Uchaguzi 2020 Lema: Msafara wa mgombea Urais, Tundu Lissu washambuliwa vibaya katika Ofisi ya CHADEMA Wilayani Hai, Kilimanjaro

Uchaguzi 2020 Lema: Msafara wa mgombea Urais, Tundu Lissu washambuliwa vibaya katika Ofisi ya CHADEMA Wilayani Hai, Kilimanjaro

Yaani cha kushangaza kuna watu hapa watatetea waleta fujo, wachoma ofisi, wavamiaji. Kama tulivyosema ukiwapata watu kwenye mioyo hakuna wa kuzuia. Wanatengeneza mazingira ya fujo halafu wasingizie upinzani!!!

Mbowe alipovunjika mguu alisingizia nini?Wako watu wana akili za kusahau kama kuku broilers.
Huyo kijana alieuliwa wako hao ambao wamekamatwa tayari wengine wataingia kwenye kesi ya maauji, wahanga wa hadaa za kisiasa. Lissu na genge lake wanafurahia mradi wa kesi mwingine huo.
 
Mbowe alipovunjika mguu alisingizia nini?Wako watu wana akili za kusahau kama kuku broilers.
Huyo kijana alieuliwa wako hao ambao wamekamatwa tayari wengine wataingia kwenye kesi ya maauji, wahanga wa hadaa za kisiasa. Lissu na genge lake wanafurahia mradi wa kesi mwingine huo.

Yaani watu wafurahie kupigwa mawe, kuchomewa ofisi, kupigwa risasi, kuvunjwa miguu inalekea tuko Dunia tofauti. Hapa Hitler kuna wajinga walikuwa wanasema kuchoma wayahudi kule ni sawa
 
Hao ni wapinzani tu. Kwa nini iwe Hai?? Tumia ubongo wako vizuri. Kwa nini kwenye jimbo la Mwenyekiti unataka kutuaminisha kuwa Lissu hakjbaliki kwenye jimbo la Mbowe??

Kuna video clip u tube wakati Lissu akihutubia Babati/Karatu leo kuhusu kuchomwa kwa ofisi Arusha. Akiwa anawapa taarifa wafuasi wa Arusha kwamba wajiandae mkutano utafanyika hapo ofisi ilipochomwa. Mchukua video alinasa picha ya Mbowe na Nyalandu wakimcheka Lissu kiana flani hivi halafu akahamisha kamera, fuatilia utaona. Sijui kama mkutano ulifanyika kwenye hiyo ofisi au la?
 
Hivi huyo Igo sirii Andakava hatuwezi kuwatuma vijana wa kanda maalum watatu wamle kiboga? Maana naona anafanya mambo ya kishenzi sana ilitakiwa atatuliwe rinda akili imkae sawa.
 
Yaani watu wafurahie kupigwa mawe, kuchomewa ofisi, kupigwa risasi, kuvunjwa miguu inalekea tuko Dunia tofauti. Hapa Hitler kuna wajinga walikuwa wanasema kuchoma wayahudi kule ni sawa

Hivi unafikiri Mbowe angekubali aibu ya kuwa alivunjika mguu akiwa kalewa? Hivi Mbowe/Nyalandu wanahiari zao Lissu kuwa mgombea wa urais ama ni mazingira yame lazimisha hawana budi. Hekima na akili ya kutafakari ni karama za Mungu na tunatofautiana.
 
Aliyekuwa Mbunge Arusha Mjini, Godbless Lema kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Twitter amesema msafara wa Tundu Lissu umevamiwa katika Ofisi za Chama hicho Wilayani Hai

Amesema "Msafara wa mgombea Urais Mh Tundu Lissu umevamiwa na kushambuliwa vibaya katika ofisi ya CHADEMA HAI,magari yame haribiwa. Mgombea Uraisi na Team yake wako salama. Polisi wako lakini wana shuhudia, mkutano umevunjika. Taarifa kamili kuwajia"

Hilo tatizo linasababishwa na mkuu Wa wilaya polisi wanaangalia wahuni walio pangwa wakirusha mawe je hao waupande mwingine wakijibu itakuweje
 
Kuna video clip u tube wakati Lissu akihutubia Babati/Karatu leo kuhusu kuchomwa kwa ofisi Arusha. Akiwa anawapa taatifa wafuasi wa Atusha kwamba wajiandae mkutano utafanyika hapo ofisi ilipochomwa. Mchukua video alinasa picha ya Mbowe na Nyalandy wakimcheka Lissu kiana flani hivi halafu akahamisha kamera, fuatilia utaona. Sijui kama mkutano ulifanyika kwenye hiyo ofisi au la?
Channel Gani hiy
 
Kwani yule waliedai ameficha "lpg"kiunoni alishindwa kuitumia?
 
Wewe mlevi hata kupiga kura huwezi hata hukujiandikisha!!
Hodiiiii
JamiiForums-561822830_720x720.jpg
 
Aliyekuwa Mbunge Arusha Mjini, Godbless Lema kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Twitter amesema msafara wa Tundu Lissu umevamiwa katika Ofisi za Chama hicho Wilayani Hai

Amesema "Msafara wa mgombea Urais Mh Tundu Lissu umevamiwa na kushambuliwa vibaya katika ofisi ya CHADEMA HAI,magari yame haribiwa. Mgombea Uraisi na Team yake wako salama. Polisi wako lakini wana shuhudia, mkutano umevunjika. Taarifa kamili kuwajia"

Bila hata kapicha tutakuaminije
 
U tube on line TV sina hakika na channel leo kama saa5 asubuhi.
Channel zipo nyingi zenye kuonesha hayo matukio ya lisu ni nguvu kukuta ni ipikama wewe mwenyew umeshindwa kutaja hiyo channel umeshapoteza point hapa
 
Tukio la uvamizi wa msafara wa Lisu linatia kinyaa na limazidi kumchafua Magufuli na serikali yake.

Tukio hili linaongeza chuki na hasira kwa watanzania wanaoamini kuwa Magufuli ni dikteta, hana utu, mbabe na mshari.

Tukio hili linaongeza orodha ya matukio mabaya yaliyowahi kutokea nchi hii kama:-
Kupotea kwa Azory Gwanda na Ben Saanane, kushambuliwa kwa risasi kwa kamanda Tundu Lisu, e.t.c
Na wengine wengi.

Matukio haya yanazidi kumchafua JPM na serikali yake mioyoni na akilini mwa wapiga kura. Na hivyo wananchi wanamuona kuwa anaogopa kupambana naLisu jukwaani.

Kuiepuka balaa hii kipindi hiki Cha uchaguzi, Magufuli aachane na tabia ya kumuona Lisu kuwa ni adui. Ajielekeze kweye sera na ahadi zake.
 
Back
Top Bottom