Mkataba (MoU) kati ya Serikali na Kanisa Katoliki na Taasisi nyingine za Kidini

Mkataba (MoU) kati ya Serikali na Kanisa Katoliki na Taasisi nyingine za Kidini

Mimi nilichogundua ni kuwa CDM na CCT/TEC ni faces of the same coin! Hushangai wapambanaji wa CHADEMA ndio hawa wanaopigania MOU!
Mimi nalijua hili swala siku nyingi hiki chama ni cha kikristo waislamu hawaamini hawajamaa ni double face
 
Tusiende huko ( Hospital, Mashuleni ) kwanini Wakati kodi zetu zina enda huko? Tumieni michango yenu ya kanisani kuudumia shule, hospital zenu alafu muone kama kuna muislam atakae kanyaga

Una maana serikali ikirudisha hizo huduma zote kwa makanisa na makanisa yakaamua kutoa huduma kwa wikristo tu nyie waislamu mtakuwa na uafadhali wowote?

your dead my friend, nyinyi shukruni hali iliyopo inawasidia sana
 
You need to go back and re-read what I have written and then do think afresh before coming back.

Just to help you, that you may think properly; do consideration of what you have written and underlined against what I had elaborated.

Mwisho wako wa maelezo ndio hapo na ni kauli ya kiungwana kwa vile muungwana akivuliwa nguo huchutama.
Ukishindwa kunielewa basi.



Katika MoU, serikali ya JMT inakubaliana na makanisa mambo mawili makubwa ya kifisadi dhidi ya waumini wengine wa Tanzania:

1) Kutoa nafasi za upendeleo kwenye vyuo vya serikali vya ualimu kwa ajili ya kufundisha walimu watakao kwenda kufundishwa shule za kanisa. Kumbuka nafasi hizo ni over and above zile ambazo wakristo huzipata kwa merits. Halafu utegemee waislamu wawe juu kielimu?

2) Serikali ilijicommit kuingiza maombi maalumu kusaida kanisa kupata misaada kutoka nje ya nchi. Hivi hata kama mimi leo hii ukinipa huo uwezo nitashindwa kuanzisha chuo kikuu?

Ombi kwa wale wabunge mashuhuri wa kupeleka hoja binafsi bungeni:

Tunataka MoU ijadiliwe na bunge na kupata maoni ya wabunge tuliowachagua kama kweli MoU inasimama katika misingi ya haki.

Cc: Zitto, Halima Mdee, John Mnyika, Tundu Lissu

Ritz utanisaidia kuwa copy wabunge a CCM ambao wako JF ili wapate message za wapiga kura wao.
 
Mimi nilichogundua ni kuwa CDM na CCT/TEC ni faces of the same coin! Hushangai wapambanaji wa CHADEMA ndio hawa wanaopigania MOU!

Umewasoma mkuu? Ndio maana wako hukohuko kaskazini2 huku cidadi hawampati mtu, maana tumeshtuka kuwa wana tumiwa na kanisa
 
Umewasoma mkuu? Ndio maana wako hukohuko kaskazini2 huku cidadi hawampati mtu, maana tumeshtuka kuwa wana tumiwa na kanisa

Na hapa ndipo mpaka kesho mimi siwezi kuunga mkono DR Slaa awe rais wa Tanzania. Kama ameshindwa hata kuwa fair na kutoa hata ushauri wa kuwasikiliza waislamu, do you think akiwa rais si wanaweza wakasaign MoU ndani ya mioyo yao? Yaani za siri ambazo hazionekani?
 
Dr Slaa bora angekaa kimya huyu ndiyo anategemea kugombea urais kupitia chama chao cha Chadema anaeleza suala la MoU kwa maslahi ya Kanisa.
 
wewe huna akili kabisa MOU imeisoma vizuri? pesa inatoka serikali ya ujerumani unyonyesha ni wapi serikali yetu ya tanzania ilikubali kutoa pesa.

Kusema tu kuwa hana akili kwa vile anatetea haki yake hakusaidii. Mimi nimeisoma MoU vizuri na kama unaweza jibu haya maswali hapa chini yanayotoana na MoU:

quote_icon.png
By Freshthinking

Ufisadi wa MoU uko hapa ambapo DR Slaa nasikitika hakuweza kutuelezea kwa undani:

‘The government shall provide vacancies in its Teachers training colleges for training qualified persons as teachers earmarked for church owned schools'. Article xi


‘The government shall endeavour to include financial assistance for church run social services in its bilateral negotiations particularly with the Federal Government of Germany. Consideration shall be made during its bilateral negotiations with other donors'. Article xiii.


Sasa wakristo tujadiliane kwa hoja:


1)
Hivi ni haki kwa serikali isiyokuwa na dini kutowa nafasi za upendeleo kwenye elimu kama artcle xi inavyosema, tena isitoshe kw manufaa ya kanisa?

2)
Ni haki kwa serikali isiyokuwa na dini kuombea kanisa misaada katika Nyanja za kimataifa.

Sasa hapa ni kipi mnahitaji kuoneshwa ili muamini kwamba serikali inawazunguka waislam?
 
hapo kwenye red kuna mjadala ama fedha zote zinatoka kwa wahisani au serikali pia inatoa. Sina jibu ni swali tu. Kama serikali inatoa basi pia tunahitaji kuwa na taarifa za kina kwa kiasi gani na kama haitoi tunahitaji kujua.

Ni kitu gani kimezuia taasisi zingine za dini kupata?

je kuna mkono wa kanisa kuzuia hilo?

Je, kuna mkono wa waislamu kujizuia kupata?

je kuna haja ya kuwepo MOU katika mazingira ya malalamiko ya sasa hasa kama serikali inahusika?

1. Ungesoma kwanza hiyo Memorandam of Understandind,ukaielewa au ukaomba ueleweshwe zaidi sehemu ambazo hujazielewa.naona unauliza maswali ambayo majibu yake yapo kwenye hiyo Memorandam na thank God Dr. Slaa akaelezea zaidi kwa ufasaha

2. Kumbuka sio kanisa lilioomba MOU but serikali baada ya kushindwa kutimiza wajibu wake kwa wananchi

3. Kama umeelewa malengo ya MOU na kama una akili timamu huwezi kuhoji uwepo wa MOU au kushindwa kuelewa madhara yatakayotokea kwa kutokuwepo MOU

4. Raisi ameshawaambia MOU is free to anyone ndomana hata Bakwata walikuwepo kwenye mazungumzo ya awali lakini inaonekana hawakuwa na on going projects at that time ambazo zingeingizwa kwenye MOU. For the time being waislam mna projects nyingi ambazo mnaweza kujipanga vizuri na kuingia makubaliano na serikali na wadhamini wenu mkaziingiza kwenye MOU
 
Mkuu inawezekana unalolisema ni kweli, labda walitaka mashirika ya kikatoliki yawasidie maana huko kwenye mashirika yao wanasaidiana namna ya kujilipua au kuutokomeza ukristu. Wanasahua kuwa kumwondoa anayeshikilia njia kuu za uchumi au huduma za kijamii ni ngumu. Kwa mfano leo hii ukiwaambia wakristu wafunge hospitali zao zote nchini, patachimbika. Hadi hao wanaouchukia ukristu wataathirika. Kwenye mashule na vyuo hayohayo

ni chuki zao tu kwa wakristo hakuna la ziada,mioyo yao inaumia sana inapoona wakristo wapo juu,wanatamani na wao abruptly wawe juu bila kuelewa kuwa maendeleo ni gradual process,wakristo wamefikia hapo walipo baada ya longterm investment and not otherwise,wafanye nao investment in the long run vizazi vyao vijavyo vitawashukuru kwa jitihada zao vinginevyo wao watakua ni watu wa kulia lia tu muda wote na kutaka waonewe huruma,mwisho kabisa wasikilize wimbo wa marehemu SHARO MILIONEA-CHUKI NI BURE
 
Ufafanuzi umeeleweka,hata hivo yapo mengine mengi tuh yaliyojificha,tokea enz hizo za nyerere,hatutaki kuipelka nchi yetu katika mgawanyiko wa kidini na kikabila,ni wazi matamko kama hayo yapo kwenye kujenga zaid,kwanini nyerere alikuwa anawabana sana waism wasijiunge kwenye oic na jumuiya zingne zilizokawa zina nia njema kawa hizi za ujerumani?kipi kilijificha katika hilo?na hali tunfaham zipo nje zingine ambazo hazina mrengo wowote wa mfumo wa uongozi wa imani na zimejiunga na jumuiya hiyo??please katika hilo kejeli zisiwepo bali hoja ziwekwe wazi,waislam tunatambua uhalisia katik hilo pamoja na upotoshaji wa serikali,ila tunatambua haya yote hata kabla ya ufanunuzi huu wa dr slaa,ukweli tunaujua,na tutaupigania.
 
Leo Yeriko sijakuelewa kama ndiyo yule ambaye hapa siku zote naona unaelewa haraka, sijajua. Kwa mtazamo wangu, "the good interpretation of any idea comes from the thinker himself". Dr. Slaa anapaswa awe ndio msemaji anayeelewa vizuri kuliko sisi tuliokuwa tunafikiri tu, ila yeye alishiriki mchakato. Naona amefanya vizuri kutufafanunulia. Kwa sasa hatutajadili kitu hiki kama siri, na mimi namshukuru aliyetuletea copy, tuweke copy hii siku ukija mjadala, tusianze kusema sijawahi kuona MoU ikoje.

Yeriko leo kapiga viroba dini yake na chama chake ndio zao
 
Katika MoU, serikali ya JMT inakubaliana na makanisa mambo mawili makubwa ya kifisadi dhidi ya waumini wengine wa Tanzania:

1) Kutoa nafasi za upendeleo kwenye vyuo vya serikali vya ualimu kwa ajili ya kufundisha walimu watakao kwenda kufundishwa shule za kanisa. Kumbuka nafasi hizo ni over and above zile ambazo wakristo huzipata kwa merits. Halafu utegemee waislamu wawe juu kielimu?

2) Serikali ilijicommit kuingiza maombi maalumu kusaida kanisa kupata misaada kutoka nje ya nchi. Hivi hata kama mimi leo hii ukinipa huo uwezo nitashindwa kuanzisha chuo kikuu?

Ombi kwa wale wabunge mashuhuri wa kupeleka hoja binafsi bungeni:

Tunataka MoU ijadiliwe na bunge na kupata maoni ya wabunge tuliowachagua kama kweli MoU inasimama katika misingi ya haki.

Cc: Zitto, Halima Mdee, John Mnyika, Tundu Lissu

Ritz utanisaidia kuwa copy wabunge a CCM ambao wako JF ili wapate message za wapiga kura wao.

Freshthinking naomba tuwekana sawa katika hili
1. Hizo nafasi za upendeleo unazozirudia rudia sana ni zipi? - Kutoa nafasi za kufundisha walimu watakaohudumu katika taasisi zinazoendeshwa na makanisa ndicho kinachozungumzwa kwenye MoU. Wakati huo hakukuwa na vyuo vya binafsi vya kufundisha walimu isipokuwa TTC za serikali. Kipengele hiki kinasema serikali itoe nafasi kwa watu watakaofundisha katika taasisi za makanisa. Sioni tatizo hapo, tafuta kipengele chengine.
2. Maombi ya misaada - Kumbuka hapa serikali ndo ilikuwa inayataka makanisa yaisaidie kuziendesha shule na hospitali ambazo walizitaifisha halafu wakashindwa kuziendesha. Makanisa yalikuwa na uwezo wa kupata misaada kutoka kwa taasisi za kutoa misaada za makanisa kutoka nchi zilizoendelea. Lakini na wao wakaishauri na serikali kwa upande wake nayo itafute misaada. Kosa lipo wapi?

Nasikitika kweli kwenye mijadala kama hii tunapotezeana muda sana tukirudia rudia vitu visivyo na tija. Nakubali kuwa ni kweli wengi wa wanaojaribu kujibu hawajibu hoja bali huonesha dharau na ufedhuli, kitu kinachokera na kuwafanya wale wanaouliza maswali kukataa majibu hata yale yenye mantiki kwa sababu majibu hayo yameshehenezwa kejeli na dharau kibao.

Vile vile ufafanuzi huu umechelewa mno. Mjadala huu umeanza siku nyingi sana hadi unavuta watu wengi ambao unadhani wangekuwa wanaelewa. Tatizo ni kuwa wale wanaoelewa kutokea mwanzoni hukaa kimya; mara nyingi kwa kudharau tu na kuyaita haya ni mambo madogo tu yataisha. Serikali walikuwa na uwezo wa kufafanua vizuri jambo hili, hawakufanya hivyo. Hata Dr. Slaa hakuuleta ufafanuzi huu wakati mjadala huu uliposhika kasi - alikaa kimya. Sababu kubwa kwa pande zote ni maslahi ya kisiasa lakini wanaoumia ni umma wa wananchi wasioelewa.

Sasa hivi hatuna kiongozi wa aina ya Nyerere aliyekuwa na uwezo wa kuelezea jambo hadi likaeleweka. Wengi wetu tunaamini kuwa watu wanaelewa, maswali madogo madogo tunayadharau, kumbe ndo tunabomoa nchi.

Wanaojibu kwa kuwakejeli waislamu wanaohoji, wanachochea chuki tu ..... halafu waislam wakikasirika wanaanza kulalama. Kejeli na dharau ndo chanzo cha chuki na migogoro yote!! Mnaojiita wakristo humu ndani kwa nini msioneshe ustahimilivu na heshima kwa wenzenu waislamu? Naomba mtafakari kisha mchukue hatua.
 
Sasa waje hapa akina Sadeeq na wote wale waliokuwa wanapotosha MOU kuwa matokeo ya mfumokristo na uonevu wa serikali kwa Waislamu. Njooni hapa tuwasikie na upotoshaji wenu.

Nisaidieni kufahamu zaidi, hii safari ya negotiation (makubaliano) baina ya serikali na taasisi za kidini, naona ilianza na dini zote, lakini baadaye MOU imebaki kati ya taasisi za kikristo na serikali, ili hali taasisi za kiislamu hazionekani? au walijitoa? ama hawakuwa na kitu kilichotaifishwa sasa ikabidi wasihusishwe?
 
Slaa kasema vizuri tu,msingi wa mou ndio huo waislam wenzangu,masheikh waache sasa hii habari jambo la msingi walilopaswa kulivalia njuga ni urejeshwaji wa mahakama ya kadhi ambayo mkapa aliwaahidi waislam akiwa mwenyekiti wa ccm na kuonyesha msisitizo kwamba jemedari mkapa alipania kutupatia waislam kadhi kama alivyopigana kiume licha ya upinzani mkali wa kanisa kuhakikisha chuo kikuu cha kiislam kinaanzishwa ndani ya utawala wake,tatizo la utekelezaji wa uanzishwaji wa mahakama ya kadhi lilianza kulegalega walipoingia madarakani kikwete na lowassa angekuwepo mkapa muda huu mahakama ingekua ilishaanza muda mrefu,masheikh muulizeni kikwete kwanini aliiondoa kabisa kwenye ilani issue ya mahakama ya kadhi?????????pengine tuanzie hapo,mjadala wa mou umefungwa rasmi sababu ni wa kitoto

We, ni muislam baridi kabisa, ninashaka na uisla wako, hivi unakwendaga masjid
 
Dr Slaa bora angekaa kimya huyu ndiyo anategemea kugombea urais kupitia chama chao cha Chadema anaeleza suala la MoU kwa maslahi ya Kanisa.
kwanini usiwe muwazi tu na kusema unaichukia dini yake? serikali ya ccm iliyosimamia haya yote na rais wako kikwete aliyeitetea mou mbele ya umma wa waislamu naye unamsemaje? anatetea maslahi ya kanisa? akili fupi mpaka inatia kinyaa...
 
Kusema tu kuwa hana akili kwa vile anatetea haki yake hakusaidii. Mimi nimeisoma MoU vizuri na kama unaweza jibu haya maswali hapa chini yanayotoana na MoU:

quote_icon.png
By Freshthinking

Ufisadi wa MoU uko hapa ambapo DR Slaa nasikitika hakuweza kutuelezea kwa undani:

‘The government shall provide vacancies in its Teachers training colleges for training qualified persons as teachers earmarked for church owned schools’. Article xi


‘The government shall endeavour to include financial assistance for church run social services in its bilateral negotiations particularly with the Federal Government of Germany. Consideration shall be made during its bilateral negotiations with other donors’. Article xiii.


Sasa wakristo tujadiliane kwa hoja:


1)
Hivi ni haki kwa serikali isiyokuwa na dini kutowa nafasi za upendeleo kwenye elimu kama artcle xi inavyosema, tena isitoshe kw manufaa ya kanisa?

2)
Ni haki kwa serikali isiyokuwa na dini kuombea kanisa misaada katika Nyanja za kimataifa.

Sasa hapa ni kipi mnahitaji kuoneshwa ili muamini kwamba serikali inawazunguka waislam?
Mkuu mbona hili swala mkuu lynxeffect22 na wengine humu wamekujibu lakini hutaki kuelewa au unataka majibu yatakayo kupendeza unatatizo kubwa sana la udini
 
Last edited by a moderator:
My take: "Tukumbuke kubomoa ni kazi nyepesi sana, sekunde lakini kujenga tena inachukua muda mrefu na ni kazi ngumu, na wakati mwingine hata ukifanikiwa huwezi kujenga kama ilivyokuwa."

Bola tubomowe kuliko kuendelea na ujinga huu, uliop sasa
 
Nisaidieni kufahamu zaidi, hii safari ya negotiation (makubaliano) baina ya serikali na taasisi za kidini, naona ilianza na dini zote, lakini baadaye MOU imebaki kati ya taasisi za kikristo na serikali, ili hali taasisi za kiislamu hazionekani? au walijitoa? ama hawakuwa na kitu kilichotaifishwa sasa ikabidi wasihusishwe?

Kutokana na maelezo ya Dr Slaa, inaonekana Bakwata walikuwepo mwanzoni; ila mambo yaliyokuwa yanajadiliwa yakawa hayawahusu. Maanake hapo suala ilikuwa ni kuhudumia taasisi zilizotaifishwa na serikali. Watoa misaada wakawa hawapendi tabia ya serikali kubinafsisha taasisi kiholela halafu inazitelekeza. Sasa wakaweka masharti lengo ikiwa ni kuzuia utaifishaji huu holela na utelekezaji ili huduma ziendelee. Sasa hapa ukiangalia nahisi Bakwata hawakuwa na interrest katika mambo haya - si kwa sababu hawakutaka, bali majadiliano yenyewe hayakuwahusu sana.
 
Naomba nijibu kipengele cha pili:


The government shall provide vacancies in its Teachers training colleges for training qualified persons as teachers earmarked for church owned schools. Article xi

Hapo nilipopigia mstari ni walimu makhsusi kwa ajili ya shule za kanisa.

Mkataba huo kwa sasa una miaka takriban 22, ni upi ukomo wake? Kama hivyo ndivyo kuna ajabu gani kwamba shule za serikali hazifanyi vizuri bali ni shule za kanisa? Huu ni ufisadi ambao hauwezi kumalizwa JF bali viongozi wa dini ya kiislamu, kanisa na serikali kukaa na kujadiliana. Kinyume chake ni maafa twendako.

Fresh,
Ukifuatilia majibu ya Mnyamahodzo na wengine utaona maswali yako 2 yamejibiwa kwa kina ila inaonekana sio majibu uliyoyataka.

Naomba nikufahamishe hivi ya kuwa ktk mikataba kuna vitu vingi vya msingi mbali na maandishi na saini ambavyo kwa pamoja huusababisha mkatana kutekelezeka na kueleweka. Moja ya kanuni za kutafsiri sheria na mikataba zinalazimisha kuheshimiwa kwa kanuni ya "Rule of Context". Huwezi kuchagua/kuchomoa sentensi fulani kisha ukaitoa nje ya muktadha na kuipa tafsiri au kutaka ipewe tafsiri kinyume na mwili wa mkataba.

Nijibu swali lako la pili, kama ulivyosisitiza hapo juu kwa kupigia mstari. Nitaenda kwa urefu kidogo.

Kanisa lilikuwa linakubaliana na serikali ya Tanzania kuhusu namna ya kutoa huduma zilizotajwa na kujadiliwa kwa kina huko juu/nyuma. Kanisa kwa vile lina utaratibu wa kutoa huduma bora likasisitiza kuwa ubora walimu watakofundisha shule (zitakazoendeshwa na kanisa) lazima uheshimiwe na kutambuliwa. Hivyo wakaleta hoja mezani kuwa serikali itoe nafasi (wewe unasoma upendeleo) kwa walimu wenye sifa kupata mafunzo.

Wewe ulitaka kuwe na kitu kama hiki'....earmarked for state (or) muslim owned schools' ndipo hisia zako zingetulia kidogo, sio?
Well, sasa kama Kanisa lingesema hiyo sentensi (nadhani ambayo wewe ulitaka iwe) je hiyo MOU ingekuwa ni baina/kati ya Serikali vs nani? i.e. offer and receivership. Kuwepo kwa hicho kipengele ktk MOU kunalazimisha kutambulika kuwa wakishahitimu wataenda wapi.

Kwa mfano Kanisa lingesema Serikali itoe mafunzo halafu lisiseme wakifuzu wataenda wapi, Serikali huenda ingekataa maana haikuwa na fedha za kutoa huduma mama husika sembuse kufikiria kutoa ajira mpya, kwani haikuwa na uwezo wa kifedha wakati. Kanisa liliweka bayana kuwa litateua watu wenye sifa na kisha litawapokea na kuwapangia kazi (ajira). Kanisa halikusema litapeleka watu wa dhehebu fulani tu, bali wenye sifa/uwezo ndio kigezo! Na hao wahitimu hawekuwa wanakwenda kufanya kazi kanisani bali mashuleni, hivyo dhana ya Kanisa kufaidika kama Kanisa ni dhaifu mno

Na kama hoja hiyo inakuumiza na kukuchefua hebu jiulize ni vipi leo inakuwa maelfu ya walimu wanahitimu kila mwaka ..... je ni % wanaopata ajira, hasa serikalini? Nadhani unaona bayana kuwa hoja yako inaelea hewani na kupotelea huko!


Kwa hivyo in context, ni kuwa Kanisa liliitaka Serikali iheshimu na kuwajibika kimkataba juu hoja muhimu ya ubora wa walimu kama sehemu ya utekelezaji wa MOU nzima. Jitahidi usisome zaidi ya kilichoandikwa.
 
kwanini usiwe muwazi tu na kusema unaichukia dini yake? serikali ya ccm iliyosimamia haya yote na rais wako kikwete aliyeitetea mou mbele ya umma wa waislamu naye unamsemaje? anatetea maslahi ya kanisa? akili fupi mpaka inatia kinyaa...
Usiwe na akili fupi kama maisha ya funza, wewe unaupenda Uislam?
 
Back
Top Bottom