Mbeya: Mlima Kawetele wameguka, nyumba zaidi ya 20 zadaiwa kufunikwa

Mbeya: Mlima Kawetele wameguka, nyumba zaidi ya 20 zadaiwa kufunikwa

Salaam, shalom!!

View attachment 2963343

Mlima kawetele ulioko ITEZI, Uyole, jijini Mbeya umeripotiwa kumeguka na kuziangukia nyumba zaidi ya 20.

Chanzo Cha janga Hilo inasemekana ni mvua nyingi zinaonyesha Nchi nzima, zilizoloanisha udongo Kwa kiasi kikubwa.

Mwanzoni, iliaminika walioko milimani wako katika USALAMA zaidi, kumbe Si Kweli, Mvua za ernino ndio kwanza zimeanza, tuendelee kuwa na Tahadhari na kudumu katika maombi.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA [emoji1241]
Amen.

Source: ITV


Itezi Mbeya

----
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Abdi Isango

Ni kweli sehemu ya mlima imeporomoka na tope kusambaa na kuharibu nyumba 17 pamoja na Shule ya Msingi ya binafsi.

Nyumba zimebomoka kabisa hazionekani, ni kama vile hakukuwa na nyumba, tope limesabaa hakuna kipande cha bati au ubao.

Hakuna madhara kwa binadamu isipokuwa wenyeji wanasema kuna ng’ombe wanne wamesombwa na tope hilo.

Uchunguzi wa awali umebaini chanzo ni mvua kubwa zinzoendelea kunyesha, mvua zilinyesha jana na usiku wa kuakia leo, ambapo Alfajiri ndipo tope likaasambaa.

Wenyeji wanasema kwa kuwa kuna shughuli za kilimo, inawezekana kilimo kimesababisha udongo ukose mshikamano na hivyo mvua inaponyesha inakuwa rahisi kukatika.

Chini ya huo Mlima kuna Mto, mbapo umesomba tope hilo Kwenda mbele zaidi, tope lilikuwa kubwa, limesambaa na kusababisha madhara pia katika nyumab nyingine kadhaa.

Mkuu wa Mkoa na Kamati ya Ulinzi wamefika eneo la tukio na kutoa maelekezo ya tahadhari, Wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari kwa kuwa mvua zinaendelea kunyesha, pia wanaojenga karibu na mito nao wametakiwa kuchukua tahadhari kwa kuwa mvua bado zinaendelea kunyesha.
View attachment 2963359

View attachment 2963656View attachment 2963657View attachment 2963658
Laana ya Mungu dhidi ya nchi ilikubali kuongozwa na subhumans CCM Kwa miaka zaidi ya sitini
 
Kwa sasa havipo, na hiyo ni jukumu la wataalam, siyo maombi.
Maombi hayajawahi kuzuia wataalamu kufanya KAZI Yao,

Tatizo pale ni mvua kuzidi limits,

Hao wataalamu wanaweza kufanya nini Ili kuzuia Ernino nchini
tumrudie mungu ili mwisho wetu uwe salama
Hilo ndilo Mungu analitaka,

Ttukiacha UOVU na kumrudia Mungu, hatutopata majanga hayo, tutaishi maisha yenye salama zaidi.

Ubarikiwe!!
 
Maombi hayajawahi kuzuia wataalamu kufanya KAZI Yao,

Tatizo pale ni mvua kuzidi limits,

Hao wataalamu wanaweza kufanya nini Ili kuzuia Ernino nchini?
Kazi ya,wataalam sio kuzui mvua ni kutafiti if there is further posibilities of posible land slides, and to advice and allocate a safe place to live, and for other human endevors.
Wakiisha hama kama ni permanet problem au kujenge kingo kuzuia kama ni tatizo la muda wataende huko kwenye maombi.
Maombi hayana tija hapo kwa sasa.
 
Kazi ya,wataalam sio kuzui mvua ni kutafiti if there is further posibilities of posible land slides, and to advice and allocate a safe place to live, and for other human endevors.
Wakiisha hama kama ni permanet problem au kujenge kingo kuzuia kama ni tatizo la muda wataende huko kwenye maombi.
Maombi hayana tija hapo kwa sasa.
Umewahi kuwa mchawi?

Kwanini hutaki wananchi wamwombe Mungu?
 
Back
Top Bottom