Lissu: Hakuna Katiba Mpya, hakuna uchaguzi

Lissu: Hakuna Katiba Mpya, hakuna uchaguzi

Hakuongelewi kususia uchaguzi. Kunaongelewa kutokuwapo uchaguzi.

Kulikoni kuwa malaika wa kushindwa (angel of doom)? Kwanini tusiwekeze kwenye kuuzuia uchaguzi? Kama wewe huwezi si uwaachie walilodhamiria kuusimamisha?

Kwani ukombozi unahitaji watu wangapi ndugu?

View attachment 2798090

Hata kwenye jeshi la Gideon ilikuwa hivyo:

..maji kwa ulimi, kama vile mbwa anywavyo, wale wote wapigao magoti ili kunywa wakipeleka mikono yao vinywani mwao, waweke upande mwingine.”

Waliokuwa wengi zaidi ndiyo walikuwa hawafai!
Haya yote nayaelewa kabisa. Lakini mimi (kwa masikitiko makubwa) nakupa hali halisi. Mimi naona ni bora hata kushiriki uchaguzi huku ukitegemea pengine wananchi wanaweza ku-react kura zitakapoibiwa ili tupate pa kuanzia. Kipindi cha kupiga kura watu wanakuwa wamejikusanya makundi makundi hivyo ni rahisi kidogo kuwa-mobilize.
 
Ni ujinga uliopitiliza kuamini katiba mpya itakutoa hapo ulipo, katiba mpya inaweza kuja ikawa na interest za kisiasa tu lakini isibadilishe chochote kwenye maisha ya watu,
Pull up your sox! Watu wanasema katiba mpya yenye input zenye manufaa kwa raia. Kwa kifupi unaposikia katiba mpya = katiba bora. Upo?
 
Akiyasema haya Tundu Lissu, yanaaminika zaidi ya mtu mwingine yeyote ndani ya CHADEMA sasa hivi.

CCM hawataki mabadiliko yoyote, kwa hiyo njia iliyobaki ni hii moja tu.
 
Akiyasema haya Tundu Lissu, yanaaminika zaidi ya mtu mwingine yeyote ndani ya CHADEMA sasa hivi.

CCM hawataki mabadiliko yoyote, kwa hiyo njia iliyobaki ni hii moja tu.
Kalamu unaamini uchaguzi unaweza usiwepo kwa sababu kuna watu hawataki uwepo kwa sababu hakuna katiba mpya?
 
Wakilazimisha uchaguzi ufanyike,

Njia pekee ni kupiga kura ya WAZI mabarabarani na Viwanjani.

Hapo ndipo hapatakuwa na kura fake au goli la mkono.

It's now or never.
 
Watashiriki uchaguzi upi usiokuwapo? Inawauma mno kusikia uchaguzi hamna? Kwani mlishakamilisha mipango yote ya wizi?
Unahisi CHADEMA wakisusa ndio hakutakuwa na uchaguzi? Yan katika vyama 20+ chama kimoja kugoma ndio kutafuta uchaguzi? Jaribuni muone kama utakuwepo au hutakuwepo
 
Kalamu unaamini uchaguzi unaweza usiwepo kwa sababu kuna watu hawataki uwepo kwa sababu hakuna katiba mpya?
Una mashaka kuhusu Hilo?

BUSARA za viongozi wa CDM na watumishi wa Mungu kupooza mambo ndo umetufikisha hapa.

Bt 2025 hapatakuwa na sababu ya msingi kuvunilia utawala dhalimu unaobadili na kupotoa HAKI, kumpa ushindi asosyahili,

Halikubaliki hili.
 
Wakilazimisha uchaguzi ufanyike,

Njia pekee ni kupiga kura ya WAZI mabarabarani na Viwanjani.

Hapo ndipo hapatakuwa na kura fake au goli la mkono.

It's now or never.
Mkuu, kuna baadhi ya vitu usiviangalie kwa jicho moja, angalia kwa macho yote mawili
 
Mkuu, kuna baadhi ya vitu usiviangalie kwa jicho moja, angalia kwa macho yote mawili
Hamwezi kuwafanya watz zaidi ya ml 60 makondoo Kila uchaguzi.

Mnapata wapi uhalali kuiba uchaguzi,

Ikiwa mna Nia njema kwann hamtaki Tume huru ambayo Haina mkono wa Rais?

Kwann kutulazimisha kututawala kimabavu ilhali wananchi hawawataki?
 
Kalamu unaamini uchaguzi unaweza usiwepo kwa sababu kuna watu hawataki uwepo kwa sababu hakuna katiba mpya?
Swali lako sijalielewa mkuu 'macho'.

Ngoja nijieleze kidogo ili unielewe ninaposimamia:

Uwepo wa Katiba Mpya katika muda uliopo kabla ya uchaguzi, sasa hivi haiwezekani. Hili limesababibshwa na CCM hao hao, wanaodai sasa kwamba inahitajika zaidi ya miaka mitatu kufundisha watu!

Kwa hiyo Katiba Mpya Haiwezekani.

Marekebisho ya sheria je zinazohusiana na uchaguzi huru?
1. Tume Huru ya uchaguzi

2. Matokeo kuhojiwa Mahakamani na mambo mengineyo.
haya nayo CCM sasa hivi wanapiga danadana ile ile kama ya Katiba Mpya.
Kiufupi ni kwamba CCM sasa hivi wanayofanya ni kutengeneza mazingira ya kuwabakisha madarakani.

Kwa hiyo, kinachotakiwa sasa hivi ni kwa wananchi kuandaliwa vyema kuzijua mbinu wanazofanya CCM. Hata uchaguzi ukifanyika katika mazingira mabovu, ijulikane wazi kwa wananchi, na wawe tayari kukabiliana na hujuma hizo.
Hii ndiyo kazi inayotakiwa kuwa inafanyika huko ndani ya CHADEMA.

Kuzuia uchaguzi inawezekana sana iwapo maandalizi mahsusi yatafanyika, na tutachangia mbinu za kuyawezesha hayo ndani ya sheria zetu.

CCM ni wahalifu. Wavunja sheria. Ni lazima pawepo na njia za kuwazuia kufanya uhalifu huo.

Dola haipo kwa minajiri ya kutumika kuvunja sheria.
 
Mkuu, kuna baadhi ya vitu usiviangalie kwa jicho moja, angalia kwa macho yote mawili
Ikiwa hii ni Nchi ya kidemokrasia,

Ni shart Sanduku la kura liheshimiwe.

Ikiwa hakuna HAKI katika kuchagua viongozi wanaotakiwa na wananchi,

Futeni vyama vyote vya upinzani na mtangaze kurudi mfumo wa chama kimoja.
 
Hamwezi kuwafanya watz zaidi ya ml 60 makondoo Kila uchaguzi.

Mbatia wapi uhalali kuiba uchaguzi,

Ikiwa mna Nia njema kwann hamtaki Tume huru ambayo Haina mkono wa Rais?

Kwann kutulazimisha kututawala kimabavu ilhali wananchi hawawataki?
Mimi sio CCM, halafu nitajie uchaguzi mmoja tu ambao CHADEMA unahisi iliporwa kwa hio ilibidi ishinde ?

Ule wa 2020 magu aliamua tu kuwakomoa CHADEMA, ila Lissu hakuwa na uwezo wowote ule wa kupata kura japo 25% hata tungepiga kura kwa majina na hadharani
 
Ikiwa hii ni Nchi ya kidemokrasia,

Ni shart Sanduku la kura liheshimiwe.

Ikiwa hakuna HAKI katika kuchagua viongozi wanaotakiwa na wananchi,

Futeni vyama vyote vya upinzani na mtangaze kurudi mfumo wa chama kimoja.
Mkuu, wew piga kelele ila jua chadema hawana ubavu wa kususia uchaguzi hapa TZ, wakisusa watakaa juu ya mawe hadi wakose nguo, na hawapo tayari
 
Swali lako sijalielewa mkuu 'macho'.

Ngoja nijieleze kidogo ili unielewe ninaposimamia:

Uwepo wa Katiba Mpya katika muda uliopo kabla ya uchaguzi, sasa hivi haiwezekani. Hili limesababibshwa na CCM hao hao, wanaodai sasa kwamba inahitajika zaidi ya miaka mitatu kufundisha watu!

Kwa hiyo Katiba Mpya Haiwezekani.

Marekebisho ya sheria je zinazohusiana na uchaguzi huru?
1. Tume Huru ya uchaguzi

2. Matokeo kuhojiwa Mahakamani na mambo mengineyo.
haya nayo CCM sasa hivi wanapiga danadana ile ile kama ya Katiba Mpya.
Kiufupi ni kwamba CCM sasa hivi wanayofanya ni kutengeneza mazingira ya kuwabakisha madarakani.

Kwa hiyo, kinachotakiwa sasa hivi ni kwa wananchi kuandaliwa vyema kuzijua mbinu wanazofanya CCM. Hata uchaguzi ukifanyika katika mazingira mabovu, ijulikane wazi kwa wananchi, na wawe tayari kukabiliana na hujuma hizo.
Hii ndiyo kazi inayotakiwa kuwa inafanyika huko ndani ya CHADEMA.

Kuzuia uchaguzi inawezekana sana iwapo maandalizi mahsusi yatafanyika, na tutachangia mbinu za kuyawezesha hayo ndani ya sheria zetu.

CCM ni wahalifu. Wavunja sheria. Ni lazima pawepo na njia za kuwazuia kufanya uhalifu huo.

Dola haipo kwa minajiri ya kutumika kuvunja sheria.
Asante sana. Nasimama na maelezo yako. Ila tu hili la kuzuia uchaguzi ndiyo nina shaka. Nina shaka kwani CCM hawahitaji uchaguzi ufanyike ndiyo waseme wameshinda. Nakuhakikisha hata kama wapiga kura wakisusia vituo vyote, CCM watadai upigaji kura umeenda vizuri sana na wameshinda kwa asilimia 80. Njia iliyopo ambayo naona ni nzuri ni kama uliyoelezea... CHADEMA waanze kuandaa watu kuanzia sasa hivi...... kukiwasha iwapo CCM wataleta longolongo.
 
Hivi bado yupo ulaya🤣🤣🤣
Muacheni aendelee kuota ndoto za mchana
 
Mkuu, wew piga kelele ila jua chadema hawana ubavu wa kususia uchaguzi hapa TZ, wakisusa watakaa juu ya mawe hadi wakose nguo, na hawapo tayari
Maandamano ya Nov 9 yatatupa kufanya tafakuri vizuri.
 
Back
Top Bottom