Mbinu nayotumia kumlea mwanangu anayesoma private awe mjanja, awe na furaha, asigeuke kuwa kuku wa kisasa

Mbinu nayotumia kumlea mwanangu anayesoma private awe mjanja, awe na furaha, asigeuke kuwa kuku wa kisasa

Safi Sana hongera kwa kutuandalia amiri Jeshi mkuu asiejua kulemba lemba, kazi kazi.


Acha hao wazazi wanaowapakia asali kwenye soseji watoto wao waje kuvuna wanachokipanda Sasa hivi. Mtoto inabidi awe ngangari .. Yuko flexible kwa mazingira yoyote hata akisikia corona ndio kwanza anapandwa na mzuka wa kuikabili , sio mitoto ya ushuani ikisikia corona inajificha chini ya uvungu na kulegeza Sana eti "Daddy I'm gonna Die" huku akirembua.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upo sahihi,lkn mimi huwa namchanganya pia kitaani,mfano huwa naenda nae mazoezin asubuh uwanjan ambapo ni mchangani na akifika hapo anacheza mpira na watoto wa shule za kata. Hii imenifanya kuona tofaut yake yeye na hao watoto, yeye anakosa ushapu lkn siku zinavyokwenda anabadilika. Nisichopenda kwa watoto wa kata ni tabia mbaya kama matusi nk, sasa nikiwepo wanaogopa kutoa hayo maneno ya ovyo.
Mkuu mtoto anaandaliwa kuja kuishi huo ulimwengu wa matusi kwanini unamzuia kuyasikia ?? , Kama ana umri mkubwa muongoze kujua hayo ni matusi hapaswi kuwa na hiyo tabia ila sio wewe kumzuia asiyasikie tunakosea maana mwisho wa siku watoto watakuja kuishi ulimwengu huu huu uliojaa kila aina ya uchafu, kazi yetu ni kuwaonesha na kuwachambulia au kuwaonesha huo uchafu wasiushiriki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tafuta peasa jomba hayo yote sijui kubinuka sarakasi, kutjifunza kutega ndege, kuogelea kwenye mabwawa ya kichocho ni umaskini tu.

Familia zenye uwezo huwezikuta na hizo mabo kaka .Mo Dewj ampeleke mwanae kutega ndege sijui sarakasi za kinyumenyume mtaani wakati wataalam wa hizo mambo wapo ni uwazimu.

Pesa ikiwepo shule unachagua mwenyewe. Mbona watoto wanakwenda matour mpaka nje yanmipaka ya nchi achilia vivutio vya humu nchini?

Pesa ikiwepo mtoto anapata exposure ya kutosha tofauti na wakwako anaeshinda anawinda ndege na sarakasi za kinyume nyume bila skills.

Tunaeapeleka watoto kwenye training za kuogelea, marshal art ili baadae ziwe fursa ya kujipatia pesa. Sasa wewe wa kwako anashinda anaogelea matopeni na kupauka inaishia hapo hawezi kushiriki hata mashindano ya kuogelea, kukimbia, marshal art kwa sababu hana skills za kutosha na hajilui rules.

Hana networks zaidi ya wahuni wa mtaani kwao, hana exposure zaidi ya mtaani kwake na bibi ake, hajawai kwenda tour ya maana zaidi ya kwenda porini kuwinda panya.

Yawezekana we ndo kwanza umeanza kuzaa na huyo ndo mtoto wako wa kwanza . Nimekuuliza malezi hayo pia ni kwa mtoto wa kike? Hukujibu.

Kuhusu mtoto kuwa kwenye kumi Bora darasani naona na wewe umekaririshwa kwamba akili inaanzianmoja mpaka kumi, pole sana.

Wenzako hatuagalii hayo manamba bali tunaangalia mtoto anapata nini, amekosa nini, anajua nini, anaweza nini, anapenda nini na anakipaji gani ili aendelezwe huko. Huwezi lazimisha mtoto awe eti kwenye kumi Bora ndo uone ni mafanikio, kumbuka kuna ngazi za elimu hakuna hizo mambo ulizo karirishwa eti kumi bora.

We unadhani hao waliofanikiwa walikuwa kwenye 10 bora? Pesa ikiwa ya mawazo mau ya uganga ndo utakuwa na kuishi katika mawazo ya karne ya 15 wakati dunia inakimbilia karne ya 22.

Nasisitiza, tafuta pesa acha kumtesa mtoto eti azoee maisha halisi.
Kwanini umtabirie mtoto maisha ya kimaskini. Basi hata viatu usimnunulie mwache atembee pekupeku maana ndo maisha halisi ya huko kijijini mnakoishi.

Mwisho jukumu la kulea na kufunza ni lako mzazi, hizo mambo ya kwa bibi ni kukimbia majukumu.
Lazima mzazi aweze kubaini kuwa mtoto anatakiwa afundishwe changamoto za dunia ya sasa na mwelekeo wa dunia ijayo.

Sasa we mshindishe kwa bibi yake afundishwe kutega mitego ya panya eti ndio ujanja tuone itamsaidia nini akisha fahamu.

Usikariri maisha ya kimaskini bro. Tafuta faranga!

Sent using Jamii Forums mobile app
Una kiwango kidogo Sana cha fikra

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunafanana kidogo, mi mwanangu yupo grade 3, akiwa likizo namfunza Javascript for kids ambayo baada ya muda ataanza ku develop cartoons na baadae web. Big up.
Hiyo unaipata wapi mkuu? Nataka nijenge misingi ya watoto wangu wote wakiwa wadogo
 
Ntaka nikupe taarifa tu, Hakuna watu ambao wapo very socially awkard kama watu wanao deal mno na computers, kuanzia hackers, software developers, n.k hawa watu asilimia kubwa mno wapo socialy awkard na ninakupa homework ufanye research,

Muwe mnawatoa toa nje watoto wenu wasishinde ndani Hayo mambo ya kujifunza lugha za computer hizo mlizozitaja ama kukesha sana na pc yanaanzaga kutenegeneza uraibu flani hivi wa kuwa na pc muda mwingi na kujitenga na jamii, Ndio maana maisha ya programmers, online workers, gamers, internet trolls, web developers wengi yanakuaga ni lonely sana na kuanza kusingizia anti social na intrivert kumbe ni maisha wanayoishi


Nawashauri watoto wenu wafanye shughuli za nje ya nyumba kuliko kukaa kaa ndani, Hayo mambo ya java script, html, n.k naona tuwaachie wenzetu wazungu ambao ni wapweke mno rafiki zao ni mbwa, Ila kama utamfundisha hakikisha ana muda wa ku participate kwenye mambo ya social.

Huyu wangu saizi kawa muongeaji na mcheshi sana na pia anaruka sarakasi na bora iwe hivi kuliko awe introverted geek
Udhaifu wa malezi usiwe sababu ya kunyooshea kidole fani nyingine. Jifunze kuweka mizania kwenye kila jambo, usidhani huko anakoshinda akiogelea na kuruka sarakasi ndio yuko salama sana. Labda hujui maana ya malezi, huko huko wapo wavuta bangi, mateja, majizi n.k.

mambo yote yafanyike kwa kiasi na pia chini ya uangalizi. Usifurahi sana kwamba mwanao ni mjanja kupita wanafunzi wote shuleni ama darasani kwao, bali furahi kwa sababu anakua katika tabia njema huku akiwa na moyo wa kujifunza. By the way, mtoto ambaye miezi kumi anakuwa shuleni boarding na wanafunzi wenzake bila computer anaweza vipi kuwa anti social? Huoni kwamba hiyo logic yako iko flawed?
 
Upo sahihi,lkn mimi huwa namchanganya pia kitaani,mfano huwa naenda nae mazoezin asubuh uwanjan ambapo ni mchangani na akifika hapo anacheza mpira na watoto wa shule za kata. Hii imenifanya kuona tofaut yake yeye na hao watoto, yeye anakosa ushapu lkn siku zinavyokwenda anabadilika. Nisichopenda kwa watoto wa kata ni tabia mbaya kama matusi nk, sasa nikiwepo wanaogopa kutoa hayo maneno ya ovyo.
Mkuu, huyu mdau anafikiri watoto wanashinda kutwa kucha kwenye kompyuta. Ni mtazamo hasi kwani mtaani watoto wengi wanaharibika kwa kuiga tabia zisizofaa, kila kitu kifanyike kwa kiasi. Mimi mwanangu nishasema ni mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya kutwa, sasa sijui huko anajifungia peke yake?
 
Udhaifu wa malezi usiwe sababu ya kunyooshea kidole fani nyingine. Jifunze kuweka mizania kwenye kila jambo, usidhani huko anakoshinda akiogelea na kuruka sarakasi ndio yuko salama sana. Labda hujui maana ya malezi, huko huko wapo wavuta bangi, mateja, majizi n.k.

mambo yote yafanyike kwa kiasi na pia chini ya uangalizi. Usifurahi sana kwamba mwanao ni mjanja kupita wanafunzi wote shuleni ama darasani kwao, bali furahi kwa sababu anakua katika tabia njema huku akiwa na moyo wa kujifunza. By the way, mtoto ambaye miezi kumi anakuwa shuleni boarding na wanafunzi wenzake bila computer anaweza vipi kuwa anti social? Huoni kwamba hiyo logic yako iko flawed?
Hapo nmekusoma sana mzee kwenye hio point yako "usifurahi sana kwamba mwanao ni mjanja kupita wanafunzi wote shuleni ama darasani kwao, bali furahi kwa sababu anakua katika tabia njema huku akiwa na moyo wa kujifunza", Kuna jambo la ziada imebidi nikubali tu liniingie.

Ohh kumbe yupo boarding hapo sawa, Computers zipo very very adictive, Nina rafiki yangu nakumbuka aikuwa hacker aisee ni balaa, anaweza kukaa ndani siku 3 huko anafanya dumoing za mizigo ya sql, n.k ni addictive sana maana mtu akijua html atataka ajue css akijua hio atataka ajue java script, before you know it kaanza kuwa addictive sana, Ila sio wote. Kwa ushauri wangu naona utafute vijana wa IT hawa ambao wamehitimu ila hawana kazi, wengi wapo nondo kwenye coding ukiwalipa hata 50 per week hawana tatizo

Kwa clarity tu kwenye paragraph yako ya kwanza, Mtoto wangu hashindi na watoto wowote tu wasio na mbele wala nyuma, Hapo nje kidogo ya mji anapokwenda nina historia na wazazi wa watoto wengi ambao ni marafiki zake mtoto wangu, Life la huko lipo kijamii sana maana muda mwingi watu wapo majumbani sio kama huku mijini hata kujua a to z za mtu fulani ni kazi
 
Hata kuwa shoga kabisa...... Lazima mtoto mfundishe mazingira yote yote.

Mimi sifurahii mazingira niliyolelewa yaani sijui kucheza mpira, sijui kuogelea, sijui kucheza draft wala bao, sio shabiki wampira aina yoyote yaani nipo ipo2 kidogo tena kidogo sana kwenda club au live band

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu unafanana na mimi
Mimi licha ya mzee kuwa mjeda na mkaksi alitufungia sana ndani. Japo mpira nilikua na kipaji ila mzee alinikazia kwenda academy ng'ambo. Ila nilikua sijui kuogelea, kuchinja kuku, kukata kuni, kupika na mengineyo.

Nimekuja kubadilika ukubwani japo kuna mambo nalipia gharama zake. Yaani nimejifunza sana aisee...binti yangu ninamkuza tofauti sanasana. Namjengea uwezo wa aina yake.
 
Tafuta peasa jomba hayo yote sijui kubinuka sarakasi, kutjifunza kutega ndege, kuogelea kwenye mabwawa ya kichocho ni umaskini tu.

Familia zenye uwezo huwezikuta na hizo mabo kaka .Mo Dewj ampeleke mwanae kutega ndege sijui sarakasi za kinyumenyume mtaani wakati wataalam wa hizo mambo wapo ni uwazimu.

Pesa ikiwepo shule unachagua mwenyewe. Mbona watoto wanakwenda matour mpaka nje yanmipaka ya nchi achilia vivutio vya humu nchini?

Pesa ikiwepo mtoto anapata exposure ya kutosha tofauti na wakwako anaeshinda anawinda ndege na sarakasi za kinyume nyume bila skills.

Tunaeapeleka watoto kwenye training za kuogelea, marshal art ili baadae ziwe fursa ya kujipatia pesa. Sasa wewe wa kwako anashinda anaogelea matopeni na kupauka inaishia hapo hawezi kushiriki hata mashindano ya kuogelea, kukimbia, marshal art kwa sababu hana skills za kutosha na hajilui rules.

Hana networks zaidi ya wahuni wa mtaani kwao, hana exposure zaidi ya mtaani kwake na bibi ake, hajawai kwenda tour ya maana zaidi ya kwenda porini kuwinda panya.

Yawezekana we ndo kwanza umeanza kuzaa na huyo ndo mtoto wako wa kwanza . Nimekuuliza malezi hayo pia ni kwa mtoto wa kike? Hukujibu.

Kuhusu mtoto kuwa kwenye kumi Bora darasani naona na wewe umekaririshwa kwamba akili inaanzianmoja mpaka kumi, pole sana.

Wenzako hatuagalii hayo manamba bali tunaangalia mtoto anapata nini, amekosa nini, anajua nini, anaweza nini, anapenda nini na anakipaji gani ili aendelezwe huko. Huwezi lazimisha mtoto awe eti kwenye kumi Bora ndo uone ni mafanikio, kumbuka kuna ngazi za elimu hakuna hizo mambo ulizo karirishwa eti kumi bora.

We unadhani hao waliofanikiwa walikuwa kwenye 10 bora? Pesa ikiwa ya mawazo mau ya uganga ndo utakuwa na kuishi katika mawazo ya karne ya 15 wakati dunia inakimbilia karne ya 22.

Nasisitiza, tafuta pesa acha kumtesa mtoto eti azoee maisha halisi.
Kwanini umtabirie mtoto maisha ya kimaskini. Basi hata viatu usimnunulie mwache atembee pekupeku maana ndo maisha halisi ya huko kijijini mnakoishi.

Mwisho jukumu la kulea na kufunza ni lako mzazi, hizo mambo ya kwa bibi ni kukimbia majukumu.
Lazima mzazi aweze kubaini kuwa mtoto anatakiwa afundishwe changamoto za dunia ya sasa na mwelekeo wa dunia ijayo.

Sasa we mshindishe kwa bibi yake afundishwe kutega mitego ya panya eti ndio ujanja tuone itamsaidia nini akisha fahamu.

Usikariri maisha ya kimaskini bro. Tafuta faranga!

Sent using Jamii Forums mobile app
Umenena vizur....
 
Una kiwango kidogo Sana cha fikra

Sent using Jamii Forums mobile app
Yuko sahihi kabisa. Huenda we ndo unakiwango kidogo cha fikra

Malezi ya mtoa mada ni ya lower class na middle class, yanamsaidia mwanae kukopi na huko huko middle class kwake na lower class kwake.

Mwanangu wa baadae eti nije kumuexpose muda wote sijui kwa bibi kwa mjomba kwa shangazi kwa watoto wa mtaa nisiojua malezi yao wala akili zao ni Noo kubwa, maana najua influence kubwa kwa mtoto kutoka kwa watu anaohusiana nao, wanamtendea vipi?! Anapitia experince zipi?! Ni za muhimu au ni garbage za kuja kumuathiri kiakili huko mbele!!
Watu maskini na wa kati ndo huwa na muda sana na ujinga mwingi wa kujua jua watu na marafiki wasio na tija maana hawana individual identity ila identity ya mtaa mara ooh kijijini kwetu mara ooh wilayani kwetu, wanataka wamjue kila mtu na wamzoee kila mtu maana hawajitegemei

Upper class hawana marafiki ila wanaconnection. Wanakutana na watu wa class yao tu, hayo yote sijui social skills wanafundishwa na proffessional mentor na wanasocialize within their class na ndio wanalead uchumi na hata nchi pia.Na wengi wapo mentally strong kutoka na exposure kubwa ya watu wa hali ya juu na Dunia kwa ujumla.Na wala hawawafungii watoto bali wana limit na mipaka, wanawapa watoto wao nafasi ya kuwa exposed kwa watu wa class yao marafiki wa class yao,na kwenda sehemu za class zao na hivyo wewe wa kawaida sio rahisi kuwaona, hawaendi endi tu eti kwa jirani, eti mtaani eti kisa tu ni kwa jirani au ni mtaani, hawahusiani na watu wasiowajua kiundani.

Kuwafungia ndani ya geti watoto anakokumaanisha mtoa mada labda ni yale maget kali yale middle class family na lower class family. Unakuta nyumba ipo katikati ya tandale lakini yenyewe tu ndo nzuri na inageti kwa hiyo wazazi wanaoishi humo watakua na akili za kitandaletandale zile hawalei chochote ila wanasema wanalea, zile mtoto anaamka anavaa anaenda shule anakula analala kesho yake mzunguko unaendelea hivyo hivyo, yaani mzazi hana muda na mtoto wala hana muda wa kuinteract na mtoto, akimpeleka tuition ni zile tuition za kemia historia jiographia, yaani anasoma ya darasani tu. Mtoto hampeleki hata tour ndani ya nchi/nje ya nchi kumfundisha vitu vya muhimu au kumsajili kwenye madarasa ya muhimu. Huyo anafuga halei, matokeo yake ndo anafikiri sasa kumfungulia mtoto ni kumfungulia kwenda kucheza na watoto wa mtaani eti ndo watamfundisha na kumfanya awe mjanja.
 
dudu jeupe,
Vipi Kama wapo swimming club za shule home Wana jifunza karate na mafunzo ya ukakamavu, wanakwenda kucheza tenesi na wenzao wa gate Kali...

Yaani sijakuelewa unataka wacheze na watto wa mitaani, Yaan wale watoto wasio na heshima Wana matusi mazito na tabia mbovu na adabu chafu...Aisee Bado ujanishawish wewe mlee mtoto Wako hivyo alafu siku akutane na junior wangu Yaan nikumuacha kwako utamrudisha mwenyewe maana utundu wake umepitilizaa... Point yangu ni kwamba sio kila mtoto wa geti kali ni boya au zoba Inategemea na malezi ya wazazi...Acha kukarir..mkuu
 
Nilistuka mapema sana juu ya madhara ya kusomesha watoto hizi private, unakuta mtoto anatoka saa 10 jioni, akitoka hapo ni tuition, akitoka hapo ni homework na wengi hawatoki nje ni geti kali ni ndani tu hii inahirbu sana maisha ya mtoto.

Pia Malezi ya siku hizi pia yamechangia mno kuwafanya watoto wawe mazube maana watoto ni kuwafuga kama kuku ndani ya mageti (geti kali) huku wazazi wengi wakijidanganya kwamba wanapata furaha kamili kwa katuni na kunanunulia games.

Nakumbuka zamani tukitoka shule tulikua hatukai ndani ucheza games au kuangalia katuni, Tulikua na vikundi vya watoto mitaani tunacheza mpira, kuogelea na hata kujifunza kuto onewa hovyo hovyo, dada zetu walicheza rede, kupika, n.k Hii michezo na maisha haya yalifanya tujue kuishi na jamii tofauti na siku hizi unakuta litoto linachojua na games, katuni na what is water. ukimpeleka huyu mtoto nje kuna uwezekano mkubwa wa yeye kuonewa na hata kuwa mpweke asiwe na marafiki maana hajui ku interact na watu (Hili tatizo ni kubwa ulaya).

Binafsi mtoto wangu wa kiume namsomesha english medium hizi, mara ya kwanza shule niliyompeleka walikua darasani 18 tu na wanatoka saa kumi, kwa huu uchache nakumbuka alikuwa ana rafiki moja tu na muda mwingi ulikuwa ni kusoma hadi saa kumi.

nikaona huu upuuzi sasa, shule ndio ni muhimu ila sio kila kitu kwa mtoto wangu kuna maisha mengi mno anayopaswa kujifunza, Nikamwamishia shule ambayo wapo 48 darasani na wanatoka saa saba na nusu ila tu darasa la saba tu ndio wanatoka saa tisa. Yeye yupo darasa la tatu shuleni huwa yumo kumi bora na hii inatosha kwangu siamini sana mambo ya kuwa wa kwanza.

akitoka shuleni anakula, anafua nguo zake, Zamani nilikuwa nimempiga geti kali ila baada ya hapo nikaanzisha utaratibu anapelekwa nje kidogo ya mjini kwa bibi yake ambako kawa na marafiki wanaocheza nae, kuogelea nae, kuwinda nae, n.k Pia kajufunza kuchinja kuku na kusonga ugali wake.

Siku hizi kawa muongeaji mno nlivyomwanzishia huu utaratibu, Kawa mjanja, Shuleni kwao kageuka kuwa aina ile ya mwanafuzni darasani ambae kila mwanafunzi anataka kuwa rafiki yake na nadhani hii ni kwasababu huwa anawapa stori ama kuwafundisha wenzake vitu alivyofundishwa au alivyofanya huko kwa bibi yake,

Shule aliyopo ni yeye peke yake anaweza kuruka zile sarakasi za nyuma basi wenzake wanamkubali sana,

Nimeitwa shuleni kwa kesi za utundu utundu huu wa wavulana kama kupiga kelele na kutania wasichana, Binafsi ndivyo navyotaka awe mchangamfu na nikiri tu nilifurahi hizi kesi japo nilimkanya kwa shingo upande , Sitaki mtoto azubae zubae

Sijamlipia school bus kwa maksudi kabisa japo nina uwezo, nilishangaa aliponiambia wenzake pia shuleni wanapenda sana wawe wanatembea kama yeye pamoja na wenzake wawili ambao hawajalipiwa school bus 🙂🙂

Michezo ambayo kuku wa kisasa wanaofungiwa ndani ambayo hawataijua

-Kutengeneza manati, kuwinda ndege porini ,shabaha na raha ya kula ulichowinda
-Kuunda magari ya waya au udongo
-Kujifunza kupigana (kuku wa kisasa wanajua kupigana kwenye game)
-Kidali poo
-Kibabababa na kimamamama
-kombolela
-Kushona makambakamba vidoleni na kuyachezesha kwa mitindo mbalimbali
-kujifunza kugawana - ukija na kimbama,kisheti,gimbi au muwa marafiki zako lazima wapate.
-Mchezo wa kuzungusha betri kwa mijeredi
-Kupuliza kimhwepelo
-kukimbiza malingi ya baiskeli
-mpira wa chandimu
-Mchezo wa goroli

Elimu ni muhimu ndio ila mwenyewe nina degree ya uhasibu na CPA nimeajiriwa vizuri tu japo nilikuwa na uwezo wa kawaida tu shuleni ila huku kazini nafanya kazi vizuri tu na kuna wenzangu waliokuwa wanakua wa kwanza darasani hadi leo wamehitimu hawana kazi. Malezi sio kumfungia mtoto na kumbana sana ukiamini ndio njia ya kumlinda , LA HASHA!! kuna siku atakua mkubwa na ataishi maisha yake anaweza kupata changamoto kibao ambazo hakupata nafasi za kukabiliana nazo utotoni.
na muda mrefu kukutana na mtu makini hivi ,hebu nisanitize mikono afu ntachangia
 
Back
Top Bottom