Mchungaji Mtikila asema CHADEMA wanahusika na kifo cha Chacha Wangwe; kumfikisha Lowassa Mahakamani

Mchungaji Mtikila asema CHADEMA wanahusika na kifo cha Chacha Wangwe; kumfikisha Lowassa Mahakamani

Mbinu zaidi za kujaribu kuiondoa treni ya Chadema/Ukawa relini ambayo sasa ipo kwenye mteremko wa mwendo kasi kuelekea ikulu.

Treni yetu ipo mwendokasi kwenye mteremko kuelekea KABURINI mzee. Kama ikulu ipo kaburini labda. Maana definetely uchaguzi tutashindwa, wananchi wameshaamua na matokeo ya tafiti zote mbili hatuwezi zidharau tena taasisi kubwa kitaifa na kimataifa. Hapo ndipo anguko la chadema na ukawa litakapotokea. Vyama hivi vitazikwa kiukweli na labda chama kipya kitaibuka na baadhi ya makamanda wa ukweli Dr Slaa na Prof Lipumba. Ngoja Lipumba arudi hija muone. Ngoja na Dr Slaa akirudi wiki ijayo muone moto wake sasa.balaaa..
 
Mtikila ni huyo ninayemskia kila siku akipeleka kesi mahakani au mwingne? Ni kesi ngapi alizopeleka amefanikiwa kushinda!
 
Ni kwa sababu anataka kuingia ikulu. Vinginevyo nani angehangaika naye. Tumia akili mzee. Hela za katiba wabunge wote wamepiga. Nani asiyepiga. Tumia akili mzee.kuna mbunge yoyote hata makamanda wetu ambae alikataa kuchukua. Tena baada ya kuona fedha zinakaribia kuisha wakajifanya kususia bunge. The last last minute. Ni usanii mtupu hatuwezi kuukubali na kuushabikia.

Asee umenishangaza sana. Kwa hiyo mtu akipiga ufisadi lakini asipotaka kuingia ikulu hamna haja ya kuhangaika naye? Hii ndio akili unayoniambia nitumie? Kumbe wee ndio UTUMIE AKILI MZEE!
Kuhusu fedha sijasema kuna mwenye afadhali, sijataka kuwaongelea hao wengine, mada ilikuwa ya huyu mchungaji aliyejivika ngozi ya uadilifu na uzalendo huku ni mwizi tu. TUMIA AKILI MZEE!
 
Ameeleza namna gari ya CHADEMA iliyokuwa imembeba Chacha Wangwe ilIvyopaki ghafla na kupigwa kichwani.

source, startv

Yani serikali ya ccm ilishindwa kulijua hilo ila mtikila alilijua sio?
 
Alileta ujuaji wake Tarime akachezea vitasa

Wengi wao humu hawakumbuki. Kwa wanaomjua huyu mzee hawapati tabu kumjadili. Rejea tukio la tarime, au tafuta mtandaoni oudio CD za "bomu la kakobe" bila kusahau alivyoumbuka na mamilioni ya Rostam Aziz miaka ile. JF ina mengi wacheni kuwa wajuwaji tuliokuwa humu miaka mi3 au mi4 walao JF imetujenga kifikra.
 
Chadema kweli ni wauwaji kumbe ndiyo walimuuwa wangwe kweli hawa watu wabaya.
 
Yes.......hii ni Tanzania.Imagine this,Mh Rais akimaliza muda wake,akae mahali pa utulivu pekee yake na atafakari katika muda wake wa miaka kumi ameisaidia Tanzania na watu wake kwenye nini.Yapo aliyosaidia na yapo hakusaidia.
 
............tushafanya maamzi....ni mwaka wa mabadiliko!
 
Nimemsikiliza na nimeamini kama kweli watanzania wanataka kujua watu wagonjwa basi mtikila amesema ukweli, tena ukweli kabisa kuwa watanzania wana ugonjwa wa kusahau.

Tena wote akiwamo na yeye maana hata anavyoongea hajielewi na hasa katika harakati zake alizotaja za muda mrefu huwa anahitaji nini?

Ni bahati mbaya kuwa mtikila mzee wangu huyu hajui. Kutokana na kaugonjwa kakusahau ambako akina Mtikila wanaonekana kuwambukiza wajukuu zao ndiyo maana hata wakipata shida na kupewa ahadi za uwongo baada ya miaka mitano wanasahau .

Tuendelee kumuomba Mungu ipo siku atatukumbusha, japo mwaka huu wengi naona wameanza kukumbuka.

Sasa watanzania wafanye nini mbona hawasaidiwi?
 
Mtikila ni msema kweli....tunaomjua hatumshangai

Sio kweli , kwa nini sio kweli? Ni kwa sababu hakuna binadamu aliyekamilika wote tumekwishasema uongo katika maisha yetu, kwani ni kweli watanzania hawamtaki lowasa? Wangekuwa hawamtaki si angesahaulika kabisa hata usingemuona mtu kwenye mikutano yake ? Si kama yeye mtikilia alivyosahaulika na kukatwa kuwania uraisi na NEC huyo ndio haitajiki kabisa ila ccm wanamhitaji kuuwa upinzani
 
Sio kweli , kwa nini sio kweli? Ni kwa sababu hakuna binadamu aliyekamilika wote tumekwishasema uongo katika maisha yetu, kwani ni kweli watanzania hawamtaki lowasa? Wangekuwa hawamtaki si angesahaulika kabisa hata usingemuona mtu kwenye mikutano yake ? Si kama yeye mtikilia alivyosahaulika na kukatwa kuwania uraisi na NEC huyo ndio haitajiki kabisa ila ccm wanamhitaji kuuwa upinzani

Sema baadhi ya Watanzania....
Mwisho wa siku uwiano wa wanaompenda na wasiompenda utaamua.
 
Kama mtakumbuka wiki kama 3 zilizopita ilisemwa kwamba Mtikila atakwenda vyombo vya habari na kumshambulia Lowassa. Baadae atakwenda Dr. Slaa akishatoka USA kurusha kombora la mwisho. Tujiulize. Kama tafiti za Twaweza na wengine zinasema Magufuli anaongoza sana, iweje shutuma, kejeli, n.k vimlenge mgombea ambaye haongozi kwenye kura za maoni? Kuwa woga wa nini? Tafakari ndogo utagundua nini kinaendelea.
 
Star TV ni kama choo cha stendi kila MTU anaingia na kuacha uchafu wake bila kujali kala nini huko atokako. Wakati kama huu kuelekea uchaguzi vituo vya Radio na Tv huwa vinaendeshwa kwa weledi mkubwa ili kutokusababisha hali ya sintofahamu. Hivi Startv hawajui kuwa Wangwe alikuwa na familia na inao uchungu na mzazi wao? Kama mtu anao ushahidi wa mauaji huwa unapelekwa studio au polisi?
Hivi mtu akijitokeza huko na kumvamia Zito au Dr Slaa na kumchoma kisu na kumuua na utetezi wake ukawa kuwa Wangwe ni ndugu yake na amemlipia kisasi kwani kasikia Startv kuwa hao ndio walopanga kumuua jee kituo hakita wajibika?
Sahara media kwa kweli ni wapuuzi sana,hawatumii weledi bali wanatumika kama vile vituo vya Rwanda wakati wa genocide
 
Tatizo kuna watanzania wengine hujiona kuwa wao wana ufahamu kuliko wengine, sijaweza mwelewa kabisa kuwaita watanzania wengine kuwa hawana busara wakati yeye mwenye akionyesha kutokuwa na busara. Sema anatumia kutokujua kwetu kama mtaji. Kutaka kuwaaminisha watu kuwa lowassa ana haki ya kuchaguliwa? shame on him, wananchi wataamua wenyewe,
 
Jamani, mbona kugombea lilikuwa suala la process, unakuwa mwanachama, unatafuta wadhamini, unaenda tume, unachukua form na kutafuta wadhamini, halafu waliipeleka kwa jaji, anahakiki, akazipitisha, zikarudishwa tume, akatangazwa mgombea, ina maana hao wote ni mataahira nusu? Mbona anakuwa farisayo hivi. Hajui kuwa Mungu ni mwingi wa rehema? Kama angekuwa mgonjwa kweli, angeshashindwa. Wajue kuwa, hayo wansyomtukana yatawapata na wao.
 
hivi makamu mwenyekiti wa chama chake ni nani na katibu mkuu wake ni nani?

He's a one man army .....................!!! Yeye ndiye kila kitu, Mwenyekiti, Makamu, Katibu na Mweka Hazina. Halafu anadai wenzake mafisadi!!
 
Mtikila jina lake lilikatwa kwenye wagombea urais so hana hela ya mboga lazima atumike

Hell no! Ukawa this is too much! Kila anayetofautiana na Lowasa basi kanunuliwa!? Ina maana hakuna tena mtu kuwa na mawazo huru against that guy!?
 
Back
Top Bottom