Mchele kutoka nje na hatma ya wakulima wetu

Mchele kutoka nje na hatma ya wakulima wetu

Hapa mimi naona wanaofaidika ni wafanya biashara sabubu hakuna mkulima anayeuza mchele sasa hivi kilo shs 3600 huyu ni mfanyabiashara na kama wapo wakulima basi ni wachache sana.

Hivi sasa wakulima wanakaribia kuvuna ukiagiza mchele wa nje huu wa ndani utashuka bei hivyo wafanyabiashara watanunua mpunga kwa bei rahisi kwa wakulima watahifadhi then baada ya muda wataacha kuagiza mchele wa nje then kutakuwa na shortage hivyo bei itapanda ndio watafungua maghala yao.

Mimi nadhani ingefaa sana wangeagiza mchele kile kipindi ambacho sio cha kukaribia mavuno.
 
Tatizo lilianza pale bei ya mchele ilipopanda, solution ikawa kuruhusu mchele wa nje kuingia. Kwa hiyo wanaoumia ni wakulima kwa sababu mchele utakapoingia utashusha bei ya mchele masokoni
Raia hamueleweki kabisaa. Serikali ikiruhusu utoke na umeisha ULIOPO ni mchache, na bei ikooo juuuu, raia wameliaaa, serikali imeruhusu uingie kutoka njee, Tena raia haohao wanalia, Sasa mnataka iwejeeee
 
Kuna vitu vingi sana vinadhihilisha hii serikali haina kichwa inakiwili wili tu yani haina akili
 
Kama unatosha bei imefikaje 4000
Mchele kutoka nje Je tumejiridhisha kwamba uliopo nchini hautoshi?
Je uzalishaji wetu wa mchele ni kiasi gani, mahitaji kiasi gani na upungufu kiasi gani
Hizo tani elf 90 za mchele zitaingizwa kwa muda gani
Je wakulima walioko shamba kwa sasa mchele wao watauza wapi wakikutana na huo wa nje?

Mchele wa nje inaweza kuwa jambo jema ila nakumbuka wosia wa Mwigulu bungeni hivi majuzi alisema mambo ya dharura ni lazima kuwa nayo makini vinginevyo unaweza kubeba na Deal za watu.
 
Kama bei sio rafiki kwa walaji bai hautoshi.... hakuna haja ya kuanza kuhesabu kuna punje ngapi.., Sababu wanaoleta wanataka faida na kama wakulima huku bei yao itakuwa juu kuliwa wao wa nje basi ni vema wa huku wakawauliza mbinu za wa kule ili nao waweze kupata faida kwa bei rafiki
 
Raia hamueleweki kabisaa. Serikali ikiruhusu utoke na umeisha ULIOPO ni mchache, na bei ikooo juuuu, raia wameliaaa, serikali imeruhusu uingie kutoka njee, Tena raia haohao wanalia, Sasa mnataka iwejeeee
wanaolia ni wafanyabiashara wa mchele sio wakulima,wao walishauza siku nyingi,wako shamban wanapanda mwingine, middle man ndio wapiga kelele
 
Mkuu; Walitunyanyasa sana na bei zao; sasa wameanza kupanic. Wanatoa kashfa na kuuhafifisha mchele kutoka nje eti ili ss walaji tuuone ni mchele duni haufai. Watakaa sana.
Yaani tutakula tu hata kama utakuwa ni mchele wa plastiki kama wanavyosema wao! Ila siyo mambo ya kuuziana chakula kwa bei ya kulangua aisee.
 
Hiki kilio sio cha wakulima bali madalali na walanguzi,wakulima chakula washamaliza kuuza tokea mwaka jana, sasa hivi wapo mashambani wanalima.
Nakubaliana na wewe kabisa mkulima hanufaiki kitu na hizi bei ila dalali.
 
Huwa zinawatosha wao wenyewe huko serikalini sasa wangefanya hivi toka mwaka jana hiyo habari ya inflation ya chakula si isingefikia kuwa janga kama ilivyo kwa sasa.

Ajabu yenyewe bei ya chakula itaanza kushuka kabla ya huo mchele wa kuagizwa kufika, kutokana na hofu za walioficha stock zao kuanza kuona madhara ya ongezeko la supply mbeleni na kujiwahi kwa kuuza wao kwanza.

Free market ni kuruhusu wazalishaji wauze wanapotaka na kuachia suppliers pia kununua wanapotaka. Watu washindane kushusha bei za production.

Kilichokua kinaendelea kwa kuzuia importation hakikuwa na lengo la kuwatetea wakulima, bali kuwalangua wananchi na kuongeza ugumu wa maisha kwa sie wenye kipato kidogo.
Serikali ya ccm ndiyo kawaida yao! Wanatengeneza tatizo kwa makusudi, halafu baadaye wanajifanya kulitatua ili wapate ujiko. Tumeshawazoea. Unaweza ukadhani kuna serikali 2!
 
Kwani wakati tunalishwa kitumbo hapakuwepo na mamlaka ya chakula na dawa?

Bado naona umekurupuka, unataka quality kwa bei rahisi, hiyo kitu haipo.
Potelea mbali! Nyinyi kuleni huo mchele wenu wa 3600! Sisi tutakula huo huo wenye low quality kutoka nje, kwa bei nafuu.

Shida iko wapi? Kila kundi lishinde mechi zake.
 
Mchele kutoka nje Je tumejiridhisha kwamba uliopo nchini hautoshi?
Je uzalishaji wetu wa mchele ni kiasi gani, mahitaji kiasi gani na upungufu kiasi gani
Hizo tani elf 90 za mchele zitaingizwa kwa muda gani
Je wakulima walioko shamba kwa sasa mchele wao watauza wapi wakikutana na huo wa nje?

Mchele wa nje inaweza kuwa jambo jema ila nakumbuka wosia wa Mwigulu bungeni hivi majuzi alisema mambo ya dharura ni lazima kuwa nayo makini vinginevyo unaweza kubeba na Deal za watu.
ukute huo mchele ni ule REJECTED, maana viongoz wetu wanavyopenda vitonga bila kujari afya za consumers,.
 
"Msije kutuletea tena ule wa Thailand Nusu kilo manakula watu 18 na unabaki kiporo cha chai"[emoji119].......pitia Account za Instagram na Facebook za ITV zilizopost hii taarifa usome maoni utajifunza vitu vingi sana. hiyo ni moja ya comment
Kama hauna madhara Cha muhimu ni kushiba tu, huu wa ndani watanunua wa masaki, obey, na mikocheni.
 
Tena kama vp wafungulie na soko la mahindi ya nje ili mwaka huu turudi kwenye bei yetu ya zamani debe tsh.3000.
 
Una uhakika gani kama huo mchele unaoletwa ni makapi? Nyinyi mchele mnao wauzia Wakenya na Wasomali ni makapi?

Wewe kijana wa Moo mbona unaleta story za kufikirika! Unataka kusema hakuna mamlaka ya chakula na dawa nchini kwa ajili ya kuchunguza ubora wa huo mchele!
Bila kumtaja mume wako huwezi ku comment?Yaani utafikiri uko obsessed. Dah
 
Unafungulia mipaka na chakula kinauzwa hovyo eti kuuwanuifasha wakulima kisha baada ya muda unaanza kuagiza tena chakula kutoka nje baada ya kibano cha njaa!

Upumbavu mtupu
 
Raia hamueleweki kabisaa. Serikali ikiruhusu utoke na umeisha ULIOPO ni mchache, na bei ikooo juuuu, raia wameliaaa, serikali imeruhusu uingie kutoka njee, Tena raia haohao wanalia, Sasa mnataka iwejeeee
Hakuna anaelia, ila iwe na takwimu sahihi ili ifanye maamuzi sahihi kutokana na takwimu na sio kelele za mitandaoni
 
Unafungulia mipaka na chakula kinauzwa hovyo eti kuuwanuifasha wakulima kisha baada ya muda unaanza kuagiza tena chakula kutoka nje baada ya kibano cha njaa!

Upumbavu mtupu
Sidhani kama uko sahihi. Kanuni za kibiashara zinaruhusu uuze e.g. kwa Juma kwa bei kubwa halafu ununue kwa Massawe kitu hicho hicho kwa bei ya chini. Na mzunguko unaendelea.
Yaani nchi au wakulima wanaweza kununua mahindi Iringa kwa bei ya chini kisha kuuza mahindi hayo Himo kwa bei ya juu ile margin wanayopata ndo faida. Vivyo hivyo Tanzania inaweza kuuza mchele Congo DRC kwa bei kubwa halafu Tanzania ikanunua au kuagiza mchele kwa bei ndogo kutoka Japan.
Ni suala la Fursa tu na kuangalia ni kipi cha kufanya ili upate faida.
"You produce what you don't eat and you eat what you don't produce".
 
Back
Top Bottom