Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi, Scotland: Rais Samia ametuangusha

Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi, Scotland: Rais Samia ametuangusha

Wanabodi,



Kama mtanzania, inawezekana umepata nafasi kufuatilia yanayojiri nchini Scotland kwenye mkutano unaohusu mabadiliko ya tabia nchi. Mkutano huu umehudhuriwa na viongozi wengi akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan ambaye alihutubia mkusanyiko huo.

Tofauti na nchi kama China, Marekani na India, Tanzania haihusishwi sana kwa kuwa chanzo cha mabadiliko ya tabia nchi. Umuhimu wa kuhudhuria mkutano huo ni kujumuika na viongozi wengine katika kujadili suala hili na kuwa na mchango unaoweza kuleta manufaa chanya kwa miaka mingi ya baadaye.

View attachment 1996340

Nimebahatika kuanglia hotuba zote za Rais Samia na kwa bahati mbaya au nzuri, aligusia zaidi kwenye umuhimu wa nchi zilizoendelea kuzisaidia nchi ambazo hazijaendelea kifedha ili kuweza kukabiliana na tatizo hili la mabadiliko ya tabia nchi.

Labda inawezekana kwamba ni kweli Tanzania inahitaji misaada hiyo lakini kwa upande wa pili haipendezi kuona kwamba mawazo haya ya kuendelea kupata misaada imetawala katika vichwa vya viongozi wetu. Kauli kama hizo zinaweza zisizae matunda.

Ingependeza sana kama Rais Samia angejizatiti zaidi katika kuongelea umuhimu wa kuwa na "balance" katika shughuli za maendeleo, maslahi ya binadamu na mikakati ya kulinda mazingira. Kama Tanzania, angezungumzia changamoto zinazo sababishwa na mabadiliko ya tabia nchi na mipango yetu haswa katika kipindi ambacho tunatamani uchumi wa viwanda.

Kwa nchi zilizoendelea, umuhimu wa sayansi katika kuvumbua njia mpya zisizo chochea uharibifu wa mazingira zinazoweza kutumika kwenye sekta mbali mbali

Mungu ni mwema, wakati wote

Large heads small brains!
 
Mnaona aibu kuomba omba? Mnamuonea aibu nani asiyejua nchi hii ni masikini wa kutupwa na inategemea misaada kuendeshwa? Ndiyo hali halisi nchi masikini kama hii haiwezi kumudu mfano tozo ya kupunguza carbon (carbon tax).

Lazima tusaidiwe au mnataka Watanzania wafe na tai shingoni kwa kuona aibu kutembeza bakuli? Ndiyo maana yule aliyepita aliona aibu za kuomba msaada wa kupambana na Covid-19, wengi wakafa kwa ajili hiyo. Tukubali nafasi yetu hapa duniani kama nchi masikini, tunaotegemea misaada miaka 60 tangu tupate uhuru.
Mkuu najua una uwezo ila si mahitaji yote unaweza kuyatatua kwa kiasili chote Cha pesa ulichonacho

Kwa kua wewe unaona Jambo hili Ni jema na linafaa....

Ukipata muda umtume mkeo kwangu nimuongezee pesa ili muweze kukamilisha Mambo mengine mliyobakisha,

Usije ukajali sana kuhusu kuchelewa kwake Cha msingi pesa unayohitaji itakufikia yote
 
Na serikali ingepunguza gharama za umeme Ili watu wajikite kwenye kupikia na kupunguza kutumia mikaa na kuanzisha kampeni za upandaji miti kitaifa, maana makazi mengi yanaanzishwa bila kuhiniza upandaji miti
Hili la kupanda miti ni muhimu sana, angalau kila kaya ipande miti kumi kwa mwaka.
 
Ni yale yale ya Maria Magdalena.Kama kuna uhaba wa mkate si wangekula keki?Kipato cha siku kwa watanzania wengi (majority wanaishi vijijini ni shillingi ngapi?)
Wana uwezo wa kutumia gesi.?Tuhimizane tusikate miti ovyo na tukikata mti tupande mti.
Kama gesi tunayo kwanini kusiwe na jinsi ya kupata bei inayowezekana kila mtu kununua au wakulima waweze kubadilisha mazao kwa mtungi wa gesi.
 
Rais kakumbushia utekelezaji wa Maazimio ya Paris. Mataifa makubwa yanayoongoza kuzalisha hewa ya ukaa, kinara akiwa China, US na Urusi na nyingine ziliji commit kutoa karibu Usd 100bilioni kukabilia mabadiliko ya Tabianchi.

Sasa kosa kukumbusha utekelezaji wa ahadi? Ina maana gani sasa kila mara viongozi wakutane halafu hakuna utekelezaji? Nilitegemea tumpongeze Rais wetu kawagonga wakubwa diplomatically...

Litaonekana wapi ?!!
Atapongezwaje nasi kwa diplomasia hiyo KUBWA?!!

Sisi tumeamua KUPINGA TU....
Sisi tunaitwa PINGA PINGA FC.....

Wengine wetu ni kutoka CHADEMA🤣
Wengine wetu ni wafuasi wa akina ndugu komredi Polepole......

KAZI YETU NI KUMPINGA MH.RAIS SAMIA NA SERIKALI YAKE YA AWAMU YA 6....

ASEME KUBWA ASEME DOGO sisi ni KUMPINGA TU 🤣🤣🤣

Siempre SSH
 
Mkuu najua una uwezo ila si mahitaji yote unaweza kuyatatua kwa kiasili chote Cha pesa ulichonacho

Kwa kua wewe unaona Jambo hili Ni jema na linafaa....

Ukipata muda umtume mkeo kwangu nimuongezee pesa ili muweze kukamilisha Mambo mengine mliyobakisha,

Usije ukajali sana kuhusu kuchelewa kwake Cha msingi pesa unayohitaji itakufikia yote
Hiyo Sasa ni dhihaka ya KITOTO...UTOTO MWINGI...

Ya mke yanahusiana vipi na diplomasia ya kimataifa Kati yetu na nchi zilizoendelea?!!!!

FYI: Ukikua utajua kuwa mke anaweza "kuuza haki ya mwenza" bila ya "kutumwa na mumewe" ama bila ya malipo yoyote....yaani huduma ikawa BUREEE BUREEE...bureee kabisaaaaa🤣

Siempre SSH💪
 
Kama gesi tunayo kwanini kusiwe na jinsi ya kupata bei inayowezekana kila mtu kununua au wakulima waweze kubadilisha mazao kwa mtungi wa gesi.
Unaishi Tanzania kweli?Hayo mawazo ya ujima.Wakitaka mahitaji mengine wabadilishe kwa kutoa mazao?Wananchi walio wengi hawana uwezo wa kupata hata mlo zaidi ya mmoja kwa siku.
Anayenunua mazao kwa kubadilishana na gesi ni nani?Serikali?Halafu hayo mazao wanapeleka wapi?
 
Hapa ndio mnapojjchanganya
Mama Samia alipokuwa bagamoyo alisema wameweka tozo ili nchi ijiendeshe iache kutegemea mikopo ambayo inakuja na mashrti magumu
Kama mnasema hao matajiri wana pesa za kuleta huku basi ondoeni tozo
Wananchi sasa ndo inabidi tusimame kidete ili tozo ziondoke!
Alafu fedha za climate finance na adaptation fund ni nyingi. Na si za mkopo kama za maendeleo chini ya WB au IMF!
Mwisho MIMI siko huo upande wa waweka tozo...
 
Unaishi Tanzania kweli?Hayo mawazo ya ujima.Wakitaka mahitaji mengine wabadilishe kwa kutoa mazao?Wananchi walio wengi hawana uwezo wa kupata hata mlo zaidi ya mmoja kwa siku.
Anayenunua mazao kwa kubadilishana na gesi ni nani?Serikali?Halafu hayo mazao wanapeleka wapi?
"....wananchi walio wengi hawawezi kupata zaidi ya mlo mmoja kwa siku"?!!

Ni hukohuko vijijini?!!!

Huku mijini inajulikana sababu ni zipi....ziko nyingi mno......
 
"....wananchi walio wengi hawawezi kupata zaidi ya mlo mmoja kwa siku"?!!

Ni hukohuko vijijini?!!!

Huku mijini inajulikana sababu ni zipi....ziko nyingi mno......
Mkuu tembea vijijini uone hali halisi. Walio wengi wanaishi kwa dhiki sana. Hawana maisha ya uhakika wa kupata milo mitatu kwa siku.
 
Litaonekana wapi ?!!
Atapongezwaje nasi kwa diplomasia hiyo KUBWA?!!

Sisi tumeamua KUPINGA TU....
Sisi tunaitwa PINGA PINGA FC.....

Wengine wetu ni kutoka CHADEMA🤣
Wengine wetu ni wafuasi wa akina ndugu komredi Polepole......

KAZI YETU NI KUMPINGA MH.RAIS SAMIA NA SERIKALI YAKE YA AWAMU YA 6....

ASEME KUBWA ASEME DOGO sisi ni KUMPINGA TU 🤣🤣🤣

Siempre SSH
Wanaopinga wawe na hoja na knowledge ya kile wanachokipinga basi. Ndiyo ukomavu katk mijadala. Sasa yaani vikao vikao...kuongea..kuongea tu kila mwaka bila utekelezaji? Rais kawagonga kidiplomasia jamaa watekeleze ya Paris kwanza. Tunasema katuangusha? Hapana sasa, si sahihi na hatuipi heshima nchi yetu.
 
Mkuu tembea vijijini uone hali halisi.Walio wengi wanaishi kwa dhiki sana.Hawana maisha ya uhakika wa kupata milo mitatu kwa siku.
Mkuu wangu hebu twende taratibu....

Katika Jambo kubwa na sumbufu aliloumbiwa mwanadamu ni UPATIKANAJI WA CHAKULA....

Ni uzito KUPATA chakula Cha kushiba....ni uzito pia KUPANGA RATIBA YA KULA/CHAKULA....

Mkuu wangu hivi unajua ni kwanini WAYAHUDI wanapoamka asubuhi basi jambo la mwanzo ni KUMSHUKURU M/MWENYEZI kuwaumba walivyo na kutoacha kuwapa MKATE WAO WA KILA SIKU??!!

Waislam hupiga dua za kabla na baada ya kula?!!

Wakristo huomba na kusali kabla na baada ya kula?!!!

Mkuu mambo ya vyakula ndani ya kaya ni zaidi ya Sera za SERIKALI....

Karibu kahawa na kashata hapa kijiweni....mchana huu 🤣🤣
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Wanaopinga wawe na hoja na knowledge ya kile wanachokipinga basi. Ndiyo ukomavu katk mijadala. Sasa yaani vikao vikao...kuongea..kuongea tu kila mwaka bila utekelezaji? Rais kawagonga kidiplomasia jamaa watekeleze ya Paris kwanza. Tunasema katuangusha? Hapana sasa, si sahihi na hatuipi heshima nchi yetu.
😍
 
Copy and paste ya utawala wa mzee wa Msoga.
FB_IMG_16307140795615105.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Unaishi Tanzania kweli?Hayo mawazo ya ujima.Wakitaka mahitaji mengine wabadilishe kwa kutoa mazao?Wananchi walio wengi hawana uwezo wa kupata hata mlo zaidi ya mmoja kwa siku.
Anayenunua mazao kwa kubadilishana na gesi ni nani?Serikali?Halafu hayo mazao wanapeleka wapi?
Kenya wanahitaji mazao yetu ya chakula, huu ni mfano mdogo tu.
 
Back
Top Bottom