanalazimisha wanne hata huwezi kupumua vizuri. Nauli yao kubwa kishenzi, kwa mfano Arusha-Karatu KM140 nauli sh. 8,000/View attachment 2292276
RC Kafulila apiga marufuku ‘michomoko’ kusafirisha abiria Mkoa wa Simiyu
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu (RC) nchini Tanzania, David Kafulila amepiga marufuku magari madogo maarufu michomoko kusafirisha abiria mkoani humo.
Ni baada ya kuhusika kwenye matukio ya ajali yaliyosababisha vifo vya watu 10 na majeruhi 17 ndani ya siku 12 zilizopita.
Amri ya Kafulila imetolewa leo Jumatano Julai 13, 2022 ikiwa ni siku moja baada ya ajali iliyotokea eneo la Magereza nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu usiku wa kuamkia jana ikihusisha "michomoko" na kusababisha vifo vya watu watano na majeruhi 11.
Wakati majina ya marehemu watano waliofariki kwenye ajali ya Simiyu bado hayajawekwa wazi na waliojeruhiwa ni Elizabeth Nestory (26), Yohana Mwita (22), Sumai Mabula (43), Joseph Masanja (32) na Neema Samson (20).
Wengine ni, Felister Maganda (54), Happy Manyama (23), Oscar Nsolo (47), Stephano Stephene (22) na Joyce Manyama (27) huku majeruhi mmoja ambaye yuko kwenye hali mbaya hajafahamika.
soma pia hii
Ajali hiyo litokea baada ya magari madogo mawili madogo aina ya Toyota pro box na Toyota wish yanayosafirisha abiria kati ya miji wa Bariadi Wilaya ya Bariadi na Lamadi wilayani Busega kugongana uso kwa uso.
Tukio hilo limetokea siku 12 pekee baada ya ajali nyingine iliyohusisha “mchomoko” aina Toyota wish iliyotokea eneo la Luguru Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu na kusababisha vifo vya watu watano na majeruhi watano.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Bariadi yaliko makao makuu ya Mkoa wa Simiyu, Kafulila amesema magari hayo madogo yanafanya shughuli ya kusafirisha abiria kinyume cha sheria na maelekezo ya Serikali kupitia Mamlaka ya Usafirishaji wa ardhini (Latra).
"Wamiliki na waendeshaji wa nigari haya ya michomoko wamepewa maelekezo ya kufuata ili kuwaruhusu waendelee kufanya kazi ya kusafirisha abiria, lakini ni zaidi ya miezi sita sasa hawajatekeleza,” amesema Kafulila
Mkuu huyo wa mkoa amesema kutokatana na ukaidi wa wamiliki hao huku watu wakiendelea kupoteza maisha na kujeruhiwa katika ajali zinazohusisha magari hayo, Serikali inasitisha shughuli za magari hayo ya kusafirisha abiria kwa mujibu wa kifungu cha 25 cha Sheria ya Usafirishaji inayoipa mamlaka ya kufanya hivyo.
Ametumia fursa hiyo kuwaalika wawekezaji katika sekta ya usafirishaji wa abiria kwenda mkoani Simiyu kuwekeza katika usafirishaji salama kwa mujibu wa sheria.
Naye ofisa mfawidhi wa Latra mkoa wa Simiyu, Amaniel Sekulu amesema kwa mujibu wa leseni, magari madogo yanayofahamika kwa jina maarufu ya ‘mchomoko’ yanayosafirisha abiria katika miji mbalimbali mkoani humo yamesajiliwa kama Taxi, akini badala yake, wamiliki wamebadilisha shughuli kwa kusafirisha abiria kinyume cha sheria.
“Magari haya yanatakiwa kusajiliwa, kupakwa rangi, kuandikwa namba za utambulisho ubavuni na kubandika vibao maalum vinavyoonyesha kuwa ni Taxi na zinatakiwa kupakia abiria kwa idadi inayoruhusiwa kisheria,” amesema Sekulu
======================
WAKATI HUOHUO LATRA YAPIGILIA MSUMALI AGIZO LA KAFULILA, MICHOMOKO YOTE KUONDOLEWA BARABARANI NCHI NZIMA!
Baraza la Ushauri la watumiaji wa huduma za usafiri ardhini( LATRA) limetoa tamko kali kuunga mkono maamuzi magumu aliyochukua Mkuu wa Mkoa Simiyu, David Kafulila ya kupiga marufuku gari ndogo zinazotumika kusafirisha abiria maarufu kama michomomoko kuanzia Julai13, 2022.
Kafulila alipiga marufuku gari hizo kuendelea kutumika kutokana na kuwa sababu kuu ya ajali mkoani Simiyu kufuatia gari hizo kutimika kubeba abiria wengi na kukaidi agizo lake la muds mrefu kutaka zitumike kama taxi badala ya kujigeuza daladala kwa kubeba abiria wengi zaidi ya uwezo. " Kwakua kutokana na mwenendo usioridhisha gari hizi zimekuwa chanzo kikubwa cha ajali, na kwakuwa gari hizi zimekaidi maelekezo ya serikali kutaka zifuate taratibu za kujiendesha kama taxi kwa kisingizio kuwa mfumo huo haulipi kibiashara, basi kuanzia leo Julai13, 2022, nasitisha usafiri wa MICHOMOKO mpaka hapo itakapoamuliwa vinginevyo" alisisitiza RC Kafulila.
Katika tamko Lao, LATRA wamesisitiza mikoa wakuu wa mikoa mingine kufuata mfano huo kukabili tatizo la ajali nchini kwani gari hizo sio salama , nihatari kwa usalama wa wananchi kwani zimekuwa chanzo cha ajali maeneo mengi nchini na kuahidi kushirikiana na vyombo vingine ikiwemo jeshi la polisi kuhakikisha inafanyika opareshen nchi nzima
View attachment 2292287View attachment 2292289
RC Kafulila anatumia kifungu cha 25 cha kwenye sheria ya Land Transport Reguratory Act
View attachment 2292293
Nae kamanda wa kikosi cha Usalama barabarani ACP Wilbroad Mtafungwa amekandamizia kuwa sasa Tanzania michomoko basi kwa usalama wa Watanzania na mali zao, msikilize mpaka mwisho huyu Mwamba,
Na ukisoma habari huoni kama sababu ya ajali ni ukaaji mbaya wa dereva au mbanano wa abiria. Uso kwa uso ni ajali inayotokea baada ya bad overtaking, sasa hiyo bad overtake haitokani na aina ya gari, ni maamuzi yasiyo sahihi ya dereva. Kuzuia madereva hawa wasiendeshe michomoko hakuwafunzi kuwa madereva bora, watahamia kwenye mabasi na watafanya overtaking za muundo huohuo, napo sijui mtayazuia mabasi!!Shida ya usafiri ndio inakuwa hivyo abiria wanataka hivyo kutokana na shida ya usafiri na dreva hana shida anasaidia wenye shida wenzie na wameshazoea hizo shida wanajua dereva ataendesha kwa shida lakini watafika kila moja akiomba Mungu wafike salama waendako maana usafiri ngumi hakuna namna.Dereva anavumilia mkao wa abiria na dereva anavumilia mkoa wa abiria sababu kuendesha mkoa huo kwahitaji dereva mvumilivu pia
Unadhani usafiri ungekuwa mzuri nani angekubali kubanana hivyo?
Hayo maamuzi wametoa ni ya kukurupuka
Hiyo inaitwa shida ya usafiri eneo husikaNoah ziondolewe barabarani, huwezi kusafirisha abiria kM 150 kutumia Noah na abiria wamebanana, line ya abiria watatu wao wanalazimisha wanne hata huwezi kupumua vizuri. Nauli yao kubwa kishenzi, kwa mfano Arusha-Karatu KM140 nauli sh. 8,000/
Uchumi wa vituo vya mafuta Simiyu lazima pia ushuke hao michomoko ndio wajaza mafuta wao vituoniRC Kafulila, rejea uamuzi wako, hapo utatesa wananchi na kuchelewesha ukuaji uchumi mkoani kwako. Wape elimu madereva na usimamizi uwe imara.
Mfano nilioutoa magari ni mengi tena sana. Arusha-Karatu kuna mabasi makubwa, kuna Coaster, kuna Hiace. Yapo mpaka mabasi ya kwenda Dar Es Salaam moja kwa moja.Hiyo inaitwa shida ya usafiri eneo husika
Kama usafiri uko vizuri nani atakubali kupanda kwa kubanana ma kilomita yote hayo na nauli ikiwa kubwa hivyo na akiwa Kakaa mkao wa kushindwa hadi kupumua ?
Hapo shida ni kubwa hivyo wakati Noah bado zipo ! Sasa ukiamka kama mkuu wa mkoa na kutaka kuanzia sasa hivi ukasema marufuku kuanzia sasa hivi Noah kuweko watu watapanda punda? Mbadala uko wapi?
Lakini hayakidhi mahitaji ndio maana watu wanabanana kwenye Noah kilomita nyingi kwa nauli kubwaMfano nilioutoa magari ni mengi tena sana. Arusha-Karatu kuna mabasi makubwa, kuna Coaster, kuna Hiace. Yapo mpaka mabasi ya kwenda Dar Es Salaam moja kwa moja.
Unatetea Sana, Pole kwa uwekezajiUchumi wa vituo vya mafuta Simiyu lazima pia ushuke hao michomoko ndio wajaza mafuta wao vituoni
Kafulila na Latra ni economic hitmenUnatetea Sana, Pole kwa uwekezaji
Unafurahi watu kufa kila siku?Kafulila na Latra ni economic hitmen
Wameamua kutumia nafasi zao ku hit economy na business chain za michomoko nchi nzima kwa kisingizio cha ajali za michomoko miwili Simiyu
Maamuzi yao ni ya kupiga Rungu uchumi kitaifa na mzunguko wa pesa kitaifa uliokuwa ukichochewa na michomoko.
Kifupi Latra na Kafulila ni wahujumu uchumi kupitia maamuzi yao
Wawekezaji wakiondoka mnaanza kubweka ohhh tutangaze mkoa wetu tuvutie wawekezaji wakija mnaleta vituko na maamuzi ya ajabu ajabu ya kuumiza wawekezaji. Halafu mnaanza kuhangaisha mama Samia akatafute wawekezaji nje watakaoongeza ajira .Huku mnaua uwekezaji wa watu wa ndani waliotoa kuwekeza vituo vya mafuta ,michomoko nk na kutoa ajira zinazoongeza mzunguko wa pesa na kuchangamsha uchumi maeneo yenu na kuongeza Mapato ya kodi kwenye huo mzunguko unaosaidia hata mishahara ya wafanyakazi wa Serikali kupandaUnatetea Sana, Pole kwa uwekezaji
Kabla ya ajali alikuwa hayaoni hayo magari?Akizungumza na waandishi wa habari mjini Bariadi yaliko makao makuu ya Mkoa wa Simiyu, Kafulila amesema magari hayo madogo yanafanya shughuli ya kusafirisha abiria kinyume cha sheria na maelekezo ya Serikali kupitia Mamlaka ya Usafirishaji wa ardhini (Latra).
Ajali kama hizo kila siku hutokea? Acha uongo.Unafurahi watu kufa kila siku?
Kazi ya michomoko ni Kuua watu? Akili wewe hazimo gombea jimbo ndio utawajua michomoko ni akina naniPole Sana YEHODAYA kwa kuwekeza kwenye ' mchomoko ' ili kuua watu
Acha ujinga wako,Kazi ya michomoko ni Kuua watu? Akili wewe hazimo gombea jimbo ndio utawajua michomoko ni akina nani
Kafulila ana mpango wa kugombea ubunge 2025 mwambieni anasubiriwa kwa hamu atawajua michomoko ni akina nani.Abiria wapenda michomoko na wamiliki watampa jibu lake hata akiteuliwa na Chama .
Hii issue sio ndogo .Kama Kafulila anavyodhani.Maamuzi yake na Latra yanachafua Serikali ,na Chama na Mama Samia nchi nzima
Nchi nzima michomoko iligongana hadi marufuku itolewe nchi nzima,? Hata Simiyu tu haikuwa sahihi kupiga marufuku mkoa mzima.Kila mtu anatakiwa kubeba mzigo wake .Huwezi bebesha zigo la michomoko miwili ukabebesha michomoko mkoa wote au nchi yoteAcha ujinga wako,
Chama kinataka watu wafe?
Rais anataka watu wafe?