Mke hataki ndugu zako, utafanyaje?

Mke hataki ndugu zako, utafanyaje?

- Mke sio ndugu yako.

- Life partiner ni mtu mnaesaidiana katika maisha, yaani shida zako azione kama zake na zake uzione kama zako.

- Mke asiyeelewa shida zako tayari amesha jiondolea kigezo cha kua life partiner wako.

- Hakuna reward kwa mtu mbinafsi, na kama ukimruhusu mke apite iyo njia basi madhara yake yatakuathiri wewe mwenyewe au hata watoto wako pia.
 
Kwenu wakuu,
Kwa muda mchache nimepata ushauri wa kutosha kazi iliyobaki ni kufikisha ujumbe.

Kuna majibu ya aina tatu hapa:
1. Kuna ambao wanakubaliana na maamuzi ya mwanamke, mtoto aondoke
2. Kuna ambao wanapinga tabia ya mwanamke, bora mwanamke aondoke.
3. Kundi la mwisho wanachukizwa na tabia ya mwanamke lakini wanashauri mtoto aondoke kuepusha ugomvi.

Binafsi naungana na kundi la pili, mwanamke asepe. Kuna sababu ya msingi kwa mfano aliotoa scolastika

Ukichunguza kwa umakini hapa mwanamke ana roho mbaya tu Hana sababu yoyote ya msingi. Kama alivyosema scolastika leo kafanyiwa mtoto kesho akimfanyia mzazi wako?!

Naenda kufunguka kwa jamaa akiona ushauri unamfaa auchukue akiona haufai auwache
Ukichangia mwanamke aondoke wewe ndo unaenda kuishi kwenye familia ya jamaa yako upike na utimize majukumu yote? Yaani mwanamke aondoke aache wanae kisa huyo mtoto?

Ndiyo kwa maelezo inaonekana mwanamke ana roho mbaya ila sisi hatujamskiliza upande wake! Usijifanye mwema mwambie rafiki yako arufishe mtoto kwao. Au mtoto aletwe kwako tuone kama mke wako hatokulaza kwenye banda la kuku.
 
- Mke sio ndugu yako.

- Life partiner ni mtu mnaesaidiana katika maisha, yaani shida zako azione kama zake na zake uzione kama zako.

- Mke asiyeelewa shida zako tayari amesha jiondolea kigezo cha kua life partiner wako.

- Hakuna reward kwa mtu mbinafsi, na kama ukimruhusu mke apite iyo njia basi madhara yake yatakuathiri wewe mwenyewe au hata watoto wako pia.
So amfukuze mke wake nyie mtaenda kulea wanae? Mnajifanya wema amfukuze mke wake nyinyi mko na wake zenu mmewakumbatia yeye aanze kulala bar.

Usitowe hukumu bila kusikiliza upande wa pili.
Mimi sina roho mbaya sitoweza kuwa na shida na ndugu wa mme ila ndugu zangu hawawezi kuja kuishi kwangu, niko tiyari kumsaidua akiwa huko huko ila sio kuja kwangu kuishi spendi maneno ya ndugu.

Mwanaume akipenda alete ukoo mzima kwake waishi ila ndugu zangu nooooo waje watembee warudi nyumbani.
 
Leo naomba mumsaidie rafiki yangu kumshauri, mimi ni nimeshashauri kwa upande wangu lakini nataka kuona fikra za watu zaidi.

Jamaa ana mke na watoto, hivi karibuni kaka yake alipoteza kazi ndugu wakamuomba asaidie kulea mtoto mmoja ambaye alikuwa kidato cha pili. Jamaa alimshirikisha mke wake kuhusu mgeni huyo mke akakubali lakini inaonekana alikubali kwa shingo upande.

Kwa sasa sio siri tena mwanamke kasema wazi kabisa hataki kuishi na huyo mtoto tena akaenda mbali zaidi kampigia simu mama wa mtoto kumueleza yeye hawezi kuishi na mtoto wake. Habari zikamfikia jamaa akashangaa sana aliporudi kumlaumu mwanamke kwanini amefanya hivyo mwanamke kaja juu na kusema hata yeye ana maamuzi kwenye familia na msimamo wake ndio huo, hataki kuishi na huyo mtoto.

Jamaa kabembeleza sana mke akawa kama kaelewa kumbe bado. Hivi juzi kalianzisha tena na sasa amefika mbali kamwambia mume wake achague moja aidha kuishi na yeye(mke) ama mtoto wa ndugu yake........

Mzozo uko hapo, mimi nilimshauri kama hana uwezo wa kumlea huyo mtoto amrudishe kwao lakini si kwasababu ya kukataliwa na mke wake maana hata yeye hajui kesho yake. Jamaa alinijibu uwezo anao maana mtoto anasoma shule za serikali halipi ada hata mia zaidi ya uniform na vifaa vya shule.

Kama nimekosea naombeni sababu, bado tuna nafasi ya kumsaidia jamaa. Kwa ndugu upande wa mume na narafiki zake wanashangaa sana maamuzi ya mwanamke lakini kwa ndugu wa mke anasema zaidi ya 80% wanamsapoti mwanamke 🤔
Mimi nilishajiwekea utaratibu.. nitawasaidia ndugu wakiwa huko huko walipo biashara ya kujaza ndugu/watoto wa ndugu nyumbani kwangu ndio mwanzo wa kuharibiana michongo kila mtu akae kwake.. dunia ishakuwa mbaya nyakati hizi.
 
Ila ifikie wakati mtu kusaidiwa iwe huko aliko na si kumleta nyumbani kwako. Labda itokee wazazi wote wamefariki. Kuna shule za boarding unaweza kumpeleka mtoto na kugharamia kila kitu na likizo anaenda kwa wazazi au mzazi aliyopo.

Hii inaleta changamoto sana kwenye familia maana tunaishi kwa mipango sasa mmepanga kuwa na watoto wawili au watatu mnaletewa wengine tena.

Mimi binafsi natoa sana msaada ila huku huko uliko

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
 
Huyu ndio wa kwanza kuishi nae ila anadai aliwahi kuishi na mtoto wa ndugu wa mke sasa hivi yuko chuo. Kuhusu tabia za mtoto hakuna malalamiko hayo
Huyo mtoto arudishwe kwa wazazi wake na huyo mwanamke siku ndugu zake wakikanyaga kwake awa timue mara moja bila kupepesa macho.
 
Ila baadhi ya wanawake wana roho mbaya sana kwa ndugu wa mume daah. Hapo soon atakuja mtoto wa ndugu yake na ataona ni halali kuishi nae hapo



Sana yani [emoji24]

Halafu atashangaa mtoto wake au wanae watakavyomsumbua mpaka ajute!

Choyo tu hapo hana lolote [emoji57][emoji19]
 
Wengi mnafurahisha sana! Hii kitu ni ngumu sana. Sijaona familia iliyosaidia ndugu akaondoka (baada ya mission completed) kwa kuishukuru. Mwisho wa yote huwa ni lawama tu.

Mtoto umejizalia mwenyewe akikua anakuita mchawi. Anakuua refer case za rombo, moshi mjini na hii ya kwimba ya juzi juzi.

Hivi humu ndani mnajua maana ya ndoa nyie? Unadhani ndoa ni mbususu? Ndoa unatafuta Rafiki wa ukweli, msaidizi wakati wa shida; mtu wa kukufichia madhaifu yako, mtu wa kukufariji etc,

Ndo maana Mie namchumbia To yeye ili Watoto awapeleke kwa Depal ili gharama ziwe kwa Demi na Antonnia awe Mchepuko
 
Mkuu amua kama mwanaume kama kweli huyo mke yupo tayari kuachana na wewe sababu ya huyo mtoto mwambie mtoto lazima muishi naye kama anaondoka aondoke


Kabisa, ningekuwa ni mimi ndie huyo mume wa familia ningekaza kama noma na iwe noma [emoji123]

Aondoke kama anaondoka huyo mwanamke.

Eti sababu ya choyo ?! [emoji848]

Halafu ukute anajifanya kusali kama ni kanisani yuko mbele mbele kumbe moyoni amejaa makorokosho ya choyo na chuki.
 
kuna shemeji yangu yeye tangu mdogo baba na mama walifariki akalelewa na ndugu lakini alivyo na roho mbaya hawezi kukaa na mtu mwingine unajiuliza hivi huyu hakumbuki alivyokua ama ni nini hichi yaani huwezi kudhania kama ni yatima aliyelelewa kwa watu
Mkuu uwezi kujua kapitia manyanyaso gani hapo alipokuwa ana lelewa
 
Ukichangia mwanamke aondoke wewe ndo unaenda kuishi kwenye familia ya jamaa yako upike na utimize majukumu yote? Yaani mwanamke aondoke aache wanae kisa huyo mtoto?

Ndiyo kwa maelezo inaonekana mwanamke ana roho mbaya ila sisi hatujamskiliza upande wake! Usijifanye mwema mwambie rafiki yako arufishe mtoto kwao. Au mtoto aletwe kwako tuone kama mke wako hatokulaza kwenye banda la kuku.
Ataamua yeye sio mimi, kwangu naishi na watoto wawili wa ndugu zangu na mmoja wa mke wangu, mimi binafsi siwezi kukataa kusaidia ndugu sababu mke wangu hataki.

Niliwahi kuwa na mtoto kabla ya ndoa mwanamke alikuja kunitupia nyumbani nikiwa likizo baada ya kusikia nataka kuoa, huyo mtoto alitunzwa na mama yangu mdogo hadi nilipooa ndio nimemchukua.

Mnaposema mtoto aondoke asaidiwe akiwa huko, je kama msaada wenyewe ni malazi?!
 
Mimi binafsi niliwahi kuishi kwa ndugu sababu ya umasikini wa baba yangu na si kwa matakwa yangu nilikuwa mdogo lakini nakumbuka mengi siwezi kuruhusu mtoto wangu akaishi kwa ndugu kamwe ila tu kwa kulazimishwa na hali ikiwemo kifo.
Mkuu sababu ulizozitaja kukusababisha wewe kuishi kwa ndugu, ndiyo hizo hizo hufanya watoto wengine kulelewa na ndugu.

Katika kulea kijana, kina mama wengi ni katili sana katika malezi hadi unashangaa.

Muda wa kumlea kijana huwa ni mfupi sana, maana akimaliza shule tayari mnaachana naye.

Lakini unakuta anafanyiwa matukio mpaka mtu unajiuliza faida yake ni nini!
 
Ataamua yeye sio mimi, kwangu naishi na watoto wawili wa ndugu zangu na mmoja wa mke wangu, mimi binafsi siwezi kukataa kusaidia ndugu sababu mke wangu hataki.

Niliwahi kuwa na mtoto kabla ya ndoa mwanamke alikuja kunitupia nyumbani nikiwa likizo baada ya kusikia nataka kuoa, huyo mtoto alitunzwa na mama yangu mdogo hadi nilipooa ndio nimemchukua.

Mnaposema mtoto aondoke asaidiwe akiwa huko, je kama msaada wenyewe ni malazi?!
Msaidie umpeleke kwako maana una familiya ndogo.atalala hata seblen.
 
Mkuu sababu ulizozitaja kukusababisha wewe kuishi kwa ndugu, ndiyo hizo hizo hufanya watoto wengine kulelewa na ndugu.

Katika kulea kijana, kina mama wengi ni katili sana katika malezi hadi unashangaa.

Muda wa kumlea kijana huwa ni mfupi sana, maana akimaliza shule tayari mnaachana naye.

Lakini unakuta anafanyiwa matukio mpaka mtu unajiuliza faida yake ni nini!
angekuwa anamsomesha sijui ingekuwaje
 
Mkuu sababu ulizozitaja kukusababisha wewe kuishi kwa ndugu, ndiyo hizo hizo hufanya watoto wengine kulelewa na ndugu.

Katika kulea kijana, kina mama wengi ni katili sana katika malezi hadi unashangaa.

Muda wa kumlea kijana huwa ni mfupi sana, maana akimaliza shule tayari mnaachana naye.

Lakini unakuta anafanyiwa matukio mpaka mtu unajiuliza faida yake ni nini!
sahihi kabisa mkuu, maranyingi hawa watoto hawapendi kukaa kwa watu ila hali huwasukuma na maranyingi wanawake ndio huwa vikwazo angalia hata kwa wadada wa kazi.
 
Huyo jamaa itakuwa ni yeye, eti ufukuze mke kisa unaforce ukae na ndugu ambaye wazazi wake wapo.
Sent using Jamii Forums mobile app


Hapana nazani tafsiri ya hicho alichofanya huyo mwanamke kina mapana na kina kwa mwerevu ndio maana maamuzi ya kukubali aondoke kama mwenyewe alivyoanza kutaka iwapo mtoto hataondolewa.

Hiyo ni indication tu lakini hiyo mwanamke si mtu mzuri.

Anaweza mzuru hata huyo mumewe.

Sasa Kwanini ikawe na mtu wa mashaka ?!
 
Back
Top Bottom