Mke wangu mtarajiwa hataki mtoto wake aliyempata kabla hatujakutana atumie ubini wangu

Mke wangu mtarajiwa hataki mtoto wake aliyempata kabla hatujakutana atumie ubini wangu

Nadhani ichi ni kibali cha kutokujihusisha na huyo mtoto kwa gharama yeyote

Natarajia ufurahie maana mtoto ana baba kwahiyo deAl na mama

Umejitakia mwenywe kujiingiza kwa hao wenye sumu
 
Wewe na singo maza wako wote mmekosea.

Tukianza na wewe ni kweli unahudumia mtoto, ila hukupaswa kubadilisha ubini bila kukaa na mwenzio mkakubaliana. ULIKOSEA KUFANYA MAAMUZI PEKE YAKO.

Tuje kwa singo maza wako, HAJIHESHIMU NA HAKUHESHIMU, ni kweli ulimkwaza na kumkosea ila ilitakiwa akwambie bila kutumia maneno makali kama "zaa wa kwako"

Kumuacha inawezekana ni sahihi au sio sahihi, hayo majibu yake yanatia mashaka.

Kusomesha mtoto na kufanya kila kitu, FANYA KAMA UNAMLEA YATIMA NA USITARAJIE LOLOTE, UKISHINDWA KUFANYA HIVYO NI BORA UACHE KABISA MAANA UTAUMIA ZAIDI YA HAPO.

Ni mimi singo maza mstaafu.

Ikiwa na wewe uliwahi kuwa single maza

Basi wewe ndo mfano halisi wa single maza ambao hawana sumu mwilini wanatastahili kuolewa maneno yako haina chembe chembe ya Chuki kwa upande wowote.Moyo mwpes
 
Rudi Kasome Thread Inayosema Kuoa Single Mother Ni Kunywa Soda Iliyofunguliwa

Kwahiyo hujisikii/umechoka kushauri

Unataka akatumie ushauri wa kwenye uzi ule[emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787]
 
Mmmh!!! [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Ila mwamba ulikua kasi mno, hilo jambo ilitakiwa ushauriane nae kwanza akubali kubadili ukoo wa mtoto kwa maslahi mapana mfano ungemwambia ili uweze kumwandalia bima ya afya, anufaike na urithi pia akue akijisikia ni ndugu na wazaliwa wa hapo kwako kwakua wote watatumia jina moja.
Hii ndio point kubwa ya kumfaa muhitaji.
Kwakweli JF pamevamiwa na watu wenye kukurupuka ktk kutoa ushauri.
Wako wapi ma GREAT THINKERS?
Andiko kama hili ni SPECIAL mno.
Linagusa Familia nyingi sana ktk jamii za kiafrika.

Usishauri jamaa amuache mdada, ila Ushauri uwe namna ya kutatua changamoto kama LUCKMAN1 anavyo pendekeza.
Kesi kama hii Nililetewa na shemeji yangu mdogo, mmoja wa ndugu za mke wangu,
Mimi na mke wangu tuliitatua vizuri kuliko wakwe zangu waliomtaka kijana wao aachane na demu mwenye watoto 2.
Leo hii ni miaka 14 wanaishi na wana watoto wengine 2.
Ubini wa watoto wa yule mwanamke haukubadilishwa. Watoto wanahudumiwa vema na Shemeji yangu na mmoja yupo UDSM.
 
Mimi Nashauri hivi;
jamaa usimuache mwanamke unaempenda kwasababu ya UBINI wa baba yao.
Kuchana madaftari, hakumaanishi kwamba demu anampenda jamaa aliyezaa nae.
Upendo unanguvu ya kuvuka mipaka ya ukomo mliojiwekea ktk kutoa huduma kwa wanajamii wenu.

Namaanisha, Upendo wako usiwe na mipaka.
Hata ndugu wa huyo mtoto wanaweza kuja kumsalimu kijana wao wakipenda.
Kubadili jina ama ubini wa mtoto kuna taratibu zake, japo si vizuri kubadili ubini wa mtoto kama baba wa kumzaa yupo hai au anajulikana na jamii inayo wazunguka.
Siku moja, atajua kwamba wewe si baba yake mzazi, ataonyeshwa mahali ukoo wake upo,,,,,,, hakika itakusumbua sana.
KIROHO,,,,,,,, ikiwa zitatokea changamoto za kiroho,,,,, mambo ya mizimu na matambiko,,,,,,,,mambo ya kiimani, hakika utapata shida mpaka utakapo mrudisha ktk ukoo wake halisi.

USIMUACHE MDADA,,,,,,,,,, MPENDE NA MUHUDUMIE MWANAE PASIPO KUBADILI JINA LAKE LA UBINI.
 
Braza upo vyema kichwani kweli ama ni Afande Swila ndio anaandika hapa? Unampiga chini kisa kakuambia ukweli utachukuaje jina la kwako ukampe mtoto wa mwanaume mwenzio? Ningekuwa mimi ndio ingekuwa fursa ya kuacha mpaka kutoa huduma na kumlipia ada huyo Kelvin. Zaa wa kwako.
Nikweli jamaa kakosea ila ilikuwa ni mambo yakuelekezana tu, huyo single mother angemwambia mwenzake kistaarabu tu kuliko maneno ya kashfa.
 
Au una jina baya mkuu, halina swagg.

Manake sisi wanawake hatuishiwi vioja.

[emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Just kidding.

That is just a dumb woman. Angeweza kuongea fresh na wewe na ukamuelewa bila drama za kukutupia maneno ya ovyo.
Yaani umenena kama mawazo yangu, alafu mleta uzi bado hajampiga chini huyo single mother ila anahitaji ushauri, kwa mimi naweza sema ampotezee huyo single mother atafute kabinti kabichiii waanze nako maisha over
 
Huyo baba wa mtoto anamtunza mwanae?,naona kama jamaa bado anatafuna huo mzigo.
 
Natarajia kuoa hivi karibuni na mke mtarajiwa ana mtoto wa miaka 5. Huyu mtoto namhudumia kwa kila kitu na namuonesha upendo wote kama baba yake mzazi.

Kuna shida imejitokeza baada ya kumpeleka mtoto aanze shule (nursery school ). Katika kujiandikisha nikampa jina langu la ukoo (Eg. Ngwengwe) madaftari full mkoba jina nimeandika Kelvin Ngwengwe.

Bhana eeh, mama yake alivyoona madaftari amechana chana, kumuuliza kisa nini mbona umechana madaftari ya mtoto?? Jibu alilonipa limeniacha hoi.

Namnukuu "Huyu mtoto baba yake yupo hai kwanini usitumie jina la ubini wa baba yake mzazi badala yake umetumia jina la ubini wa kwenu! Zaa mtoto wako umuite jina la kwenu"

Maamuzi niliyochukua ni kumpiga chini tu
PIGA CHINI HUYOO

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app
 
Achana naye sasa kama baba yake yupo kwa nn hamuhudumii mtoto wake mkuu fukuza hyo ng'ombe haraka sana.
 
Mimi Nashauri hivi;
jamaa usimuache mwanamke unaempenda kwasababu ya UBINI wa baba yao.
Kuchana madaftari, hakumaanishi kwamba demu anampenda jamaa aliyezaa nae.
Upendo unanguvu ya kuvuka mipaka ya ukomo mliojiwekea ktk kutoa huduma kwa wanajamii wenu.

Namaanisha, Upendo wako usiwe na mipaka.
Hata ndugu wa huyo mtoto wanaweza kuja kumsalimu kijana wao wakipenda.
Kubadili jina ama ubini wa mtoto kuna taratibu zake, japo si vizuri kubadili ubini wa mtoto kama baba wa kumzaa yupo hai au anajulikana na jamii inayo wazunguka.
Siku moja, atajua kwamba wewe si baba yake mzazi, ataonyeshwa mahali ukoo wake upo,,,,,,, hakika itakusumbua sana.
KIROHO,,,,,,,, ikiwa zitatokea changamoto za kiroho,,,,, mambo ya mizimu na matambiko,,,,,,,,mambo ya kiimani, hakika utapata shida mpaka utakapo mrudisha ktk ukoo wake halisi.

USIMUACHE MDADA,,,,,,,,,, MPENDE NA MUHUDUMIE MWANAE PASIPO KUBADILI JINA LAKE LA UBINI.
Sasa mkuu shida ni moja nataka kumpiga chini huyu mwanamke ila kila nikimuangalia huyu mtoto roho inaniuma sana sababu huyu mtoto nimemlea tangu akiwa na mwaka mmoja (1) na anajua kabisa mimi ndio baba yake mzazi.
Mama yake ni kichwa panzi katika kipindi chote iko cha miaka 4 hataki kuzaa mpaka nimuoe.
Dogo upstairs yupo vizuri sana Naona nikimpiga chini mama yake huyu dogo ataharibikiwa sana
 
Achana nae mara moja kabla hujaenda katika hatua nyingine ya kuwa wife wako, utaendasumbuka bure huko mbeleni
 
Let say unaitwa Ngwengwe, Mme mwenzio ...maana mkeo ana mitala ....anaitwa Sida.
Mtoto anaitwa Jane.
Shuleni ni "Jane Sida". Siku ukienda shuleni kwa mtoto lazima uitwe jina LA Mme mwenzio.
" Hello Mr sida ,mzazi wa Jane" utasalimiwa hivo kumbe wewe ni Ngwengwe.
 
Sasa mkuu shida ni moja nataka kumpiga chini huyu mwanamke ila kila nikimuangalia huyu mtoto roho inaniuma sana sababu huyu mtoto nimemlea tangu akiwa na mwaka mmoja (1) na anajua kabisa mimi ndio baba yake mzazi.
Mama yake ni kichwa panzi katika kipindi chote iko cha miaka 4 hataki kuzaa mpaka nimuoe.
Dogo upstairs yupo vizuri sana Naona nikimpiga chini mama yake huyu dogo ataharibikiwa sana
Sasa wewe, obviously mama mwenye mtoto mwaka mmoja, jua baba take hayupo mbali.
 
Hahaha, atoe mahitaji yote ya mtoto halafu baba mzazi yupo hai lakini kwenye matunzo ya mtoto ni marehemu. Halafu bado huyo mwanamke amkingie kifua kisa baba mzazi. There is something very wrong somewhere. Hao watu wanakulana.. full stop
Huna mbegu za kumzalisha mtoto wa kumwita ubini wako? Acha ubinafsi uliopindukia.

Piga chini ndio. Mwanamke amefanya maamuzi sahihi kabisa. Wanaume wapo tuu.... Tena wa kutosha kwa wanawake wanaojielewa.
 
Back
Top Bottom