Uchaguzi 2020 Mama Salma Kikwete achukua fomu ya kuwania kuteuliwa kugombea jimbo la Mchinga kupitia CCM

Nchi kama Nchi kuna mahali imefeli..
 
Wapo busy wanakimbizana na siasa badala ya kumalizia uzee wao salama

Hapo alitakiwa sasa awe amelala kifuani kwa JK anamalizia uzee kwa kujibebisha maana maisha yao mengi walikua busy kutumikia wananchi

Cha kushangaza bado anakimhi anakimbizana tuuu
Kwani mabibi siku hizi hawachezi na wajukuu? Hawalei wajukuu?
 
Nadhani kuna post yangu pale chini hukuisoma.
Naogopa sana kuichambua hii hoja nisije mkwaza mama na familia yake.
Ni kati ya watu ninao waheshimu sana na nisingependa kuwaweka ktk nafasi hiyo ya kuniona namuandama.

Hoja yangu kuu ni uwezo wa kisiasa wa mama yetu Salma. Hivi unahisi anafikia hata nusu ya uwezo wa mama Hilary Clinton the former US Secretary of State, Governor, writer, public speaker, and a lawyer?
Walinganishe elimu, uwezo wa kuongea, nyadhifa zao za kisiasa n.k.
Angalia michango ya mama Salma Kikwete bungeni kisha angalia michango na machapisho ya mama Hilary Clinton!!
Mama Salma hata kuongea tu bungeni ni shida, rudia kusikiliza michango yake bungeni. Ametusaidia sana kujenga nchi kwa kuwa mke mwema kwa raisi wetu kwa kumsaidia kila aliloweza, sasa aachane na sisa za uwakilishi majimboni na majukwaani. Abaki huko NEC ya CCM na kwingineko.

Kwanini tulinganishe matufaa na machungwa?
I mean comparing apples and oranges.
Tuwalinganishe Matumla na Tyson, Mwakinyo na Joshua, Cheka na Lenox Lewis ni haki kweli?
Tuwalinanishe Harmorapa na Diamond (Naseeb), au Marijan Rajabu na Ally Choki ni haki?
 
Kuna watu bila vyeo vya kisiasa wanajiona hawajakamilika.

Usishangae akajifanya Hilary Clinton kutaka kugombea urais.
Kuna mtu humu kamfananisha na Hilary Clinton ilibidi nicheke mkuu.

Mimi nikamjibu hivi
 
Kwani shida itakuwa wapi?

Kuna kipengele cha Katiba kinachomzuia?
Hakuna kipengele cha katiba kinachomzuia rais kuimilikisha ardhi yote ya Tanzania familia yake.

Rais ndiye muhifadhi wa mwisho wa ardhi Tanzania na kikatiba hakuna kitu kinachomzuia kufanya hivyo.

Je, kwa sababu hakuna kipengele chochote cha katiba kinachomzuia kufanya hivyo, akifanya hivyo itakuwa sawa?

Pia, hakuna kipengele cha katiba kinachomzuia rais kujikojolea, kujiharishia na kujipaka mavi usoni wakati anahutubia taifa.

Je, kwa kuwa hakuna kipengele cha katiba kinachomzuia rais kufanya hivyo, akifanya hivyo itakuwa sawa?
 


Uchu wa mdaraka lakini kichwani zero
 
Hakuna first lady kama huyu aliekuwa ana madili mengi ya kinamama enzi za Rais Kikwete, alitumia fursa kweli kweli pale Ikulu
 
Huu uchaguzi una kasheshe sana,mjengoni kutamu,ni suala la kusubiri na kuona.
 
Mama jipumzikie ule pension
 
Hizo taasisi za ma 1st lady hazikuwahi kusaidia nchi wala mtu ila mitumbo yao wenyewe.

Hoja yako ya msingi ila kutokana na ubinafsi wao na kukosa intelligence ya ku run hiyo mifuko yenye hadhi na heshima na pesa nene heri aende tu kwa ubunge.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…