Body languages, tones na facial expressions za viongozi waandamizi wa chadema hususani wa kamati kuu, zinaonyesha kabisa bado kuna migawanyiko na uhasama ndani ya chadema.
Lakini pia jana pale Ikungi Singida tumeshuhudia kwa uwazi zaidi kwamba umoja ni changamoto ndani ya uongozi mpya wa chadema, kuaminiana kwa viongozi wapya wa chadema kuna tia mashaka sana, na nikama kuna kamgomo baridi hivi kwa baadhi ya viongozi wa kanda jirani, wilaya na mikoa jirani katika kujitolea kwenye shughuli za chama hususani kwenye kuhudhuria tukio kubwa kama la kumpokea kiongozi wa chadema taifa pale Singida.
Kuna mnyukano na kushughulikiana kimya kimya kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhujumiana au kususiana kwenye kufanikisha agenda za chama. Bilashaka kwenye uchaguzi, hii itakua fimbo muhimu ya kukomoana chadema.
Ni mwendo wa kulazimisha furaha na smile za kinafiki miongoni mwa viongozi waandamizi wa chadema. Unaona kabisa kiongozi wa chadema kashika mike anaongea but mwili uko pale but moyo unawaza kwingineko kabisa.
Ni muhimu sana hatua za makusudi za maridhiano zikachukuliwa ili kuepusha kuumizana wenyewe kwa wenyewe, kitu ambacho pia kitawaharibia na kuwarudisha nyuma wao wenyewe.
Wasione aibu kutumia falsafa ya 4Rs za Dr.Samia Suluhu Hassan zitawasaidia sana kua pamoja.Chadema kuna changamoto ya ummoja.
Una maoni gani ndugu mdau?π
Mungu Ibariki Tanzania.
Hivi mnataka nchi ya namna gani ?
Chadema wametuonyesha njia ya demokrasia na uchaguzi huru na wa Haki.
Kwenye uchaguzi wowote ni lazima mshindi apatikane Hata kwa kura mbili.
Na anayeshindwa hawezi kushangilia bali anahuzunika .
Huo ndio uchaguzi .
Demokrasi gharama yake ndiyo hiyo kushindwa na kukubali kushindwa.
Duniani kote uchaguzi unapoisha wanaoshabikia ni sale walio shida . Mambo ya maridhiano ni upuuzi .Maridhiano ni ngonjera za CCM kutokana na kutesa wetu ,kuua,kuteka wetu ,kuiba kura ,kuengua wagombea na kila aina ya dhululuma . Sasa hapo CCM wakaona aibu kua wamefanya uovu mbaya . Hata hivyo maridhiano ya upende mmoja sio maridhiano bali ni sakosaji walitakiwa waombe msamaha .
Samia alitakiwa aseme tusameheane sio maridhiano .
Maridhiano hua inaundwa tume kabisa ili kupaanisha pande mbili zilizoumizana kwa ubaya.
maridhiano yanatakiwa yawe ya wazi na yawahusu walioumizwa na pia familia zao.
Maridhiano ya Chadema na CCM yamezaa matunda gani kama CCM wenyewe hawana uvumilivu.
Yaani kwa miaka 30nm CCM na serikali yake wamekua wakiwaumiza Chadema halafu leo bado eti Njooni tuzungumze?
Mazungumzo ya Simba na Swala ni Hadaa.