Uchaguzi 2020 Lissu adai kucheleweshwa KIA makusudi na TCAA

Uchaguzi 2020 Lissu adai kucheleweshwa KIA makusudi na TCAA

Once a mistake, twice a habit

Ni wafuasi wa CDM ndio wanaweza amini uongo wa Lissu. Kuna rubani anaweza ingia angani bila ya kuwa na mawasiliano.

Yaani rubani arushe ndege bila ya mamlaka ya anga labda kama anataka kufutiwa leseni yake.

Hakuna cha kucheleweshwa na mamlaka ya anga wala nini alikuwa anavuta upepo kama watu wamejaa kwanza uwanjani ndio aamue aende au aukache mkutano.

Sijui yukoje huyu mtu yaani anawadharau kweli wafuasi wa CDM mtu ana uongo wa kishamba kweli halafu unakuta mijitu inatetea tu.
Kweli wewe ni Kilaza
 
Hatuwezi kuishi kwenye nchi ya kipuuzi namna hii. Yaaani binadamu mwenzetu anaonewa kiasi hiki tena waziwazi na wala tusichukue hatua...
Utazilinda ukiwa na nani mzee?😂😂😂 Huyo unaetegemea kulinda nae anakusubiria kwake akiwa katega Channel ten
 
Sasa kibali hajapewa analazimisha kuruka,muhimu jeshi liwe makini akilazisha kurusha ipopolewe tu na kombora.
Hii nchi ina safari ndefu sana kama watu ndio kama wewe wanaodhani uhai wa wenzao hauna maana kwa sababu tu ya madaraka
 
Hatuwezi kuishi kwenye nchi ya kipuuzi namna hii. Yaaani binadamu mwenzetu anaonewa kiasi hiki tena waziwazi na wala tusichukue hatua.

Walimpiga risasi wakitaka kumuua, akapona mauti ila wakamnyima matibabu, akapona kabis wakamvua ubunge na kukataa kumlipa hata kiinua mgongo kwa kipindi alichotumikia.

Sasa amegombea uraisi hawaachi figisu, mikoa ya kusini wamemzuia kufanya mikutano zaidi ya 10, na Mkoa wa Pwani pia, kisa magufuli ameshindwa kufanya kampeni kusini.

Sasa leo anakuja kufunga kampeni Dar wanamletea figisu tena kwa makusudi. Sasa tunasema imetosha!!!!

Kesho kwa hasira tunaenda kupiga kura nyingi kwa Lissu na tutalizilinda hakika kwa gharama ya damu zetu. Hata tukifa ila historia itatukumbuka.
Nazidi kukushauri upunguze munkari ndugu yangu. Umelishwa uongo mwingi na bahati mbaya unazikubali kama zilivyo. Hayo yote uliyoyaeleza hapo juu hazina hata chembe ndogo ya ukweli. Nazidi kukushauri, tunakupenda kama mtanzania mwenzetu punguza munkari. Pressure itakuuwa bure. Lingine nakushauri uwe unasemea nafsi yako na siyo kutumia neno tuta.....Ni wewe mwenyewe utakayemwaga damu yako. Siyo watanzania wengine.
 
Back
Top Bottom