Mama yangu alifariki huku akijua simpendi

Mama yangu alifariki huku akijua simpendi

Acha kusingizia ukamilifu
Kuna vitu vingine havihitaji hata maelezo vinahitaji umakini mkubwa hasa wazazi .

Kwanini hukuja kuomba msaada mwanzo ukaamua mwenyewe?
Sasa utaambiwa nini tuku comfort na mzazi ameshakwenda?
hongera mkuu
 
Kuna dogo mmoja alikuwa hasalimiani na mama yake. Sijui walikosana nini. Bahati nzuri niliongea naye na akanipa hiyo ishu. Nikamuuliza mama yako yuko wapi? Akasema alikuwa amelazwa hospitalini anasumbuliwa na shida ya figo.

Nilimuuliza swali rahisi sana. Ati, huyo mamako akikata roho leo, wewe utakuwa na hali gani? Hutajuta maisha yako yote?

Nilimwambia sasa hivi acha kila kitu unachofanya. Nenda hospitalini alikolazwa mama yako. Wala usinunue zawadi yo yote. Nenda kamsalimie mama yako. Nenda ukamkumbatie. Mwambie mama nakupenda sana na nisamehe kwa kujaribu kukosana nawe. Lia naye. Mfute machozi. Mwangalie machoni. Mwambie mama utapona. Nakupenda sana!

Nafurahi kwamba alifanya hivyo maana baada ya siku kama tano hivi mama yake alifariki. Mpaka kesho na kesho kutwa huwa ananishukuru hatari na huwa ananiona kama nabii au apostle fulani hivi. Na ukimuuliza ni tukio gani la muhimu sana ambalo limeshawahi kumtokea katika maisha yake atakutajia kuwa ni siku ile alipojishusha na kwenda kuomba msamaha na kuagana na mama yake aliyekuwa anapambania maisha yake hospitalini.

Na maneno ya mwisho kutoka kwa mama yake ameyaandika kabisa: Asante mwanangu James. Na mimi nisamehe. Sikuwa mama mkamilifu lakini nakupenda mwanangu. Nakuombea mibaraka katika maisha yako. Utaishi maisha mema mwanangu"

Kwako wewe kwa vile umeshachelewa kuomba msamaha kwa mama yako fanya yafuatayo:

Kwanza msamehe mama yako kwa makosa aliyokukosea mpaka ukafikia kumchukia. Mwachilie kabisa kabisa kwa moyo wako wote. Mwambie kabisa: Mama mimi nimeshakusamehe! Na wewe nisamehe mamangu. Tusameheane! Ukiweza nenda kaburini kwake alipolala mkasameheane huko!


Pili kimbilia kwa Mungu (kama unaamini katika uwepo wake). Mwambie Mungu Akusamehe pia kwa niaba ya mama yako maana kumchukia mama yako ulivunja amri mojawapo ya Mungu - amri ya muhimu sana na iliyofungamanishwa na urefu wa muda wako wa kuishi hapa duniani.

Ukishamsamehe mama yako na Mungu Akakusamehe, basi chukua kisadaka kidogo ukipeleke madhabahuni au kwa watoto yatima huko kama ishara ya neema, msamaha, upendo na kusonga mbele. Na kila unapopiga magoti kuomba muombee mama yako na mshukuru Mungu kwa muda wote aliomuweka hapa duniani....

Ukiyafanya haya kwa moyo mweupe, chuki yako itaisha, mahangaiko unayopitia na hii sense of guilty inayokutesa pole pole itaanza kupungua na hatimaye utakuwa huru. Utakuwa mwenye furaha mpya na mambo yako mengi tu yataanza kufunguka.

[emoji3591][emoji3591][emoji3591] Na hili liwe funzo kwa nyinyi ambao bado mna wazazi. Epukeni sana mabifu na wazazi wenu. Wasameheni. Jishusheni kwao. Wajalini, kuwaombea na kuwasikiliza maana wakija kuondoka aisee ni mtihani sana. Na hakuna majuto yanayouma kama mzazi wako kufariki wakati mmekosana na mpaka kufikia hata kutosalimiana.

Kila la heri mkuu....
View attachment 2447445
Hii post yako imenisaidia sana
Mama yangu nilimzika mwenyewe na alifariki akiwa na furaha na amani kubwa sana. Alinipatia baraka.

Baba huwa ana roho mbaya sana...to the extent nilitamani mama yangu abaki atangulie baba...! Baba ni mbinafsi na always ananiombea mabaya. Nikifanikiwa hana raha na atafanya juu chini kunishusha.
Ila kwa post hii sitafunga mwaka bila kwenda kwa baba yangu kujishusha na kumuomba msamaha hata kama amekosea yeye. Ila ukaribu wa sana sitaupenda.
 
Habarini za asubuhi wana MMU poleni na majukumu ya kujenga taifa na familia kiujumla.

Kijana wenu nimekuja hapa mbele yenu sijui nahitajI ushauri ama nahitaj nini ila ntafurahi kama ntarejesha amani ya moyo na akili yangu.

Ni hivi mama yangu mzazi alikufa huku akitambua kua mimi mwanae simpendi na kweli sijawahi kumpenda. Kinachoniuma nilishindwa kulificha hili nilimuonesha moja kwa moja so hadi anakata roho alijua fika simpendi.

Kuna muda nikikaa huwa naona nilikosea sana kumuonesha chuki yangu na hili kosa huwa nalijutia sana. Kila siku nawaza namna ya kujisawazisha ila nakosa majibu.

Naombeni ushauri au maelekezo yoyote yanaweza rejesha amani ya moyo wangu.

Natanguliza shukrani.
hivi inakuwaje mtu usimpende mzazi wako? hivi unajua mzazi asipokubariki hata wewe huwezi kuwa na baraka kwa ajili ya watoto wako?
 
what if ikawa ni zaidi ya kunitoa uhai?

usijione mkamilifu mkuu usijikute unaakili sana kuzidi engine maisha haya ni mapito


Kuna kosa kubwa zaidi ya kifo??, au alitaka kukufanya msukule??!!-- hayo mambo yapo kwa baadhi ya wazazi.
 
hivi inakuwaje mtu usimpende mzazi wako? hivi unajua mzazi asipokubariki hata wewe huwezi kuwa na baraka kwa ajili ya watoto wako?


Mimi nadhani hakuna haja ya kumlaumu huyu ndugu kwani wazazi wetu wanatofautiana, hatujui ni kitu gani kibaya huyo ndugu alifanyiwa na Mama yake na ni hapo tu wengine tunashindwa kutoa ushauri.
 
Habarini za asubuhi wana MMU poleni na majukumu ya kujenga taifa na familia kiujumla.

Kijana wenu nimekuja hapa mbele yenu sijui nahitajI ushauri ama nahitaj nini ila ntafurahi kama ntarejesha amani ya moyo na akili yangu.

Ni hivi mama yangu mzazi alikufa huku akitambua kua mimi mwanae simpendi na kweli sijawahi kumpenda. Kinachoniuma nilishindwa kulificha hili nilimuonesha moja kwa moja so hadi anakata roho alijua fika simpendi.

Kuna muda nikikaa huwa naona nilikosea sana kumuonesha chuki yangu na hili kosa huwa nalijutia sana. Kila siku nawaza namna ya kujisawazisha ila nakosa majibu.

Naombeni ushauri au maelekezo yoyote yanaweza rejesha amani ya moyo wangu.

Natanguliza shukrani.
Mama ni mama tu, lazma alikata roho akiwa amekusamehe kwa ulchokuwa unamfanyia, nenda katubu naamin utakuwa na aman moyon
 
Habarini za asubuhi wana MMU poleni na majukumu ya kujenga taifa na familia kiujumla.

Kijana wenu nimekuja hapa mbele yenu sijui nahitajI ushauri ama nahitaj nini ila ntafurahi kama ntarejesha amani ya moyo na akili yangu.

Ni hivi mama yangu mzazi alikufa huku akitambua kua mimi mwanae simpendi na kweli sijawahi kumpenda. Kinachoniuma nilishindwa kulificha hili nilimuonesha moja kwa moja so hadi anakata roho alijua fika simpendi.

Kuna muda nikikaa huwa naona nilikosea sana kumuonesha chuki yangu na hili kosa huwa nalijutia sana. Kila siku nawaza namna ya kujisawazisha ila nakosa majibu.

Naombeni ushauri au maelekezo yoyote yanaweza rejesha amani ya moyo wangu.

Natanguliza shukrani.
Hujaeleza sbb za kumchukia lkn
 
Hii post yako imenisaidia sana
Mama yangu nilimzika mwenyewe na alifariki akiwa na furaha na amani kubwa sana. Alinipatia baraka.

Baba huwa ana roho mbaya sana...to the extent nilitamani mama yangu abaki atangulie baba...! Baba ni mbinafsi na always ananiombea mabaya. Nikifanikiwa hana raha na atafanya juu chini kunishusha.
Ila kwa post hii sitafunga mwaka bila kwenda kwa baba yangu kujishusha na kumuomba msamaha hata kama amekosea yeye. Ila ukaribu wa sana sitaupenda.
Asante sana Nakadori

Nimetimiza miaka 77 majuzi tu hapa. Nimeona mengi kidogo kuliko ninyi vijana.

Ndiyo. Pamoja na kwamba mzee ana hayo matatizo, kama kweli ni baba yako wa damu deep down anakupenda sana. Siku anakata roho kama utakuwa karibu naye si ajabu akakuomba msamaha. We anza right away kwa kumsamehe na kumtakia mema.

Wajua nini? You can break him kijanja tu. Kimatani matani tu mwambie we baba najua hunipendi hata sijui nilikukoseaga nini. Unaniangusha sana dad maana mi nakupenda sana. Mpe kielfu hamsini chake halafu sepa!

Na mara moja kila mwezi mpigie tu na kumsalimia. Baba nilikuwa namwomba Mungu hapa basi Roho Mtakatifu akaniongoza nikuombee. Nakupenda sana babangu. Na ukiwa na kielfu 20 mrushie hata kama ana hela zake anajitegemea.

Utaona!

Lakini kamwe usikubali akaja kukata moto wakati mna mahusiano mabaya.

Wabeja
 
Mama ako kukubeba tumboni miezi tisa ni upendo wa ajabu kwako.hakuna wa kufananisha nao.
Alipitia mengi mazito kwa ajili yako.
Hata akosee nini kikubwa kiasi gani.hukupaswa kumchukia hata siku moja.
Unaambiwa mzazi hakosei.
Binadamu sio mkamilifu,kuna muda anakosea

Mzazi hakosei kivipi?ama mzazi tunamtoa kwenye kundi la binadamu?

Wazazi wanazinguaga kinyama tu,wewe sema hatutakiwi kuwa na chuki kama ya mleta mada
 
Hii post yako imenisaidia sana
Mama yangu nilimzika mwenyewe na alifariki akiwa na furaha na amani kubwa sana. Alinipatia baraka.

Baba huwa ana roho mbaya sana...to the extent nilitamani mama yangu abaki atangulie baba...! Baba ni mbinafsi na always ananiombea mabaya. Nikifanikiwa hana raha na atafanya juu chini kunishusha.
Ila kwa post hii sitafunga mwaka bila kwenda kwa baba yangu kujishusha na kumuomba msamaha hata kama amekosea yeye. Ila ukaribu wa sana sitaupenda.
Fanya hivyo utakuja kushuhudia hapa, Mungu atafungua milango ya baraka hadi utashangaa mwenyewe.
 
Mwandikie barua!
Andika kila ulichotamani asikie kuwa ni hisia zako.
Mweleze kila ulitaamani ajue hasira yako
mwambie alipokosea
mwambie ulivyoumia
mwambie ulivyokuwa na hasira nae
mwambie umemsamehe
mwombe akusamehe kwa kushindwa kuzungumza nae mpk anakata roho
mwambie unatamani mnegeweza kurekebisha kabla hajafa
Talk to her!
ANDIKA!
Ukimaliza nenda kaburini kwake, read that letter .
kisha ichome moto!
Utamake peace with her.
Utaface your fears
Utamface yeye kimawazo.
Inawea kukusaidia, it helped me facing my past demons!
 
Asante sana Nakadori

Nimetimiza miaka 77 majuzi tu hapa. Nimeona mengi kidogo kuliko ninyi vijana.

Ndiyo. Pamoja na kwamba mzee ana hayo matatizo, kama kweli ni baba yako wa damu deep down anakupenda sana. Siku anakata roho kama utakuwa karibu naye si ajabu akakuomba msamaha. We anza right away kwa kumsamehe na kumtakia mema.

Wajua nini? You can break him kijanja tu. Kimatani matani tu mwambie we baba najua hunipendi hata sijui nilikukoseaga nini. Unaniangusha sana dad maana mi nakupenda sana. Mpe kielfu hamsini chake halafu sepa!

Na mara moja kila mwezi mpigie tu na kumsalimia. Baba nilikuwa namwomba Mungu hapa basi Roho Mtakatifu akaniongoza nikuombee. Nakupenda sana babangu. Na ukiwa na kielfu 20 mrushie hata kama ana hela zake anajitegemea.

Utaona!

Lakini kamwe usikubali akaja kukata moto wakati mna mahusiano mabaya.

Wabeja
Huwa hata umpe nini ana dharau sana
Me ninachotaka kufanya ni kumuomba msamaha then niwe namsalimia mara moja moja maana hata kabla mama hajafa alinambia nitengeneze amani na baba kwakuwa ndie baba yangu bila kujali madhaifu yake.
 
Hii post yako imenisaidia sana
Mama yangu nilimzika mwenyewe na alifariki akiwa na furaha na amani kubwa sana. Alinipatia baraka.

Baba huwa ana roho mbaya sana...to the extent nilitamani mama yangu abaki atangulie baba...! Baba ni mbinafsi na always ananiombea mabaya. Nikifanikiwa hana raha na atafanya juu chini kunishusha.
Ila kwa post hii sitafunga mwaka bila kwenda kwa baba yangu kujishusha na kumuomba msamaha hata kama amekosea yeye. Ila ukaribu wa sana sitaupenda.
katuokoa wengi kwa kweli abarikiwe sana
 
kuna mambo hua inapaswa kuyarekebisha before its too late
 
Mwandikie barua!
Andika kila ulichotamani asikie kuwa ni hisia zako.
Mweleze kila ulitaamani ajue hasira yako
mwambie alipokosea
mwambie ulivyoumia
mwambie ulivyokuwa na hasira nae
mwambie umemsamehe
mwombe akusamehe kwa kushindwa kuzungumza nae mpk anakata roho
mwambie unatamani mnegeweza kurekebisha kabla hajafa
Talk to her!
ANDIKA!
Ukimaliza nenda kaburini kwake, read that letter .
kisha ichome moto!
Utamake peace with her.
Utaface your fears
Utamface yeye kimawazo.
Inawea kukusaidia, it helped me facing my past demons!
asante mkuu
 
Binadamu sio mkamilifu,kuna muda anakosea

Mzazi hakosei kivipi?ama mzazi tunamtoa kwenye kundi la binadamu?

Wazazi wanazinguaga kinyama tu,wewe sema hatutakiwi kuwa na chuki kama ya mleta mada
kweli kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom