Mkoa wa Pwani watoa Mawaziri watano kwenye baraza jipya; ni bahati mbaya au ndiyo tuseme sasa zamu ya watu wa Pwani?

Mama Samia yupo vizuri na yupo sahihi.Hatuna shida hata lingekuwa baraza zima,cha muhimu ni kuwa hao walioteuliwa ni watanzani,wasomi na wanauwezo wa kuyafanya halo majukumu.

Kama sifa wanazo hao masnitch wanaomdis mama waendelee kuumia tu.
Tunambariki mama KAZI IENDELEE.
 
Msoga anaiharibu Sana hii nchi.Hata aibu Hana.
 
Greetings Wana JF!

Kwenye baraza hili la mawaziri, viongozi watano wametoka katika mkoa wa Pwani peke yake. Nimekuwa nikijiuliza ina maana mkoa wa Pwani una mchango mkubwa sana kwenye nchi hii, na ni "wachapakazi" sana au ina "viongozi wenye akili nyingi sana" mpaka wateuliwe kwa wingi hivi kwenye baraza la mawaziri?

Mawaziri na manaibu mawaziri walioteliwa kwenye baraza la mawaziri katika mkeka uliotoka hivi karibuni wanaotokea mkoa wa Pwani ni;
1. Selemani Said Jaffo - Mbunge wa Kisarawe ( Waziri wa Ofisi ya makamu wa Rais - mazingira)
2. Mohamed Omary Mchengerwa - Mbunge wa Rufiji (Waziri wa Utamaduni na michezo)
3. Abdallah Hamis Ulega - mbunge wa Mkuranga ( Naibu waziri mifugo)
4. Ridhwan Jakaya Kikwete - mbunge wa Chalinze ( Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi)
5. Omary Kipanga - mbunge wa Mafia ( Naibu waziri wa Elimu)

Kitu ninachojiuliza inakuaje kamkoa kadogo kama Pwani kanatoa mawaziri na manaibu mawaziri wengi kiasi hicho? Wakati kuna mikoa mingine mikubwa tu na yenye mchango mkubwa sana kwenye taifa hili haijatoa kabisa, na kama imetoa kiongozi ni mmoja tu? Kitu ninachokiona sasa hivi ni kuwa uongozi wa nchi hii unaegemea zaidi mikoa ya Pwani na Zanzibar. Ukihesabu viongozi wote waliopo kwenye baraza la mawaziri nusu wanatokea mikoa ya pwani ( Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara na Zanzibar)

Hii kitu haipendezi kabisa na haina afya kwa umoja wa kitaifa. Na inaonyesha kuwa Kuna kakikundi kadogo cha wanafamilia (Makamba, Kikwete, Mwinyi na Nnauye) na wapambe wao wa mikoa ya pwani ndo wanatawala nchi hii sasaiv na wanagawana madaraka wanavyotaka bila aibu.
#Acha ukweli usemwe
Nawasilisha
 
Usipotumia akili yako kujijibu kitu unachokiona jua hata minyoo tumboni kwako itakuwa na leseni ya kuutafuna utumbo wako!.
 
Ina maana yule bedui alipojaza Wasukuma kuanzia kwenye Uwaziri hadi ukurugenzi wa halmashauri alikuwa na maana kwamba wao ndio walikuwa na mchango zaidi!
 
Na hao wote ni wakazi wa Kinondoni.

Kwahiyo Kinondoni imetoa mawaziri Watano.

Tuache mambo ya kugawanya nafasi za uwaziri kwa sababu ya eneo.

Tanzania sio nchi ya Muungano ya Majimbo, hivyo uongozi haulazimiki kufuata mgawanyo ama uwakilishi wa majimbo.

#Mama yupo kazini.
 
We mpuusi mbona unaendekeza ukabila? Kwamba watu wa pwani si watu? Kipindi cha mwendazake ulizungumza kuhusu usukuma? Kutawala Baraza la mawaziri?
 
Pwani oyeee

1. Dr. Jaffo - kisarawe
2. Mchengelwa - Rufiji
3. Ridhiwani - Chalinze
4. Ulega - Mkuranga
5.kipanga - Mafia

Hivi siku hizi uongozi wa nchi hakuna regional representation?

Rais Samia hapa washauri wamekubambika.
Kipindi cha magufuli mlisema?
 
Ostadh gang. Hii inaitwa ostadh gang

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
 
Ina maana yule bedui alipojaza Wasukuma kuanzia kwenye Uwaziri hadi ukurugenzi wa halmashauri alikuwa na maana kwamba wao ndio walikuwa na mchango zaidi!
Jibu hoja usilete utoto hapa. Ni wapi mkoa mmoja wa usukumani ulitoa mawaziri watano ?
 
Nani anakataa kwamba hayuko kazini ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…