Miaka mitano ya hayati Magufuli, bei za nafaka hazikupanda namna hii. Sasa zimepanda na wananchi wanakula mlo mmoja na nusu



Baadhi ya wajanja wa mjini walikuwa wanafurahia na kusherehekea sana kufungwa mipaka bei za mazao zinaanguka wao wanakula kwa bei chee
 
Kuna mkulima anayeenda kuuza mazao huko nje,
Bei ya shambani bado iko chini Ila inapandishwa na wafanyabiashara

Bei ya shambani ni shilingi ngapi na sokoni ni shilingi ngapi usafiri nao ni shilingi ngapi ? Haya nendeni shambani si ndio kuna bei nzuri
 

Mlo mmoja wapi watu wanashinda kwenye pombe hela zinachezewa kwenye pombe,bangi,ukahaba na anasa
 
Huyu dereva nchi imemshinda kabisa.watu wameanza kula mara moja tu kwa siku kutokana na vitu kupanda bei kiholela.Hadi tufike 2025 tutakuwa kila mwananchi amejikondea na kuonesha mbavu zake zote mwili mzima


Wasiomudu kwanini wasilime kama wakulima tu wapate hivyo vya shambani katika bei wanazozitaka
 
Hakuna mkulima anayepata faida, mnaopata faida ni nyinyi madalali na matapeli mnaompa mkulima bei ndogo na bado mnabana mizani, kujaza lumbesa na kununua mazao shambani aka. kangomba, hovyo kabisa....

kumbe kuna uwezekano wa kupata kwa bei ndogo kwa mkulima sasa waKanunue kwa bei ndogo kama walivyoweza hao madalali kununua kwa bei ndogo haina haja ya mbeleko ya nguvu za serikali bei ziporomoke
 
Na wewe ni tapeli unayejiita mfanyabiashara wa mazao?

Wakulima ni watu kama wewe hawajatenda kosa lolote mpaka wapewe mzigo wa kukulimia zao upate kwa bei chee bei unazozitaka weee ilhali hujasaidia chochote kwenye kulima kwao
 
Jana nimenunua sembe kilo 5 shilingi 8,500/= na kuna watu wanashabikia mahindi yaendelee kupelekwa nje.
Gharama za uzalishaji mwaka jana pia zilikuwa juu mno. Acha wauze kwa Bei yoyote.
Mwakani pigeni kelele Bei zishuke sababu angalau mbolea zitanunuliwa kwa 70,000
 
Wanaouza mahindi kwa gharama sio wakulima ni wafanya biashara so kama selikal inasema wakulima wauze bei watakayo uhalisia inakuwa inasema na wafanya biashara wa mazao
 
Kwani Magufuri alikuwa anawapelekea wananchi wote chakula??
 
Wanaouza mahindi kwa gharama sio wakulima ni wafanya biashara so kama selikal inasema wakulima wauze bei watakayo uhalisia inakuwa inasema na wafanya biashara wa mazao

Wanaotaka bei rahisi si ndio hapo sasa kumbe wakulima wanauza kwa bei rahisi kwa nini sasa wasiende wanakonunua wafanyabiashara
 
WATANZANIA ROHO YENYE INDA TUMEITOA WAPI KUTAKA WENGINE WATESEKE?

05 September 2022
Dar es Salaam, Tanzania

Wengine ni hawa hapa wanajiita ni Wadau wa Stendi ya mabasi ya Magufuli jijini Dar es Salaam wenyewe umimi na roho ya inda wanataka wasafiri wateseke ili wao wapate mlo na kwenda mbali kubeba mabango kuichagiza serikali iwatese abiria wa mabasi yaendayo mikoani

MamaNtilie, machinga, wenye mogahawa n.k katika stendi ya kuu ya mabasi ya kwenda mikoa iliyopo jijini Dar es Salaam wataka waziri mkuu, waziri wa TAMISEMI Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa pamoja na mkuu wa mkoa waingilie kati ili kusiwepo vituo vidogo vya kupakia na kuteremsha abiria katika jiji la DSM ambalo ni jiji lenye eneo kubwa (upana) kupita yote Afrika Mashariki hata kama bado mabasi hayo yatapita kituo kikuu cha mabasi cha Magufuli.

Kubwa wadau hao wafanyabiashara ktk kituo cha mabasi cha Magufuli wanataka abiria wateseke ili biashara zao zineemeke
Source : millard ayo
 
Anza kulima hutalalamikia bei.

Ni kweli waondoke mjini wakafanye shughuli zingine zenye faida au wabaki lakini waanzishe kilimo cha mazao ya chakula . Wakulima wavunja jasho wanajituma sana kwa kujitegemea wenyewe sana sana anayewasaidia wakulima hawa ni mnunuzi mfanyabishara wa nafaka.

Mjini kila mtu anataka kuwa waendesha bodaboda au bajaji n.k kwa kuisikiliza CCM ikigawa mikopo ya pikipiki za bodaboda, bajaji na umachinga hivyo sekta yao kuzidiwa na utitiri wa watoa huduma za usafiri au chinga mitaani.

Wajiulize mbona waendesha teksi / taxi wa miaka mingi mjini walikubali ushindani wa uber, bodaboda na bajaji wakajiongeza kwa kuamua kufanya shughuli zingine au kuboresha huduma zao hivyo kuwa na abiria wa uhakika kwa kutumia simu n.k
 

Hakuna muendesha taxi mwenye mshahara mmoja/anayetegemea taxi tu ambaye bado yuko sokoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…