Madaktari wa Bongo washindwa kutema yai

Madaktari wa Bongo washindwa kutema yai

Ila Kiingereza bado ni changamoto kubwa sana Kwa wasomi wetu.

Ajabu wale waliosoma miaka ya 60/70/80 wanatema Lugha barabara sijui sisi wengine tunaferi wapi.

Nina rafiki yangu Mzungu anaishi London, weekend hii alinipigia simu Whatsapp, niliongea naye dakika 15 hivi baada ya kumaliza kuongea naye nikawahi Panadol faster maana kichwa kilishaanza kuniuma

Imagine sasa hao Madaktari wenyeji walipaswa kuongea nao Kila Siku masaa 7 ama 8 Kwa Siku 🙌
Sio poa.

Madaktari walitakiwa kuongea Kingereza muda wote wa kazi😆😆😆
 
Hauna akili, niwapi Masomo ya udaktari yanafundishwa kwa kiswahili Tanzania hii hadi upeleke lalamiko lako kwa lugha tamu ya Kiswahili?

Huko india madaktari kibao hawajui vizuri lugha ya kingereza, huko china madaktari, wahandisi kibao hawajui lugha ya kingereza, walishawahi kufuta kichina kisiwe lugha ya kufundishia??

Wakati mataifa wanakikimbilia kiswahili sisi tunakikimbia kwa ujinga wetu.

Tatizo letu sio kiswahili, tatizo letu ni kujifunza vitu tusivyovijua kwa lugha tusioijua, mwisho wasiku tunahitimu tukiwa hatujui vyote na kuishia kukariri.

Usitegemee mtu aliyekariri kitu awe msaada kwa mtu mwingine anayehitaji kuelewa hilo jambo.
Ni kweli kabisa kiongozi, wengi hawajui tatizo liko wapi na hatutaki kujifunza kwa wengine kama china na india. Tumekalia ulimbukeni wa kiingereza bila mafanikio. Ni muda wa kutumia kiswahili katika kupata maarifa kiingereza iwe kama somo la lugha tu.

Hii itasaidia kutuhamasisha katika kujitafutia maarifa na kufanya tafiti wenyewe na sio kuwa tegemezi kwa nchi za magharibi.
 
Mkuu kwamba MD walioko vituoni wanashindwa kuwasiliana na hao wanafunzi kwa kigezo cha lugha ya kiingereza? hii haiwezi kuwa kweli maana masomo na hata mawasiliano ya kidaktari ni kwa lugha ya kiingereza, labda utuambie muhimbili wameanza kufundisha degree ya udaktari kwa lugha ya kiswahili.
 
Mkuu kwamba MD walioko vituoni wanashindwa kuwasiliana na hao wanafunzi kwa kigezo cha lugha ya kiingereza? hii haiwezi kuwa kweli maana masomo na hata mawasiliano ya kidaktari ni kwa lugha ya kiingereza, labda utuambie muhimbili wameanza kufundisha degree ya udaktari kwa lugha ya kiswahili.
Hata mimi nilibisha kama wewe Lakin tulikuja kuupata ukweli English haipandi Kwa ma daktari wetu
 
Hata mimi nilibisha kama wewe Lakin tulikuja kuupata ukweli English haipandi Kwa ma daktari wetu
Lugha ya mawasilino ya kidaktari siyo sawa na hii inayotumiwa kwenye mazungumzo ya kawaida mitaani, yenyewe inakuwa imejikita zaidi kwenye mambo ya kiganga na hivyo ni rahisi madaktari wenyewe kwa wenyewe kuwasiliana. Miaka mitano usome udaktari kwa kiingereza ushindwe kuwasiliana na daktari mwenzako kwa lugha hiyo hiyo ni jambo lisiloingia akilini. Inawezekana hao siyo madaktari bali ni vishoka...​
 
Ukiniuliza mimi Ntakwambia kuna Shida nyingine tofauti na Language barrier..
Kwanini..
Kwanza Daktari ndo translator Mkubwa kwenye tasnia..

Kwa sababu anasikiliza Hostoria ya Mgonjwa kwa Kiswahili anaiandika maelezo kwa kingereza..
Halafu akishaiandika anaelezea kwa kiswahili kwa mgonjwa..

Pili sitaki kuamini kwamba Daktari akiwa Muhimbili anakuwa anaongea Kingereza vizuri ila akiwa Temeke,Mwananyamala na Ubongo kingereza kinamponyoka...

Maana yake ni kwamba Daktari akipata ajira mubimbili anaingiwa na pepo la kingereza anaongea.kingereza fresh kabisa....

Daktari huyo huyo akiajiriwa Temeke au Kigamboni pepo la kingereza linamtoka anakuwa hajui kingereza na anakuwa mkali..

Kuna kitu ambacho kinafichwa nyuma ya pazia..

Anywei..
Mafunzo ya Udaktari yote MD mpaka Zaidi ya hapo yanafundishwa kwa lugha ya kingereza hata Practical.zake zote hufundishwa kwa kingereza Presentation za wagonjwa Wodini plus mitihani ya Wagonjwa na clinical yote ni kwa lugha ya kingereza hata akiwa wodini ni hivyo hivyo...

Sasa ghafla mtu ambaye kasoma kingereza miaka 6 bila Chembe ya kiswahili ghalfa anasahau kingereza????
Mkuu kila course chuo inafundishwa kiingereza.
Hao wasudani wasitujazie inzi hapa na kama vipi watupishe tu na kiinglishi chao.
 
Ni kweli kabisa kiongozi, wengi hawajui tatizo liko wapi na hatutaki kujifunza kwa wengine kama china na india. Tumekalia ulimbukeni wa kiingereza bila mafanikio. Ni muda wa kutumia kiswahili katika kupata maarifa kiingereza iwe kama somo la lugha tu.

Hii itasaidia kutuhamasisha katika kujitafutia maarifa na kufanya tafiti wenyewe na sio kuwa tegemezi kwa nchi za magharibi.
Mkuu nchi imegeuzwa kuwa ni wachuuzi watupu viwanda ni vichache,
Mchuchuma wanataka kuumpa mchina achimbe na kusepa badala ya kuichakata hapahapa Bongo,
Bukoba wamempa UK achimbe Tu 😂 bila kujenga kiwanda cha battery, ili vijana wapate ajira.
Gairo nako kapewa Australia nako ni kuchimba Tu hakuna kungeneza final product ya kuuza.

Ni kuchimba Tu 😂 na kubaki na mashimo
 
Kujifunza kiswahili for that period of time ya practical ni uongo, is why english ipo, even madkatari wetu entire syllabus ni english, sasa kama wamefuzu na hawajui, i doupt kiwango cha elimu yetu
Mwenye shida ndio unajifunza kama Umekuja Bongo kwa Waswahili jifunze lugha...; Unadhani ukienda Russia huko hautajifunza lugha yao ?

Kujua na kuongea lugha au confidence ya kuongea lugha nyingine ni vitu viwili tofauti kabisa; In short Doctors prowess is not measured by mastering a certain lingo...; kuelewa syllabus na masomo huitaji kuwa mahiri wa language; english ya kuunga unga haikufanyi hushindwe kuelewa human anatomy
 
Serikali na taifa linatakiwa kuona kiswahili ni lugha kubwa kama ambavyo mataifa mengine yanavyokiona kiswahili,
Iwe lugha ya kufundishia kuanzia elimu ya chini mpaka juu,
Kila taifa lenye lugha kubwa linaitumia lugha yake kufundishia
Ie. France,England,China na nyinginezo
Tuache kuchukulia poa kiswahili
Kiswahili hakitoshi, kina mapungufu mengi, hata ukisema tukitumie kufundishia bado kuna mengi sana ya kukopa.
 
Hata mimi nilibisha kama wewe Lakin tulikuja kuupata ukweli English haipandi Kwa ma daktari wetu
Sio madaktari tu mkuu, Wahitimu wa vyuo vikuu wengi lugha ya kingereza ni tatizo, Tafuta hata mwalimu wa English wa Sekondary uone.

Kifupi Kingereza sio lugha yetu wakuu ili tuijue vizuri inatakiwa nguvu ya ziada.
 
Back
Top Bottom