Pre GE2025 Mbowe yupo kimya anatafuta kura, Lissu yupo bize mitandaoni kukilaumu chama

Pre GE2025 Mbowe yupo kimya anatafuta kura, Lissu yupo bize mitandaoni kukilaumu chama

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Safari hii Mbowe atajua watu wamemchoka, hata akishinda kwenye hizo kura kwa kuhonga, bado hatakuwa na uwezo wa kupandisha hamasa ya wafuasinwa cdm. Ukweli ni kuwa wakati ukuta.
Chadema ni kubwa haitegemei mtu mmoja kufanya hamasa nikuulize kabla ya Lissu kujiunga Chadema nani alikuwa anafanya hamasa.
 
Yaani Mbowe sasa kawa rafiki wa maccm. Hata maneno ya maccm ya kusema vyama vya upizani vinashindwa kwasababu havikujipanga. Naye anasema Lissu hakujipanga huku akiwa anagawa hela kwa wajumbe. Ccm wanamtumia mbowe kuuwa chadema wakifikiri chadema ndio adui yao . Ila ccm wasicho juwa chadema imewasaidia kuendelea kuwa madarakani kama chadema asinge kuwepo ccm ingekuwa imeisha ondolewa . Hivi sasa ngoja chadema ichukuliwa na Mbowe imfia mikononi mwake. Halafu uone moto wake . Kama hakuna upizani unao aminika basi atatokea mtu anaye aminika na ataongoza wote walikata tamaa na utawala mbovu wa ccm na wataiangusha serikali.
Nimeishia uliposema CCM wanamtumia Mbowe kuiua Chadema, inaonekana huijui Chadema.
 
Kama ni hivyo kwa nini wanaharakati wanalia mitandaoni kuwa Mbowe aachie kwa busara na si kwa box la kura?
TAL aachane na wanaharakati bali awashawishi wajumbe wampigie kura.
Shida ya chama chao kila mmoja mjuaji na kujifanya kuwa yeye ndio chama. Hii ya kujifanya kuwa mtu ndio chama imeshapitwa na wakati, na kama chama chao kitakuwa kimejijenga kwa sababu ya mtu basi CCM itatawala hadi mwisho wa dunia.
Taasisi inatakiwa kuwa na nguvu kuliko mtu. Watu wanakuja na kuondoka ila taasisi itabakia milele.
Kama chadema inasimama kwa sababu ya TAL basi kuna tatizo. Au unafikiri CCM/Serikali inaogopa maneno ya mtu? Ili taasisi isimame lazime ijijengee ideology ambayo ndio itakuwa inaendesha taasisi na sio mtu. We need strong institution and not a strong person.
Ndio maana Malema wa Afrika Kusini amebakia kupiga domo tu wakati wenzie wanachukua majimbo na kujenga taasisi zao. Zuma kasajili chama kipya na kilipata uwakilishi mkubwa kuliko Malema wa siku nyingi na chama chao.
Achana na wanaharakati mkuu, Tundu Lissu ni mwanachama wa CHADEMA, Odero ni mwanachama wa CHADEMA, Mapunda ni mwanachama wa CHADEMA.

Wote hao ni wanachama na hawajasema Mbowe aachie uenyekiti kwa busara.

Sasa wewe inakuwaje unaacha kusikiliza maneno ya wanachama wanaoenda kugombea uenyekiti, unasikiliza maneno ya wanaharakati wa mitandaoni ambao hata kura hawapigi?

Unasemaje shida ya chama chao kila mtu mjuaji kwa kusikiliza maneno ya wanaharakati wasio wanachama? Wanaharakati usiwahesabu kama CHADEMA. Hawana hata kadi ya uanachama.

Kuhusu tatizo la kuangalia sana mtu, Tundu Lissu mwenyewe kashasema moja ya ajenda zake ni kufanya chama kiende kimfumo zaidi, kisimtegemee mwenyekiti sana, kifanye mabadililo ya katiba, kifanye ugatuzi wa madaraka yaende chini zaidi, kufanya uongozi wa kushirikiana zaidi. Kwa hiyo hayo yote Tundu Lissu kashayasema.

Nenda Clubhouse kasikilize Tundu Lissu akiwaonya sio tu CHADEMA, bali Watanzania wote, kuw anchi inaongozwa kwa sheria, kanuni, katiba, si kwa matakwa ya mtu.

Kasikilize chawa mmoja wa Lissu anaitwa Baba Mary alivyokuwa anampamba Lissu kwa kusema "Lissu ni mwenyekiti mtarajiwa, Lissu kashapita" halafu Lissu alivyomjibu kuwa mto huo hatujauvuka bado, tufanye kazi inayotakiw akufanywa kuuvuka, Lissu alimrudisha chawa kwenye mstari kwa kuchambua mambo kwa ukweli na uwazi bila kupenda kusifiwa na chawa.

Sasa kama Lissu mwenyewe anakataa uchawa, kwa nini unamsikiliza chawa badala ya kumsikiliza Lissu?
 
Kwa hiyo hoja ni kumuondoa na si kushindana kidemokrasia! Kama wamejitokeza wanaohitaji hiyo nafasi mimi naona ni jambo la heri kwa chama chao ili tuone demokrasia kweli ipo au limebaki jina tu.
Namaanisha kumuondoa Mbowe kwa kutumia uchaguzi wa kidemokrasia CHADEMA, kwani wapi nimesema Mbowe asishiriki uchaguzi?

Mbona unaweka strawman fallacy ya kujitungia vitu ambavyo mimi sijasema halafu kunirushia?

Kuna uzi una heading inasema

"Mbowe iokoe CHADEMA kwa kuchukua maamuzi mazito ya kumuunga mkono Lissu, usisubiri kesho!"​

"

Nikampinga mtoa mada hii na sababu nikampa, kwamba Mbowe ana haki ya kikatiba CHADEMA kugombe auongozi, wanachama wa CHADEMA wana haki ya kuchagua wanamtaka nani awe mwenyekiti, na hatujui kati ya Mbowe na Lissu na hao wengine atakayeshinda ni nani.

Hata kama unampenda Lissu, hatujui wanachama wa CHADEMA watakaopiga kura wengi watamtaka nani. Waachiwe uhuru wa kuamua.

Sasa kwa nini unaniletea mimi habari za watu wasiotaka Mbowe ashiriki kwenye uchaguzi?

Mimi rekodi yangu iko clear, nishaipinga hii hoja.

Ukitaka ushahidi soma hapa nilivyoipinga hii hoja.

 
Kama ni hivyo kwa nini wanaharakati wanalia mitandaoni kuwa Mbowe aachie kwa busara na si kwa box la kura?
TAL aachane na wanaharakati bali awashawishi wajumbe wampigie kura.
Shida ya chama chao kila mmoja mjuaji na kujifanya kuwa yeye ndio chama. Hii ya kujifanya kuwa mtu ndio chama imeshapitwa na wakati, na kama chama chao kitakuwa kimejijenga kwa sababu ya mtu basi CCM itatawala hadi mwisho wa dunia.
Taasisi inatakiwa kuwa na nguvu kuliko mtu. Watu wanakuja na kuondoka ila taasisi itabakia milele.
Kama chadema inasimama kwa sababu ya TAL basi kuna tatizo. Au unafikiri CCM/Serikali inaogopa maneno ya mtu? Ili taasisi isimame lazime ijijengee ideology ambayo ndio itakuwa inaendesha taasisi na sio mtu. We need strong institution and not a strong person.
Ndio maana Malema wa Afrika Kusini amebakia kupiga domo tu wakati wenzie wanachukua majimbo na kujenga taasisi zao. Zuma kasajili chama kipya na kilipata uwakilishi mkubwa kuliko Malema wa siku nyingi na chama chao.

RIP Maalim Seif, Jamaa alikuwa ni Taasisi ya kujitoshela
 
Ok, basi tuache sanduku la kura liamue.
Hapa uchaguzi wa kweli uliopo si uenyekiti wa CHADEMA.

Hapa uchaguzi wa kweli uliopo ni mustakabali wa CHADEMA.

Na katika uchaguzi huo, Tundu Lissu kashashinda regardless ya uchaguzi wa mwenyekiti wa CHADEMA matokeo yatakuwa vipi.

Tundu Lissu ndiye mtu mwenye credibility ya kuongoz aCHADEMA sasa hivi.

Akishinda, wananchi watakipa nafasi na kumuangalia uongozi wake.

Akishindwa, CHADEMA kinaenda kuungana na vyama vingi vya kwenye briefcase vinavyoibuka wakati wa uchaguzi tu.
 
The difference is clear.

Baada ya kutangaza nia kinachofuata ni kutafuta kura kwa wajumbe, kutangaza sera zako wajumbe wazipime, tofauti na hapo utaonekana kama mpiga kelele.

As a result ukishindwa unaanza kusingizia umeibiwa kura kumbe muda mwingi uliutumia kutoa lawama kwa mshindani wako tena pasipo na ushahidi.

Wajumbe hawaangalii wingi wa lawama wanaangalia ubora wa sera dhidi ya mpinzani wako ni kwa kiasi gani zitakisaidia chama kuvuka pale kilipo.
Mjumbe yeyote ambaye mpaka sasa hajui atampigia nani kura mpaka kwanza asikie sera za Mbowe na Lissu, kachelewa katika siasa na hafai katika cheo hicho labda hizo "sera" ziwe na mrengo wa financial benefits.
 
Mjumbe yeyote ambaye mpaka sasa hajui atampigia nani kura mpaka kwanza asikie sera za Mbowe na Lissu, kachelewa katika siasa na hafai katika cheo hicho labda hizo "sera" ziwe na mrengo wa financial benefits.
Kwahiyo hakuna haja ya wagombea kufanya kampeni, hii mbona mpya.
 
Lissu hakujiandaa kuwa Mkiti, alijiandaa kuwa makamu alikurupuka baada ya kuhisi Wenje atachukua nafasi yake hana mtu wa kufanyanae kazi kama makamu endapo atashinda.

Kupigania haki bila kufuata utaratibu ni fujo ndio maana tuhuma zake zinaonekana ni uzushi hazina tangible facts za uhakika.
Ilikuwa aende kozi gani ya kujiandaa kuwa Mkiti? Utaratibu gani aliouvuka au kuuacha?
 
Ndio maana nikasema Chadema haitegemei mtu mmoja aondoke yeyote itapata mwingine.
Uko sahihi, lakini this time around Mbowe akiwa mwenyekiti tena, cdm itakuwa kama CUF.
 
Uko sahihi, lakini this time around Mbowe akiwa mwenyekiti tena, cdm itakuwa kama CUF.
Watu wenye mahaba na Mbowe hawataki kukubali ukweli huu.

Mbowe akishinda uenyekiti watu wengi sana watakosa imani na CHADEMA.
 
Back
Top Bottom