Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewaita kazini vijana 1,453 kati ya 2,100 baada ya kupata kibali cha Rais Samia

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewaita kazini vijana 1,453 kati ya 2,100 baada ya kupata kibali cha Rais Samia

muda wa kutukamua mpka utumbo sasa sisi wajasiriamali.
Toeni risiti tuu,next year mama anataka kujenga vituo vya afya 304, hospital 28 na nyumba za watumishi 150 👇

Screenshot_20220410-093346.png
 
Walimu kweli wanaonewa Mwenye elimu ya shahada analipwaga kiivyo 2.3 M TRA ? Hivi mwenye Diploma analipwa ngapi? Unaweza kuta mshahara wa Dip sawa namwalimu mwenye Master yake anaefundisha Sekondari.
Kuna mgawanyo serikali imeuweka kwenye muundo wa utumishi.

Kuna watu wanatambulika kama wako kwenye service moja kwa moja na wengine wako kwenye Idara za kuzalisha kwa hiyo malipo ni tofauti.

Ukisema walimu wanaonewa Polisi je ambao wanatumikia miaka Zaidi ya 8 kama vibarua ikiisha hiyo ndio wanaajiriwa..
 
Kabisa kabisa my dear kuna watu wanavuta mpunga mrefu sana juzi kuna position ilitoka Ireland Embassy nikamtumia sister aombe aisee, jamaa waliweka na salary yao kabisa per annum, tulivyokuja kuigawa tukakuta kwa mwezi salary anayotakiwa kulipwa ni almost 9m my lovely.

Acha kabisa my dear...!
Ukipata Kazi nje ya Nchi nenda,hapo tuu Oman dereva wa truck anavuta hadi mil.3 za bongo na stahiki zingine..

Ukifanya zako Kazi miaka 3-7 unarudi na mpunga kama wote,ila tuu connection.
 
Mzee mimi mwanzo nilikuwa napewa hizi info ila nilikuwa siamini lakini baada ya kuingia kwenye hizi kazi za International Organizations nimeamini kweli kuna watu wanavuta mpunga kiongozi.

Acha kabisa mkuu...!
Shida ya wabongo wamekariri ajira ni za serikali tuu,wanaogopa kwenda kushinda a nje ya Nchi nk

Ila to be honest organization za Nje wanalipa vizuri sana ila lazima upige Kazi kweli kweli hakuna janja janja.
 
Vumilieni next week kuna zingine zaidi ya 30,000 zinakuja hasa walimu,madaktari na manesi..

Za kada zingine zitakuwa kiasi.Hata hivyo wale waliosomea Mambo ya kilimo na mifugo kuna ajira za mkataba wizara imemwaga ziko kama zote ingia page yao muombe.
Watuongezee na za Uhasibu pia tuombe double double
 
Shida ya wabongo wamekariri ajira ni za serikali tuu,wanaogopa kwenda kushinda a nje ya Nchi nk

Ila to be honest organization za Nje wanalipa vizuri sana ila lazima upige Kazi kweli kweli hakuna janja janja.
Kuna jamaa flani anafanya kwenye organization flani iko chini ya UN huko kigoma, analipwa mls 45 kwa mwezi.
 
Sasa wahaya huwajui na majivuno ?, Ulipwe milioni 40 Kwa uzuri gani ?
Labda ni story ila mimi nilikuwa kigoma huko nikakutana na jamaa anafanya hapo ni engineer tukawa tunapiga story za miradi yao na masuala ya mishahara. Wao wakawa wanaponda serikali kuwa hakuna pesa yeye analipwa 8 kwa mwezi ndio akaniambia yule jamaa boss wetu anakula 45 kwa mwezi.
Tena akaniambia karibu watu wote wanaofanya kazi kigoma watakudanganya wanafanya UN ila kuna mashirika mengi tu ila UN ndio wanalipa ela kubwa hao wengine wana mishahara ya kawaida.
 
Ni kawaida ya maisha kutafuta greener pastures zaidi kwa sababu the high income high expenditures

Unachosema ni sahihi kabisa hasa ukitoka mtaani ambapo ulikuwa unaviskia vitu kwenye bomba tu, ila ukishaingia mzigoni ukazichezea chezea kidogo njuruku utajua jinsi ya kuzi-control.

Vijana wanasema chezea pesa ikuzoee...!
 
Back
Top Bottom