Maridhiano ya CCM na CHADEMA Ndiyo Kawaida ya Vyama vya Siasa Duniani Ilivyo?

Maridhiano ya CCM na CHADEMA Ndiyo Kawaida ya Vyama vya Siasa Duniani Ilivyo?

Hata utawala wa makaburu Africa Kusini uliisha kwa mazungumzo na maridhiano, CCM hata hawajafikia kiwango cha makaburu. Mandela na ANC walikaa mezani na makaburu, hiyo kwa wengine walitafsiri ni kuungana.
Nilijuwa huko kichwani kuna kitu.

Lakini, huoni mwisho wa siku ANC walishika hatamu?
Yale maridhiano hayakuwa ya ANC kujisalimisha kwa makaburu kwa njia yoyote ile.
 
Vyama vya siasa vikimalizwa kwa siasa za mazungumzo na maridhiano ni sawa kabisa na hiyo ni sehemu ya demokrasia, ila sio kwa hofu na vitisho vya risasi, utekaji, unyang'anyi na njia nyingine haramu za binadamu wasiostaarabika.
Hapana, hili sikubaliani nawe.

Vyama vya siasa kiuhalisia vinakuwepo, kwa sababu ya kuwepo na tofauti zao katika mambo wanayoyaamini.
Kuvimaliza, hata kama ni kwa njia ya mazungumzo, maana yake ni kwamba havikuwa na zaidi walichokisimamia kama vyama, bali vilikuwepo kwa maslahi tu, ambayo sasa yatapatikana kwa njia za maridhiano.
 
Mbona unalalama humu kama mbwa koko?,kama umeona haki yako inaminywa push back ,usitegemee upiganiwe wakati wewe umejificha na I'd fake hizi na elewa wewe sio msemaji wa watanzania!usinisemee mimi bcs mimi ninajipigania haki yangu bila kutegemea watu wengine wanipiganie.
Mkuu Nkanini jibu swali ,Mimi Sina chama Cha siasa ,,lakini je hayo yanayofanywa na mwenyekiti kukutana na mwenyekiti ndio maridhiano yanavyokuwa???
 
Siasa zetu hazina budi kuzingatia mazingira yetu, desturi zetu, mila zetu, miiko na utamaduni wetu wa kitanzania na wa kiafrika na siyo lazima kufuata ya kimagharibi na vivyo hivyo kwa misingi ya maridhiano ya sasa uichukulie katika sura hiyo. Achana na Democrats na Labour

Lakini Zanzibar hakuna utamaduni wala Mila, kuna Uislamu tu, sasa huo utamaduni wa Kitanzania unaouongelea ni upi?
 
Wewe mkuu unaona CCM iko sawa kama ilivyo kimkakati ila CHADEMA ndio inatakiwa “ikaze” kutoruhusu dhulma na udhalimu inaotendewa na CCM (irrespective of the president in office). Sawa?

CCM bado inamiliki na kudhibiti vyombo vya dola. Watanzania hawana ujasiri wa kusimama na upinzani dhidi ya vipigo, mateso na manyanyaso ya vyombo vya dola kama ilivyokuwa katika awamu ya tano. Hawako tayari kuvuja damu kama kina Mawazo, Lissu na wengineo.

Na madhila aina hiyo toka vyombo vya dola hayapo katika nchi za kidemokrasia zilizoendelea.

Sasa ukitaka CHADEMA wakaze tu wasikubali muafaka wa aina yoyote na SERIKALI - not CCM by the way (kama mkakati wa kuendelea na siasa) maana yake, katika mazingira haya, unataka CHADEMA waachane na siasa au wajigeuze kuwa TLP and the likes. Yaani wawe completely ineffectual as a political force kama alivyotaka JPM. NDIVYO NILIVYOKUELEWA! Just be honest.
Ninakuelewa unayosema hapa, ila sikubaliani kamwe na hitimisho lako, kwamb kazi kuu ya maridhiano ni kuondoa ukandamizaji huo, na kwa sababu hiyo ndiyo uwe sababu ya vyama vya upinzani kubwaga manyanga hata katika msisingi ya wanayoyasimamia kama vyama pinzani.

Ndiyo, ridhiana kuondoa ukandamizaji, lakini huwezi kuweka rehani misingi ya chama katika kuyaondoa hayo maovu.
 
Tanzania ina vyama vya siasa karibia 20, kikimalizwa chama kimoja au viwili vitatu bado utabakiwa na vingine vingi tu vya kuchagua kuendelea navyo. Pia nchi hii kuna urahisi sana wa kuanzisha chama cha siasa, kikimalizwa chama kimoja kuna fursa kubwa ya kuanzisha chama kingine.

Usiogope.
Hapana, hili sikubaliani nawe.

Vyama vya siasa kiuhalisia vinakuwepo, kwa sababu ya kuwepo na tofauti zao katika mambo wanayoyaamini.
Kuvimaliza, hata kama ni kwa njia ya mazungumzo, maana yake ni kwamba havikuwa na zaidi walichokisimamia kama vyama, bali vilikuwepo kwa maslahi tu, ambayo sasa yatapatikana kwa njia za maridhiano.
 
Mkuu Nkanini jibu swali ,Mimi Sina chama Cha siasa ,,lakini je hayo yanayofanywa na mwenyekiti kukutana na mwenyekiti ndio maridhiano yanavyokuwa???
Exactly mkuu, politics sio vita sisi wote ni watanzania, na pia elewa President Samia ameenda hapo kama President sio chairperson wa ccm,na vikao vyote kati ya viongozi wa CDM na President Samia vilifanyika state House SIO LUMUMBA (Kwenye centre of power),mbona President Obama alimtumia President Bush Jr kumwakilisha wakati wanatoka vyama tofauti?sasa soma hili,CIC Malema (alijitoa ANC kwa hasira kubwa)sasa amekubaliana kufanya kazi na ANC!,kumbuka fujo za EFF bungeni dhidi ya serikali ya ANC,Leo wanatawala pamoja jiji la Durban!
 
Tanzania ina vyama vya siasa karibia 20, kikimalizwa chama kimoja au viwili vitatu bado utabakiwa na vingine vingi tu vya kuchagua kuendelea navyo. Pia nchi hii kuna urahisi sana wa kuanzisha chama cha siasa, kikimalizwa chama kimoja kuna fursa kubwa ya kuanzisha chama kingine.

Usiogope.
Nimekuelewa zaidi ya ulivyoeleza hapa.
Kwa hiyo sina sababu ya kufafanua zaidi.
 
Mara nyingi sisi hupenda kuiga au kujilinganisha na hawa wenye demokrasia yao waliyoitengeneza kwa muda mrefu.

Sasa nauliza, hizi mbinu za CCM ya Samia na CHADEMA ya Mbowe inakidhi kweli mlinganisho wowote na wayafanyayo Democratic Party na Republican wa Marekani au Chama cha Labour na Conservative vya Uingereza; au hata vile vilivyoko Ujeruman kwa namna yoyte ilei?

Nionavyo mimi, haya majadiliano na maridhiano ni njia tu za kutafuta ulaji kwa raha toka kila upande, bila kujali maslahi ya nchi na wananchi wake.

Ninaelewa, kuna mambo ambayo huwaleta pamoja hao wakubwa wa dunia, na yote ni yale yanayohusu siasa za nje, hasa wanapopambania maslahi ya nchi zao dhidi ya mataifa wanayoyaona kuwa hatarishi kwa maslahi yao.

Haiwezi hata siku moja ikatokea watu wa Democratic Party wakawaalika wenzao wa Republican kusherehekea shughuli zao za kichama. Hali ni hiyo hiyo na Labor party na Conservatives; na hata kule Canada, Australia, hata Japan, Korea Kusini na kwingineko.
Hii haina maana kwamba hawapendani kama ndugu, au kwamba kuna uhasama kati ya vyama vyao, lakini ndivyo ilivyo ni kama utamaduni kwao.

Sasa sisi tunaiga kitu gani, kama siyo njia tu za kuhalalisha kugawiana mafao ya jasho la wananchi.
Kwani tinapangiwa na watu wa Duniani?
 
Mbona Ruzuku ya CHADEMA Ina kuuma Sana?. Hiyo ni haki ya CHADEMA waitumie wapendavyo. Ruzuku inatolewa kwenda kwenye akaunti ya chama sio ya mtu binafsi.
Huyo bado ana hasira za kuachwa
 
Unajichanganya sana mkuu, katika andiko lako hili, ambalo umetumia "kisheria", sijui mara ngapi katika andiko fupi kama hili.

Ni "sheria" ipi iliyohalalisha uchaguzi na matokeo ya uchaguzi uliofanyika?

Lakini ngoja nirudi mwanzo wa andiko lako.
Unaniuliza "kwa nini ninataka tuige wazungu...", kwani ni mambo mangapi tunawaiga hao wazungu, hili kweli linaweza kuwa swali la kumuuliza mtu ajibu?
Kwa kuwa unaonekana kupenda sana mambo ya "sheria", nikuulize wewe, kwa nini CCM isifuate sheria, kama hao Democrats wanavyofuata sheria kwa kutowanyima haki zao wapinzani?

Kwa hiyo, unaposema "...mazingira yetu hayafanani...", maana yake sisi hatupashwi kufuata sheria tunazoiga kutoka kwa hao wazungu? Tumetunga sheria zetu wenyewe hapa, lakini hatuzifuati hizo sheria, sasa unadai ni mazingira yetu ndiyo yanayotufanya tukaidi kuzifuata?

Hata upende ku'spin' vipi kuhusu maamuzi ya CHADEMA wakati huu, haiwezekani kamwe kuondoa msukumo wa manufaa kwao katika kuingizwa kwao kwenye chaka nene hili waliloingizwa na Samia, kwa ufundi mkubwa sana wa Kinana, na pengine Kikwete.
Hebu kwanza jibu nilichokuuliza mwanzo, usijibu swali kwa kuuliza swali lingine, hiyo kwangu inaonesha hujui mantiki ya kile unachosimamia.

Naona unaendelea tu kuzungumzia mambo yasiyo na standard, unapenda sana kujadili hisia ndio maana neno sheria limekukera, nani aliesema tuwaige wazungu kila wanachofanya? una hoja nyepesi unazoziamini ni nzito, hatubanwi na yeyote kuiga kila wanachofanya wazungu- fact.

Nimetumia neno sheria kwasababu hiyo ndio standard ya kujua kama mtu/taasisi fulani imekosea au vinginevyo, sijui kwanini matumizi ya hilo neno yakukere! itakuwa ni kwasababu unajua hauna majibu ya kile ulichoulizwa.

Nakuuliza tena, hiyo asali unayolalamika Chadema wamelambishwa [ kupokea ruzuku] au kama huzungumzii ruzuku kwenye asali yako useme, ipo kisheria au haipo kisheria?

Usitake kubadili maana ya kile nilichokuuliza bila sababu, mimi sijawaambia CCM wasifuate sheria popote, sasa unaponiambia mbona wao huwa hawafuati sheria, maana yake unataka na Chadema wavunje sheria!

Unaposema nachojaribu ku-spin hakiwezekani, huo ni mtazamo wako, sikulazimishi uamini tofauti, lakini pia, nawe usilazimishe wengine waamini kile unachoamini wewe, kama umeamua kuimba "asali" bila ushahidi, endelea kuimba mapambio yako ...
 
Hakuna mwenye 'conviction' wala 'commitment' juu ya jambo lolote katika hawa wanaojiita wanasiasa tulionao sasa hivi. Mwanzo hadi mwisho wao ni kujinufaisha wao wenyewe.

Ndiyo maana watu kama Mbowe, baada ya kupitia kwenye misukosuko mikubwa sana kama ile aliyoipitia, na baada ya kuona kama watu hawatambui kujitoa kwake, amefikia hatua ya "kwa nini nihangaikie watu wasiokuwa na shukrani!
Hii ndiyo tafsiri ninayoipata kutokana na matendo yake na maamuzi yake baada ya kutoka jela.
Unaendeshwa na hisia zaidi, hauna fact, na bahati mbaya unatumia hisia zako kuhukumu jambo negatively, this is not fair.

Unaposema Mbowe ameamua kwamba kwanini ahangaike na watu wasio na shukrani, ulikaa nae wapi akakwambia haya?

Unaposema wakina Mbowe wamejinufaisha, kwa lipi baya walilofanya mpaka useme hivyo? hebu tujibu nasi tujue.

Punguza kukataa tamaa kunakosababishwa na kuamini hisia zako potofu, hoja zako zinachekesha sana.
 
Sasa nauliza, hizi mbinu za CCM ya Samia na CHADEMA ya Mbowe inakidhi kweli mlinganisho wowote na wayafanyayo Democratic Party na Republican wa Marekani au Chama cha Labour na Conservative vya Uingereza; au hata vile vilivyoko Ujeruman kwa namna yoyte ilei?
Ila nyie wasomi mnashangaza sana, wapinzani walisema tunahitaji tume huru, bunge live, sijui demokrasia kama USA mnatusema kwamba tunataka kuiga wakati mazingira ni tofauti!!

Kujibu swali lako, hawahitaji kufanya maridhiano huko nje maana mtu akiangushwa anaangushwa wazi bila excuse sio kama huku rafu nyingi so Kila chaguzi ni zaidi ya vita.

So kwa context ya Africa maridhiano kibao yamefanyika, tuliona Tsvangirai Zimbabwe, Tuliona Mandela sauzi, Odinga Kenya, na Garang kule Sudan.

So kwa Afrika sio kitu kigeni
 
'Of course' hatuwezi kuwa "waigaji" siku zote, sasa niambie tuanze kuhimiza waje waige nini, kutekana, kuvunja sheria tunazotunga sisi wenyewe, n.k..?
Kumbe unajua hatuwezi kuwa waigaji siku zote, basi ulichoandika kule juu kwangu hakina maana tena, ndio maana nikakwambia huna hakika na mantiki ya hoja unayosimamia, ndio maana ukajibu swali langu kwa kuniuliza maswali yako, pale ulikuwa unanikwepa tu, lakini jibu ndio hili uliloandika hapa!.
 
Ninakusikiliza wewe mkuu, lakini dalili zote zinaonyesha CHADEMA iliyohimiri zile "risasi" haipo tena; ishateketezwa na njia mbadala ambazo hazikuhitaji matumizi ya risasi.

Kuna watu mafundi sana wa mambo haya, kwa hiyo usije ukashangaa ukiona mwisho wa siku ile CHADEMA uliyokuwa ukiifahamu haipo tena.
Kadri navyozidi kukusoma nacheka tu, unazungumzia dalili na sio fact, halafu unahukumu kupitia hizo dalili, subiri fact ndio uhukumu, haraka na pressure za nini?

Inaonekana propaganda za lumumba zimekuingia sana, wale waliosema leo Mbowe atatangaza kuwasamehe kina Mdee, vipi wamesahewa?!

Rilaxx.
 
Back
Top Bottom