Maafisa uhamiaji Walivyomtesa mtuhumiwa, Je, Sheria inawaruhusu?

Maafisa uhamiaji Walivyomtesa mtuhumiwa, Je, Sheria inawaruhusu?

Hii imekaa vizuri sana, wapo watu wameanza kudharau mamlaka za serikali kisa tu JPM hayupo. Huyu Kama ameweza kuingia ofisi nyeti hivyo nakudanganya eti anatoka TAKUKURU ameshadhulumu watu wangapi? Yawezekana huyu mtu ni jambaza au muhalifu ni vyema tukapata taarifa rasmi.

Kuingia kwenye vyombo Kama TAKUKURU ukijua siyo mtumishi wa chombo hicho then utegemee kutoka salama hicho chombo kitakuwa kimekufa.

Hawa watu ndiyo wanaotuibia kwa sms za namba zisizofahamika. Na wakikukamata usiku ndo utajua haki za binadamu au la.

Vibaka wamezagaa kila kona imefika wakati Sasa wanajitutumia Hadi kwenye vyombo vya dola, no. Vyombo vyetu vijiimarishe kuwashughulikia Hawa watu la sivyo wakiruhusiwa kutetewa tutawapa kiburi.

Mtu hata bia haishuki kisa vibaka Kama Hawa, juzi wamepiga mtu mbezi mara kituo Cha mafuta wamenyang'anya silaha......kwanini haya yatokee Kama siyo kujaribu nguvu ya utawala mpya
Halafu eti Mhaya! Ametudhalilisha sana Wahaya. Hata kama amedhalilishwa ni malipizi tosha kabisa kwa kutudhalilisha Wahaya!
 
Mpaka sasa sielewi watu wanatetea nini humu, yaani mtu uingie sehemu jeshini kwa kusudi la kuwatapeli wakuumbue halafu utegemee uletewe chai kwa birika....kuna nadharia za sheria na uhalsia wa mambo, hapo unapaswa usalimu amri na kushukuru ukitoka mzima. Hao wote huwa wamepitia mafunzo ya uwenda wazimu ambayo huwafanya wawe kama machizi.

Tena hawa wanaonekana wastaarab maana wanarekodi wenyewe, maana kwamba jamaa yuko sehemu ndani ya majengo yao sio nje kwenye kandamnasi, hapo ukijifanya komando na kuwakaidi wanaweza wakakufanya chochote na kufuta video ujifie mbele....

kuna watu wajasiri sana, unatoka zako kitaani na kwenda kutapeli jeshini....hehehehe!!! Bangi haijawahi kumuacha mtu salama.
Uhamiaji ni jeshi?
 
Punguza upumbavu wa kujifanya una huruma,Huwezi kuidharau mamlaka zetu kwa upuuzi kama huu.Mijitu kama wewe mnatakiwa kupata elimu kwa zawadi hiyo hiyo unayoikosoa,Idiot
Unasema hivyo kwaa sababu siyo wewe unayefanyiwa hayo - si mtoto wako, si mfanyakazi au mfanyabiashara mwenzako, si rafiki yako wala ndugu yako. Hakuna kitu kibaya kama kujichukulia sheria mkononi wakati serikali imeweka utaratibu wa kufanya kwa watuhumiwa wa uhalifu. Maana kwa mawazo yako, ukiwa mjini na askari wanamtafuta mhalifu na wakimfananisha na wewe upate kichapo hapo, uviringishwe chini kwenye sehemu rough na pengine kwenye maji machafu au tu uadhibiwe kwa namna yoyote ile - maana hiyo ndiyo kujichukulia sheria mkononi. Matendo kama hayo ndiyo unayopenda wewe. Ngoja niwe idiot, lakini Mungu anakuona.
 
Hapa ndipo utaujua Unafiki wa Watanzania. Mpuuzi aliyedanganya na kutaka Kutapeli anaonewa Huruma na Kutetewa ila wanaomfundisha Adabu kwa Kumpa Adhabu wanaonekana ni Maadui na Makatili.

Tena hizo Adhabu ni kama vile naona Wamemdekeza na Kumuonea tu Huruma ila huyo alitakiwa apewe Adhabu Kali hata inayokaribia Kuichungulia Kaburi ili akome na iwe Fundisho kwa Wapuuzi wengine wa Mfano wake.

Ninawapongeza waliompa Drill hiyo.
Sheria mkononi inakubalika wapi?
 
Hapa ndipo utaujua Unafiki wa Watanzania. Mpuuzi aliyedanganya na kutaka Kutapeli anaonewa Huruma na Kutetewa ila wanaomfundisha Adabu kwa Kumpa Adhabu wanaonekana ni Maadui na Makatili.

Tena hizo Adhabu ni kama vile naona Wamemdekeza na Kumuonea tu Huruma ila huyo alitakiwa apewe Adhabu Kali hata inayokaribia Kuichungulia Kaburi ili akome na iwe Fundisho kwa Wapuuzi wengine wa Mfano wake.

Ninawapongeza waliompa Drill hiyo.
Sheria mkononi inakubalika wapi?
 
Ni suala la mida tu,anapewa Mkuu wa Uhamiaji na Waziri wake pengine isizidi wiki kama hawakuchukua hatua kali basi wajue wanakwenda na maji. Sina zaidi.
Kadhia iliyotokea haina nafasi kwa Raisi aliepo,pale anahisi ni kama mwanawe na anakaa akijiuliza kwanini wasimkamate ? Mateso kama hayo yametokea Zanzibar miezi michache iliyopita,polisi wote waliohusika katika aina hio ya mateso katika nchi ya walio huru,wote wapo ndani na kesi inaendelea,kwa ufupi hawatopi. Na Hawa maofisa wa uhamiaji ni aibu na wanamuhatarishia Raisi juu ya usimamizi wa madaraka yake na kuona haki inatendeka, Kuchukua kideo na kuirusha ni kumpima ? Ni Kumharibia ? Ni kumsaboteji ?
Uhamiaji wamefanya jambo la kipumbavu sn
 
We uliona mateso pale zaidi ya mazoezi...au maji na mchanga wa kujigalagaza ni mateso? hukwenda hata JKT?
Mbona sie drill tumechezea sana na lockup juu. Walipita jeshini wote wakafungue mashitaka ya kuteswa.
Ulikuwa unajua hali ya afya yake? acha kutetea ujinga na JKT yako, mbona sasa wamesimamishwa kama ni mazoezi? ulienda JKT bila kupima afya yako?
 
We uliona mateso pale zaidi ya mazoezi...au maji na mchanga wa kujigalagaza ni mateso? hukwenda hata JKT?
Mbona sie drill tumechezea sana na lockup juu. Walipita jeshini wote wakafungue mashitaka ya kuteswa.
Hapa kuna ''brain malnutrition'' hapa. Siyo kosa lako.
 
Nianze kwa kukiri huyu jamaa kama amedanganya kwa kile kinachosemwa amekosea na ni mtuhumiwa anapaswa aadhibiwe kwa mujibu wa Sheria.

Lakini haya yanayofanywa kwenye hii video ni moja ya majukumu ya hawa maofisa waliomkamata huyu Jamaa? Je, tunafahamu athari zake ikiwa vyombo hivi vitaachwa kijichukulia sheria mkononi?

Nachelea kusema haya mambo yakiachwa raia wengi watakuja athirika nayo. Hizi athabu zikiachwa ziwe zinatolewa na vyombo vya dola ubinadamu wote utaondoka. Tutabakia na Unyani.

Jamaa alipaswa akamatwe na apelekwe sehemu stahiki ili sheria zikafuate mkondo wake.

Zaidi, soma; Askari 3 wa Uhamiaji wasimamishwa kazi kwa kosa la kutumia nguvu dhidi ya Alex Raphael
Safi sana
 
Kuna kukosea RAIA wenzio na kukosea chombo cha dola. Na huyo alifanya makusudi kukosea, haikuwa bahati mbaya. Bahati mbaya zipo. Zipo sana tu. Na hakuwa anatania.
Kudanganya chombo cha dola ni hatari sana.

Baada ya hiyo nginjengije apelekwe mahakamani

Wew unafikiri kwanini RAIA hatupendi kufanya majaribio ya kwenda kwenye kambi za jeshi na kuiba silaha au chochote kile?
 
Kwangu mimi naona kama walimpa kaazabu kadogo sana ataemtetea huyu jamaa nitamuona nae tapeli au ndio huyo huyo jamaa kaja kujitetea hapa
 
Ulikuwa unajua hali ya afya yake? acha kutetea ujinga na JKT yako, mbona sasa wamesimamishwa kama ni mazoezi? ulienda JKT bila kupima afya yako?
Yaani mijitu kwa kutetea na kushabikia ujinga... Mmekubuhu. Tapeli yeyote ni mhalifu kama wahalifu wengine muhalifu unampima afya? Kenge kabisa. Tuko hapa kama watafukuzwa kazi utaja niambia.
 
Yaani mijitu kwa kutetea na kushabikia ujinga... Mmekubuhu. Tapeli yeyote ni mhalifu kama wahalifu wengine muhalifu unampima afya? Kenge kabisa. Tuko hapa kama watafukuzwa kazi utaja niambia.
Sifa za kijinga kisha unarudi home kulala njaa zinasaidia nn,wangemtoa uhai je.
Thus kuua kibaka hata kama amekuibia huwezi halalisha kosa juu ya kosa.
Utaratibu unafahamika ni kumkamata mtuhumiwa na kumpeleka kwenye sheria,askari wa wapi unamtesa mtuhumiwa kisha unaionyesha dunia unavyotesa.Hata vituoni wezi wanasulubiwa hasa lakini huwezi kuta wakirekodi tukio na kulirusha duniani.
 
Back
Top Bottom