Mabeberu, Vibaraka wa Mabeberu, Wazalendo wa Hayati Magufuli, na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo

Mabeberu, Vibaraka wa Mabeberu, Wazalendo wa Hayati Magufuli, na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo

Thubutu yake mwenyewe!

Si bora hata angekuwa na hiyo flag ya kuwa mlamba viatu, manake tungesema huwa anaambulia angalau makombo!

Mi nakuambia hivi! Majority ya haya majamaa ni majinga tu, yasiyo na mbele wala nyuma! KInachowasukuma kufanya utetezi hata kwa mambo ya kijinga ni ukabila tu, kwa sababu zile zile nilizotaja hapo awali!!

Hawa hanawana hata itikadi za kisiasa, na ndo maana usishangae wakaanza kumpinga Samia kwa sababu wao hawapo hapa kuitetea CCM na serikali yake, bali walikuwa hapa kumtetea Mwendazake!!
Lugha unazotumia zinaonyesha hauko smart, acha ushabiki maandazi, jikite kwenye hoja yako.
 
Hatutaki porojo mkataba umesha kuwa na mashaka upelekwe bungeni watu wapewe muda kuusoma then wajadili vinginevyo ni uhujumu uchumi full stop.
Kama ulivyowahi kupelekwa bungeni mkataba upi?
Akili ya kawaidatu inakataa kukubali kwamba mchina ataruhusu bandari nyingine zifanye kazi, mchina hataruhusu maana patakuwa na ushindani na itapelekea kuchelewesha kurudisha garamazao za uwekezaji.
Na kwanini basi Dar es salam Maritime Gateway Project ilikuwa inaenda sambasamba na miradi mingine, ukiwemo Mradi wa Bandari ya Bagamoyo?

Unajua nyie watu sijui vp! Yaani Mchina aigope bandari hii hii moja wakati kuna nchi zina msururu wa bandari na bado watu wanawekeza kwenye projects mpya!
Vinginevyo bandari zote zitakufa zenyewe kwakuwa zitakosa mbinu za kushindana na hiyo bandari ya kisasa ya bagamoyo kwenye viwezeshi, pia wanaweza kuzielekeza melizao na nyingine watakazoweza kupitisha mizigo bagamoyo na kuathiri bandarizetu.
Kwanini zife? Nimekwambia role kubwa ya Bandari ya Bagamoyo ilitarajiwa kuwa transshipment port, na pia kuhudumia industrial park iliyokuwa inarajiwa kujengwa sambamba na mradi!

Kwa sasa kuna bandari ipi TZ inayofanya hizo roles hadi uamini zitakufa?
Mkataba uwekwe wazi, ujadiliwe.
Kama hatutaweza kupata kodi inayolingana na mapato tunayo pata sasaivi katika bandarizetu na yanayo kuwa kila mwaka, itakuwa ni ujuha wakiwango cha lami kukubali huo mradi.
Hilo la mkataba kuwekwa wazi litakuwa limeandika historia mpya Tanzania kwa sababu hata watunga sheria wenyewe (Wabunge) ni nadra sana kupata fursa ya kuiona hii mikataba!!
 
Hatutaki porojo mkataba umesha kuwa na mashaka upelekwe bungeni watu wapewe muda kuusoma then wajadili vinginevyo ni uhujumu uchumi full stop.

Akili ya kawaidatu inakataa kukubali kwamba mchina ataruhusu bandari nyingine zifanye kazi, mchina hataruhusu maana patakuwa na ushindani na itapelekea kuchelewesha kurudisha garamazao za uwekezaji.

Vinginevyo bandari zote zitakufa zenyewe kwakuwa zitakosa mbinu za kushindana na hiyo bandari ya kisasa ya bagamoyo kwenye viwezeshi, pia wanaweza kuzielekeza melizao na nyingine watakazoweza kupitisha mizigo bagamoyo na kuathiri bandarizetu.

Mkataba uwekwe wazi, ujadiliwe.
Kama hatutaweza kupata kodi inayolingana na mapato tunayo pata sasaivi katika bandarizetu na yanayo kuwa kila mwaka, itakuwa ni ujuha wakiwango cha lami kukubali huo mradi.
Mkuu je ni mkataba upi umewahi kuwekewa wazi ukaujadili? Songas? SGR? Manunuzi ya ndege? JNIA T3? NK. Jikite kwenye mada...
 
Lugha unazotumia zinaonyesha hauko smart, acha ushabiki maandazi, jikite kwenye hoja yako.
Unaweza kunikumbusha ni wapi hasa nimewahi kusema kwamba "I'm smart"!

Btw, umeangalia hiyo mada ilikotokea? Umeangalia huyo jamaa alivyoibuka from nowhere na kuanza kunimwagia matusi?!

Umejaribu kumwambia huyo mmwaga matusi kwa watu hayo unayosema hapa? Kama sio, sasa ni nani shabiki maandazi kama sio wewe mwenyewe?!
 
Unajua kuna jambo tunapokua kwenye ulaji wa kodi za wananchi tunalisahau.

Serikali ni watu wachache waliopewa dhamana ili wasimamie mifumo tuliyojiwekea.
Lakini kuna mamilioni ya watu wanaishi maisha yao ya kila siku hata kama pangekua hakuna serikali wangeishi raha mustarehe.
Lakini serikali bila watu wanaofanya shughuli zao na kulipa kodi haiwezi kuwa na nguvu ya kiuchumi. China na Marekani zinahangaika Dunia nzima ili watu wao wapate masoko makubwa zaidi sio tu tu wabanane kule ndani wenyewe kwa wenyewe.

Hujanielewa !
Kuna maelfu ya Hekari za Ardhi kutokea Mtukula mpaka Tanga ambayo huwezi ukalima,ukajenga,ukafungua Hoteli,ukafungua ,baa,ukaweka soko,ukaweka kiwanja cha mpira , ukajenga Josho la ng'ombe,ukajenga shule ,ukajenga kiwanda , ukachimba madini hata kama utagundua kuwa yapo, ukapanda miti ,ukatunza misitu, ukachimba kisima ,yaani ni maelfu ya ekari toka Mtukula mpaka Tanga hayataruhusiwa kufanya shughuli yoyote ya uzalishaji au biashara kwa mwananchi maskini zaidi ya mabeberu na serikali inayolinda maslahi ya mabeberu wa Kirumi yaani Ulaya na Marekani !

Ardhi ya Bagamoyo kwenye Bandari kubwa Barani Afrika kutakua na shuguli nyingi za migahawa, mahoteli,nyumba za kupanga wafanyakazi wengi sana,biashara ya mabasi,daladala, mama lishe, wamachinga, viwanda vingi, Malori Maelfu kwa maelfu toka nchi jirani kuja kuchukua mizigo hivyo yataweka mafuta kwenye Sheli zetu na kutuingizia kodi ,pesa za Ewura,Tanroad,Rea, tarura n.k. Pia Biashara za magereji kutokana na magari kuwa mengi , ajira za walinzi ambao ni watu wa kawaida kabisa n.k.

Kwa hiyo kuleta stori za uzalendo wa ardhi ya Bomba la mafuta na kupinda ardhi ya Bandari ya Bagamoyo ni Uzalendo feki wa kikabila kwa sababu yule ni wa Pwani na yule ni wa mtukula . Tuwe wazalendo wa kweli wanaojali nchi yetu bila kujali nani amekaa kwenye ofisi ya Magogoni. Jambo jema ni jema tu hata likifanywa na mkoloni. Tuweke ushabiki pembeni.

Kenya kupitisha lile bomba ilikua ni shughuli kutokana na gharama kubwa ya kufidia ardhi kwa mabeberu wenye ardhi kule. Na ardhi yao ni ndogo hivyo mtu anamiliki ardhi na anapanga bei anayotaka alipwe . Wakakimbilia huku kwenye ardhi ya serikali inayoweza kuichukua bure na kumpa mwekezaji bila mwananchi kupata kitu anachoona kinamtosha.
Mkuu 1000, unajitahidi sana kuniondoa kwenye mada hii nzuri ya mkuu Chige, na kiukweli unashawishi hasa, kwa sababu mawazo hayo yako napingana nayo kwelikweli.
Lakini, hayo tuyajadili siku nyingine. Leo ni hii mada ya Bagamoyo na ushawishi alionao mkuu Chige juu yake.

Bado sikubaliani kamwe na hiyo dhana yako katika maandishi hayo hapo juu.
 
Unaweza kunikumbusha ni wapi hasa nimewahi kusema kwamba "I'm smart"!

Btw, umeangalia hiyo mada ilikotokea? Umeangalia huyo jamaa alivyoibuka from nowhere na kuanza kunimwagia matusi?!

Umejaribu kumwambia huyo mmwaga matusi kwa watu hayo unayosema hapa? Kama sio, sasa ni nani shabiki maandazi kama sio wewe mwenyewe?!
Mkuu hawezi kuona hayo wala kumkemea "yule.." ni WALEWALE ukitazama vyema "nyayo na visigino vyao"
 
Mkuu Chige , Thanks for this. Kuna Watanzania wenzetu uwezo wao wa kuona mbali ni mwisho wa pua zao!. Tunajenga SGR, ile treni ina uwezo wa kuvuta mabehewa zaidi ya 100, ya 40ft container zikiwa double, zimepakatana!. SGR ukikamilika, huo mzigo wa kubebwa na SGR ili ijiendeshe kwa faida utatoka wapi?.
Niliuliza hili swali
Sikuwahi kujibiwa!.
Jibu la mzigo wa kuishibisha reli ya SGR ni bandari ya Bagamoyo.
P
SGR haiwezikuwa ndio sababu ya kuruhusu huo mradi.
Watu wana njiazao nyingine za kusafirisha mizigoyao, usijifanye mgeni na hii nchi Pasco, kumbuka SGR ni ya serikali ikitokea ukapata viongizi ambao sio wazalendo wata ihujumi hiyo reli ili maroliyao na ya washirika wao yafanye kazi, tunauzoefu wa mambo hayo.

Hapa tuangalie mkataba kama utatufanya kupata mapato sawa na tunayo pata sasaivi kwenye bandarizetu vinginevyo tumeliwa.
 
Man, upo JF kwa miaka 11 sasa!! Ni muda mrefu sana huo!!!

Je, umewahi kujadili mada zipi hapa JF ambazo zimeambatanishwa na mikataba? Hivi una hoja ya kujadili kweli wewe? Au kwavile umekosa hoja na ndo unataka kujificha kwenye kivuli cha kutaka mkataba?!
Kwa kifupi ni WANAFIKI wanaotaka kuvaa joho lisilowatosha UZALENDO...
Mada imezidi upeo wao...
 
Mkuu Chige , Thanks for this. Kuna Watanzania wenzetu uwezo wao wa kuona mbali ni mwisho wa pua zao!. Tunajenga SGR, ile treni ina uwezo wa kuvuta mabehewa zaidi ya 100, ya 40ft container zikiwa double, zimepakatana!. SGR ukikamilika, huo mzigo wa kubebwa na SGR ili ijiendeshe kwa faida utatoka wapi?.
Niliuliza hili swali
Sikuwahi kujibiwa!.
Jibu la mzigo wa kuishibisha reli ya SGR ni bandari ya Bagamoyo.
P
Mkuu "hatupendi vitu vyenye akili wala kufikirisha.." ndio maana hatujibu hoja bali kushangilia kila msala upitao HUO NDIO UZALENDO WETU!!
 
Mkuu je ni mkataba upi umewahi kuwekewa wazi ukaujadili? Songas? SGR? Manunuzi ya ndege? JNIA T3? NK. Jikite kwenye mada...
Huu wa bandari ya bagamoyo ukiwa wa kwanza sita shangaa sababu unaleta utata kwakuwa mkuu wa nchi aliupinga waziwazi na sasa baada ya kifochake tunautaka urudi ndio maana tunataka uwekwe wazi tujue nini kiko sahihi.
 
Mkuu Chige,, hii ni mada uliyoifanyia kazi. Ni wazi uliweka muda kuiandaa na kuiwasilisha.

Kwa hilo nakupongeza sana, kwani ni nadra sana hapa JF kusoma mada zilizoandaliwa vyema; zikafanyiwa utafiti na kukusanya ushahidi juu ya yanayowasilishwa. Hii imekuwa nadra sana siku hizi hapa JF.

Baada ya kusoma sehemu zote ulizoziweka hapa, mawazo yangu ya mwanzo kabisa niliyochangia katika bandiko langu la mwanzo yanabaki vile vile, na pengine kuyatilia mkazo zaidi.

Bagamoyo ni yetu, tutaamua vyovyote tutakavyo ona ni vya manufaa kwa taifa letu.

Hatuwezi kuingia tu kwenye mradi, eti kwa sababu tu tusichelewe, na fursa hiyo ikanyang'anywa na watu wengine. Huo hauwezi kuwa msingi wa maamuzi yetu.

Maendeleo ya Tanzania hayawezi kutegemea mradi mmoja tu, kiasi kwamba usipotekelezwa hatuwezi kujiletea maendeleo kwa kufanya mambo mengine.

Tatizo tu na andiko lako refu vile, kwanza inakuwa vigumu kwa wasomaji wengi wa hapa JF kulihimili. Wengi wetu hapa ni wa vi-mistari miwili, sana sana mistari mitano.
Kwa hiyo, hata katika kujibu inabidi labda kila sehemu ijibiwe kivyake, bila kuangalia ujumla wa mada nzima.

Labda nichukue tu sehemu moja ndogo inayomhusu Kakoko.

Wewe ume-'dismiss' mno aliyokuwa anasema na yote kuyasema kuwa ni uongo! Na badala yake, umechukulia ya huyo Mchina kuwa ndiyo ya ukweli, hata kama umefanya 'deductions' tu katika matamshi yao. Huna ushahidi wowote wa moja kwa moja kutoka pande zote mbili.

Mi nadhani, ingesaidia pia, kama ungechukua mifano mingine, zaidi ya hizo bandari za Greece na Sri Lanka kuongeza uzito katika mada yako. Tuna mfano mzuri sana wa mradi wa mchina hapa jirani yetu, huo wa SGR hapo juu. Kuna mambo mengi yanayojulikana juu ya mradi huo, na hata yale yasiyotakiwa kufahamika (mchina hataki yafahamike); lakini yamekuwa yakitoka taratibu na kujenga taswira isiyopendeza.

Ya pembeni: Mchina aliwahi kutujengea TAZARA, safi kabisa, bila ya masharti magumu wala nini. Tumeshindwa tu sisi wenyewe kuitumia na jirani zetu Zambia kwa manufaa. Hiyo ilikuwa enzi hizo, hizi ni enzi hizi. Mchina na "Mabeberu" siku hizi hawapishani sana!

Hata hivyo, tuonbe atuimarishie reli yetu hiyo ili tuitumie kwa ufanisi, huku tukiangalia ni jinsi gani tutakavyoshiriki kwenye BRI.
 
Story ndefu aina kichwa wala miguu ujajibu hoja za Kakoko hata moja.

Hakuna mahala Kakoko kaongelea mabeberu yeye alijikita purely on financial aspect za mradi na concession ambazo wachina wanataka wapewe.

Halafu huko kwenye kodi ndio salalee umeboronga hatari. Vitu vingine tuwaachie wataalamu serikalini au tuone terms za mradi wenyewe.

Not sure ata kama unaelewa at what point capital allowance is claimed and it has nothing to do VAT.
 
UTANGULIZI

Amini usiamini, wale wale ambao wamekuwa wakijivika uzalendo, linapokuja suala la Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, ndiyo hao hao wanaotumikia Mabeberu bila wao kujijua!

Nitajadili mada hii katika sehemu mbili:-
  • Kwanini wale wanaoitwa Mabeberu hawawezi kuwa tayari kuona miradi kama ya Bandari ya Bagamoyo inafanikiwa, na
  • Hoja zinazotolewa na Wazalendo Kupinga Mradi wa Bandari ya Bagamoyo.
Kwa bahati, binafsi mwaka 2016 nilikuwa “Mbeba Mikoba” wa Researcher mmoja wa Kimarekani (Beberu?) aliyekuwa anafanya utafiti kuhusu Belt and Road Initiative (BRI).

Kazi yangu kubwa ilikuwa Literature Review!

Kwa wanaofahamu mambo ya Resech, ukifanya Literature Reviews, hususani ya wasomi kama huyu bwana, basi unapata fursa ya kufahamu mambo mengi zaidi yaliyopata kutokea hapo kabla kwenye eneo husika!

Kwa wasiofahamu, Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni matokeo ya (BRI) ambayo, Rais wa China, Xi, anailezea BRI kwamba:


Kwa lugha nyepesi, malengo ya China kupitia BRI ni kuiunganisha nchi hiyo na sehemu zingine duniani, hususani Asia, Afrika, na Ulaya! Uunganishaji huo ni kwa ujenzi wa miundombinu, hususani ya bandari, reli, na viwanja vya ndege.

Ndugu yangu MALCOM LUMUMBA alipata kuchambua kwa undani kabisa suala la Belt and Road Initiative!!

Na hapo sidhani kama mtu anahitaji kuwa na Shahada ya Diplomasia ya Uchumi na Ushikirikiano wa Kimataifa kunusa “threat” ya mpango huo wa China kwa mataifa makubwa, hususani Marekani!

Kutokana na ukweli huo, ndo maana haishangazi mara tu BRI ilipotangazwa, Waandishi na Watafiti mbalimbali kutoka nchi za magharibi wakaanza kulivalia njuga suala hilo.

Makala zikaandikwa, na tafiti zikafanywa kuhusu BRI, lakini makala nyingi kama sio zote zililenga kuyatisha mataifa mengine kuwa makini na BRI!

Watu hawa wakageuka kuwa “Wajomba Zetu” Afrika, huku wakituasa tusije tukaingia kwenye mtego huo hatari wa China!

Ni kupitia hizo tafiti ndipo nami nikajikuta nipo na huyo Mtafiti Msomi kweli kweli wa Kimarekani.

Huyu Bwana case studies zake zilikuwa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, Bandari ya Hambantota (Sri-Lanka), pamoja na Bandari ya Piraeus (Ugiriki).

Ukweli ni kwamba, ilinichukua chini ya dakika 3 kugundua Mtafiti huyu ni kama tayari alishakuwa na “matokeo” ya utafiti wake hata kabla kazi haijaanza! Kwa kifupi, alionesha dalili zote za kutounga mkono Mradi wa Bandari ya Bagamoyo!

Hata "beberu" niliyekuwa namtumikia, nae alikuwa pamoja na "Wazalendo" wetu!!

Binafsi, nilikuwa “in favor of” Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, kwahiyo tukaanzisha kimdaharo kisicho rasmi!

Baada ya kuona hoja zake nyingi nazipangua, akaishia kuuliza ikiwa nadhani ni busara kwa taifa maskini kama Tanzania kuwa na bandari kubwa kama ya Bagamoyo!!

Jibu langu kwake lilikuwa rahisi sana, kwamba: Bandari ya Bagamoyo itakuwa ni kubwa mno kwa Tanzania endapo tu unaamini Tanzania na majirani zake wataendelea kuwa maskini kwa miongo kadhaa ijayo, vinginevyo, huwezi kusema ni “kubwa mno”!

Kwa ufupi, Mheshimiwa huyu, kama walivyokuwa wenzake wengine, nyimbo zao zilikuwa ni agenda ya siri ya China kuitumia BRI kama Mtego wa Madeni kwa nchi maskini!

Lilipokuja suala la Bandari ya Hambantota kule Sri-Lanka, propaganda zikasambazwa kwamba China IMEITWAA bandari ya Sri Lanka ili kufidia deni lake!

Wazalendo wetu nao wakazidaka propaganda hizo, na bila kufanya utafiti, wakaanza kutueleza kwamba “tukishindwa kulipa deni, Wachina wataichukua Bandari ya Bagamoyo kama walivyofanya kule Sri-Lanka.”

Kuweka kumbukumbu sawa, habari za Wachina KUITWAA bandari hiyo zilipotoshwa. Nitaeleza hili kinaga ubaga hapo baada kwenye makala hii.

Pamoja na suala la “Debt Trap”, watu hawa tunaowaita Mabeberu ambao kwa hili tunawaona wanajali maslahi yetu, pia wakawa wanatuambia agenda nyingine ya siri ya China ya kuanzisha “military base” kupitia BRI.

Hapa wakawa wanalenga kutuambia, hata mradi kama wa Bandari ya Bagamoyo, lengo lake ni Wachina kutaka kuweka kambi za kijeshi eneo hili la Afrika Mashariki!

Hata hivyo, hawatuambii ukweli kwamba, ni wao wenyewe ndio wanaozihofia hizo “military bases” za China endapo zitawepo!

Kila mfuatiliaji wa mambo duniani, anafahamu Marekani ina kambi za kijeshi sehemu kadhaa duniani, lakini linapokuja suala la China au mataifa mengine kufanya yale yale ambayo yeye keshayafanya kwa miongo kadhaa, hapo inageuka kuwa nongwa!

Waingereza wana msemo “If you can’t beat them, join them.”

Guys, amini usiamini, juzi yule Mtafiti niliyekuwa nae ametoa makala kwenye moja ya majarida maarufu sana duniani! Baada ya kuisoma makala ile, hapo hapo nikajisikia uchungu, na kumhurumia!

Yaani yule yule aliyekuwa anaipinga BRI, kwenye hiyo makala anaulaumu wazi wazi Utawala wa Trump kwa kutumia kete ya Debt Trap kama njia ya kuidhoofisha BRI.

Kwenye makala hiyo, kuna sehemu anahoji “Kama kweli BRI ni kitu kibaya kiasi hicho, ni kwanini basi China inaendelea kutafuta Washirika walio tayari kujiunga na BRI.”

Mwishowe, Mtafiti huyu anaisemanga serikali yake kwamba ”USA haitaweza kumzuia Rais wa China kuwekeza kupitia BRI endapo US haitakuwa na mbadala kwa mataifa yanayoshirikiana na China!

Ufaransa, imeanza kuliona hilo kama ilivyowahi kuripotiwa na France24 kwamba:


Desperation ya Mtafiti huyu bila shaka inatokana na vile anavyoona jinsi ambavyo nchi mbalimbali duniani jzinavyojiunga na BRI, kinyume na matarajio ya USA ambayo ilikuwa ina-lobby nchi zingine, hususani Washirika wake kutojiunga na BRI.

Kwa bahati mbaya sana, si Afrika, si Asia! Hadi baadhi ya nchi za Ulaya na Carribean zinaingia kwenye BRI. Mbaya zaidi, miradi ya BRI inaonekana kufanya vizuri sana!

Kwa mfano, mwaka 2016 Bandari ya Piraeus ilikuwa ndio ya kwanza barani Ulaya kubinafsishwa chini ya BRI. Bandari hii ndiyo bandari kubwa kuliko zote nchini Ugiriki, na ndio langu kuu la bahari linalounganisha nchi za EU na Asia!

Hapo kabla, bandari hii ilikuwa haifanyi vizuri, na ripoti za nyuma zilikuwa zinaiweka bandari hiyo kama bandari ya 17 barani Ulaya!

Baada ya Wachina kuchukua 51% ya hisa za bandari hiyo, na hatimae hisa hizo kufikia 67%; ripoti ya mwaka huu kupitia Port Economics inasema kwa sasa Bandari ya Piraeus ndiyo bandari kubwa zaidi (kwa kiwango cha makontena) kwenye ukanda wa Bahari ya Mediterranean, na ya 5 Barani Ulaya!!

Sasa haya ndo mambo ambayo watu hawakuyataka! Yaani bandari iliyo kwenye ardhi ya Mzungu, 67% imilikiwe na Mchina, na hapo hapo inaanza kutishia ushawishi wa bandari zingine zinazomilikiwa na Wazungu wenyewe!

JokaKuu
Watu wa JK mnapoteza muda, hakuna asiyeona umuhimu wa huo mradi; Tatizo masharti ya mradi
 
Mkuu Chige , Thanks for this. Kuna Watanzania wenzetu uwezo wao wa kuona mbali ni mwisho wa pua zao!. Tunajenga SGR, ile treni ina uwezo wa kuvuta mabehewa zaidi ya 100, ya 40ft container zikiwa double, zimepakatana!. SGR ukikamilika, huo mzigo wa kubebwa na SGR ili ijiendeshe kwa faida utatoka wapi?.
Niliuliza hili swali
Sikuwahi kujibiwa!.
Jibu la mzigo wa kuishibisha reli ya SGR ni bandari ya Bagamoyo.
P
Watanzania wengi tuna macho lakini hatuoni, tuna masikio lakini hatusikii hili ni tatizo kubwa sana. Leo hii mizigo mingi inakwenda Rwanda, Uganda, Congo inapitia Kahama kwa ya barabara na kusababisha barabara zetu zisidumu kwa muda mrefu bado tu mnaona hakuna mzigo wa kuirisha Sgr? Bado hamuoni kuwa Sgr itasafirisha mzigo mkubwa kwa muda mfupi na gharama nafuu?
 
Sawa...
Ila unapomlaumi Kakoko wakati yeye aliyarudia maneno ya JPM ndo sikuelewi...
 
Unaweza kunikumbusha ni wapi hasa nimewahi kusema kwamba "I'm smart"!

Btw, umeangalia hiyo mada ilikotokea? Umeangalia huyo jamaa alivyoibuka from nowhere na kuanza kunimwagia matusi?!

Umejaribu kumwambia huyo mmwaga matusi kwa watu hayo unayosema hapa? Kama sio, sasa ni nani shabiki maandazi kama sio wewe mwenyewe?!
Sio mbaka useme kama wewe ni smart ama sio, watu watakupima tu haijalishi.

Mi nimekushauri ujikite kutetea hojayako maana umeandika sana, tuliza akiliyako.
 
Story ndefu aina kichwa wala miguu ujajibu hoja za Kakoko hata moja.

Hakuna mahala Kakoko kaongelea mabeberu yeye alijikita purely on financial aspect za mradi na concession ambazo wachina wanataka wapewe.

Halafu huko kwenye kodi ndio salalee umeboronga hatari. Vitu vingine tuwaachie wataalamu serikalini au tuone terms za mradi wenyewe.

Not sure ata kama unaelewa at what point capital allowance is claimed and it has nothing to do VAT.
Kwanini unamiamini kakoko ?upi uhakika wa kile alichokisema?
 
Nimegindua kuwa wengi wetu tunapinga au kukubali utekelezaji wa mradi wa bandari ya Bagamoyo huku tukiwa hatujui chochote ila ima tutapinga au tutakubali Cha ajabu pia hatuingizi akili zetu katika kuchambua Mambo ya msingi yanayoambatanishwa ktk mradi huu zaidi ya kuzishabikia propaganda.
 
Back
Top Bottom