Milioni 350 za faini ya kina Mbowe zinazorudishwa na mahakama unashauri zifanye kazi gani?

Milioni 350 za faini ya kina Mbowe zinazorudishwa na mahakama unashauri zifanye kazi gani?

Ni kiasi cha US$ 150,000 sawa na milioni 350.
  1. Zijenge ofisi makao makuu?
  2. Zisaidie kulipa faini na mawakili wa kesi zilizobaki?
  3. Zisaidie mchakato wa katiba mpya?
  4. Zinunue kiwanja cha ofisi makao makuu Dodoma au Dar es salaam.
  5. Zisaidie ujenzi wa ofisi za kanda?
  6. Zinunue vitendea kazi vya chama.
  7. Zigawanywe kwa viongozi waliohukumiwa.

Maoni yenu tafadhali.

Ijengewe ofisi ya makao makuu, ama zitolewe 50m@ ili zijengwe ofisi za kanda.
 
Kweli haki ya mtu hucheleweshwa tu ila ipo siku hupatikana.
... imagine wangeshindwa kulipa faini wakaenda jela; ndio hivyo tena haki yao ingekuwa imepotea. Kweli nimeamini mhimili wa utoaji haki hautakiwi kutiliwa shaka au kuwa na watendaji wenye mazongezonge hata chembe. Mahakama ijitafakari.
 
Kwani hizi pesa zinarudishwa chamani au anarudishiwa mtu mmoja mmoja kutokana na faini aliyolipia?
Zitarejeshwa kwa wadhamini waliolipa faini kwa niaba ya waliohukumiwa.
 
Kwani ulichanga?
Unajua zilitoka wapi?
Nakuona wewe ni mwanaume lkn una vinasaba vya kike.
 
Hizo hela hazikutolewta na chama, bali tulitoa sisi wafuasi kwa imani ya chama, ndio maana hatumkutolea Mashinji maana alienda kuunga juhudi za ibilisi.
Yes kama zililipwa kutoka acvount ya chama basi zitarusishwa kwenyw acviunt ya chama, na ni maki ya chama maana tukichanga kwa dhumuni la kukisaidia chama chetu pendwa
 
zinarudi kwenye mfuko wa chama kama zilitoka kwenye huo mfuko
 
Hizo hela hazikutolewta na chama, bali tulitoa sisi wafuasi kwa imani ya chama, ndio maana hatumkutolea Mashinji maana alienda kuunga juhudi za ibilisi.
Kwahiyo Jamhuri itazirudisha kwa nani?

1.Kwa Chama.

2. Kwa wakina Mbowe, Mashinji, Mnyika, Mdee n.k

3. Au kwa waliochangia.

Mimi navyoona namba 2 ndio jibu, maan hao ndio walipigwa faini hiyo.
 
Back
Top Bottom