Mambo 30 usiyoyajua kuhusu utapeli wa Q-Net (Network Marketing)

Mambo 30 usiyoyajua kuhusu utapeli wa Q-Net (Network Marketing)

Mkuu habari ya majukumu tunaomba miendelezo kuhusu qnet naona mkuu wa wilaya ya hai kashawadaka huko
 
Good morning hata saa sita [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hawana lolote zaidi ya utapeli na ile salamu yao ya 'good morning " hata kama ni mchana au jioni huwa siielewi.
Hahahaha mimi mwenyewe kwa mara ya kwanza walinishangaza na hiyo salamu yao ya "Good Morning" eti kwa vile imeenea sehemu mbalimbali duniani kama kwako ni mchana kwa wenzako ni asubuhi.
 
QNET ni wafanyabiashara wenye sura ya kitapeli ambao wanauza bidhaa za mtandaoni. Ubaya wa hii biashara ni huu hapa:

1. Watu wanaokutaka ujiunge kwenye hii biashara wanakupotezea muda wako wa kuhudumia wateja na jamii kwa kukuzonga kwa maneno mengi sana yanayohusu kuachana na umaskini milele (financial freedom).

2. Mchakato wa kujiunga na Qnet utakuchukulia muda wako mwingi sana, ikijumlisha kwenda kuhudhuria mafunzo mara mbili mpaka ulainike na kuchagua bidhaa hata kama huijui wala kuipenda.

3. Ukishajiunga na QNET Mchakato kutafuta wateja wapya wa kujiunga na QNET ili ukomboe hela yako utakuchukulia muda mwingi na utawachukulia watu wengine unaotaka kuwaunga muda wao mwingi sana pia. Hivyo kazi za mwajili na kazi zako zitazorota wakati wa harakati za kuingiza watu

4. QNet watakuuzia bidhaa ambayo huitaki kwenye malengo yako ila utalazimika kuinunua tu kama kiingilio kwenye biashara yao kwa ahadi ya kupata faida kubwa sana kupitia qnet.

5. Qnet watakushauri uache kazi ya mwajili ili ufanye kazi ya kuwatafutia wateja wapya. Hapa nimeona madaktari, manesi, walimu, wakiacha kazi zao ili wafanye kazi ya kukimbizana na wateja, wale ambao hawajaacha kazi wanageuka wababaishaji kazini na kuwapotezea muda wafanyakazi wenzao wajiunge nao.

6. Qnet hawatoi risiti, hivyo hatujui serikali inapataje kodi yake, VAT, holding tax

7. Qnet inawawinda wastaafu kwakuwa wanafahamu wamepata hela ya mafao, hivyo ni rahisi kutoa kiingilio.

8. Qnet wanakushawishi kwa nguvu uache miradi yako mingine ili uhamishie hela na muda wako kwao

9. QNET wanawawinda watu muhimu kwenye jamii ambao wanaheshimika kujiunga ili kuwavuta watu wa kawaida kujiunga nao

10. QNET inatumia vishawishi kama picha za magari, nyumba, boti, ndege ili kuwa kama chambo cha kukunasa ujiunge.

11. QNET inakufundisha namna ya ku manipulate watu kujiunga na Qnet

12. QNet watakupigia simu kila wakati hata usiku wa manane kukushawishi ujiunge

13. Qnet utawakusanyia sh. 72,000,000 wewe wanakupa faida ya dola 200 sawa na shilingi 460,000

QNET kama ikiachiwa iendelee kama ilivyo sasa kuna kitu kibaya kwa watu, familia, waajili, jamii na serikali kitatokea.
 
Ni ujinga na upumbavu wa hali ya juu kuchukuliwa hela kizembe kama wanavyozivuna matapeli wa Q-NET. Pole hasa walimu
 
Samahani wadau, mimi ninahitaji anayeweza kunishawishi hadi nikajiunga na hawa Qnet aje inbox chap. Hata niwe na mabilioni siwezi kushawishika kirahisi namna hiyo ila ukiweza mpaka nikasarenda nakuahidi nitalipia mara mbili ya kiasi tajwa.
 
Biashara hiyo ingekuwa inalipa MO, BAKHRESSA Wote wangekuwepo QNET
 
QNET ni wafanyabiashara wenye sura ya kitapeli ambao wanauza bidhaa za mtandaoni. Ubaya wa hii biashara ni huu hapa:

1. Watu wanaokutaka ujiunge kwenye hii biashara wanakupotezea muda wako wa kuhudumia wateja na jamii kwa kukuzonga kwa maneno mengi sana yanahusu kuachana na umaskini.

2. Mchakato wa kujiunga na Qnet utakuchukulia muda wako mwingi sana

3. Ukishajiunga na QNET Mchakato kutafuta wateja wapya wa kujiunga na QNET ili ukomboe hela yako utakuchukulia muda mwingi na utawachukulia watu wengine unaotaka kuwaunga muda wao mwingi sana pia. Hivyo kazi za mwajili na kazi zako zitazorota wakati wa harakati za kuingiza watu

4. QNet watakuuzia bidhaa ambayo huitaki kwenye malengo yako ila utalazimika kuinunua tu kama kiingilio kwenye biashara yao kwa ahadi ya kupata faida kubwa sana kupitia qnet.

5. Qnet watakushauri uache kazi ya mwajili ili ufanye kazi ya kuwatafutia wateja wapya. Hapa nimeona madaktari, manesi, walimu, wakiacha kazi zao ili wafanye kazi ya kukimbizana na wateja, wale ambao hawajaacha kazi wanageuka wababaishaji kazini na kuwapotezea muda wafanyakazi wenzao wajiunge nao.

6. Qnet hawatoi risiti, hivyo hatujui serikali inapataje kodi yake, VAT, holding tax

7. Qnet inawawinda wastaafu kwakuwa wanafahamu wamepata hela ya mafao, hivyo ni rahisi kutoa kiingilio.

8. Qnet wanakushawishi kwa nguvu uache miradi yako mingine ili uhamishie hela na muda wako kwao

9. QNET wanawawinda watu muhimu kwenye jamii ambao wanaheshimika kujiunga ili kuwavuta watu wa kawaida kujiunga nao

10. QNET inatumia vishawishi kama picha za magari, nyumba, boti, ndege ili kuwa kama chambo cha kukunasa ujiunge.

11. QNET inakufundisha namna ya ku manipulate watu kujiunga na Qnet

12. QNet watakupigia simu kila wakati hata usiku wa manane kukushawishi ujiunge

13. Qnet utawakusanyia sh. 72,000,000 wewe wanakupa faida ya dola 200 sawa na shilingi 460,000

QNET kama ikiachiwa iendelee kama ilivyo sasa kuna kitu kibaya kwa watu, familia, waajili, jamii na serikali kitatokea.
Kabisa, wadhibitiwe, ila shida ni wale ambao wameshajiunga, ndio wanaifanyanya iendelee, maana wanahangaika kugomboa fedha zao
 
Dunia haijawahi kukaukiwa na waking kama hawa wanaofikia hatua ya kuquit kazi ili wakomae na mapamidi
 
Luna jams tunafanya nae Nazi daily ananishawushi kuingia Qnet bahat mbaya kila akija kunishawisshi ananikuta nimelewa so naishia kumuambia tu anipge peg ya buku anatembea

Matak* yako huko alipo
 
20201217_090837.jpg
 
Back
Top Bottom