Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wala hawafanani,mmoja sura yake pana kuliko mwenzake.Chuo kikuu cha Ardhi kimetoa Taarifa kwa umma kikieleza kuwa Mapacha wawili wanaofanana ambao walifanya mahojiano na kituo Cha Wasafi FM 06/03/2024 kuwa Mapacha hao watachunguzwa kutokana na kusema kuwa mmoja kati yao amewahi kumfanyia mwenzake mtihani wakati wakisoma shahada ya kwanza katika chuo hicho.
Katika mahojiano hayo Mapacha hao walisikika wakisema mmoja kati yao amewahi kumfanyia mwenzake mtihani wa Hydrolojia ambao ulikuwa n mtihani wa marudio (Supplementary) kwa kutumia kitambulisho Cha pacha mwingine.
Mbona povu mkuu wote tunajaribu kuwaza kwa sauti tu hapa.Unajua Handwritting forensic, Pamoja na fingerprint zinagharimu Kiasi gani?
NA booklets zinaharibiwa kwa miaka 10 ,Umejua lini walimaliza?
Je Chuo Kinaweza kujitosa kwa gharama ya kuchunguza Kitu kilichokwisha pata
Kufika mahakamani wanasema ilikuwa furahisha genge kipindi kipate promo tu, huo ushahidi wa kuongea hivyo redioni haujitosheleziKama wana kazi wanafukuzwa. Na wanadaiwa mishahara. Na mwisho wanaenda mahakamani kesi ya kulaghai. Jamuhuri inachukua kesi.
Halafu pia wameharibu credibility ya chuo.Walimaliza 2021 sio mbali mkuu.
Hao mabinti walikosea, hii kitu itawapotezea muda.
Kwa nature ya nchi zetu, akitokea mwanasiasa hapo kati akalivalia njuga ili apate umaarufu hawatoboi hao.
Wangejitahidi sana basi wasikitaje chuo wala mtihani, sasa wao hadi mtihani wameutaja, muda wa kuufanya wameutaja.
Acha tusubiri.
Hakuna povu mkuu hapoMbona povu mkuu wote tunajaribu kuwaza kwa sauti tu hapa.
Baba levo haijui SupplementaryHivi unakiri vipi kwenye kweye TV inayotazamwa na watu wengi hivyo jambo linaloweza kukuingiza matatani? Haya sasa mambo yameharibika!
Chuo Kikuu Ardhi kimepata taarifa kupitia Wasafi FM, chaneli ya YouTube ya mahojiano kati ya waandishi wa habari na mapacha wawili wanaofanana. Mahojiano hayo yalirushwa siku ya Jumatano, tarehe 6 Machi, 2024 kwenye kipindi cha Jana na Leo.
Kwenye mahojiano hayo, mapacha hao walisikika kupitia chombo hicho cha habari kuwa walisoma “Chuo cha Ardhi” na kufanya mtihani wa Hydrolojia. Katika mtihani huo, mmoja wa mapacha hao alikiri kumfanyia pacha mwenzake mtihani wa marudio (supplementary) kwa kutumia kitambulisho cha pacha mwingine.
Chuo Kikuu Ardhi tunchunguza ukweli wa taarifa hizo na baada ya uchunguzi kukamilika, umma utajulishwa matokeo ya uchunguzi huo
Imetolewa na:
Prof. Evaristo Liwa
Makamu Mkuu – Chuo Kikuu Ardhi
7 Machi, 2024
View attachment 2927199
Pia soma: Chuo cha Ardhi kinapaswa kuchukua hatua dhidi ya mabinti mapacha waliokiri kufanyiana mitihani
Daah kumbe ulifuatilia mi nilikuwa makini hadi shoo inaishaBaba Levo alishtuka kwamba hawa wameshachemka, ila wao mpaka wanamaliza kipindi hawajashtuka! Ina maana Baba Levo ana akili kuliko hao wadada 😀
Hawakutaja chuo chochote.Ni watu viherehere vyao tu.Halafu pia wameharibu credibility ya chuo.
Pepa huwa zinatunzwa kwa miaka mitatu. Ikipita hapo zinateketezwa!Kwenye uchunguzi mwandiko unaweza kuchunguzwa kujua ni wa nani kwa hiyo hapo wajiandae kisaikolojia😂😂😂😂
WameyatimbaWalijua sifa. Kula vichwa. Haina haja kuchunguza si wamekiri wenyewe.
Hivi unakiri vipi kwenye kweye TV inayotazamwa na watu wengi hivyo jambo linaloweza kukuingiza matatani? Haya sasa mambo yameharibika!
Chuo Kikuu Ardhi kimepata taarifa kupitia Wasafi FM, chaneli ya YouTube ya mahojiano kati ya waandishi wa habari na mapacha wawili wanaofanana. Mahojiano hayo yalirushwa siku ya Jumatano, tarehe 6 Machi, 2024 kwenye kipindi cha Jana na Leo.
Kwenye mahojiano hayo, mapacha hao walisikika kupitia chombo hicho cha habari kuwa walisoma “Chuo cha Ardhi” na kufanya mtihani wa Hydrolojia. Katika mtihani huo, mmoja wa mapacha hao alikiri kumfanyia pacha mwenzake mtihani wa marudio (supplementary) kwa kutumia kitambulisho cha pacha mwingine.
Chuo Kikuu Ardhi tunchunguza ukweli wa taarifa hizo na baada ya uchunguzi kukamilika, umma utajulishwa matokeo ya uchunguzi huo
Imetolewa na:
Prof. Evaristo Liwa
Makamu Mkuu – Chuo Kikuu Ardhi
7 Machi, 2024
View attachment 2927199
Pia soma: Chuo cha Ardhi kinapaswa kuchukua hatua dhidi ya mabinti mapacha waliokiri kufanyiana mitihani
Kinacho chunguzwa ni kama kweli walisoma hapo au la. Kama mmoja wapo au wate walisoma hapo mwaka mmoja au miaka tofauti. Degree zao zitayeyuka, simple as that.Hapo ndio ngoma. watathibitishaje huo uchunguzi wao?
Hawana cha kujitetea....Katika sheria lazima kuwe na ushahidi wa bila shaka,kama nilivyokuambia lazima watajitetea.
Hao wanaweza kukataa tu kirahisi kwamba walikuwa wameongopa kutafuta umaarufu.Chuo kitawezaje kuthibitisha hili?