Mnakomaa kupata Tume Huru ya Uchaguzi, mnadhani itawaweka madarakani?

Mnakomaa kupata Tume Huru ya Uchaguzi, mnadhani itawaweka madarakani?

Mkuu sijapinga, nimehoji labda hujaelewa.
Mawazo ya wafuasi wa watawala na ma dictator popote huwa ni dhidi ya wananchi.

Tuboreshe katiba na tume kwa ajili ya vizazi na wajukuu wetu . Tusiwaachie ugomvi kwa sababu tu za kiitikadi .
 
Mawazo ya wafuasi wa watawala na ma dictator popote huwa ni dhidi ya wananchi.

Tuboreshe katiba na tume kwa ajili ya vizazi na wajukuu wetu . Tusiwaachie ugomvi kwa sababu tu za kiitikadi .
Katiba mpya. Je,tukibadili katiba alafu ikakosa mtu thabiti wa kuisimamia? Tume huru itapatikana kwa mfumo imara ambao utaondo watu wenye nasaba na siasa kabisa. Sio huu mnaoulilia nyie waganga njaa.
 
Katiba mpya. Je,tukibadili katiba alafu ikakosa mtu thabiti wa kuisimamia? Tume huru itapatikana kwa mfumo imara ambao utaondo watu wenye nasaba na siasa kabisa. Sio huu mnaoulilia nyie waganga njaa.
Ndiyo maana nikasema mawazo yako huwa ni ya hovyo mno humu Jf . Mtu imara ni yupi ?!

Tanzania inahitaji TAASISI imara na siyo mtu imara. Taasisi zikiwa imara zitadhibiti viongozi wa hovyo . Kama hawa wanaovunja katiba na kuiba kura.
 
Watanzania kwa sasa tunataka Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi! Tatizo liko wapi ikiendelea kushinda CCM katika mazingira ya uchaguzi huru na wa haki? Nyinyi kubalini tu uwepo wa hiyo Tume, lakini pia kuurejesha mchakato wa Katiba Mpya. Nyinyi si mnapendwa! Mmenunua ndege, mmeifanya nchi kuwa uchumi wa kati! Sasa hofu iko wapi?

Kinachotukera Watanzania wengi kiasi cha kutufanya kususia zoezi la upigaji wa kura, ni uwepo wa hiyo tume hovyo ya uchaguzi, mamlaka makubwa ya Rais kuingilia huo mchakato mzima wa uchaguzi, na uwepo wa wale nyau policcm wanao tumika kuwatisha wagombea wa upinzani, mawakala na pia wapiga kura.
katiba mpya na tume huru? sisi kijijini kwetu tunataka madalali wasitupangie bei ya mazao, pia tunataka maji yawe yanapatikana muda wote, barabara na umeme hakuna tatizo ila maji yanaweza kukata siku nzima, yanatoka kwa wiki mara nne au tano tu, tunataka yawepo muda wote, halafu na bei ya mafuta ya kula ishuke. yaani lita moja imekua karibu elfu 10 sasa hivi, hayo makatiba na matume yafuatie baada ya mambo hayo ya msingi
 
Kwa mujibu wa ibara ya 190 ya rasimu ya katiba ya JMT iliyoundwa na tume ya Jaji warioba ni kuwa kutakuwa na tume huru.

Mwenyekiti, makamu mwenyekiti na wajumbe saba wa tume watakuwa wanateuliwa na rais. Kama mwenyekiti akitoka bara,makamu atatoka Zanzibar vivyo hivyo makamu akitoka Zanzibar mwenyekiti atatoka bara.

Pia ibara ya 191 imeanisha kuwa kutakuwa na kamati ya uteuzi. Ambayo itachambua majina ya waliomba kisha kumpelekea rais na yeye atateua jina walilopitisha. Na kisha jina kurudishwa bungeni na kisha kuthibitishwa na bunge.

Je hao wajumbe wa kamati ya uteuzi mnajua wanapatikana vipi? Hata kama nafasi za Ujaji zitakuwa ni za kuomba kisha kuteuliwa na rais mnajua watakuwa na mamlaka gani? Hawatakuwa na nasaba za kisiasa?

Hao wataoomba nafasi za kuingia tume huru ya uchaguzi mtakuwa na uhakika hawana nasaba za kisiasa?

My take; Kama mnataka kuingia madarakani ni bora mkajenga imani kwa wananchi kuwa nyie ni wanansiasa mnaofaa kwa kila namna. Maana hata ikipatikana hiyo mnayoita tume huru mtapigwa tu.
Nikifikiria kichefu chefu cha tumeccm nasikia kutapika
 
Ndiyo maana nikasema mawazo yako huwa ni ya hovyo mno humu Jf . Mtu imara ni yupi ?!

Tanzania inahitaji TAASISI imara na siyo mtu imara. Taasisi zikiwa imara zitadhibiti viongozi wa hovyo . Kama hawa wanaovunja katiba na kuiba kura.
Taasisi imara hujengwa na watu imara,amabao wanasimamia misingi ya katiba. Habari za kuiba kura achana nazo discuss mada husika. Niko gado natoa mawazo sahihi.
 
Usinitishe we jamaa,kama kuanza hata kama ni 1990. Je, hii itabadilisha mfumo wa upendeleo kwenye tume kama mnavyolalamika? Maana hata ikiwa kama tume ya warioba ilivyopendekeza hao wanaopitishwa kisha kuteuliwa na rais wataacha kuwa na mizengwe kama manavyolalamika? Tumia akili acha ushamba wa kisiasa.
Nasema hivi acha utoto, kwakuwa umejiunga hapa jukwaani hiyo 2020, basi unajua hata katiba mpya imeanza kudaiwa kwa sababu ya ule upuuzi uitwa uchaguzi wa 2020.
 
Nasema hivi acha utoto, kwakuwa umejiunga hapa jukwaani hiyo 2020, basi unajua hata katiba mpya imeanza kudaiwa kwa sababu ya ule upuuzi uitwa uchaguzi wa 2020.
Haya basi tokea mwaka 1992 mnadai katiba mpya,je ikibadilishwa mtapata ushindi wa ubunge ambao na wewe umeukosa mpaka roho inataka ipasuke?

Je haya malalamiko kuwa Mkurugenzi na Mwenyekiti wanateuliwa na kupendelea Ccm yatakuwa ndio mwisho?
 
Haya basi tokea mwaka 1992 mnadai katiba mpya,je ikibadilishwa mtapata ushindi wa ubunge ambao na wewe umeukosa mpaka roho inataka ipasuke?

Je haya malalamiko kuwa Mkurugenzi na Mwenyekiti wanateuliwa na kupendelea Ccm yatakuwa ndio mwisho?

Ndio maana nakuambia hujui lolote kwenye katiba mpya, ndio maana unadhani katiba mpya ni kwa ajili ya kuitoa ccm madarakani. Narudia tena, punguza utoto kwenye majukwaa ya wanaume.
 
Huja haja ya kutukana, jibu swali kisha toa ushahidi. Au zile picha za Kawe ndio ushahidi wako? Mpaka leo mwezi wa nne hujaenda mahakani?

Pia kumbuka mada ni tume huru,je utakutoa?
Katiba mpya na tume huru ya uchaguzi
 
Hii technique naona inaelekea kupendwa, ukikosa majibu ya wananchi unanyooshea mkono Chadema Kwa sababu ndio angalau unaweza kuja na majibu japo swali halikuwa Hilo. Njia sahihi za kupambana na changamoto zikikushinda, kimbilia Imani.
 
Kwa mujibu wa ibara ya 190 ya rasimu ya katiba ya JMT iliyoundwa na tume ya Jaji warioba ni kuwa kutakuwa na tume huru.

Mwenyekiti, makamu mwenyekiti na wajumbe saba wa tume watakuwa wanateuliwa na rais. Kama mwenyekiti akitoka bara,makamu atatoka Zanzibar vivyo hivyo makamu akitoka Zanzibar mwenyekiti atatoka bara.

Pia ibara ya 191 imeanisha kuwa kutakuwa na kamati ya uteuzi. Ambayo itachambua majina ya waliomba kisha kumpelekea rais na yeye atateua jina walilopitisha. Na kisha jina kurudishwa bungeni na kisha kuthibitishwa na bunge.

Je hao wajumbe wa kamati ya uteuzi mnajua wanapatikana vipi? Hata kama nafasi za Ujaji zitakuwa ni za kuomba kisha kuteuliwa na rais mnajua watakuwa na mamlaka gani? Hawatakuwa na nasaba za kisiasa?

Hao wataoomba nafasi za kuingia tume huru ya uchaguzi mtakuwa na uhakika hawana nasaba za kisiasa?

My take; Kama mnataka kuingia madarakani ni bora mkajenga imani kwa wananchi kuwa nyie ni wanansiasa mnaofaa kwa kila namna. Maana hata ikipatikana hiyo mnayoita tume huru mtapigwa tu.
Rubbish
 
Sio tume huru tu hata matokeo ya uraisi kupingwa mahakamani
 
Msikilize huyo bosi wako wakati ana akili zake timamu
 

Attachments

  • pole_pole_na_uchaguzi_huru_na_haki.mp4
    299.1 KB
Ndio maana nakuambia hujui lolote kwenye katiba mpya, ndio maana unadhani katiba mpya ni kwa ajili ya kuitoa ccm madarakani. Narudia tena, punguza utoto kwenye majukwaa ya wanaume.
Ninyi wahafidhina wa Chadema nia yenu mnadhani mkipata katiba mpya mtapata madaraka.
 
Tunahitaji Katiba mpya ambayo itatoa haki, hata tusipopata madaraka lakini atakayepata madaraka atapatikana kwa haki fullstop.
Mh.. hivi kama serikali imeingia bila ridhaa ya wananchi itatawala?
 
Ninyi wahafidhina wa Chadema nia yenu mnadhani mkipata katiba mpya mtapata madaraka.
We mburura sio kuchukua madaraka wananchi wanataka viongozi waliopatikana kwa haki na Uhuru
Sio Hawa waliowekwa kutokana na mfumo mbovu wa katiba ya Sasa
Embu kuwa na akili hata kidogo.
Tunataka katiba ambayo itaunda mfumo wa upatikanaji viongozi kwa Uhuru na haki.
Wakiwa wa ccm,act,cuf,chadema, tlp ,chauma sawa lakini wapatikane katika utaratibu wa Uhuru na haki.
Tumeshuhudia ktk uchafuzi uliopita msimamizi wa uchaguzi DED anakataa kupokea fomu za mgombea just because ni wa upinzani, wengine walifunga ofisi .
Just ili kusababisha wagombea wa ccm kupita bila kupingwa.
It was all rubbish election and misuse of public funds
 
Mh.. hivi kama serikali imeingia bila ridhaa ya wananchi itatawala?
Ni hivi mtaani kwetu sisi tumemkataa mwenyekiti wa mtaa kwani ni mpuudhi flani hivi na Wala hatukumchagua
Yaani ni shida akiitisha mkutano wananchi Wala hatuhudhuria , mtaani hata hatuna time naye, alifiwa na mtoto wake wananchi wala hatukwenda kwenye msiba, walikuja ndugu zake tu
Kiufupi anapata shida sana kuongoza kwani alipata uenyekiti bila ridhaa ya wananchi ,huo ni mfano tu nakupatia
 
Back
Top Bottom