Pre GE2025 Majeshi yote yanatarajia kufanya Usafi tarehe 23/24 January 2024 siku iliyopangwa kwa maandamano
Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila ametangaza kufanyika kwa zoezi la usafi katika Wilaya zote 5 kuanzia January 23 hadi 24 January zoezi ambalo litahusisha Wanajeshi zaidi ya 5000, Polisi zaidi ya 3000, FFU na Vyombo vingine vya dola.

RC Chalamila ameyasema hayo leo katika ibada ya kuwekwa Wakfu Mwangalizi wa Jimbo la Babtist la Dar es Salaam, Makamu , Katibu, Katibu Msaidizi, Mhasibu na Mhasibu Msaidizi ambapo amewataka Wakazi wa Dar es Salaam kutokuwa na shaka watakapoviona Vyombo vya Dola vikifanya usafi.

Chalamila amesema katika kufanya usafi huo pia kutakuwa na magari mbalimbali ya kijeshi kwa ajili ya kukusanya takataka na kuwataka Waumini kuwa Mabalozi wazuri wa kampeni ya usafi ili kupambana na magonjwa mbalimbali.

My Take
Maridhiano na Samia ilikuwa utapeli
Viongozi wetu wanashindwa kujua, hakuna jeshi lililowahi ishinda nguvu ya umma. Washukuru hii hofu ya Mungu iliyopo mioyoni mwa watanzania na wasijisifu kuwa wana jeshi bora.
 
Kwa jinsi hii hali inavyokwenda Serikali ijiandae na kama kuna shida sehemu basi ijaribu kuleta solution mapema

Coz mpaka kuleteana wajeda road hili jambo limekwenda mbali sana na soon wananchi watazoea na kitakachofatia hapo hii nchi haitakalika tena na amani ndio bye bye Tanzania

Kuna stage kwenye maisha ukifika hakuna kurudi nyuma tena coz enough is enough na ukiangalia hauna cha kupoteza, ukiangalia maisha magumu, pesa kitaa hamna, viongozi hawaelewiki, shida za wananchi hazitatuliwi, mafisadi hawawajibishwi na mkitaka kubadilsha mfumo wa utawala kwenye box la kupiga kula nako ni kipengele, yaani shida shidani.

Asee Nyinyi Viongozi hii nchi mtaiponza for real
 
Kwanza nitoe pongezi kwa Mh. Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Dar kwa kuamrisha vikosi vya JWTZ, Polisi na Zima Moto ifikapo tarehe 24 - 25 January kufanya usafi kwa kufagia, kuzibua mitaro yote ya majitaka na kuzoa takataka zote za Jiji ili kukabiliana na magonjwa ya mlipuko. Hii inatokana na kugundua kuwa vikosi vyetu vya ulinzi vimekaa kihasara hasara kwa kukosa kazi za kufanya na hivyo kulisababishia Taifa matumizi mabaya ya fedha na nguvu kazi.

Nitoe wito kwa Wana Darisalaam wakati mkijiandaa na maandamano ya amani yaliyoandaliwa na Chadema kupiga miswada mibovu kuhusu Tume huru ya uchaguzi, uchaguzi wa serikali za mitaa na vyama vya siasa kuhakikisha takataka zote zilizopo katika mazingira yenu mnaziweka barabarani ili kuvirahisishia utendaji kazi vikosi vya ulinzi.

Aidha nitoe wito kwa Wakuu wa Mikoa nchini kote kuiga mfano wa Mh. Chalamila ili vikosi vyetu visikae bure bila kazi ya kufanya na hivyo kuongeza tija ya matumizi ya kodi zetu.
 
Yes anaweza,yeye ndio Mwenyekiti wa ulinzi na usalama wa Mkoa
Sio mwenyekiti wa Ulinzi,Tanzania tutaelewa lini sheria na katiba?

Ni mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama..
Kwahyo hawez kutoa maamuzi bila kamati kukaa maamuzi yake hayana mashiko kuhusu ulinzi na usalama mpaka yawe ni maamuzi ya kamati..

So Unatakiwa ujifunze kuhusu Kamati au Commitee ina tifauti gani na Mamlaka (Authority)
Shukrani
 
Yes anaweza,yeye ndio Mwenyekiti wa ulinzi na usalama wa Mkoa
20240114_121636.jpg
 
Kwa jinsi hii hali inavyokwenda Serikali ijiandae na kama kuna shida sehemu basi ijaribu kuleta solution mapema

Coz mpaka kuleteana wajeda road hili jambo limekwenda mbali sana na soon wananchi watazoea na kitakachofatia hapo hii nchi haitakalika tena na amani ndio bye bye Tanzania

Kuna stage kwenye maisha ukifika hakuna kurudi nyuma tena coz enough is enough na ukiangalia hauna cha kupoteza, ukiangalia maisha magumu, pesa kitaa hamna, viongozi hawaelewiki, shida za wananchi hazitatuliwi, mafisadi hawawajibishwi na mkitaka kubadilsha mfumo wa utawala kwenye box la kupiga kula nako ni kipengele, yaani shida shidani.

Asee Nyinyi Viongozi hii nchi mtaiponza for real
Na hakuna silaha inaweza kuushinda utashi wa binadamu ambaye haogopi kifo
 
Chalamila hii kwake ni exit way ya jiji la dar. Kwa kauli yake tu, bila kujali matokeo ya hizo tarehe.
 
Kwanza nitoe pongezi kwa Mh. Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Dar kwa kuamrisha vikosi vya JWTZ, Polisi na Zima Moto ifikapo tarehe 24 - 25 January kufanya usafi kwa kufagia, kuzibua mitaro yote ya majitaka na kuzoa takataka zote za Jiji ili kukabiliana na magonjwa ya mlipuko. Hii inatokana na kugundua kuwa vikosi vyetu vya ulinzi vimekaa kihasara hasara kwa kukosa kazi za kufanya na hivyo kulisababishia Taifa matumizi mabaya ya fedha na nguvu kazi.

Nitoe wito kwa Wana Darisalaam wakati mkijiandaa na maandamano ya amani yaliyoandaliwa na Chadema kupiga miswada mibovu kuhusu Tume huru ya uchaguzi, uchaguzi wa serikali za mitaa na vyama vya siasa kuhakikisha takataka zote zilizopo katika mazingira yenu mnaziweka barabarani ili kuvirahisishia utendaji kazi vikosi vya ulinzi.

Aidha nitoe wito kwa Wakuu wa Mikoa nchini kote kuiga mfano wa Mh. Chalamila ili vikosi vyetu visikae bure bila kazi ya kufanya na hivyo kuongeza tija ya matumizi ya kodi zetu.

Tena waanzie kamata pale wakanyonye maji yote yaliyofunguliwa kutoka chemba za vyoo kariakoo.
 
Back
Top Bottom