Miaka mitano ya hayati Magufuli, bei za nafaka hazikupanda namna hii. Sasa zimepanda na wananchi wanakula mlo mmoja na nusu

Miaka mitano ya hayati Magufuli, bei za nafaka hazikupanda namna hii. Sasa zimepanda na wananchi wanakula mlo mmoja na nusu

Kwa Tz, hakuna mkulima anayeweza kuwa na uwezo wa kufanya hiyo biashara eti maefu ya tani za mchele kwa mwezi?

Hujanielewa, mimi nilikuwa namkatalia jamaa, aliyesema kuwa wakulima msimu huu wamefaidika kutokana na nafaka kuwa juu, nikasema sio kweli, kwani wakulima wetu wengi wakaishavuna wao ni kuuza tu, ila wanao kuja kufaidika ni wafanya biashara ambao wao hununua mazao mengi kipindi cha mavuno na kuyaweka kwenye maghara hadi bei zipande, ndipo wauze, sikatai nao kuna wakati wanapata hasara kutokana na bei, kuwa chini, kwa muda mrefu, hii biashara ya mazao nimeifanya sana hada mpunga ninajua nini nasema.Mfano kipindi cha mavuno una nunua gunia la mpunga kwa tsh.25, 000 ukiuhifadhi baada ya muda hasa kuanzia miezi ya 12-1, hilo gunia unaweza kuliuza kwa 80, 000-100, 000!!


Mpunga wa elfu 25 gunia ilikuwa wapi hiyo nami nijue aisee? Maana huu mwakaa kote bei zimefumuka na zinarandana vibaya sana hii nchi yote hapa sijui bei za Mpanda tu
 
Gharama za uzalishaji mwaka jana pia zilikuwa juu mno. Acha wauze kwa Bei yoyote.
Mwakani pigeni kelele Bei zishuke sababu angalau mbolea zitanunuliwa kwa 70,000
Inshu sio gharama za uzarishaji kwa mwaka jana ndio zimefanya bei ya nafaka kuwa juu kiasi hicho.Kwani ni mwaka jana tu ambapo pembejeo zilikuwa juu?!!Sababu ni ukosefu wa mvua tu kwa maeneo mengi ya nchi, kwani hii mikoa ya Rukwa, mbeya, katavi, Ruvuma na Morogoro ikishakuwa na uhaba wa mvua tu, uhaba wa chakula lazima utokee tu.
 
Mimi pia nafanya ukulima ila bei ya mbolea ni cheche mkuu
Ndio hapo tuombee bei za mazao ziwege juu ili gharama za kulima tuweze kuwa tunazimudu sasa tukiitikia wimbo wa hawa wajanja wa mjini wanaotakaga bei ziwe chini kwa maslahi yao peke yao ndio hapo sasa mitaji ya shamba inakata fikiria mbolea mfuko ni mara tatu ya kabla ya Corona sasa bei mazao yakiwa chini kutakuwa na kulima hapo?
 
Mpunga wa elfu 25 gunia ilikuwa wapi hiyo nami nijue aisee? Maana huu mwakaa kote bei zimefumuka na zinarandana vibaya sana hii nchi yote hapa sijui bei za Mpanda tu
Bei huwa ni 25, 000-30, 000 kwa mapoli yote ya mkoa wa katavi, lakini kwa mwaka huu, hakukuwa na bei hizo kwani hata huko mavuno yalikuwa machache sana, japo huwezi kulinganisha na mikoa mingine.Mwaka huu bei zilianzia 60, 000 ambapo sio kawaida kwani wanunuzi walikuwa wengi sana kutoka mikoa mingine.
 
Ndio hapo tuombee bei za mazao ziwege juu ili gharama za kulima tuweze kuwa tunazimudu sasa tukiitikia wimbo wa hawa wajanja wa mjini wanaotakaga bei ziwe chini kwa maslahi yao peke yao ndio hapo sasa mitaji ya shamba inakata fikiria mbolea mfuko ni mara tatu ya kabla ya Corona sasa bei mazao yakiwa chini kutakuwa na kulima hapo?
Kwa tanzania ni bora uwe mfanyabiashara wa mazao sio mkulima, ukulima ni maumivu aiseee, wee utalimaaa wee dalali anakuja na bei yake
 
Watoto wa marehemu mmeshaanza Tena.

Ukweli huwa unajitetea wenyewe, huitaji kutumia nguvu kuutetea ukweli.
Nipashe ndio unawaita WATOTO WA MAREHEMU ? Umesahau aliwafungia?
 
Kwa tanzania ni bora uwe mfanyabiashara wa mazao sio mkulima, ukulima ni maumivu aiseee, wee utalimaaa wee dalali anakuja na bei yake


Simu zimekuja kuokoa jahazi walaliaji sahivi cha moto wanakiona maana wakulima wanapigiana simu na hili limeonesha nguvu yake miaka hii simu zilivyoenea unakuta zao fulani bei moja kanda zote za nchi iwe mbali na soko haijalishi
 
Simu zimekuja kuokoa jahazi walaliaji sahivi cha moto wanakiona maana wakulima wanapigiana simu na hili limeonesha nguvu yake miaka hii simu zilivyoenea unakuta zao fulani bei moja kanda zote za nchi iwe mbali na soko haijalishi
Na madalali wanapigiana vilevile
 
Mazao bei moja maeneo yote hata wakapigiana simu haisaidii na sio kwamba madalali wanapendana wanazibiana riziki sana tu
Sijakataaa ila hata wazibiane kiasi gani hawaja wahi kuwa upande wa mkulima
 
Mkuu, kwenye katiba ya JMT hakuna kifungu kinachokukataza wewe na familia yako kujihusisha na shughuli za kilimo!
Kama unaona bei zimepanda sana na hauko tayari kununua mazao kwa bei hizo, ingia shambani ukalime.

Hivyo vivyo kwa wewe Mkuu Katiba ya JMT hamna mahali inakulazimisha kuendelea kuwa kiongozi kama umeshindwa kupatia majibu changamoto unazo takiwa kuzifanyia kazi kwa faida ya unaowaongoza.
 
Hivyo vivyo kwa wewe Mkuu Katiba ya JMT hamna mahali inakulazimisha kuendelea kuwa kiongozi kama umeshindwa kupatia majibu changamoto unazo takiwa kuzifanyia kazi kwa faida ya unaowaongoza.
Majibu yapo. Tafuta kipande cha ardhi nusu heka, lima mihogo au viazi mviringo au viazi vitamu au ndizi.
Utakula wewe na familia yako, 'mwaka mzima' bila ya 'kukanyaga sokoni'.
 
Majibu yapo. Tafuta kipande cha ardhi nusu heka, lima mihogo au viazi mviringo au viazi vitamu au ndizi.
Utakula wewe na familia yako, 'mwaka mzima'.

Mafuta ya kupikia hivi unayatoa wapi kama lita moja VO imetoka 3,500/= hadi 8,000/=? Wataalamu watuambie ni %age ngapi ya ongezeko la bei hapo?
 
Ngoja nianze kuimba huu wimbo kabla ya 2025 : " Mlitupenda wenyewe ,mkatuchagua wenyewe , wacha waisome namba weee CCM mbele kwa mbele "
CCM Oyeeeeeee !
Umoja wa Wamama CCM Oyeeeee!
UVCCM Oyeeeeeeeee!
Kidumu chama cha mapinduzi , kidumuuuuu
 
Mpumbavu yule....sisi wakulima tulishindwa hata kununua uniform za shule kisa bei za mazao kuwa chini....
tunashukuru sasa ingalao
Huo nao ni uongo mwingine kwa mtu asiyejua maisha ya wakulima!

Ukiona bei ya mazao chukulia mahindi kama zao kuu zimepanda anayefaidika ni mfanyabiasha na wakati huo huo mkulima anaumia zaidi.

Kwa nini?
1. Mkulima anauza mazao mwanzoni kabisa anapovuna au hata yakiwa shambani. Na trend ya bei ya mazao hayo ilivyo kipindi hicho inakuwa iko chini sana lakini itaendelea kupanda kadri siku zinavyoongezeka.
2. Na kwa sababu wakulima wengi ni desperate wanauza mazao yote bila kuweka akiba, ili aweze kutatua matatizo kibao aliyo nayo kwa wakati huo. Na kukiwa na ongezeko kidogo la bei ndiyo kabisaa.
3. Bei ikipanda eanaofaidi ni chain ya wafanyabiashara kuanzia walioweka stock, wanaosafirisha toka vijijini kwenda centres za mjini na wanaosafirisha toka kwenye hizo centre (ndogo) kwenda masoko makubwa ya mjini nk
4. Bei inapokuwa kubwa zaidi baada ya muda kupita mkulima yule yule sasa atauziwa chakula(hana, aliuza chote) na wafanyabiashara kwa bei kubwa sana ya soko.
5. Kutokana na hilo na ukweli kwamba purchasing power ya mkulima wavkijijini ni ndogo sana ukilinganisha na wengi wanaoishi mjini, yeye ndiyo kupanda kwa bei kuna muathiri zaidi kuliko watu wa mjini.

Kwa hiyo dhana ya kwamba bei ikipanda mkulima ananufaika zaidi siyo kweli, ila ni kinyume chake. Na hii tumeshuhudia kwa miaka mingi hata nadhani 2016 au 2017 bei ya mahindi ilipopanda sana.
 
Back
Top Bottom