Mke wangu mtarajiwa hataki mtoto wake aliyempata kabla hatujakutana atumie ubini wangu

Ahaaaahaaahaaa[emoji12][emoji12][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
[emoji1732][emoji1732][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Mkuu Kwahiyo wewe kutoa msaada kwako mpaka umpe mtu mashariti ? Ni Mara ngapi tunawapa watu misaada bila kuwapa mashariti? Kiufupi huyu mleta hoja nimemuona Kama hazijatimia,(samahani kwa mleta hoja) can you imagine mwanamme na uume wako unalilia kumuita ubini wako mtoto asiye wako? Kama unataka kumsaidia wewe msaidie tu Ila Kama hutaki wewe acha ,Ila sikubaliani na hoja yako ya kulilia kumpa ubini wako mtoto ambaye si wako

Pambana upate wako umuite kwa ubini utakao
 
Kazana kumwaga ndani.... Zaa mtoto wa kwako na huyo mwanamke. Si unajua watoto wanarithi akili za mama zao. So upstairs mwanao mtarajiwa atakuwa vizuri pia.
 
Mnasema tu sababu hayajawakuta,hivi unawezaje kuishi na mtoto ambaye unatumia jina la mwingine huku wewe ukimuhudumia kila kitu??
unamhudumia kwani babake hayupo? hata mimi ningekuwa baba nitakubali mwanaume mwingine ahudumie mtoto wangu? upande wangu, enzi hizo niko misri, nilizaaga na mwanamke mmoja hivi nina mtoto naye hadi leo. huwa natuma ada nahudumia kila kitu huko huko, sasa ilifika kipindi kuna shule moja ya wazungu walikuwa wanataka kutoa msaada kusomesha watoto wasio na uwezo, hasa wale wenye wazazi wasiojiweza, ni shule nzuri mno ya english medium mkoa fulani hivi....mwanamke yule akataka kujifanya ati mimi sipo mtoto aingie kwenye kusaidia na wazungu huko ili anipunguzie majukumu. nilikinukisha balaa, mttoto wangu asaidiwe as if mimi sipo? alafu akija kuwa mzima ionekane nilimtelekeza akasomeshwa na wanadamu wengine? sikukubaliana na icho kitu.
 
ubabe usio na maana. Yaani umkute mtu na mwanae utake kujipachika kwenye kila kitu chao. Sio fair
 
Ikiwa na wewe uliwahi kuwa single maza

Basi wewe ndo mfano halisi wa single maza ambao hawana sumu mwilini wanatastahili kuolewa maneno yako haina chembe chembe ya Chuki kwa upande wowote.Moyo mwpes
Shukran mkuu
 
Jina lako la mwisho kama bakeri,yakobo ,ng’ombe .Jina ni muhimu
 
You have ego .Si wa kwako mtot
 
Umenifurahisha.... The most Beautiful Comment for this Saturday 😘
 
Misaada tunayowapa watu bila masharti ni misaada yenye scenario za kawaida sana, hata mimi hua ninawasaidia sana watu wenye uhitaji tena bila masharti yoyote lakini

Hii issue ya huyu jamaa ni sensitive sana, naona watu wanaongea tu juu juu kurahisisha mambo, kama jamaa yupo tayari kumsomesha mtoto kuna ugumu gani mtoto kutumia jina lake?
Baba mtoto si yupo hai ana umuhimu gani wa mtoto kutumia jina lake ikiwa wajibu wake unatekelezwa na mwanaume mwingine.

Kwa hiyo nyie mnaona ni vigumu mtoto kubadilisha jina kuliko utayari wa jukumu la kumsomesha alilojipa jamaa?

Kama issue ya kupata watoto wake ni suala la muda la jamaa kulitekeleza, ila ni shida hata watoto wengine wakipatikana tayari wakakuta familia ina matabaka, huyu mtoto anatumia ubini huu, wao wanatumia huu, halafu kwa dalili hizo za huyo mama mtu usikute jamaa atakatazwa hata kumcharaza mtoto bakora kisa sio wake.

Mtoa maada, badilisha jina huyo mtoto then msomeshe, kama mama mtu hataki akamwambie mwenye ubini anaoutetea alete ada.
Kwa mama mwenye uelewa na umuhimu wa elimu asingekukatalia ila hadi anakataa usikute bado anampenda baba wa huyo mtoto na pengine bado wanawasiliana na kushauriana namna ya kukuona wewe boya.
 
watoto ni zawadi.
iwe umemzaa, umemuokota, umekabidhiwa umlee ama iwe umemrithi.
Yamkini mama yake hapo awali alidanganywa ataolea ila akajikuta amezalishwa bila ya kuolewa na mwishowe akaachika akiwa na kachanga unakokalea.
Atakuwa ni mwanamke mpumbavu kurudia kosa la awali.
yaani umtie mimba bila ya ndoa tena? hakika anajiona jinsi atakavyokuwa duni.
Wewe timiza ahadi yako ya kufunga nae ndoa, kisha utona jinsi atakavyo kutotoleshea watoto.
MTENDEE WEMA PLEASE WALA USIMKIMBIE MAMA NA MTOTO.
 
HIVI, UKIMUDUMIA MTOTO WA MWENZI WAKO, UNAKUWA UMETOA MSAADA AMA UMETIMIZA WAJIBU WAKO?
Mtu umempata mwanamke mzuri mwenye mtoto. Then hautaki kumuhudumia mtoto ila kwa masharti.
Je, akikwambia umruhusu aende kwa baba wa mtoto akachukue ADA ya mtoto utaridhia?
Ukimpenda Mtu, kubaliana na Madhaifu yake na changamoto zake.
 
Achana na huyo malaya
 
Winner takes all !
Baba sio jina la ubatizo , ni jina la kubeba majukumu .
Kama baba ameshindwa kumlea mtoto wake wa kumzaa mwenyewe , automatically anakosa mandate ya kuitwa baba.
Mtoto anahaki ya kumjua baba yake mzazi, ndugu na ukoo wake.
Kumbadilisha jina la ubini na ukoo wake ulitaka kumnyima mtoto haki hiyo, ulikurupuka bro single mother yupo sahihi
 
Shida unayo wewe mkuu,uliambiwa wanajitaji ubini wako?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…