Maswali kwa Profesa Musa Assad kuhusu mkataba wa Bandari

Maswali kwa Profesa Musa Assad kuhusu mkataba wa Bandari

Mnakubaliana chumbani? Mnaliondoa kwa siri? Au waliliondoa baada ya kuwa na wazo la kuuza za Watanganyika? Kuna kitu mbaya kitakuja, sidhani kama watanganyika watakubali hili kutendeka kwao......
Hebu kwanza: Hivi hili swala la kuiondoa bandari ya Zanzibar kutokuwemo kwenye maswala ya Muungano, lilijadiliwa na kupitishwa Bungeni?
Au ni ule utaratibu tu wa kushughulikia "kero za muungano' ndio uliotumika?

Mwenye kujua hili tafadhali alieleze hapa vizuri nasi tuelewe utaratibu uliofuatwa hadi bandari ya Zanzibar likawa siyo swala la muungano.

Kuna mambo mengi yamefanyika kienyeji enyeji tu, huko Zanzibar wanajiamlia kufanya mambo ambayo hawana mamlaka nayo.
 
For the first time ndo nagundua kwanini JPM alimstaafisha.
 
Kuna Bosi wangu mmoja aliwahi kuniambiaga.

"Don't Believe a Muslim when he talks about other Muslims"

Sikuelewaga alimaanishaga nini hadi hii leo.
 
Nimekuuliza swali, je umeshaona hayo maeneo ya kipaumbele?
Ni nani anayeamua kipaumbele kiwe nini, anayefanyiwa kazi, au anayetafuta riziki ya kufanya kazi hiyo?

Kipaumbele cha leo, hakiwezi kuwa tofauti na kile cha kesho?
Itakuwaje wewe unayetafuta ajira kwangu ndiye unipangie kipaumbele kwa vile unaona utanufaika zaidi na kazi unayochagua mwenyewe uifanye hata kama kwangu hainiletei manufaa makubwa?

DP World, siyo mwekezaji pekee duniani kwenye maswala haya, kwa nini apewe kipaumbele yeye na upendeleo, zaidi ya wengine?
 
Mkataba hauna shida yoyote. Twenye shida sisi wasomaji wa mkataba
Inawezekana wewe unasoma mkataba ambao wengine hawajauona, vinginevyo usingehitimisha namna hii hata kama ungezima akili yote isione dosari zilizomo kwenye mkataba huo.
Hao walioandika huo mkataba walitoka wapi, peponi?
Walijua kuwa mkataba huu ndio sahihi kabisa kwa kila kitu kwa nchi inayoitwa Tanzania; kwa hiyo usihojiwe na yeyote, atakayehoji "anashida"?
Hizi ni fikra za ajabu sana. Inashangaza kwa mtu kuziwasilisha mbele za watu wenye akili timamu waone kilichomo ndani ya fikra hizo.
 
Profesa Emaratius Issa Shivji ni pure genius.

Unadhani kila mwanasheria ni Wakili? Kichwa kisicho na akili kama chako ni mzigo tu kwa shingo.
He is just a philosopher and purely rhetorical man hakuna lawyer pale. shauri yako.
 
pande zote mbili zinatawaliwa na udini
Ni pamoja na wale wanaopiga mayowe ya Mwarabu Mwarabu Mwarabu.
Je ingekuwa DP World ni ya Mmarekani wangepiga mayowe ya Mmaraekani Mmaekani? Sidhani
 
Haya siyo maswali ya kujibu Professor Assad. Hata sisi wanafunzi wake tunaweza kukujibu vizuri kabisa.

Jibu kwa swali la Kwanza.
Bandari ya Zanzibar haipo kwasababu muwekezaji hana interest na Bandari hiyo kutokana na Investment Plan yake. Hajaona faida ya kuendeleza Bandari ya Zanzibar huku akijua biashara ipo Rwanda, Zambia, Malawi, DRC, Burundi na mikoa ya mbali. Hiyo mizigo atayoishushia Zanzibar itaenda wapi? Hivi hili nalo linahitaji muende mahakamani nyie wapinga maendeleo.

2. Jibu kwa swali la pili
Japo kuna mgawo wa kitaaluma lakini hakuna ownership of knowledge. Yeyote anaweza kuelewa chochote.

3. Jibu kwa swali la tatu
Hakuna hoja ya maana ndio maana professor Asad hakuna haja ya kujibu upotofu. By the way, hoja zenyewe zimekuwa zikibadilika siku hata siku na kutokana na mtu na mtu. Wako wanaosema mkataba, wako wanaosema mgeni asipewe nafasi ya kufanya uwekezaji katika Bandari, wako wanaosema watanzania tuna uwezo, mitaji na teknolojia. Yaani vurugu mechi.
Professor Asad amekuwa smart kwa kugusia upotoshaji unaofanywa kwenye maeneo machache hususan umiliki na matumizi ya ardhi.

Kama mizigo inayoshushwa bandari ya Zanzibar haina kwa kwenda kuna umuhimu gani wa kuwepo hiyo bandari ya Zanzibar? Fikiri kwa kutumia kichwa cha juu!
 
Kwa hiyo kuendeleza bandari ni kwa manufaa ya mwekezaji tu? Je, baada ya 'ukomo' wa mkataba, Tanzania isingependa kubaki kunufaika na miundombinu itakayoachwa na mwekezaji? Kwa nini utaje faida anazoangalia mwekezaji tu, na sio pia za nchi inayohost? Kwani Tanzania haitaki kuachiwa bandari ya Zanzibar ikiwa nzuri ya kisasa hata kama ilikuwa haimlipi mwekezaji?

Tena umemwuliza swali sana na kwa nyongeza ni kuwa kama bandari ya Zanzibar isingekuwa na manufaa basi isingekuwepo, lazima ajue hilo.
 
Mnaabudu vyeti!
Bakhresa hana cheti lkn huyo Nshala mwenyewe analipwa na Matajiri ambao hata fom4 hawaijui

Ndiyo lazima alipwe kwa utaalamu wake, kwani wao nani aliwazuia wasisome? Wajinga ndiyo waliwao!
 
Kuitwa Professor haimanishi huwezi kuwa pumbavu... He's just a shithole ktk masuala ya international treaties
 
Mkataba hauna shida yoyote. Twenye shida sisi wasomaji wa mkataba. Wewe unadhani DPW wataendeza kila Bandari kama mnavyoaminishwa na akila TL? Yaani akajenge Bandari kisorya au Lindi?? Kwani wanaosema maeneo ya kipaumbele unadhani ni yepi? Ushasikia popote duniani DPW anaendeleza na kuendesha Bandari za kuvulia dagaa tonge? Unajua baadhi ya mambo inabidi mtumie akili zenu hata za kuzaliwa basi! Believe me, tunaaminishana ujinga mkubwa sana mitaani kuliko uhalisia wa jambo lilivyo.

Kwa nini sasa wanekwenda mpaka bandari za Mwanza, Nyasa, n.k?
 
Wewe unamjua huyo "mwanasheria wenu wa Ujerumani", mimi simjui, kwa hiyo usinihusishe na hilo.
Hizo hatua 4 zilizoonyeshwa hapo kama kuelimisha ni upuuzi mtupu.
Elezeni, IGA inahusika vipi na hizo IGA na hizo hatua za upotoshaji mnazofanya hapo?

Kama mnaona IGA haina maana kwenu, iondoeni, tuendelee na hizo HGA, tupigiwe huko huko.
Ukisema humjui mwanasheria wa Ujerumani maana yake umeingia kwenye uzi bila kusoma hoja na video za muanzisha uzi😇😇
 
Nimesoma andiko lako kuwa watu HAWANA UELEWA ndiyo maana wanakataa mkataba wa DP World. Nomba kwa manufaa ya wengi ujibu hoja hizi mbili tu. Kumbuka wewe ni "national Figure" in academics, tamko lako linaamsha maswali)

1. Kama mkataba una manufaa , kwanini bandari za Zanzibar hazipo? (kizuri kweli uache kula na ndugu zako Zanzibar, uwape jirani?)

2. Wewe si mwanasheria (unaweza ukawa na uelewa kidogo wa sheria za uhasibu and the like). sasa authority ya kusema akina Shivji, Lugemeleza, Lisu, Mwabukusi, Madeleka na wengine hawana uelewa katika International treaties unaitoa wapi?

3. Mbona hujajibu hoja kwa hoja ambazo hao niliowataja hapo juu wanazilalamikia? Umetoa blanket answers kama za Joseph Kasheku Msukuma, Kitenge, Wasira na watu kama hao. Kama msomi you need to be specific when answering questions...kama ilivyokuwa ukiwataka wanafunzi wako wajibu



Hii habari ya prof. Asad imepostiwa kama vichapisho. Ukimuuliza atakwambia sio yeye. Watu wanatumia tu jina lake. Siamini kama Prof. Anawezaisahau AUDITING kwa kiwango cha lami.
Tunatafuta mwekezaji. Je, tulikuwa na HADIDU ZA REJEA? Yaani Client's requirements? Kwa lugha nyepesi ni vitu gani tulitaka viboreshwe na mwekezaji?
Je, tuliitamgaza au hata kuteuawa wawekezaji hata watatu tuwashindanishe? Kama sheria Na. 7 ya mwaka 2011 inavyotutaka? Ikisomwa pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2016.
Je, tutapimaje ufanisi wa mwekezaji kama hatuja ahinisha vipaumbele tunavyokusudia kuviboresha?
MKataba umesema, hataondolewa hata akikiuka masharti ya mkataba, hata hivyo madharti kapewa na nani? Wakati inavyoonekana, mkataba kaudraft mwenyewe masharti siyaoni!!
Prof. Asad anasingiziwa tu. Tusimsumbue. Sisi tusubiri hukumu. Walalamikaji wakishindwa, WAKATE RUFAA. Walalamikiwa wakishindwa WAKATE RUFAA. Mpaka kitaeleweka tu. Ngoma ikilala 2025 yaja. Pia ni maamuzi.
 
Alitimuliwa huyu profesa kiazi na Magufuri
watu tukamuonea huruma na IST yake

Ila HAKIKA Magufuri alikuwa na kitu cha ziada mno
basi hatukumuelewa!

Magufuri alikuwa ameishaona humu hakuna cha uprofesa bali ni njaa na ubwege

Wote aliowatosa akina Lugola, Makanba, Nape na wengine
hapo awali tulihisi anawaonea
Kumbe hawafai hata kuwa Balozi nyumba 10/10

Huyu Assad kwanza anatokea wapi
sio Zanzibar kweli?

coz it’s like wote wametuzoea mno
Kuna kitu inabidi tu kifanywe
 
Nimesoma andiko lako kuwa watu HAWANA UELEWA ndiyo maana wanakataa mkataba wa DP World. Nomba kwa manufaa ya wengi ujibu hoja hizi mbili tu. Kumbuka wewe ni "national Figure" in academics, tamko lako linaamsha maswali)

1. Kama mkataba una manufaa , kwanini bandari za Zanzibar hazipo? (kizuri kweli uache kula na ndugu zako Zanzibar, uwape jirani?)

2. Wewe si mwanasheria (unaweza ukawa na uelewa kidogo wa sheria za uhasibu and the like). sasa authority ya kusema akina Shivji, Lugemeleza, Lisu, Mwabukusi, Madeleka na wengine hawana uelewa katika International treaties unaitoa wapi?

3. Mbona hujajibu hoja kwa hoja ambazo hao niliowataja hapo juu wanazilalamikia? Umetoa blanket answers kama za Joseph Kasheku Msukuma, Kitenge, Wasira na watu kama hao. Kama msomi you need to be specific when answering questions...kama ilivyokuwa ukiwataka wanafunzi wako wajibu


njaa mbaya mkuu na yeye siyo yeye tangu awamu ya tano imvuruge hajakaa sawa kabisa huyo mzee
 
Back
Top Bottom