Mimi binafsi, siwezi kumsikiliza rais Samia

Mimi binafsi, siwezi kumsikiliza rais Samia

Aliyeandikiwa na Mungu ameandikiwa tu, ni riziki yake urais wa JMT
Hayo maandishi ya mungu yaliyotaja marais waliowahi kuwa / watakaokuwa naipata wapi mdau ?
. Wasomi wangapi wana mashahada mengi lakini wanapopewa kazi zenye kuendana na elimu zao wanaishia kuvurunda?.
Kwahiyo kama wasomi waliowahi kupewa nafasi za uongozi wakavurunda ndio tuhamie kuchagua kuongozwa na vilaza?

Taifa lilisilofuata "meritocracy" kuendelea ni ngumu sana.

Kwahiyo pia unashauri shule zifungwe madarasa wafugie kuku?
 
Hayo maandishi ya mungu yaliyotaja marais waliowahi kuwa / watakaokuwa naipata wapi mdau ?

Kwahiyo kama wasomi waliowahi kupewa nafasi za uongozi wakavurunda ndio tuhamie kuchagua kuongozwa na vilaza?

Taifa lilisilofuata "meritocracy" kuendelea ni ngumu sana.

Kwahiyo pia unashauri shule zifungwe madarasa wafugie kuku?
Masuala ya meritocracy ni mbwembwe tu. Trump kule USA ana elimu ya kawaida tu lakini aliwaongoza kwa miaka minne na wafanyabiashara wakubwa walifurahia sana namna uchumi ulivyofanikiwa katika muda huo.

Anao wasaidizi wenye elimu za juu sana ambao wanafidia upungufu wa elimu yake kuwa ni ya kawaida tu.
 
Mh!! Ndugu mleta mada naona kavurugwa kabisa - maana si kwa kutiririka huko.
Sema TISS mlioko humu - na wengine - mnajukumu kubwa la kufanya kuokoa taifa hili - TISS fanyeni mission ambayo vizazi vya miaka 200 mbele vitawakumbuka...Hiyo I kwenye TISS ni INTELLIGENCY...watu tuone kweli kuna vichwa kule otherwise ni disaster.Fanyeni hivi:
1.Pandikiza watu wafia nchi -CCM..achaneni na watu wenu ambao kwao CCM mbele - taifa linafuata
2.Ivunjeni CCM vipande viwili - vyenye nguvu visivyoweza kuelewana.Tupate vyama viwili heavy ambavyo vinanguvu sawa - connection sawa - ushawishi sawa..LKN hakikisheni havi- helewani kamwe..
Hii CCM ya sasa hivi ndo shida nchi hii - kujuana - Monarchy - wachache ndo wanakula hii nchi tena wako untouchable.
3.Mkivunja CCM tukapata A & B: Hapo hapo amsheni mambo ya katiba mpya.Hivi vyama vyote vikubali katiba mpya - them.l mchakato wa katiba urudi...Hakikisheni wananchi, vyama, vyote, mashirika ya kiraia yanashirikishwa - Tupate katiba itskayotatua changamoto zote tulizoziona kwa miaka hii zaidi ya 60 tumepata..ikiwezekana wekeni wasomi wayahighlight kabisa mapema.
Mkiweza kufanya hivyo bila vurugu, bila hata watu kuelewa how changes zimetokea - huko mambo yakiendelea kama kawaida - kwa amani - YOU WILL GO DOWN IN HISTORY KAMA moja ya Taasisi reputable zenye vijana wenye akili - Vijana watawapenda - watu wengi wenye akili above normal human beings watapenda kufanyakazi na nyinyi..
Subirini miaka 5 ya Mama ipite - 2030..najua CCM patachimbika sana - hapo ndo penyewe.
Chance nyingine ilikuwa vuguvugu la Lowassa 2015 - kipindi kile CCM wanamnanga mwenyekiti wao - hapohapo...CCM ilikuwa imepasuka pale - mngeendeleza ule mpasuko to the maximum yaani watu wavurugane hatari..
Bila hivyo watu wataendelea kulalamika na kuumia sana kama mleta mada.
CCM ndo shida hii nchi - waondoeni hao - gawanyisheni watu wake tupate vyama vya kisasa
 
Nina swali hapo.
Hio kauli ulioiandika humu JF.ili kujua Bongo hamna FREEDOM OF SPEECH/ uhuru wa habari.
Mimi hili halinihusu video si inajieleza hapo alisema mwenyewe au hujatazama video.
Ukiisema hio kauli hadharani utajikuta porini katavi.
Watateka watu wangapi?

Edgar walimteka na kumtupa Katavi ila leo hii yupo na anazungumza yale yale na ukweli kuhusu utekaji.

Pia tangu wamteke Edgar je Samia ndio alipendwa na watu wote mdau??

Ngoja nikupe mifano mitatu ili ujue kuteka /kuua sio suluhu ya watu unaopishana nao mawazo.

Nakurudisha darasa la historia pengine hutopenda kuisikia .

1.Nyerere aliyeitwa baba wa demokrasia hakuwa mtu aliyependa mawazo mbadala alifanya ushawishu muswada wa nchi kuwa ya chama kimoja 1963 na hadi 1965 muswada ulipita na Tanzania ikawa rasmi taifa la chama kimoja kisheria , Nyerere akaingia katika uchaguzi mkuu wa kiini macho kama huu wa CCM matokeo kwenye karatasi ni picha [ndio ] kivuli [hapana] mwisho wa siku matokeo yalikuwa hivi.

Kura za ndio 2,410,903 sawa na asilimia 96.46

Kura za hapana ni 88,600 sawa na asilimia 3.54 .

Hapo ni funzo kuwa licha ya Nyere kutaka nchi iwe ya chama kimoja bado sio wote walimkubali kisera akaishia kupata hapa 3.54 % na pia hata huo uhalali wa 96.46 ungeweza kupungua zaidi kama asingejipa mamlaka ya kuwa na chama kimoja kihalali kisheria.

Nyerere katika awamu miaka yake yote ya utawala tangu kuzaliwa Tanzania hajawahi kupitia uchaguzi wa vyama vingi ila bado haikuzuia watu kumpinga mwishoni ndio akawa mkosoaji wa demokrasia huku akimkosoa Mwinyi hadi kumuandika katika kitabu jinsi anavyoendesha serikali huyu dakika za mwisho ndio akageuka "champion" wa kuhamasisha vyama vingi vya siasa kurudishwa.

2.Joseph Mobutu huyu alimiliki kila kitu hadi kubadilisha jina la nchi , viwanja , miji bila utaratibu maalum huyu upigaji kura ulikuwa ni wazi uchague ndio au hapana alijimilikisha kila kitu hadi kujenga kasri na uwanja wa ndege kijijini kwao .

Kwa nguvu na mauaji aliyofanya Mobutu kule kwao ni alikojenga sasa ni magofu na hakuweza hata kuzikwa kwao bali alizikwa Morocco.

3.Iddi Amin huyu alijipa vyeo vikubwa vya kijeshi na alikuwa ni mtu wa kauli moja licha ya mauaji na utekaji wake kujilimbikizia mali huyu nae hakufanikiwa kuzikwa kwake na alipofariki waligomewa asizikwe Uganda mwisho wa siku alizikwa Saudi Arabia.

Mimi sio mwandishi mzuri sana ila nimekupa mifano michache uone jibsi gani madaraka ni kitu cha kupita na kuua,kuteka,kutesa hakukufanyi upendwe na watu wote au watu wote wawe na mawazo sawa na wewe.
Je CEO wa JF ametuhakikishia ulinzi, sio polisi wakamuhitaji mwa JF alietoa kauli fulani. Akatolewa?
Wao wasihangaike na Max walimsumbua Max miaka ile sana wao wenyewe humo una uhakika wanapenda yanayoendelea au ni uniform na viapo ndio vinawabana .

Kama unabisha itisha opinion poll za wazi kuhusu Samia humu na hata moja ipo jukwaa hili kaone matokeo utabaki na mshangao.

Mimi nimetishiwa awamu ile na ID 3 hivi enzi za jiwe hawa watu leo hii wamebadili ID ila ndio vinara wa kumponda Samia , jibu silijui ni kwanini huenda walinufaika na utawala ule na sasa huu nao huyu kaja na wake.
 
Masuala ya meritocracy ni mbwembwe tu. Trump kule USA ana elimu ya kawaida tu lakini aliwaongoza kwa miaka minne na wafanyabiashara wakubwa walifurahia sana namna uchumi ulivyofanikiwa katika muda huo.
Hivi huoni aibu kudanganya?

Trump ana shahada ya kwanza ya uchumi sio hizi za kutunukiwa Samia unasema ni elimu ya kawaida?

Samia anayo shahada ya kwanza ya kitu gani?
Anao wasaidizi wenye elimu za juu sana ambao wanafidia upungufu wa elimu yake kuwa ni ya kawaida tu.
Wasaidizi kwa nchi ambayo rais ni kila kitu hawana nguvu yoyote .

Umesahau yule mzee mhandisi aliyeweka elevator akafokewa sasa Magufuli alikuwa mhandisi?

Uliona jibu la kitaalam alilotoa yule mzee, Magufuli akabaki kutumia ubabe tu ila utaalam hana!
 
Hana uwezo lakini uwezo wa kuiba kura anao ndo utajua uwezo anao au hana.
 
Huyo jamaa akilin zake zimeishia tumboni tu sio kutazama mustakabali wa taifa zima. Watanzania hatuoneani huruma tumetanguliza ubinafsi mbele.
Hali hiyo ya ubinafsi ndiyo anayo itengeneza Samia. Si unaona utitiri wa "chawa", hata humu JF?

Ndani ya chama, ambacho Samia ndiye mwenyekiti, hali ni hiyo hiyo; kuhakikisha ubinafsi ndiyo kazi muhimu anayo itengeneza Samia, kwa sababu anajuwa kukiwa na kundi lenye mawazo nje ya ubinafsi litamletea matatizo.
 
Uwezo gani zaidi unataka? Ana mwaka wa 3 anatawala, nini kimepungua?
"Kupungua" ni jambo jingine linalo jibika pia, lakini binafsi najuwa "kuongezeka".
Chawa wanao pigana vikumbo kunyonya uchafu wa mama wameongezeka sana. Sasa hapo sijui kama huo ni uwezo wa "kuongoza" nchi au la!
 
Hivi huoni aibu kudanganya?

Trump ana shahada ya kwanza ya uchumi sio hizi za kutunukiwa Samia unasema ni elimu ya kawaida?

Samia anayo shahada ya kwanza ya kitu gani?

Wasaidizi kwa nchi ambayo rais ni kila kitu hawana nguvu yoyote .

Umesahau yule mzee mhandisi aliyeweka elevator akafokewa sasa Magufuli alikuwa mhandisi?

Uliona jibu la kitaalam alilotoa yule mzee, Magufuli akabaki kutumia ubabe tu ila utaalam hana!
Shahada ya Trump ni sawa na hizi za wanasiasa wetu, ya kuandikiwa. Ni mtupu sana yule mzee. Punguza unyonge na kujidharau.

Nina uhakika Babu zako hawajui hata kuandika majina yao. Samia anayo shahada ya chuo kikuu, tafuta CV yake achana na hizi story za chuki za mitandaoni.

Ndio Rais atakayekuwa na mafanikio makubwa kuliko watangulizi wake watano. Kasambaza umeme nchi nzima, kaifanya Tanzania yote imekuwa rahisi kufikika na kutokeka kwa kumaliza ujenzi wa miundo mbinu mingi.
 
"Kupungua" ni jambo jingine linalo jibika pia, lakini binafsi najuwa "kuongezeka".
Chawa wanao pigana vikumbo kunyonya uchafu wa mama wameongezeka sana. Sasa hapo sijui kama huo ni uwezo wa "kuongoza" nchi au la!
Chawa ni vijana wa mijini wenye kutafuta riziki zao kwa ujanja wa maongezi yao. Samia kagusa maisha ya kiuchumi ya Tanzania.

Pita hapo mkoa wa Pwani utakutana na viwanda vingi vinavyozalisha mali muda huu. Treini ya SGR kaimalizia na imeshaingiza bilioni karibu 20 kwa kipindi cha miezi sita iliyofanya kazi.

Sijaongelea ndege za ATCL zinazopishana huko angani.
 
Shahada ya Trump ni sawa na hizi za wanasiasa wetu, ya kuandikiwa. Ni mtupu sana yule mzee. Punguza unyonge na kujidharau.
Narudia tena huoni aibu kudanganya?

Shahada ya kwanza US ni sawa na shahada ya Tanzania?

Nina uhakika Babu zako hawajui hata kuandika majina yao.
Babu zangu walisoma mapema sababu walinufaika na elimu ya wamisionari waliokuja enzi hizo mmoja alipata shahada yake ya Kwanza Uingereza.
Samia anayo shahada ya chuo kikuu, tafuta CV yake achana na hizi story za chuki za mitandaoni.
Shahada gani naomba niifahamu.
Ndio Rais atakayekuwa na mafanikio makubwa kuliko watangulizi wake watano. Kasambaza umeme nchi nzima,
Naomba takwimu/namba zinazoonyesha huo mpango wa kufikisha umeme nchi nzima ulianza lini na sasa umefikia asilimia ngapi.
kaifanya Tanzania yote imekuwa rahisi kufikika na kutokeka kwa kumaliza ujenzi wa miundo mbinu mingi.
Miundombinu ipi ya kimkati amejenga

Nitajie 10 tu.
 
Mkuu waweza kuwa sawa au sio sawa ila kiongozi hupatikana kutokana na mfumo uliopo wa kutambua vipaji.

Kunakuwa na shule maalum na baadae vyuo maalum hadi kiongozi sahihi apatikana.

Mfumo huo pia waweza kuwa "compromised" na kukapatikana watu ambao hawana sifa za kuongoza.
Sio kwa Tanzania..Hapa uongozi mkubwa hutolewa kama zawadi... Hivi unajua Bashite kwa mfumo wetu nae anawaza kuja kuwa Rais wa hii nchi.
 
Sio kwa Tanzania..Hapa uongozi mkubwa hutolewa kama zawadi... Hivi unajua Bashite kwa mfumo wetu nae anawaza kuja kuwa Rais wa hii nchi.
Hata Kingwendu anaweza kuwa rais Tanzania.

Ni mtu kutafuta ushawishi na kupata fungu la kutosha kuhonga machawa, kuteka media zote na vyombo vya usalama.
 
Narudia tena huoni aibu kudanganya?

Shahada ya kwanza US ni sawa na shahada ya Tanzania?


Babu zangu walisoma mapema sababu walinufaika na elimu ya wamisionari waliokuja enzi hizo mmoja alipata shahada yake ya Kwanza Uingereza.

Shahada gani naomba niifahamu.

Naomba takwimu/namba zinazoonyesha huo mpango wa kufikisha umeme nchi nzima ulianza lini na sasa umefikia asilimia ngapi.

Miundo mbinu ipi ya kimkati amejenga

Nitajie 10 tu.
Ingia google utakuta taarifa sahihi za SSH, ni shughuli nyepesi kuifanya.

Trump mjinga tu, tazama namna wamarekani wenyewe wanavyomgeuza kichekesho kila siku.

Kama mababu zako walisoma basi punguza kutumia elimu kama ndio kigezo cha kufanikiwa, unaweza ukawa na elimu ndogo tu lakini akili ukawa na akili kubwa ya kutafuta maisha.

Bakhresa ana elimu gani ya chuo kikuu?. alianza na kazi ya ufundi viatu miaka ile ya 80 mwanzoni leo ni bilionea mkubwa.

Umeme wa REA umesambazwa Tanzania nzima, nenda wizara ya nishati watakupa takwimu halisia za wapi umeshafikishwa na wapi bado haujafika.

Punguza utumwa wa kudhani elimu ndio kila kitu, unaweza kuwa nayo bado ukawa kichekesho kwa kulinganishwa na wasio na elimu kubwa lakini wenye hekima na busara vichwani.
 
Chawa ni vijana wa mijini wenye kutafuta riziki zao kwa ujanja wa maongezi yao. Samia kagusa maisha ya kiuchumi ya Tanzania.

Pita hapo mkoa wa Pwani utakutana na viwanda vingi vinavyozalisha mali muda huu. Treini ya SGR kaimalizia na imeshaingiza bilioni karibu 20 kwa kipindi cha miezi sita iliyofanya kazi.

Sijaongelea ndege za ATCL zinazopishana huko angani.
Heshima mkuu 'Steve'.
Mi nilidhani wewe na mimi tulisha malizana juu ya huyu kongozi wetu; ndiyo maana hunisikii/hunioni nikijibu hoja zako.

Sasa sijui unataka nijieleze vipi kwako ili uweze kunielewa vizuri misimamo yangu juu ya uongozi wa huyu mama yetu! Nilikwisha jieleza kwa kadri ya uwezo wangu kwako; sasa sijui kimebaki nini cha ziada.
Nilicho baki nacho tu mkuu wangu 'Steve', wacha Muumba wetu na wa taifa letu aamue hatma ya taifa lake hili. Kama anataka kutuangamiza kama taifa, basi kampata wakala wake mzuri kabisa wa kuifanya kazi hiyo kupitia kwa huyu kiongozi.
Ngoja tuisubiri hiyo 2025.
 
Ingia google utakuta taarifa sahihi za SSH, ni shughuli nyepesi kuifanya.
Kwani ukiweka hapa kiambatanisho kuna shida gani?
Trump mjinga tu, tazama namna wamarekani wenyewe wanavyomgeuza kichekesho kila siku.
Sio mjinga kuliko Samia lakini?
Kama mababu zako walisoma basi punguza kutumia elimu kama ndio kigezo cha kufanikiwa, unaweza ukawa na elimu ndogo tu lakini akili ukawa na akili kubwa ya kutafuta maisha.
Umebadilisha mada?

Wapi nimesema elimu ndio kigezo cha kufanikiwa.

Halafu kufanikiwa /mafanikio ni suala subjective.

Mwingine ili kufanikiwa ni kuwa na gari nyumba, n.k

Mwingine mafanikio yake ni kuisaidia jamii kupitia elimu yake ya darasani, ujuzi n.k

Hivyo usibadili mada.
Bakhresa ana elimu gani ya chuo kikuu?. alianza na kazi ya ufundi viatu miaka ile ya 80 mwanzoni leo ni bilionea mkubwa.
Bakhresa ni rais wa Taifa gani?

Hapa mada tunaongelea umuhimu wa elimu katika ngazi ya urais.
Umeme wa REA umesambazwa Tanzania nzima, nenda wizara ya nishati watakupa takwimu halisia za wapi umeshafikishwa na wapi bado haujafika.
Kama siwezi kufika hizo takwimu nazipata wapi?

Nisaidie link maana ndio umesema "mama " amesambaza umeme nchi nzima.
Punguza utumwa wa kudhani elimu ndio kila kitu,
Kwahiyo tufunge shule watu wasisome ndio hawatokuwa watumwa?
unaweza kuwa nayo bado ukawa kichekesho kwa kulinganishwa na wasio na elimu kubwa lakini wenye hekima na busara vichwani.
Kwahiyo mtu anaenda kusoma shule awe kichekesho baadae?

Mwisho nimeomba uniorodheshee miundombinu 10 ya kimkakati aliyoijenga "mama "kuwezesha Tanzania kufikima kote .

Hilo ni suala gumu kwako kuorodhesha na umekwishasema huyu ndio rais aliyefanikiwa kuliko watangulizi wake wote?

Kama hutonijibu sioni sababu ya kuendeleza mjadala na wewe maana itakuwa uwezo wako ni sawa na unayemtetea katika mada iliyopo mezani.
 
Ingia google utakuta taarifa sahihi za SSH, ni shughuli nyepesi kuifanya.

Trump mjinga tu, tazama namna wamarekani wenyewe wanavyomgeuza kichekesho kila siku.

Kama mababu zako walisoma basi punguza kutumia elimu kama ndio kigezo cha kufanikiwa, unaweza ukawa na elimu ndogo tu lakini akili ukawa na akili kubwa ya kutafuta maisha.

Bakhresa ana elimu gani ya chuo kikuu?. alianza na kazi ya ufundi viatu miaka ile ya 80 mwanzoni leo ni bilionea mkubwa.

Umeme wa REA umesambazwa Tanzania nzima, nenda wizara ya nishati watakupa takwimu halisia za wapi umeshafikishwa na wapi bado haujafika.

Punguza utumwa wa kudhani elimu ndio kila kitu, unaweza kuwa nayo bado ukawa kichekesho kwa kulinganishwa na wasio na elimu kubwa lakini wenye hekima na busara vichwani.
Tatizo liko hapa...
 
Kusikiliza na kubaki kimya ni bora zaidi kuliko kutomsikiliza kabisa ..

Chuki ni Adhabu ya kihisia unayoupa Mwili wako kwa kosa/Upumbavu wa mtu mwingine .

Hata mimi simuelewi ila kwakua siwezi kubadili chochote ninahaki ya kumsikiliza na kutulia Kimya , No complaining .
 
"Kupungua" ni jambo jingine linalo jibika pia, lakini binafsi najuwa "kuongezeka".
Chawa wanao pigana vikumbo kunyonya uchafu wa mama wameongezeka sana. Sasa hapo sijui kama huo ni uwezo wa "kuongoza" nchi au la!
Wewe unanyonya uchafu wa nani mkeo au malaya?
 
Wewe unanyonya uchafu wa nani mkeo au malaya?
Mimi nanyonya wa taifa linalo najisiwa sasa hivi; na nitaendelea kuunyonya hadi pumzi ya mwisho. Kwa hiyo naomba usinilulize swala kama hilo tena. teana
 
Back
Top Bottom