Pre GE2025 Lissu: Sijui ilikuwaje CHADEMA tukamualika Rais Samia, ila mbeleni tutaelezana

Pre GE2025 Lissu: Sijui ilikuwaje CHADEMA tukamualika Rais Samia, ila mbeleni tutaelezana

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wenyewe huwa wanaona wanatetea "status quo" kumbe siyo Kila wakati ni wa vita.

Hapa Iringa kuna Siasa zinageuzwa za kitaifa kumbe ni za kwetu sisi wenyewe wanyalukolo.

Mwembetogwa mara kadhaa imetumika kuharibu urari wa Siasa za Iringa.

Hapo alilengwa Msigwa ambaye wapinzani wake ndiyo wanamtuhumu kutumia Hela za mama Abdullah.

Ukiwaambia walete ushahidi HAWANA.
Katika maeneo ambayo Chadema ina Nguvu za Asili ni Iringa, Mbeya, Arusha, Mara, Morogoro na Mwanza

Na CCM inaiangalia Mikoa hii kwa jicho la 3

Kila nikikumbuka kipute Cha Mwalimu wangu Kibasa wa NCCR mageuzi 1995 sionagi aibu kuufagilia Upinzani wa Iringa Mjini

Rip Gervas Kalolo
 
Nadhani analalamika kwa kile kinachotokea baada ya kualikwa Mama.
 
Lakini pia hiki ni kitu cha ajabu kidogo ni sawa na Simba wawaalike Yanga kwenye mkutano wao mkuu unajadili jinsi ya kuchukua ubingwa.
Mimi nafikiri ni lazima kuelewa muktadha kwanza ndio maana nikaanza na utangulizi jinsi ya siasa za nchi hii zilivyokua kabla ya Samia kuingia madarakani, kulikuwa na chuki na uhasama mkubwa sana hadi watu kukimbia nchi kwa kuhofia kuuawa,
Ili kuondoa hizo chuki na uhasama, ndio ikaja maridhiano, kuleta tena watanzania pamoja

Na ule haukuwa mkutano wa kupanga chochote ilikuwa ni siku ya wanawake duniani, sio kupanga kushinda uchaguzi

Sasa kama wapinzani wanataka siasa za uadui na vita, wahanga wakubwa watakuwa ni wao, sio CCM, CCM wana dola na wawaweza kufanya chochote wapinzani bila kuchukuliwa hatua yoyote
 
Sasa Tundu Lissu anataka turudi kwenye zile siasa za chuki, kwenye mikutano yake huko Iringa anahoji kwa nini Samia alialikwa kwenye mkutano wa Chadema

Kunielewa hebu turudi kidogo nyuma kipindi cha Magufuli mambo yalivyokuwa

Kipindi cha Magufuli, siasa za CCM vs Chadema, zilikuwa ni siasa extreme sana, CCM na Chadema ilikuwa kama makundi ya Wahutu na Watusti kule Rwanda kabla ya mauaji ya kimbari

Kuna kipindi Wabunge wa CCM walipewa onyo kali kumtembelea mbunge mwenzao Lema gerezani alipowekwa rumande kwa miezi kadhaa
Wabunge wa CCM wakapigwa marufuku kumtembelea Lissu hospitalini alipopigwa risasi, na Lazaro Nyalandu mbunge pekee wa CCM aliyemtembelea Lissu aliingia matatizoni na chama chake kwa kufanya jambo hilo hadi ikambidi kuhama

Wananchi nao wakaambiwa waziwazi hawatatatuliwa shida zao kwa sababu walichagua wabunge wa upinzani
Bado kulikuwa na visa vingi vya kesi za kisiasa, kutekwa, mauaji hadi wapinzani akiwemo Lissu na Lema kukimbia nchi.

Fast Forward leo hii, Rais Samia pamoja na mapungufu yake ameondoa siasa hizo za extremism
Samia ameweka mbele kuwa sisi wote ni Watanzania kwanza kabla ya kuwa CCM ama Upinzani
Ndio maana hata Samia alialikwa kwenye mkutano wa Chadema akahudhuria, alikutana na viongozi wa Chadema, kufuta kesi, waliokuwa wamekimbia wakaambiwa warudi, mikutano imeruhusiwa na mengine mengi

Sasa Tundu Lissu anataka turudi kwenye zile siasa za chuki, kwenye mikutano yake huko Iringa anahoji kwa nini Samia alialikwa kwenye mkutano wa Chadema
Anasema pia anakusudia kumshtaki Samia kwa kuweka picha aliyopiga na viongozi wa Chadema kwenye bango

Hizi siasa za kuonana maadui kutokana tu na tofauti ya vyama vyetu tukirudi tena huko waathirika wakubwa ni Chadema, sio CCM, actually kundi kubwa la CCM linatamani turudi huko kwa sababu wao wanaweza kufanya lolote kwa upinzani bila kufanywa chochote kama tulivyoona kipindi cha Magufuli

Ni muda sasa viongozi wa Chadema wakamuonya Tundu Lissu
 
Lisu awe makini sana na mwenyekiti wake maana huyo ndio anaendekeza hizo pesa chafu za ccm.
ila pesa na mabwenyenye wa ng'ambo ni tamu na zinafanya kibaraka awe na kiburi sana 🐒
 
ila pesa na mabwenyenye wa ng'ambo ni tamu na zinafanya kibaraka awe na kiburi sana 🐒
Hizo pesa za wazungu hakuna asiyezipata, kuanzia serekali mpaka wananchi wake. Kama kupata hela ya mzungu ni ukibaraka na kiburi, basi serekali ndio kibaraka namba moja kwenye hilo.
 
Hizo pesa za wazungu hakuna asiyezipata, kuanzia serekali mpaka wananchi wake. Kama kupata hela ya mzungu ni ukibaraka na kiburi, basi serekali ndio kibaraka namba moja kwenye hilo.
sawa 🐒
 
1. Jamii yoyote yenye kubagaza wasomi wake ni jamii ya ki wenda wazimu.

Ule Moto wa nyika wa migomo Marekani, wapindukia Canada!

2. Wasomi ni tunu na ndiyo pekee watakao tukomboa!

3. Wajinga, wapumbavu wenye macho kwenye maokoto, ubunge na udiwani ni Laana!

Migomo vyuo vikuu imeangusha serikali; Marekani siyo kisiwa, la sasa halimwachi salama!

4. Haipo shaka, Proved, Zawadini Lissu ana wakati mgumu sana Chadema.

5. Lissu huru asingeacha kumpa Biden vidonge vyake lakini siyo hizi mbuzi zingine!
Kumezuka huu mtindo ambao kwangu nauona ni mbaya, wa kubeza vyuo vikuu, hasa UDSM. Ni ajabu jambo hili kutokea kwenye jamii ya wastaarabu. Huenda wanaofanya hivi sio alumni wa Mlimani. Natamani vyuo vikuu vipewe heshima yake.

Huwa najiuliza hivi chuo kikuu alichosoma Prof. Shivji na baadae kufundisha hapo kinakuwa jaa? -Kiswahili kingine cha neno 'jalala. Hivi Chuo Kikuu alichofundisha Prof. Goran Hyden kinakuwa jaa? Hii jamii yetu inaelekea wapi?
 
Tanzania INATOKANA na Muungano wa Nchi mbili, inasema Katiba ya Zanzibar 1984

Haisemi " ilitokana"

Hivyo zipo Nchi 2 na Katiba 2 Ndio sababu DP World anaitazama Nchi ya Zanzibar akiwa mbali 😂😂😂
Mzee hii ni ishu nyingine ambayo haikuwa kwenye mada yangu, mada yangu ililenga umoja wa Watanzania katika vyama tofauti vya siasa na sio mambo ya Muungano
 
Nani kakuambia Marekani ndio role model wetu kwenye kila kitu? Marekani wanaruhusu ushoga, so turuhusu ushoga kisa Marekani anaruhusu?

Marekani kulishatokea Rais kichaa kama Magufuli na kuvuruga nchi vile? Nchi ikivurugwa kwa misingi ya vyama kama alivyofanya Magufuli unadhani haihitaji kuileta pamoja tena?
Magufuli alivuruga vyama kwa kufanya kazi zaidi ya maneno ya wanasiasa kwa hiyo wakabaki hawana hoja zaidi ya kuleta visingizio vya demokrasia
 
Aisee sikujua Tundu Lissu ana chuki hivi hadi awamu hii ya Samia....Kwa hiyo Samia kualikwa kwenye mkutano wa Chadema kuna na akahudhuria ameona ni shida kubwa, anataka zile siasa za Kihutu na Kitutsi na sio siasa za kuona CCM na Chadema wote ni watanzania
Haya mambo tuliyaonja kidogo kipindi cha Magufuli na Lissu alikuwa mhanga, ila ndio anayatamani?
yule maza ni kigeugeu kwa masilahi yake binafsi haaminiki hafai
 
Nani kakuambia Marekani ndio role model wetu kwenye kila kitu? Marekani wanaruhusu ushoga, so turuhusu ushoga kisa Marekani anaruhusu?

Marekani kulishatokea Rais kichaa kama Magufuli na kuvuruga nchi vile? Nchi ikivurugwa kwa misingi ya vyama kama alivyofanya Magufuli unadhani haihitaji kuileta pamoja tena?

..mtaruhusu ushoga muda si mrefu.

..hamjasikia kuna anayetuhumiwa usagaji na ana madaraka makubwa?
 
Back
Top Bottom