TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

Utoto ni nini na ukubwa ni nini ndugu?
Kutoa kwa ajili ya kizazi kijacho.
Hii tabia tulitakiwa tuwe nayo tangu utoto na tungeenda nayo hadi ukubwani.
Ila tabia ambayo tunayo ni ile utoe ili unufaike. Na hiki ndicho kimesababisha hadi leo bukoba ipo nyuma.
Akili nyingi huondoa maalifa. Mmejenga mashule mengi Dar kwa easy payback.
Je mngejenga Bukoba mjini ingekuwaje?no easy payback
 
Kutoa kwa ajili ya kizazi kijacho.
Hii tabia tulitakiwa tuwe nayo tangu utoto na tungeenda nayo hadi ukubwani.
Ila tabia ambayo tunayo ni ile utoe ili unufaike. Na hiki ndicho kimesababisha hadi leo bukoba ipo nyuma.
Akili nyingi huondoa maalifa. Mmejenga mashule mengi Dar kwa easy payback.
Je mngejenga Bukoba mjini ingekuwaje?no easy payback
Tuanze sasa, inawezekana[emoji4]
 
Sisi tuna nyumba pale mtaa wa uswahilini.
Ni ya late bibi.nimejaribu kuwashauli Mama zetu ambao ni warithi watuachie sisi watoto wao. Tuijenge iwe ya kisasa na vizazi vyetu baadae nao kila likizo wawe na sehemu nzuri ya kufikia. Nimegonga mwamba.
Wamepiga hesabu zao nani kabaki bk na kuna ambaye anahitaji kurudi bk kati yao.wameamua kuiuza. Kwa kuwa wao wapo Dar na majumba mazuri they dont care.
Imagine utajili tuliouweka nje ungekuwa pale town Bk ingekuwaje?
Elimu imetuharibu.
Ndio maana mchaga ambae hana elimu ya mzungu akibahatisha town anainvest kwao.
Now Moshi pana heshima sio only ya mashule bali pia uwekezaji ukilinganisha na sisi ambao tunaongoza kuwa na civilized elimu ya mzungu.
Ningeshauli ipite kwanza elimu ya kujua uthamini wa nyumbani kwanza
 
NAPAZA SAUTI!!

Naomba sauti hii iwafikie wajeolojia waliokuja mkoani kufatilia tetemeko la ardhi lakini pia Wakala wa Jeolojia TZ.

Ziwa victoria kwa muda mrefu sasa limekua likisogea nchi kavu taratibu na kufikia kumega sehemu kubwa ya nchi kavu. Hali hii si salama kwa maana kuna majengo yamekwisha ondoshwa na maji na mengine si salama kwa kuishi hasa yaliyoko pembezoni mwa ziwa.

Hali hii inashuhudiwa katika picha zifuatazo zilizopigwa eneo la Spice Beach na eneo la wazi kati ya Spice Beach na Bukoba Cooperative Hotel zamani Yasira.

Tungependa kujua inakadiriwa maji yatafikia sehemu gani ya mji, kwa muda gani na tahadhari zinazoweza kuchukuliwa kabla ya hali ya hatari kujitokeza. Kwasababu kuna uwekezaji na miradi mbali mbali inaendelea ndani ya mji ni vyema taarifa na elimu juu ya hiki kinachotokea kutolewa mapema na kuhakikisha zinawafikia watu wengi zaidi kama si wote

53ce36751ab3a71463a48e30acfc56bc.jpg
a3e3a382b0be90054c9680807352a29f.jpg
a8f4ee22aaa685409b1d65f73a172f6f.jpg
IMG

b7db00fb766bd999ec3353bbeb3d89ae.jpg
 
UTATU ULIOBARIKIWA!!

239e2e8424632a72e1c9f114bb0fccbd.jpg
ab20a3778b1ce7e52bd3a6cddcb62a57.jpg
6ab4ff38012e4f47dee090c139464a69.jpg


Ndugu Alex ambaye ni katibu wa mbunge, Bi Rahel ambaye ni mchumi wa BMC na afisa habari wa JF-Tushirikishane (mpiga picha) katika kikao kidogo cha kupitia mpango-kazi wa Tushirikishane Bukoba. Kikao hiki kilifanyika juzi tar 14-10-2016

Utekelezaji wa Mradi wa Tushirikishane unahusisha taasisi tatu ambazo ni Jamiiforums, Mbunge na Bukoba Manispaa.

Vipaumbele vyetu ni;

1. Ujenzi wa Soko Kuu, Soko la Kashai na Stand kuu ya Mabasi

2. Urasimishaji Makazi

3. Mikopo kwa Vijana na kina Mama, na

4. Bima ya Afya

Vipaumbele hivi ndivyo tutakua tukijadili zaidi na kutoa ripoti ya hatua zinazofikiwa kila wiki na ripoti ya jumla kwa kila mwezi na hatimaye ripoti ya mwisho ya mradi.

Usiache kufatilia


Bwana atuwezeshe[emoji120]
 
RASILIMALI MFU KATIKATI YA MJI WA BUKOBA (CBD)

95c74c1292f08048524861cb2c4030f4.jpg
8a50a70fadadb73dc0a6780dd009c285.jpg
eabac2a2bf563cc8f32c634bed024ca2.jpg


Haya ni majengo ya kihistoria (monuments) yanayoelezea historia ya mji wa Bukoba. Majengo haya yana hadhi sana na mejengo mengine ya kihistoria kama yaliyoko Stone Town, Bagamoyo, Kilwa na kwingineko. Pamoja na kuwa majengo haya ni muhimu kihistoria lakini pia ni vivutio vya kitalii na kitafiti. Majengo haya yanapaswa kuwa chini ya idara ya Antiquity-Wizara ya Maliasili na utalii, yanapaswa kutunzwa, kurekebishwa bila kupoteza asili yake na pia kutangazwa ili wazawa wafahamu na pia kuvutia watalii.

Majengo haya yamepakana na ofisi ya mkuu wa mkoa na mbunge. Yapo majengo mengine ya yenye hadhi sawa na haya katika Bukoba manispaa

9621cd1c4ddc3bb15c72cc6fa4662c0c.jpg
ee83c74de0437294935e0b34bb89a3d4.jpg
8f4fe666cded8ae98aef992cef5927d1.jpg
efe2ec73141461712334a8468cd4ab6a.jpg

cf3e553e255d15ed0818c216ec738e06.jpg
af37cd0247422a1c1e6f84a85b261b89.jpg


Jengo hili ambalo linamilikiwa na CCM pia ni rasilimali mfu. Jengo hili linatumika kama tuition center[emoji85] kama shughuli yake maalum. Nalo limepakana na ofisi ya mkuu wa mkoa
 
UKARABATI

a62b266a31f15b2b42181105dc3038d6.jpg
14243b0ebd8e2061638f9d1d732e57b4.jpg
d2e9d7d4cc9e3d80a114e7b6584edea0.jpg
cd00165af260092fc081d74361061917.jpg


Ukarabati wa barabara ya Kastamu, eneo la Kasarani ukiendelea. Barabara hii iliathiriwa na tetemeko la ardhi lililotokea tarehe 10 September. Ukarabati huu ni moja kati ya jitihada za serikali kuhakikisha miundombinu na taasisi za umma zilizoathiriwa na tetemeko la ardhi zinarejea katika matumizi yake ya awali
 
HISTORIA

Hili ndilo jengo lililopata umaarufu sana kuliko majengo yote ya mkoa wa Kagera. Jengo hili linafahamika kwa jina na "Duka kubwa". Duka kubwa ni jengo la kwanza la kisasa katika mkoa wa Kagera ambalo lilijengwa na wajerumani. Jengo hili lilikua likitumika kama supermarket.

Kanisa la Bunena ndilo lilikua la kwanza kujengwa huku Duka Kubwa likifuata. Duka Kubwa lilikamilika ujenzi wake kabla ya kanisa la Bunena hivyo kuwa jengo la kwanza la kisasa mkoani Kagera.

ab441e245e78b37d7e13689b1952f94d.jpg
d1e5d499953e34772bf53e2d6f66738f.jpg
 
HISTORIA

Anaandika mzee Ramadhan Kingi

Baada ya Mwalimi J.K. Nyerere kufika Bukoba 1957, Watawala waingereza walihakikisha hakuna nyumba yoyote ya Wageni kumpokea ama kumpa nafasi ya kulala. Wenyeji wake walikwishaijua hii harakati.
Mzee Sued Kagasheki aliamua Mwalimu afikie kwake mjini mtaa wa Uhuru. Wazungu wakalifahamu hilo. Mzee Sued alikwishapanga plan b Mzee Sued aliiweka siri hiyo moyoni. Ilipofika saa Sued alimhamishia nyumba yake ya Rwamishenye na Mwalimu akaweza kupumzika raha mustarehe

da967d4add3152852089ecd8f49b9e00.jpg
ce485d730cf42b2810516ded5a240696.jpg


Maoni;
Nyumba hii inapaswa kutunzwa na kuwèkwa kwenye kumbukumbu ya kihistoria kama zilivyo nyumba nyingine ambazo alifiki/aliishi Baba wa Taifa kwaajili ya vizazi vijavyo
 
Tumuombe mbunge wetu awasiliane na Twaha Taslima kuhusu uhuwishaji wa bandari ya Kemondo katika kusafirisha mizigo kuanzia Kemondo
Reli ya Kati( standard gauge iwe mpaka Mwanza halafu meli ya MV. Umoja isafirishe hadi Kemondo!
Reli kwenda Kigali na Burundi na mizigo kwenda kwa Barbara hadi ya Uganda.Haya ndio mapendekezo ya EAC ya 1977
 
Isaka ni ghali kwani uwezo wa meli ya mizigo ni konteina za futi 40 Umoja ilikuwa ni kontena 40. Semi trela moja hubeba kontena moja. Pia kwa maji bukoba hadi port bell Uganda ni karibu ukitokea kemondo.Pia Kisumu ni karibu ukitokea bukoba kuliko kutokea Mz. Isaka ni bandari ya nchi kavu ambayo iko pale kwa maslahi ya watu binafsi.
 
KUMBUKUMBU YA MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU BUKOBA

Mwaka 1966 Bukoba kulikuwa na timu iliitwa "Bulwark" ilianzishwa na Sheikh Fadhil na mmoja wa wachezaji wake mahiri ni Alhaj Profesa Issa Kaboko Musoke! Makao Makuu ya timu hiyo ni mkabala name TTCL kwa Al almarhum Juma Mwanandege.

Timu nyingine maarufu ilikua ni Balimi miaka ya 1970. Timu hii ilifanya vizuri, iliweza kuunganisha vijana wengi na baadhi ya wachezaji waliweza kushika nyazifa mbali mbali za kiutawala baadae

be6648033df32f3c18f668ecb92a4409.jpg
1544def339889968979f858014c9ac5f.jpg


Picha inayofuata[emoji116] ilikua ni mechi kati ya Balimi na Simba. Wageni wa heshima walikua ni Marehemu Mzee Juma Suedi na Marehemu Meya wa mji Mzee Rugusha. Marehemu Juma Suedi alikua Mwenyekiti wa FAT Kagera.
Katika mechi hiyo Simba walilazwa goli moja kwa sifuri uwanja wa Kaitaba kwa shuti kali kutoka mguuni mwa Adallah.

c6856c06bd2b364cf0d92633c97f5954.jpg


Baadhi ya wachezaji wa Balimi ni Kayumbe, Burchard, Adallah, Goalkeeper na 11, Mar. Abubakar Kulewa, Juma Mhina, Mkuya, Juma Kikwemu, Abdulgaddy, Alhaj Sheikh Haruna Kichwabuta (Sheikh wa Mkoa-Kiongozi), Ishebo, Coach Catanasio,
Ramadhani Kingi, Alhaj Dr. Abdallah Mporokosh, Morris Mapalala, Leopold "Tasso" Mukebezi Saleh Jordan Moyo, Elias Robert, Mar.Kasabo na Salum Mawingo.

Wengine ni Mar. Nurdin, Mikidadi, Masoud Said el-Khusaiby, Mutimba, Boniphace, Lubega ama Kato, Godfrey, Mar. Juma Manyara, Ruhinda, Hussein Kingi, simkumbuki jina, linesman Mar. Mzee Sudi Brandes Badru Nsubuga, Alhaj Juma Suedi Kagasheki, Nuru Suedi Kagasheki, kyebijuna, George Kyangenyenka, Paul Tosi, Tadeo, cyprian, Shariff na Libenti Oyogya.

Source: Mzee Ramadhan Kingi
 
Hivi ndivyo jinsi majengo ya Soko Kuu yatakavyofanana juu ya ardhi

368a6f7e09e045c0b66a1781bd3204ff.jpg


Ujenzi wa Soko Kuu ni kipaumbele namba moja katika mradi wa Tushirikishane. Hii inatikana na ukweli kwamba katika vitu ambavyo wanaBukoba wanahamu sana ya kuona vikifanyika ni ujenzi wa Soko
 
43f9ced2122e54f8b468a85c37701093.jpg


Huo[emoji115] ni mwonekano wa ndani wa stand mpya ya mabasi itakayojengwa eneo la Kyakailabwa.

ae4910968890d20bd049c6de3108670d.jpg


[emoji115] Mwonekano wa nje wa stand mpya ya mabasi ya kyakailabwa
 
  • Thanks
Reactions: MC7
Ujenzi wa stend ukikamilika itakuwa vizuri sana kwa kukuza utalii maana sasa watalii wengi wanaokuja kwa bus wakifika stend ya Bukoba wanashangaa ilivyo na mvua ikinyesha hali inakuwa mbaya.
Mkoa WA Kagera umejaliwa kuwa na vivutio vingi sana vya utalii tembelea website ya www.kageratourism.com kujionea.

KAGERA TOURISM | Home
 
Back
Top Bottom