Miaka mitano ya hayati Magufuli, bei za nafaka hazikupanda namna hii. Sasa zimepanda na wananchi wanakula mlo mmoja na nusu

Miaka mitano ya hayati Magufuli, bei za nafaka hazikupanda namna hii. Sasa zimepanda na wananchi wanakula mlo mmoja na nusu

Hakuna muendesha taxi mwenye mshahara mmoja/anayetegemea taxi tu ambaye bado yuko sokoni.

Ndiyo maana yake wanaolalamika kuwa kipato chao ni kidogo ktk shughuli wafanyazo mjini wasililie mkulima au sekta ya kilimo ibanwe na serikali.

Bali wafanye shughuli zingine za ziada. Tanzania ni tajiri wa rasilimali za asili ikiwemo ardhi. Nchi zingine ardhi yote inamilikiwa watu wenye hati miliki za ardhi, hivyo hawana fursa ya kurudi kijijini au mkoani wakalime au kufuga na kuvua samaki. Tanzania mapori na ardhi ya rutuba zipo na hazimilikiwi wala kuhodhiwa na watu.

Bado kuna shughuli za uvuvi, mifugo n.k ni wakati wa kuachana na umachinga, bodaboda na bajaji turudi mikoani tukafanye shughuli zingine.
 
Ndiyo maana yake wanaolalamika kuwa kipato chao ni kidogo ktk shughuli wafanyazo mjini wasililie mkulima au sekta ya kilimo ibanwe na serikali.

Bali wafanye shughuli zingine za ziada. Tanzania ni tajiri wa rasilimali za asili ikiwemo ardhi. Nchi zingine ardhi yote inamilikiwa watu wenye hati miliki za ardhi. Tanzania mapori na ardhi ya rutuba zipo na hazimilikiwi wala kuhodhiwa na watu.

Bado kuna shughuli za uvuvi, mifugo n.k ni wakati wa kuachana na umachinga, bodaboda na bajaji turudi mikoani tukafanye shughuli zingine.
Uko sahihi 100% kwa sababu tukitegemea tu aina moja ya uzalishaji tunajiwekea mazingira magumu,tufanye kazi halali ili baadaye zitusaidie sisi na jamii inayotuzunguka.
 

KATIBU MKUU KILIMO ARIDHISHWA NA SKIMU YA UMWAGILIAJI MVUMI KILOSA​

KM_NA_GATA_2_612_408shar-50brig-20_c1_c_t.jpg

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya amesema ameridhishwa na hatua ya ujenzi wa skimu ya umwagiliaji kijiji cha Mvumi wilaya ya Kilosa ambayo imefikia asilimia 94 ya ujenzi na tayari wakulima wameanza kunufaika.
Ametoa kauli hiyo alipofanya ziara ya kushtukiza kukagua maendeleo ya mradi huo uliopo wilaya ya Kilosa Mkoa wa Morogoro chini ya mradi wa Kuongeza Tija na uzalishaji wa zao la Mpunga (ERPP).Katibu Mkuu huyo alisema mradi wa umwagiliaji kijiji cha Mvumi umegharimu shilingi Bilioni 1.97 na utanufaisha wakulima wengi wa zao la mpunga katika wilaya ya Kilosa kuongeza uzalishaji na tija.
Source : KATIBU MKUU KILIMO ARIDHISHWA NA SKIMU YA UMWAGILIAJI MVUMI KILOSA – Tanzania Agricultural Development Bank
 
Serikali yetu ingefanya juhudi ili Diesel isipande, wangeacha Petroli hata ipande vipi haina athari sana kwenye mfumuko wa bei,
Diesel iondolewe makodi kodi mengi.
Gari za petroli ni nyingi kuliko za Diesel na kuna gari za petrol ambazo zinafanyiwa biashara. Sasa usichukulie poa kisa unaendesha Civilian ya hesabu.
 
Ndiyo maana yake wanaolalamika kuwa kipato chao ni kidogo ktk shughuli wafanyazo mjini wasililie mkulima au sekta ya kilimo ibanwe na serikali.

Bali wafanye shughuli zingine za ziada. Tanzania ni tajiri wa rasilimali za asili ikiwemo ardhi. Nchi zingine ardhi yote inamilikiwa watu wenye hati miliki za ardhi, hivyo hawana fursa ya kurudi kijijini au mkoani wakalime au kufuga na kuvua samaki. Tanzania mapori na ardhi ya rutuba zipo na hazimilikiwi wala kuhodhiwa na watu.

Bado kuna shughuli za uvuvi, mifugo n.k ni wakati wa kuachana na umachinga, bodaboda na bajaji turudi mikoani tukafanye shughuli zingine.

Serikali inayojielewa hutoa ruzuku inayoeleweka kwa wakulima.
 
Morogoro, Tanzania

Mkulima mwanamke aliyepata mafanikio makubwa kupitia kilimo



Source : Kilimo TV
 
Tulipokuwa tunasema Magu ni genius na mzalendo watu walikuwa hawaelewi. Wakaruhusu kudanganywa na propaganda za upinzani na wanaharakati wanaotekeleza ajenda za wazungu.

Sasa wengine ndiyo wataelewa!
Mpumbavu yule....sisi wakulima tulishindwa hata kununua uniform za shule kisa bei za mazao kuwa chini....
tunashukuru sasa ingalao
 
Wanachi wataumia sana, hawana mtetezi.
[emoji116]

Nipashe ilitembelea maeneo mbalimbali ya Dar es Salam na kubaini kupanda bei za bidhaa zinazotumiwa na kwa mlo wa kila siku ambazo ni mchele, maharagwe, unga wa ngano, unga wa sembe, dona na choroko.

Mchele kilo moja umepanda kutoka sh. 1,800 au 2,000 hadi sh. 2,700 daraja la kwanza na super kutoka sh. 2,500 hadi 3,500, unga wa sembe na dona umetoka sh. 1,200 hadi sh. 1,600 na unga wa ngano sh. 1,300 hadi 2,000 kwa kilo huku choroko ikipanda kutoka sh. 1,500 hadi sh. 2,500. Bei ya mfuko wa kilo tano za unga imepanda kutoka sh. 6,000 hadi 8,000.

Wakizungumza na Nipashe kwa nyakati tofauti, baadhi ya wananchi wamesema kutokana na kupanda kwa bei ya bidhaa hizo, wamelazimika kula milo miwili kwa siku badala ya mitatu.

Mkazi wa Tabata, James Macha, alisema analazimika kutokunywa chai ya asubuhi kutokana na kupanda kwa bei za vitafunwa ikiwamo chapati, maandazi na vitumbua, hivyo ili aweze kumudu gharama nyingine za maisha ikiwamo kulipa kodi ya nyumba na kulipa ada ya shule.

Macha, mwenye mke na watoto wawili, alisema kabla ya kuchukua uamuzi huo, sasa anatumia sh. 3,000 kwa ajili ya kununua vitafunwa asubuhi kutoka sh. 1,200 aliyokuwa anatumia awali. Alisema hali hiyo imetokana na vitafunwa hivyo kupunguzwa kipimo, hivyo kumlazimu kununua vingi ili vitosheleze.

Naye Mkazi wa Salasala, Mwajabu Abdul, mwenye watoto watatu anayefanya kazi ya saluni, alisema hali hiyo inawalazimu kutokula chakula cha mchana ili kuepuka gharama kubwa kutokana na kuwa na kipato kidogo.
"Wakati mwingine unajikuta umeamka na sh. 5,000, hivyo kuigawanya upate miko mitatu si rahisi.

Tunachofanya na wanangu tunachemsha mihogo ya buku (sh. 1,000) tunakunywa na chai saa tano asubuhi. Tukishashiba tena tunakuja kupika chakula saa 11:00 jioni, tunakula saa moja tunalala, siku zinasogea," alisema.

Mwajabu alisema awali walipata shida kwa sababu walikuwa wameshazoea kula milo mitatu hali iliyosababisha watoto kulegea na kusinzia wakati wa mchana lakini sasa wameshazoea na maisha yanakwenda sawa.

Dereva wa bodaboda eneo la Mwenge, Alex Mushi, alisema alichukua uamuzi wa kutokula chakula cha mchana baada ya kugundua kuwa anatumia pesa nyingi kula kwa mama ntilie.

"Kwa siku nikipata sana katika biashara yangu ni Sh. 25,000. Hapo Sh. 10,000 ni ya mwenye bodaboda, nabaki na sh. 15,000. Asubuhi chai tu sh. 2,500, mchana ili ushibe lazima ule pande mbili za ugali maana unapimwa kidogo sana jumla sh. 4,000. Jioni pia utumie sh. 4,000 jumla sh. 10,500 bado hujanywa maji. Sioni hata dalili ya kununua kiwanja," alisema.

Kutokana na kupanda huko kwa bidhaa, Mushi alisema kuna haja ya serikali kuangalia namna ya kupunguza gharama za nafaka kwa kuwa ndizo inasababisha gharama za vyakula kupanda huku watu wa hali ya chini wakiathirika zaidi.

Nipashe ilifunga safari mpaka kwa wauzaji wa vyakula ambapo Angela Maganga, muuzaji wa vitumbua Temeke, alisema amepoteza baadhi ya wateja baada ya kupunguza kipimo cha vitumbua ili apate faida kutokana na kupanda gharama za nafaka na mafuta ya kupikia.

Alisema ndani ya mwaka mmoja kilo moja ya mchele wa vitumbua imepanda kutoka Sh.1,400 hadi Sh.2,000 na mafuta lita moja ilikuwa sh. 3,500 sasa sh.5,000.

"Ni kweli dada nimepunguza kipimo cha upawa ili na mimi nipate faida nihudumie familia yangu, ndicho kimewakimbiza wateja. Serikali iangalie hizi nafaka mbona zinazopanda kila kukicha na zinaelekea kuua biashara zetu ambazo ndizo tunategemea kusomesha watoto,” alisema.

Naye Maria Kallaghe, mamalishe katika soko la Tandale, alisema kitendo cha wateja katika eneo hilo kutokula chakula cha mchana, kimemrudisha nyuma kimaendeleo kwa sababu anapata faida nusu ya aliyokuwa anapata mwanzo.

"Mauzo yameshuka kutoka sh. 50,000 hadi sh. 30,000. Hapo nikitoa hela ya mtaji najikuta napata sh. 10,000 faida na inategemea na siku. Ukiamka ukakuta mchele umepanda hapo tena faida inazidi kupungua. Kwa ufupi maisha ni magumu,” alisema.

SERIKALI IKO KAZINI
Agosti 15, mwaka huu, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Dk. Ashatu Kijaji, alipozungumza jijini Dodoma, alisema serikali inaendelea kuchukua hatua ili kuwapunguzia wananchi athari zitokanazo na kupanda kwa bei ya bidhaa muhimu.

Alisema hatua hizo ni pamoja na kuwapunguzia gharama za uzalishaji, uagizaji na usambazaji wa bidhaa, ili kuleta uhimilivu wa bei kwenye soko lengo likiwa kumlinda mlaji kwa kuhakikisha anapata bidhaa bora kwa bei stahiki na kuzuia upandishwaji holela wa bei za bidhaa.

Pia alisema serikali imeondoa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa wazalishaji wa mbolea kwa kipindi cha mwaka mmoja ili kuwapunguzia wakulima gharama za uzalishaji, hivyo kuleta unafuu wa bei ya mazao muhimu ya chakula pamoja na kupunguza ushuru kwa maroli yanayosafirisha bidhaa.

Ripoti ya Shirika la Ushirikiano na Maendeleo ya Uchumi (OECD), Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), kuhusu Mtazamo wa Kilimo 2022-2031 inaonyesha mazao ya kilimo kote duniani yatakabiliwa na changamoto za kimsingi kwa miaka 10 ijayo na kuzitaka nchi kuchukua hatua endelevu kukabiliana na changamoto hiyo.

Ripoti hiyo inaeleza changamoto hizo ni kupanda kwa bei za mazao ya kilimo kulikosababishwa na mlipuko wa virusi vya corona, hali mbaya ya hewa katoka nchi muhimu za utoaji wa mazao, kupanda kwa gharama za uzalishaji na usafirishaji na uuzaji usio na uhakika wa mazao ya kilimo kutoka Ukraine na Russia ambazo ni nchi muhimu zaidi za utoaji wa nafaka umeifanya hali ya hivi sasa izidi kuwa mbaya.

Chanzo: Nipashe
Huwa mnakera sana mnapomtaja huyo marehemu
 
Serikali inayojielewa hutoa ruzuku inayoeleweka kwa wakulima.

Upo sahihi lakini ndiyo hivyo tena mkulima hapati ruzuku ambayo itahakikisha bei za mazao yake kama zikiporomoka bei ktk soko huria, basi mkulima alindwe kwa kupatiwa ruzuku aweze kurudisha gharama za uzalishaji ili msimu unaofuta aendelee kulima tena.

Ruzuku kwa Tanzania zipo kwa wakubwa wanaopatiwa maVX-8 ya shilingi milioni 500,000,000, marupurupu kugharamia fenicha za nyumbani na ofisini za bei ghali kabisa, safari za 'kikazi' na ziara kibao zinazoambatana na posho kubwa n.k
 
Wanachi wataumia sana, hawana mtetezi.
[emoji116]

Nipashe ilitembelea maeneo mbalimbali ya Dar es Salam na kubaini kupanda bei za bidhaa zinazotumiwa na kwa mlo wa kila siku ambazo ni mchele, maharagwe, unga wa ngano, unga wa sembe, dona na choroko.

Mchele kilo moja umepanda kutoka sh. 1,800 au 2,000 hadi sh. 2,700 daraja la kwanza na super kutoka sh. 2,500 hadi 3,500, unga wa sembe na dona umetoka sh. 1,200 hadi sh. 1,600 na unga wa ngano sh. 1,300 hadi 2,000 kwa kilo huku choroko ikipanda kutoka sh. 1,500 hadi sh. 2,500. Bei ya mfuko wa kilo tano za unga imepanda kutoka sh. 6,000 hadi 8,000.

Wakizungumza na Nipashe kwa nyakati tofauti, baadhi ya wananchi wamesema kutokana na kupanda kwa bei ya bidhaa hizo, wamelazimika kula milo miwili kwa siku badala ya mitatu.

Mkazi wa Tabata, James Macha, alisema analazimika kutokunywa chai ya asubuhi kutokana na kupanda kwa bei za vitafunwa ikiwamo chapati, maandazi na vitumbua, hivyo ili aweze kumudu gharama nyingine za maisha ikiwamo kulipa kodi ya nyumba na kulipa ada ya shule.

Macha, mwenye mke na watoto wawili, alisema kabla ya kuchukua uamuzi huo, sasa anatumia sh. 3,000 kwa ajili ya kununua vitafunwa asubuhi kutoka sh. 1,200 aliyokuwa anatumia awali. Alisema hali hiyo imetokana na vitafunwa hivyo kupunguzwa kipimo, hivyo kumlazimu kununua vingi ili vitosheleze.

Naye Mkazi wa Salasala, Mwajabu Abdul, mwenye watoto watatu anayefanya kazi ya saluni, alisema hali hiyo inawalazimu kutokula chakula cha mchana ili kuepuka gharama kubwa kutokana na kuwa na kipato kidogo.
"Wakati mwingine unajikuta umeamka na sh. 5,000, hivyo kuigawanya upate miko mitatu si rahisi.

Tunachofanya na wanangu tunachemsha mihogo ya buku (sh. 1,000) tunakunywa na chai saa tano asubuhi. Tukishashiba tena tunakuja kupika chakula saa 11:00 jioni, tunakula saa moja tunalala, siku zinasogea," alisema.

Mwajabu alisema awali walipata shida kwa sababu walikuwa wameshazoea kula milo mitatu hali iliyosababisha watoto kulegea na kusinzia wakati wa mchana lakini sasa wameshazoea na maisha yanakwenda sawa.

Dereva wa bodaboda eneo la Mwenge, Alex Mushi, alisema alichukua uamuzi wa kutokula chakula cha mchana baada ya kugundua kuwa anatumia pesa nyingi kula kwa mama ntilie.

"Kwa siku nikipata sana katika biashara yangu ni Sh. 25,000. Hapo Sh. 10,000 ni ya mwenye bodaboda, nabaki na sh. 15,000. Asubuhi chai tu sh. 2,500, mchana ili ushibe lazima ule pande mbili za ugali maana unapimwa kidogo sana jumla sh. 4,000. Jioni pia utumie sh. 4,000 jumla sh. 10,500 bado hujanywa maji. Sioni hata dalili ya kununua kiwanja," alisema.

Kutokana na kupanda huko kwa bidhaa, Mushi alisema kuna haja ya serikali kuangalia namna ya kupunguza gharama za nafaka kwa kuwa ndizo inasababisha gharama za vyakula kupanda huku watu wa hali ya chini wakiathirika zaidi.

Nipashe ilifunga safari mpaka kwa wauzaji wa vyakula ambapo Angela Maganga, muuzaji wa vitumbua Temeke, alisema amepoteza baadhi ya wateja baada ya kupunguza kipimo cha vitumbua ili apate faida kutokana na kupanda gharama za nafaka na mafuta ya kupikia.

Alisema ndani ya mwaka mmoja kilo moja ya mchele wa vitumbua imepanda kutoka Sh.1,400 hadi Sh.2,000 na mafuta lita moja ilikuwa sh. 3,500 sasa sh.5,000.

"Ni kweli dada nimepunguza kipimo cha upawa ili na mimi nipate faida nihudumie familia yangu, ndicho kimewakimbiza wateja. Serikali iangalie hizi nafaka mbona zinazopanda kila kukicha na zinaelekea kuua biashara zetu ambazo ndizo tunategemea kusomesha watoto,” alisema.

Naye Maria Kallaghe, mamalishe katika soko la Tandale, alisema kitendo cha wateja katika eneo hilo kutokula chakula cha mchana, kimemrudisha nyuma kimaendeleo kwa sababu anapata faida nusu ya aliyokuwa anapata mwanzo.

"Mauzo yameshuka kutoka sh. 50,000 hadi sh. 30,000. Hapo nikitoa hela ya mtaji najikuta napata sh. 10,000 faida na inategemea na siku. Ukiamka ukakuta mchele umepanda hapo tena faida inazidi kupungua. Kwa ufupi maisha ni magumu,” alisema.

SERIKALI IKO KAZINI
Agosti 15, mwaka huu, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Dk. Ashatu Kijaji, alipozungumza jijini Dodoma, alisema serikali inaendelea kuchukua hatua ili kuwapunguzia wananchi athari zitokanazo na kupanda kwa bei ya bidhaa muhimu.

Alisema hatua hizo ni pamoja na kuwapunguzia gharama za uzalishaji, uagizaji na usambazaji wa bidhaa, ili kuleta uhimilivu wa bei kwenye soko lengo likiwa kumlinda mlaji kwa kuhakikisha anapata bidhaa bora kwa bei stahiki na kuzuia upandishwaji holela wa bei za bidhaa.

Pia alisema serikali imeondoa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa wazalishaji wa mbolea kwa kipindi cha mwaka mmoja ili kuwapunguzia wakulima gharama za uzalishaji, hivyo kuleta unafuu wa bei ya mazao muhimu ya chakula pamoja na kupunguza ushuru kwa maroli yanayosafirisha bidhaa.

Ripoti ya Shirika la Ushirikiano na Maendeleo ya Uchumi (OECD), Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), kuhusu Mtazamo wa Kilimo 2022-2031 inaonyesha mazao ya kilimo kote duniani yatakabiliwa na changamoto za kimsingi kwa miaka 10 ijayo na kuzitaka nchi kuchukua hatua endelevu kukabiliana na changamoto hiyo.

Ripoti hiyo inaeleza changamoto hizo ni kupanda kwa bei za mazao ya kilimo kulikosababishwa na mlipuko wa virusi vya corona, hali mbaya ya hewa katoka nchi muhimu za utoaji wa mazao, kupanda kwa gharama za uzalishaji na usafirishaji na uuzaji usio na uhakika wa mazao ya kilimo kutoka Ukraine na Russia ambazo ni nchi muhimu zaidi za utoaji wa nafaka umeifanya hali ya hivi sasa izidi kuwa mbaya.

Chanzo: Nipashe
Hali mbaya unaambiwa vita ya Ukraine kila kitu nivita tu..
 
Mimi mwenyewe ni muhanga nakula asubuhi na jioni saa 12 jioni tuu, siku imeisha
 
Serikali haijapandisha nafaka kilichotokea ni kwamba msimu uliopita mvua zilinyesha kwa kusua sua hvyo mazao yalipatikana kwa kiasi ambacho sio kikubwa sana hasa mahindi

Lakini kipindi cha Magufuri karibia miaka yake yote ya utawala mvua zilikuwa nyingi kwahyo mazao yalipatikana yakutosha na hata umeme haukutusumbua maana mabwawa yalikuwa yamejaa
Wameuza sana nje mazao wakati ndani chakula hakitoshi eti wapate kupendwa na wafanyabiashara..
 
Mimi mwenyewe ni muhanga nakula asubuhi na jioni saa 12 jioni tuu, siku imeisha


Mkuu maeneo ya kulima hayajaisha na vibarua wa kuwaweka wakufanyie kazi ukiwalipa wapo wamejaa vijijini kwanini tusiwe tunalima kuepuka adha hizi
 
Wapo mkuu na kuna mkulima maarufu wa mchele mbeya juzi tu kapata tenda ya kuuza maelfu ya tani za mchele kila mwezi kwenda Kenya au nae huyo sio mtanzania?
Kwa Tz, hakuna mkulima anayeweza kuwa na uwezo wa kufanya hiyo biashara eti maefu ya tani za mchele kwa mwezi?
Mkuu dunia imebadilika na kama unadhani mazingira yanaruhusu utajirikie kupitia bei za shamba ingia uone moto wake watu wanasafirisha mahindi anafika na mzigo anakula loss
Hujanielewa, mimi nilikuwa namkatalia jamaa, aliyesema kuwa wakulima msimu huu wamefaidika kutokana na nafaka kuwa juu, nikasema sio kweli, kwani wakulima wetu wengi wakaishavuna wao ni kuuza tu, ila wanao kuja kufaidika ni wafanya biashara ambao wao hununua mazao mengi kipindi cha mavuno na kuyaweka kwenye maghara hadi bei zipande, ndipo wauze, sikatai nao kuna wakati wanapata hasara kutokana na bei, kuwa chini, kwa muda mrefu, hii biashara ya mazao nimeifanya sana hada mpunga ninajua nini nasema.Mfano kipindi cha mavuno una nunua gunia la mpunga kwa tsh.25, 000 ukiuhifadhi baada ya muda hasa kuanzia miezi ya 12-1, hilo gunia unaweza kuliuza kwa 80, 000-100, 000!!
 
Wameuza sana nje mazao wakati ndani chakula hakitoshi eti wapate kupendwa na wafanyabiashara..

Usijali mkuu serikali inayo maghala ya chakula hivyo kikipingua itafungulia maghala isitoshe zipo njia nyingine nyingi tu ilimradi bei zisishuke
 
Back
Top Bottom