Mboga nisizopenda katika maisha yangu

Mboga nisizopenda katika maisha yangu

We utakuwa unaongelea yale mabilinganya (mabilingani) yale makubwaaa hayana ladha. Zanzibar kuna mabiilingani madogo madogo yana kokwa nyingi. Hayo pishi lolote yanakubali. Lkn zaidi ya kukaanga tena yapikwe na maganda yake. Mmhh, yummy 😋😋😋
Hayo hayo makubwa ukitafuna domo linajaa mimaji kama mjamzito kweli mabilingani kiboko🤣🤣
 
😂Biringanya ❌ bomoa
😂Ndizi napenda mzuzu tu zingine ❌
😂Cabbage ❌
😂Dagaa inategemea na upishi, mpishi akiwa na CPA nakula zote kasoro kigoma zile kama vijiti vya ngubiti hapana.
😂Mboga za majani kwangu ni tembele, majani maboga, spinach OG, mnavu.✅
😂Nyanya chungu ❌
😂Maharage ila usiunge na chochote zaidi ya kitunguu maji✅
😂Macaroni au noodles ❌
😂Dengu❌
😂Kuna maharage flani ya gololi yakipikwa yanakuwa kama mahindi ya kande nimesahau jina lake.❌
😂Mlenda❌ naona kama nakula denda la ng'ombe
Hayo maharage kama gololi ni njugu mawe. Ukitaka nilale njaa pika hayo hata jikoni sitakuja.
 
Ajipikie mwenyewe tu au na hio pia kesi?
We ule wali wako na chukuchuku 😅
Aiseeee naweza piga mtu mimi..
Alafu unajua nakuaga na hasira mbaya sana mtu akipika kitu sipendi mfano hapo kapika NYANYACHUNGU na ugali

Hiyo siku naweza piga mtu mpaka wakaja polisi..

Akijipikia basi aombe apikie kwa jirani mimi nipo very sensitive kwa harufu ya hayo madude tuu
 
Aiseeee naweza piga mtu mimi..
Alafu unajua nakuaga na hasira mbaya sana mtu akipika kitu sipendi mfano hapo kapika NYANYACHUNGU na ugali

Hiyo siku naweza piga mtu mpaka wakaja polisi..

Akijipikia basi aombe apikie kwa jirani mimi nipo very sensitive kwa harufu ya hayo madude tuu
😂 Wewe ungekua unakaa na mimi ungekua ushaniua. Nyanyachungu na jamii yake nazipenda kama napika nyama, samaki au dagaa napenda kuchanganya.
 
Kwa namna ile mboga inayofanana nakubali kabisa kuliwa kama lettuce,, the way ilivyo ungwa that day ilinifanya nipate taste moja Mbaya sana 😣
Yap. Figili inaliwa raw, bila kupikwa. Na ina kiazi chake cheupe hivi kinawashawasha ila kuna watu wanakila pia.
Pole sn
 
😂 Wewe ungekua unakaa na mimi ungekua ushaniua. Nyanyachungu na jamii yake nazipenda kama napika nyama, samaki au dagaa napenda kuchanganya.
Yaan mi nikiona tu mtu yupo karibu na hivo vitu naona kabisa nishapotezana nae aiseee....

Mi hii ya NYANYACHUNGU mpaka ukoo sasa unaenda kujua aiseee...

Kama una uwezo wa kula NYANYACHUNGU bila shaka huwa unafatilia kipindi cha aridhio TBC1 sio
 
Yaan mi nikiona tu mtu yupo karibu na hivo vitu naona kabisa nishapotezana nae aiseee....

Mi hii ya NYANYACHUNGU mpaka ukoo sasa unaenda kujua aiseee...

Kama una uwezo wa kula NYANYACHUNGU bila shaka huwa unafatilia kipindi cha aridhio TBC1 sio
Hakuna cha kufatilia TBC wala nini basi tu huwa nazipenda.
 
Back
Top Bottom